Wahenga tukumbushane Klorokwini na mambo yake

Dawa ili nifanya mpaka leo naogopa kunywa dawa .Na kupenda kuchokwa sindano hadi leo hii
 
kuna mzee mmoja alikuwa fundi maji wa DAWASA ya Enzi hizo maeneo ya Kibaha alikuwa anakunywa vile vidonge kwa kumung'unya kama pipi. Alikuwa akija kutengeneza maji anaomba kama mna akiba ya chrolokwini anajisikia malaria ukimpa anakula kama pipi. Yeye alikuwa teja kabisa wa zile dawa akizikosa hafanyi hata kazi
Duh huyo mtu kama yupo mwambie aagize kinywaji chochote nitalipa. Nimemvulia kofia
 
'Kolokwini' ile dawa ina nguvu za ajabu, yaani ikikaribia kugusa ulimi tu ina uwezo wa kukivuta nje chakula chote ulichokula. Dawa chungu kama imetengenezwa na mashetani, halafu bahati mbaya iwe inakuonea, yaani ukinywa ni full kuwashwa kwa muda siku tatu mfululizo bila kupumzika, halafu muwasho wake ni hadi kwenye kinyeo na makende. Ukianza kuwashwa hujitokezi mbele za watu, maana kuna maeneo utashindwa kujikuna. Ukigusa maji hata tone tu kuwasha kunaongezeka mara tatu zaidi.
Hizi dawa zilikuwa zinanionea kwenye kuniwasha,sitakagi hata kukumbuka.Usiku mmoja kulikuwa na mvua usiku mm nawashwa,mtu pekee aliyekuwa akinifariji ni marehemu mama lkn nayeye alifika wakati akachochoka akalala,sitasahau usiku ule ,ilikuwa mrefu ka mwezi mzima vile.Mwishoni hapa ndo tuligundua unameza piriton nusu saa kabla hujazimeza hapo huwashwi.Cloroquen ww Mungu anakuona.
 
Hiyo dawa hafai dadeki sitasahau, ilitaka kumtoa mama yangu uhai hiyo sio dawa ni poison wallah
 
Niliwahi ku-over dose, nilwashwa na jasho adi godoro lililowa. Usiku ulikuwa mrefu asubuhi nilipewa maziwa nikatapika ndio nzima. Kilichofata drip za kutosha
 
Hizi dawa zilikuwa zinanionea kwenye kuniwasha,sitakagi hata kukumbuka.Usiku mmoja kulikuwa na mvua usiku mm nawashwa,mtu pekee aliyekuwa akinifariji ni marehemu mama lkn nayeye alifika wakati akachochoka akalala,sitasahau usiku ule ,ilikuwa mrefu ka mwezi mzima vile.Mwishoni hapa ndo tuligundua unameza piriton nusu saa kabla hujazimeza hapo huwashwi.Cloroquen ww Mungu anakuona.
Zimenitesa sana hizi kitu. Zilikua zinanifanya kama njuka wake...
 
Back
Top Bottom