Wahitimu wa Tanzania hamuajiriki

Wahitimu wa Tanzania hamuajiriki

Tatzo la wengi we2 mawazo mgando....
Guys dnt wanna face da reality n work on challenges.
Vyuo vngi saiv coni aibu kuviita vya kata hku wakijitotoleshea degree viza kibao mpk zinachefua.
Alone mpk leo kuna watu wapo mtaan mwk wa tatu huu wanatukan ajira hawana mpe karatas na kalamu mwambie aandike applcn leta.i swea utavunja mbavu.
Ni wengi wengi tn wengi saaaana.
 
Corse ya kuandika barua alimaarufu communication skills vyuo ving huwa inafundishwa semista moja tuu ya mwaka wa kwanza na mtu unakuta anamiaka mitatu au mnne ndo anamalza unadhani atakumbuka kweli kuandika cv au official letter? Sasa change inabidi ianzie vyuoni ikiwezekana ilo somo lisomwe semista zote mwanafunzi awapo chuoni

Napingana na wewe mkuu,kweli katika information age hii tuliyomo CS ifundishwe kila semester!

Kazi ya internet ni nini?unashindwa vp msomi kujifunza/kujikumbusha skills ndogondogo kama uandishi wa barua na wasifu wakati mtandao umejaa vitabu na notes kibao?
 
Corse ya kuandika barua alimaarufu communication skills vyuo ving huwa inafundishwa semista moja tuu ya mwaka wa kwanza na mtu unakuta anamiaka mitatu au mnne ndo anamalza unadhani atakumbuka kweli kuandika cv au official letter? Sasa change inabidi ianzie vyuoni ikiwezekana ilo somo lisomwe semista zote mwanafunzi awapo chuoni

Mkuu hadi uandishi wa barua na CV mtu anasahau? huo ni uzembe, kama tunasoma ili tusahau basi hamna haja ya elimu, tunasoma ili tuapply tulichosoma kusolve matatizo mbalimbali, ingekua kila engineer anasoma anasahau kila kitu, leo hii tusingekua na computer za kutumia... Na internet ipo ya kazi gani, google official letter zitakuja search results zaidi ya milioni, badala ya kufanya vitu systematic ndo kwenda kuomba kazi mtu anaelezea matatizo waliyo nayo nyumbani? kuna tofauti ya kuomba kazi na kuomba msaada..

Change inabidi ianzie kwa wanafunzi wenyewe, washiriki effectively kwenye masomo na si kusomea mitihani then wakimaliza mitihani kila kitu kimefutika.
 
Ni ukweli mtupu. Kuna mmoja ni mdada alituma CV zake ofisini, kwa jinsi alivyoiandaa tukaona tumuite tumfanyie usaili. Cha ajabu hiyo computer yenyewe hajui programu yoyote ile. Baada ya kumuliza atauambie kipi yeye anachojua kuhusu computer bila aibu akajibu yeye computer anatumiaga kwenye facebook/ ku chati chati, mpaka huruma yani. Alafu ati ndiyo kamaliza chuo huyo.

I saw for myself one bimbo of this sort ,so sad dude.Didn't know even how to send an attachment thru e mail. I thought she was joking at first:disapointed:
 
Hiyo yote ni mbinu ya kuhakikisha kuwa wakenya na waganda wanapata ajira zetu.

Kuna Professa mmoja juzi alikuwa ananichekesha sana pale chuon.Anasema nasikia sana hii kitu kuwa elimu yetu ni mbovu sana.But sisi tukienda ulaya tunaongoza ,huku hao wenye elimu nzur wakitufuata.

Pia hao wenye elimu nzur wamejaa hapa vyuon kwetu wanafanya masters na Phd.Sasa hii kitu kuwa sisi elimu yetu si nzur na hatuajiriki ni siasa au ni maneno tu.
 
Graduate wanaomaliza TZ kwa asilimia kubwa ni weupe na hawataki kukubali hili ukiwaambia wanatokwa povu mtu ana bachelor ya marketin hawez hata kuji market yy tu apate ajira anapopata chances za kufanya hvyo mtu ana A ya computer kwenye chet ukimpa machine ataangaika hapo mpk huruma tutalaumu sana waajir kwa hili laptop ni za Fifa11 na facebook tu kwao sio kujifunza basic skills
 
Graduate wanaomaliza TZ kwa asilimia kubwa ni weupe na hawataki kukubali hili ukiwaambia wanatokwa povu mtu ana bachelor ya marketin hawez hata kuji market yy tu apate ajira anapopata chances za kufanya hvyo mtu ana A ya computer kwenye chet ukimpa machine ataangaika hapo mpk huruma tutalaumu sana waajir kwa hili laptop ni za Fifa11 na facebook tu kwao sio kujifunza basic skills

Fifa 15 sasa hivi mkuu. 🙂
 
Corse ya kuandika barua alimaarufu communication skills vyuo ving huwa inafundishwa semista moja tuu ya mwaka wa kwanza na mtu unakuta anamiaka mitatu au mnne ndo anamalza unadhani atakumbuka kweli kuandika cv au official letter? Sasa change inabidi ianzie vyuoni ikiwezekana ilo somo lisomwe semista zote mwanafunzi awapo chuoni

Sio kweli kwamba kwa kuwa communication skills inafundishwa semister 1 basi huwa shida kuitumia baada ya kumaliza. Shida ni kwamba wanafunzi walio wengi hawapendi somo la communication skills. Wengi wao hulisoma ikitangazwa test ama final exam. Kinachowafanya wanafunzi wachukie communication skills ni msingi usio mzuri wa somo la kiingereza tokea shule za msingi.
 
lawama zote huenda vyuoni maana ndo kama stage ya mwisho ya kumkamilisha msomi. Ila pia inabid kujiuliza kule kwenye msingi huyo tunayemuita msomi alipata maandalizi sahihi.

Maana tusilaumu shamba kuto toa mazao bora tu, je maandalizi kabla ya kulima yalikua sahihi. Unakuta mwanafunzi wa chuo Internet na Laptop kaanza vitumia chuoni hata matumizi mazuri ya Google hayajui kweli wategemea atajifunza vitu vingi huyo.

Wengine wanakuambia hawawez somea Laptop hawajazoea. Wengine Lugha ya kufundishia haipandi ila utasikia mtu ana laumu mwanafunzi ana maliza chuo ajui English kweli kile chuo cha kata, ana sahau kujiuliza yule mwanafunzi alipita Primary akaenda Secondary huko ina maana walimfundisha English vizur ila alivyo fika chuo cha kata English ikaharibiwa na icho chuo au?.

Kabla ya kuwaalaumu wahitimu turudi nyuma tuangalie chanzo cha tatizo.

Wahitimu wengine wanamaliza chuo bila kufanya zile field wakat wa masomo kisa Chuo na Serikali havijaanda mpango uo kwa kozi husika. Sasa mafunzo bila vitendo yanawezekana vipi. Muhitimu kama huyo hawez kuingia kwenye interview akawashtua ma-Hr.

Cha mwisho, wakati wa kuchagua kozi za kusoma kwa vyuoni pale wanafunzi wengi huchagua kozi ili mradi aende chuo mara nyingi unakuta mwanafunzi amejaanza kozi mbili anazo zipenda alafu ana malizia na zingine kama tu kumalizia ujazaji wa form husika. Sasa ikitokea akichaguliwa izo alizojaza ili mrad ndo hapo tunatengeneza bomu uraiani.

Pia wengi wakati wa kuchagua hizo kozi wanakua na uelewa mdogo wa kozi husika wanazoenda zisomea na wengi hukuta mambo ndivyo sivyo walivyo tarajia.

Kuna matatizo mengi ambayi siyo lazima yote yatatuliwe ila yakipunguzwa basi tutakua na wahitimu bora na sio bora wahitimu.
 
Shule yako haijakufuta tongo tongo we we mtoa hoja. Sina tatizo na wahitimu wa Tanzania hata kidogo. wameandaliwa hivyo na iko hivyo siku zote. tofauti no kwamba babu alikuwa na familia ya MTU mmoja na mtoto ana familia ya Watu 2000 kwa mfumo ule ule wa elimu. Wape muda wa kidogo uone kama awafanyi kazi na hawaakiriki. acha kukurupika pembua kwanza. unataka form four wa kenya aje kufanya kaxi ya mtanzania?

Acha kutoa povu kwa mihemuko ....it is a fact kwamba vijana wetu hawandaliwi vizuri.Lakini kibaya zaidi hawajiongezi.Una kuta msomi mzima na degree yake hajasoma kitabu hata kimoja kwa muda wa miaka minne....kazi yake ni kusoma magazeti ya Shigongo na kushinda Instagram na FB......mtu kama huyo atapata wapi writing and communication skills?Watanzania hatuna culture ya kujisomea.Nakumbuka kipindi cha Zain University Challange tulikuwa tunapigwa sana bao na Wanafunzi wa Kenya na Uganda...tena kwa general knowledge questions tu...
There are several facts here:
1:Waajiri wakubwa siku hizi hapa nchini ni makampuni kutoka nje....either ni Barrick,Tigo,Airtel,TBL,ABSA,KPMG...au NGOs kama RTI,Cambridge Education,Room to Read etc...they don't take half-baked graduates!THAT IS A FACT!

2;Uvivu wa kujisomea utaliangamiza taifa....unakutana na graduate ambaeye hawezi kabisa ku-communicate...sasa atafanyaje kazi in a multicultural set-up?Infact hata hiyo kazi anaipataje in the first place?Maarifa mengi sana yamefichwa kwenye vitabu...and we don't read!

3.One of the most common Question in interviews siku hizi ni " Which book are you currently reading?" especially ukiingia kwenye interview yenye wazungu ktk panel.....why? labda wameshajua hatusomi kabisaa...

4;Tusitetee graduates wetu...dunia inakwenda kasi sana...lakini sisi tumelala tu!Katika dunia ya leo kuongea na kuandika Kiingereza vizuri sio option...ni lazima!Mpaka wafaransa ambao ni very proud na lugha yao wamebadilika.Baadhi ya vyuo vyao vikubwa sana Ufaransa, Thesis zinaandikwa kwa kiingereza.Sasa hivi tumekuja na sera ya mpya ya Elimu kutumia Kiswahili kuanzia std 1 MPAKA chuo kikuu...TUMEKWISHA!
 
Hayo ni makosa ya wachache,lakini usiseme watanzania hatuajiriki.kwani hii nchi imejengwa na wageni au hao hao watanzania?sasa watanzania ndo wameshaamua kuwa lazima kuwe na sheria ya ajira itakayozingatia wazawa kwanza,mtu ambae hawezi aondoke Tanzania hatumtaki.
 
Kusema haujafundishwa kuandika barua/kuomba kazi huu ni uzembe wa hali ya juu kwa mtu mzima, hili sio swala gumu kihivyo kama physics au medicine.
Ukiingia Youtube uka search kidogo CV writing/job application/cover letter etc na ukaangalia video 1-2 hours unapata picha kamili ya ni nini waajiri wanategemea katika application yako.

Pamoja na hayo lazima kuwe na ulinzi wa ajira kwa ajili ya Watanzania hili lipo karibia kila nchi hauwezi kuzuka tu Marekani/Canada/Australia ukapewa kazi bila kupitia processes ndefu sana ambazo zinahakikisha hakuna raia anayeweza kuifanya hiyo kazi hata kama uko qualified.

Hata kama Watanzania ni wabovu kuliko watu wa nje (Sijui kama ni kweli) inabidi tuburuzane tu hivyo hivyo.
 
Kiukweli graduates wengi sana hamna kitu, kiingereza ndo kabisa hakipandi na pia licha ya yote hayo watu hawataki kuomba msaada mtu anaandika carrier badala ya career nigger are you serious..mimi wakati na graduate kuna mshikaji wangu flani nakiri yuko vizuri na pia updated anajua vitu vingi nikamuomba ebana eeh hivi cover letter unaandikaje akanipa sample yake yangu mimi ilikua ya kimagumashi vibaya basi kuunganisha na yangu Mungu mkubwa kijana nikatokelezea, nimefika ofisini kuna mshikaji alikua anapenda kuomba kazi anajua kutengeneza CV hatari nikamuomba anitengenezee yangu sasa hivi iko full vibaya mno, kama hauwezi kitu omba msaada usione aibu...kama haujui kitu omba ufundishwe....
 
Kama discussion vyuoni zinafanyika kwa kiswahili hicho kingereza mtu atakifanyia mazoezi muda gani,mambo mengine tusilaumu vyuo ni issue ya wewe kama wewe kujifunza.Mimi binafsi mambo mengi na ya muhimu katika kazi na maisha nimejifunza nje ya maisha yangu ya chuo,tatizo hatuna utaratibu wa kujisomea mbona kuna resources na vitabu vingi kwa kila kitu unachohitaji?
Sometimes tunalalamika kwamba hakuna kazi kumbe kazi zipo ila hatuna vigezo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom