Mtaka yote
Senior Member
- Nov 30, 2014
- 136
- 103
- Thread starter
- #61
Wewe ndo utumbo tena wa bata aliyemeza konokono
Kwa nin?
Wewe ndo utumbo tena wa bata aliyemeza konokono
uliza la kwako
unategemea nini wakati kila mhariri naskia alipewa Laki Tatu NA wengine walisafirishwa NA Ndiege ! Si ndio maana walimpigia makofi! Tangu nizaliwe hii ndiyo mara ya kwanza kuiona hata Mwalimu alipokuwa anaita press conference pale Msasani walikuwa wanaenda ma chief reporters au senior journalists lakini these days editors wana chase stories na waandishi basi ni Ngumu kutofautisha editor ni nani na Mwandishi ni nani. Wahariri tujirekebishe! Hivi na Makaidi na Mtikila akiwaita mtaandika kama mlivyofanya kwa mzee LeigwananiHaya ndiyo maswali ambayo wahariri wetu walimuuliza Lowassa jana mjini Dodoma.
1.Mara nyingi nimekuwa nikisikia watu wanakuita Edward,na wewe unawanyamazia tu,huoni ni kama vile hawakupi heshima?
2.Huko mtaani kuna maneno mengi sana yanasemwa juu yako,mengi ya kukuchafua na mengine ya hovyohovyo,kwa nini umekaa kimya?
3.Kwa kipindi cha miezi kumi na mbili ,wewe na wenzako mlikuwa kifungoni,juzi chama chako kilitangaza kuwa adhabu yenu imekwisha,hebu tueleze nini sababu kuingia kifungo hicho?
4.Suala la afya yako limekuwa ni ajenda kubwa huko mtaani,leo tuko hapa,hebu tueleze kama inavyosemwa ni tofauti.
5.Nataka kujua chanzo cha wewe kutoka serikalini,ilikuwa ni nini?hivi ni kweli ulihusika kwenye sakata la Richmond au lilikuwa zengwe la
kisiasa?
6.Umewahi kunukuliwa mara nyingi ukisisitiza kuhusu elimu kwanza,tofauti na kauli mbiu ya serikali yan kilimom kwanza,huoni kama unapingana na mipango ya serikali?
7.Umekuwa ukilitazama tatizo la ukosefu wa ajira kama bomu linalosubiri kuripuka,pili umekuwa ukiitwa majina mabaya mara mwizi mara fisadi,lakini sasa hali ni tofauti,naona kama vile nyota yako inang'aa,siri ya jambo hili ni nini?.
8.Huko nyuma wewe na raisi Kikwete mliitwa Boys ii men,na wakati mwingine ulisema wewe na JK hamjakutana barabarani,hebu tueleze urafiki wenu ukoje?
9.Ipo dhana wewe kuwa ni tajiri sana na umejirimbikizia mali na wengine wanasema hilo linaweza kuwa kikwazo katika safari yako ya matumaini,nataka kujua chanzo cha utajiri wako.
10.Nini mtazamo wako kuhusu serikali ijayo,unafikiri serikali ya awamu ya tano inatakiwa ijielekeze kwenye ipaumbele gani?pili katika suala la uchumi unalitazama vipi suala la dola kuporomoka,pia unatoa tahadhari gani kwa ccm katika kuelekea uchaguzi mkuu?
11.Katika mchakato huu wa uraisi,ikiwa hutateuliwa na chama chako,nini plan B yako?
12.Ipo dhana kuwa wewe ni mtu wa visasi na inasemwa kuwa ukiingia madarakani utalipiza visasi kwa wabaya wako,unalizungumziaje hili?
13.Mtandao ulionao hauna tofauti na ule uliomuingiza Kikwete madarakani,seikali ya awamu ya tano itakuwa na tofauti gani na serikali ya
awamu ya nne?
My take,
Maswali ya kitoto sana,kuna mawili tu ambayo angalau yanahadhi ya mwanahabari aliyeiva.
Mengne utumbo tu
Weka hayo maini yako tuyaone siyo unaishia kupakazia tu?
Halafu weka na chanzo cha hayo maswali uliyoandika isije ngonjera Tu.
Hivi Kibanda alishapotea eeee? Maswali ya kijinga kabisa yaani hata hayahitaji mtu kufikiri. Hizi shule hizi, taabu tupu tunaenda kutafuta sijui nini shuleni. Maswali gani hayo hata mtoto wa chekechea mengine anajua majibu yake?