Wahalifu siyo wa kucheka nao, hiki ndicho walichofanya El Salvador

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,239
12,756
El Salvador ni nchi ndogo ya Amerika ya Kati. Ina watu kama milioni saba hivi. Lakini ni nchi ambayo ilikuwa imeandamwa vibaya sana na magenge ya uhalifu na mauaji. Ilikuwa ni moja ya nchi zinazoongoza duniani kwa mauji. Kati ya watu laki moja watu 53 waliuwawa kwa mwaka(Nchi kama Tanzania ni watu kama 5 wanauwawa kwa kila watu laki moja).

Mwaka 2019 El Salvador walimchagua Nayib Bukele mwenye miaka 37 kuwa Rais wao. Moja ya ahadi yake kubwa ilikuwa ni kupambana na uhalifu. Baada ya kuingia madarakani akajenga gereza kubwa la kuchukua wafungwa kama 60,000. Ikaanza kamata kamata ya wote wenye tatuu za magenge na wote waliotiliwa shaka ya uhalifu. Na sheria zikabadilishwa ili aweze kuwashikilia na kuwashtaki kirahisi. Mpaka sasa inadaiwa kuwa zaidi ya watu 73,000 wamekamatwa na gereza lile kubwa lina watu 40,000 mpaka sasa.

Matokeo yake ni El Salvador kutoka kuwa moja ya nchi hatari duniani hadi kuwa nchi salama zaidi katika Latin Amerika. Vifo kutokana na mauaji kati ya watu 100,000 vilitoka 53 hadi 2.4! Leo watu wengi wanashangilia hilo. Bahati mbaya au nzuri vyombo vya haki za binadamu vimeanza kupiga kelele kuwa anashikilia watu kinyume na sheria!!

Wahalifu gerezani humo.

1704882592802.jpeg
 
El Salvador ni nchi ndogo ya Amerika ya Kati. Ina watu kama milioni saba hivi. Lakini ni nchi ambayo ilikuwa imeandamwa vibaya sana na magenge ya uhalifu na mauaji. Ilikuwa ni moja ya nchi zinazoongoza duniani kwa mauji. Kati ya watu laki moja watu 53 waliuwawa kwa mwaka(Nchi kama Tanzania ni watu kama 5 wanauwawa kwa kila watu laki moja).
Njia bora ya kupambana na uhalifu ni raia kupata fursa za masomo bora, biashara nzuri , huduma bora za jamii, ukosefu wa rushwa na ushiriki wa raia katika siasa. Njia nyingine zozote ni shotikati ambazo hazidumu muda mrefu.
 
Njia bora ya kupambana na uhalifu ni raia kupata fursa za masomo bora, biashara nzuri , ukosefu wa rushwa na ushiriki wa raia katika siasa. Njia nyingine zozote ni shotikati ambazo hazidumu muda mrefu.
Mkuu, unachosema ni sawa, ila sio sahihi kwa 100%, huwez wapa hizo fursa hao watu waliokubuhu, inabidi usafishe kwanza hao watu ili uanze upya na kizazi fresh, yan watu wateseke kusoma kisa kuna madarasa wakati anajua anaweza pita kwenye magenge ya uhalifu akaiba mali akawa tajiri ndani ya mwezi mmoja, na hakuna kitu atafanywa ? Dawa ni hio, kamata hao wapuuzi wote, piga vya kutosha ili wengine wajue uhalifu sio njia ya maisha, kisha endelea kutoa elimu na mazingira bora ya biashara ili kutoleta wimbi la pili la uhalifu,

Huyo raisi yuko sawaaa
 
Njia bora ya kupambana na uhalifu ni raia kupata fursa za masomo bora, biashara nzuri , ukosefu wa rushwa na ushiriki wa raia katika siasa. Njia nyingine zozote ni shotikati ambazo hazidumu muda mrefu.
Tanzania ina wasome wengi na ndiyo wanaoongoza kwa uhalifu....
 
Rais Bukele anachofanya ni unyama na wala si jambo la kukaa na kulisifia!
Na hasa yanayoendelea ndani ya gereza la Secot !
 
Njia bora ya kupambana na uhalifu ni raia kupata fursa za masomo bora, biashara nzuri , ukosefu wa rushwa na ushiriki wa raia katika siasa. Njia nyingine zozote ni shotikati ambazo hazidumu muda mrefu.
Si kweli mkuu. South Africa wana maisha mazuri kuliko sisi ila ndiyo vinara wa uhalisfu duniani. Brazil wanamaisha na fursa kuliko sisi ila ni vinara kwa uhalifu. Hata US kuna majiji ni hatari kuliko miji mingi ya Africa. Wahalifu wengi ni watu wenye hulka za ki anti social, kisociopath na kipsychopath. Wakiona mamlaka ni legelege hamna picha wataacha kuwaonyesha.
 
Msiisahau Haiti. Ambao wameomba msaada wa polisi milioni toka umoja wa mataifa, na Kenya inapeleka laki moja ili kukabiliana na wahalifu.
Waliachiwa achiwa mwishowe wahalifu wamechukua nchi. Mexico nayo inalea macartels, mwisho watachukua nchi. Wahalifu si wa kuwachekea hata kidogo.
 
Back
Top Bottom