Wahadhiri UDSM Waongelea tatizo la Udini

Wahadhiri UDSM Waongelea tatizo la Udini

hii inamaanisha umefanya utafiti na kugundua sehemu zenye waislam wengi hazina skuli za kutosha, je, ulitafiti kwanini maeneo hayo hayana skuli za kutosha? (kipi kilisababisha hayo maeneo yakose skuli?) hapo kwenye uwiano, ni pagumu zaidi ya ufikiriavyo sababu mwisho wake tutaleta udini wa pili (udini wa kwanza ni kipindi hiki ), just imagine zinatakiwa nafasi 8 za watumishi na ktk hao nane mmewafanyia usaili watu 100 na ktk hao 100 hamsini ni wakristo and the rest are muslims. Kama wakristo wawili tu kati ya 50 wamefanya vizuri na waislam zaidi ya 8 wamefanya vizuri zaidi ya wale wakristo wawili,je, mtaenda kuwachukua wakristo wengine wawili ktk kundi la waliofanya vibaya usaili na kuwapunguza waislam wanne waliofanya vizuri ili kupata idadi ya waislam wa4 na wakristo wa4 ili kubalance? hapa pia nakubaliana nawewe ila kuhusu kuitwa vilaza, kumbuka kwenye msafara wa mamba kenge wamo,kuna wakristo jina tu, japo haya matusi dini zote mbili haziepuki dhambi hii,kama unataka kuhakiki fungua mitandao ya kizanzibar jinsi wakristo wanavyotukanwahapo nitaongea mtazamo wangu,mimi ukiniambia yesu sio Mungu sipungukiwi kitu,hata ukisema hakuwahi tokea mtu hapa duniani aitwaye Yesu napo haitani-affect sababu nafuata biblia inanifundisha nini, ila akiongea mkristo mwenzangu hayo maneno nitakaa naye ili tuelimishane (sio nimuelimishe, bali tuelimishane) tuko pamoja ktk hili nataka ingekuwa hivi, mikataba ya serikali na taasisi za kidini iwe WAZI isifanywe siri sawa kabisahaya ni maajabu kwangu kwa serikali kuwaundia waislam chombo huku ikisema haina dini hapo katiba itakuwa inavunjwa,kila mtu ana uhuru wa kuwa muumini wa dini aitakayo, je, ikiwakataza hao watu itawalipa? Labda katiba iseme hvyo ila ni vigumu sana
Nawasilisha

asante![/QUOTE]

Nikianza na hoja yangu ya kwanza,asababu ya maeneo yenye waislamu wengi kuto kuwa na shule za kutosha,na shule zilizopo hazina walimu ni nyingi;
1.Mkoloni alikuwa mkristo hakujenga shule maeneo ya waislamu,maeneo haya waislamu walijikitika katika elimu ya dini.Kumbuka muarabu aliwafundisha watu kiarabu na kuandika lugha ya kiarabu kwa kutumia herufi za kirumi,hivyo kabla ya mjerumani waislamu ndio walikuwa wasomi katka nchi hii.Alipokuja Mjerumani akasema watu wote waliokuwa wanajua kusoma na kuandika kiarabu hawajuai kusoma na kuandika,dunia ikabadilika kama vile kutoka mfumo wa analojia kwenda digitali.

2.Baada ya uhuru serikali haikuchukua hatua zozte kuhakikisha maeneo haya yanakuwa na shule za kutosha na walimu wa kutosha ili kubalance gap lililokuwepo kabla ya uhuru,kwa hiyo maeneo haya yakaendelea kubaki nyuma kielimu na kimaendeleo.

3.Serikali haikujenga miundombinu yya maana kwenye maeneo yenye waislamu wengi,hivyo wafanyakazi wengi wakiwemo walimu waliopelekwa huko walikimbia,pia iliwanyima wenyeji wa huko fursa ya maendeleo,uwezi kulima nyanya mtwara kisha uisafirishe mpaka Dar

4.Kwa kuwa makazi wa maeneo haya walikosa elimu na barabara basi pia umasikini ulitamalaki katika jamii yao hivyo wasingeweza kuwapeleka watoto wao kwenye shule nzuri wala kujenga shule.

5.Mtu akikosa elimu hajui thamani ya elimu,hivyo serikali ilipaswa kupeleka nguvu zake huko ili watu waende shule.

Katika hoja yangu namba tatu na kumi,tukitaka kujenga taifa lililoimara,hasa katika nchi kama hii ambayo idadi ya waislamu na wakristo inalingana au kuzidiana kidogo tu,lazima tufanye mambo ambayo tunaona hayawezekani yawe yanawezekana.Nasema hili linawezekana tukihamua labda wanaofaidika na mfumo kristo walipinge.

Katika hoja yangu namba saba,nasema serikali ijitoe kabisa kusaidia taasisi za dini kwa fedha na wafanyakazi,hakuna cha mkataba wala nini,hizo taasisi zijiendeshe kwa pesa za sadaka za waumini,kama hawawezi wafunge taasisi zao na serikali iwahudumie wananchi wake ndio jukumu lake,hili sio jukumu la misikiti na makanisa.
 
kwahiyo wewe umesoma sana sio?.
Hebu tuwekee maendeleo yako hapa tufanye analysis.

Issue sio ''kusoma sana'' kama unavyotaka kuniwekea maneno mdomoni (hakuna mahali nimesema nimesoma sana ila kama uliota). Issue ni kusoma na kufanya kazi kwa bidii.
 
Mwaka 1996 wakati namaliza shule ya msingi,wilaya ya kilwa mkoani Lindi ilikuwa na shule ya sekondari ya serikali moja yenye walimu wawili wakati wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro ilikuwa na shule za sekondari za serikali zenye walimu wa kutosha 17(kumi na saba).Wakati huo wanafunzi tuliokuwa tunatoka mikioa ya kusini kwenda kusoma shule za bweni katika mikao mingine ilikuwa inatuchukua mwezi na zaidi ili tufike Dar wakati wa masika.


Baba wa kanisa Nyerere aling'oa reli Mtwara na akapiga marufuku kilimo cha pamba kanda ya kusini.Mataa ya uwanjwa wa ndege Mtwara yalihamishiwa Arusha,jenereta ya umeme ya kisasa ya mtwara ilihamishiwa Bukoba


Viwanda na mashamba ya mmonge Tanga Nyerer aliyaua kupitia vibaraka wake wa mfumo kristo.


Tabora ilikuwa kitivu cha harakati za uhuru,baada ya uhuru Nyerere akaiua Tabora kupitia vibaraka wake wa mfumi kristo


Shule zilizopo mkoa wa Pwani zimejazwa Wakristo kutoka mikoa ya Bara.


Serikali ya mfumo kristo tokea uhuru imefanya juhudi gani kuondoa upogo huu wa mgawanyo wa maendeleo katkia nchi hii,ndio kwanza maendeleo yanaelekezwa mikoa ya wikristo wengi na mikoa ya waislamu wengi inaachwa na kuambiwa ni wavivu wakati hawana miundombinu yoyote katika mikoa yao.


Naomba nipe mfano mmoja tu wa mkoa wenye waislamu wengi ulioendelea?Ni juhudu za mfumo kristo ulioasisiwa na Baba wa Kanisa Nyerere.


Tupigie Jicho upande wa Pili,mtoto aliyezaliwa katika familia ambayo ilisomeshwa na mfumo kristo kabla na baada ya uhuru,katika familia yao kuna watu wenye Phd zaidi ya watatu,madaktari,walimu,wahasibu,na watu wa fani mbali mbali,na mtoto aliyezaliwa katika familia iliyopigwa teke na mfumo kristo,familia ambayo,mama aliuza vitumbua,baba anetembeza njegere,mjomba anauza dagaa,je ni mtoto gani ambaye serikali inapasa ifanye juhudi kuhakikisha anasoma.


Niliongoza kimasomo kuanzia darasa la kwanza mpaka form two mama yangu akakosa shilingi 40000 ya ada ya shule,mama akalia sana,nikaenda wilayani kwetu na ripoti zangu,na kabla ya hapo wanajua nilipokuwa shule ya msingi nilikuwa naongoza mitihani yote ya wilaya,huko nikakutana na mawakala wa mfumo kristo walinitukana na kunikejeli kwa sababu ya dini yangu.Nilishindwa kurudi shule mpaka form four mwezi wa sita ndio nikarudi shule,yaani nilikaa mwaka mmoja na nusa nyumbani bila ya kusoma,nikafanya mtihani wa form four nikapata division one point 17.


Jamani tuache porojo tuondoe mfumo kristo kwa ustawi wa taifa letu,namkumbuka second master wangu aliyekuwa wakala wa mfumo kristo alivyotutukana mimi na mama yangu kipindi kile aliponipeka shuleni form four tena tukiwa na barua ya wizara inayoelezea matatizo yangu.
NGUVUKAZI
Hongera sana ila punguza jazba na visasi havitakufikisha popote. Ktk hili la udini hakuna mshindi. Nilitegemea hizo pointi 17 ulizodai kupata kama ni kweli zingekusaidia kupata fikra sahihi za kuleta mshikamano miongoni mwa watz. Shule haikusadii kitu kwa chuki zako.....
 
Last edited by a moderator:

1.Mkoloni alikuwa mkristo hakujenga shule maeneo ya waislamu,maeneo haya waislamu walijikitika katika elimu ya dini.Kumbuka muarabu aliwafundisha watu kiarabu na kuandika lugha ya kiarabu kwa kutumia herufi za kirumi,hivyo kabla ya mjerumani waislamu ndio walikuwa wasomi katka nchi hii.Alipokuja Mjerumani akasema watu wote waliokuwa wanajua kusoma na kuandika kiarabu hawajuai kusoma na kuandika,dunia ikabadilika kama vile kutoka mfumo wa analojia kwenda digitali
[/QUOTE]
hakika huu ndio msingi wa yote, mkuu unajua kujenga hoja ila mwanzoni ulitawaliwa na hasira kiasi kwamba ilikuwa ni ngumu kuamini zimetoka kwa mtu msomi..umeeleweka vizuri sana.
 
Kwanza kabisa serikali ijenge shule za maana na kupeleka walimu wa kutosha pamoja na vifaa vya kufundishia katika maeneo yenye waislamu wengi.

Pili serikali iboreshe miundombinu kwenye haya maeneo yenye waislamu wengi ili wafanyakazi wanaopelekwa huko wasikimbie kwasababu ya maisha magumu.

Tatu,katika taasisi muhimu zote za serikali na serikali kuu yenyewe kuwa na uwiano sawa wa watendaji ili kuavoid bias kama ile ya kuandaa ratiba ya mitihani ya taifa ya Clinical bila ya kuzingatia sikukuu ya idd,tatizo pale mafunzo wizarani wapo wakristo watupu,nani atakumbuka IDD.

Nne,wakristo wakubali kwamba waislamu wameachwa nyuma kielimu kwasababu za kihistoria,hivyo hivi sasa wan haki ya kusaidia ila at least waweze kulingana na wao,badala ya kutoa maneno ya kejeli,dharau na jeuri kwamba waislamu vilaza,watu wa madrasa,haya maneno hayatatusaidia na badala yake yatatuletea vita.

Tano,Kuvumiliana katika dini baina ya waislamu na wakristo,wewe kama unaamini yesu ni mungu mimi naamini yesu sio mungu,wala sikukashifu,kama unaona ninakashifu imani yako kwa kusema kwangu yesu sio mungu nawe unaikashifu Imani yangu kwa kusema kwako yesu ni mungu,tuvumiliane katika Imani zetu na matendo yetu ya kiimani.

Sita,viongozi wa dini watumie hekima,busara na hoja katika kuwalingania watu katika dini zao badala ya kutumia matusi,kejeli na dharau kuwalingania watu katika dini zao.

Saba,serikali ijitoae kuchangia pesa au wafanyakazi katika taasisi zote za kidini,taasisi za kidini zijeendeshe zenyewe kwa asilimia mia moja.

Nane,serikali hirudishe mali za taasisi zote za kidini ilizozitaifasha,na ijenge shule na mahospitali yake.

Tisa,serikali hisiwalamizimishe waislamu kuwa BAKWATA ndio chombo chao ch maamuzi,ikiwezekana BAKWATA ivunje kabisa na kuundwa chombo cha kitaifa kwa kuwahusisha waislamu wate.

Kumi,mali zote za waislmu zilizouzwa na BAKWATA,serikali hizirudishe kwa waislamu wenyewe,ikiwemo kiwanjwa cha markazi palipotakwa kujengwa chuo kiukuu cha kiislamu.

Kumi na moja,watu wote wenye vyeo vya Shekhe,Ustadhi,maalimu,padri,askofu,mchungaji,poroko,wasiwe viongozo wa serikali na taasisi zake,ikiwezekana wasifanye kazi kabisa katlka serikali na taasisi zake,waendeshe taasisi zao za kidini.

Nawasilisha


Moja hilo la kujenga shule limeanza zipo za kata na kuna haja ya kuongeza juhudi za makusudi kuziboresha. Kuna tofauti ya equity na equality kaka. Hata wagonjwa huwa hawalingani kuna wengine haina haraka kumfanyia operation na wengine ni emergency ila mwisho wa siku wote watibiwe..
Pli- wakazi wa haya maeneo nao wabadilike wapende elimu na wakae vizuri na wafanyakazi wanaopelkwa huko, waache ushirikina, tabia za kurudishan nyuma kimaendeleo.
tattu nakuunga mkono asilimia 100%
Nne hayo maneneo atakayekuwa anayatoa atakuwa sio mstaarabu. Heshima hujengwa pande mbili unaheshimu na kuhemiwa. Shule nyingi za kiikristo na kiislam hazibagui dini hili napendekeza liendelezwe na linondosha sana chuki na ujinga dhidi ya dini nyingine kama shule ikiwa ni ya dini moja tuu.
Tano, kama unaamini kwamba yesu sio mungu why uniambie hali ya kuwa unajua utaniuthi kama si uchokozi wa makusudi. Hizi dini mbili zinafanana sana maan uislam unaamini Issa ibin Mariam atarudi siku ya kiama, unaamini vitbu vya torati, injili na quraan. Ukiisoma biblia utagundua Issa Ibin Mariam ni Yesu, na utavikuta hivyo vitabu, na Mwarabu na myahudi historikali ni ndugu. Mbona sioni chuki kuu na ugomvi kati ya waislam na budha.
Sita - hili lipo sana upande wako kiongozi likemee.
Saba- Inawezekana lakini serikali inauwezo wa kujenga vyuo na taasisi za kutosha peke yake bila msaada wa taasisi za kidini na watu binafsi?
Nane- wasiwasi wangu mbona naona waislam watendelea kuumia. Coz hizo taasisi zina uwezo wa kifedha na washajiandaa muda mrefu kwa hilo, ndio maana wana wafadhili na wana miradi mingine ya kujingiza fedha.
Tisa- KAZI KWENU. Hivi tec na mabaraza mbalimbali ya wakristo yaliundwa kwa msaada wa serikali?!
Kumi- naona lipo kisheria zaidi, na nasikia mali hizi nyingi ziliuzwa na mahekh na kununuliwa na waislam. NADHANI HAPO MFUMO KRISTO UNAHUSIKA SANAA. MAADUI WA WAISLAM NI WAISLAM WENYEWE. Nakumbuka kuna msikiti mmoja ulikuwa ukijenjwa dodoma kwa msaada wa Ghadaf, pale palikuwa na malalamiko kibao kwamba meshekh walihujumu ile fedha hadi ikabidi atume mtu wake wa karibu kuusimamia. Malalamiko ya aina yako mengi sanaa lakini badala yeke mnahamisha chuki kwenda kwa wakristo.

TUTAIJENGA TANZANIA PAMOJA
 
wakimaliza hilo wazungumzie pia reasons za poor performance za wanafunzi wao wengi na Tz kiujumla
 
NGUVUKAZI
Hongera sana ila punguza jazba na visasi havitakufikisha popote. Ktk hili la udini hakuna mshindi. Nilitegemea hizo pointi 17 ulizodai kupata kama ni kweli zingekusaidia kupata fikra sahihi za kuleta mshikamano miongoni mwa watz. Shule haikusadii kitu kwa chuki zako.....

Asante.
Lakini nikukumbushe tu kwamba sikuweka matokeo yangu hapa hili munisifie,nimeweka matokea yangu hapa hli kuonesha namna gani vijana wakiislamu tunavyosumbuliwa na mfumo kristo,maana wale mawakala wa mfumo kristo kule wilayani kwangu pamoja na kujua niliongoza mtihani wa darasa la saba kiwilaya,na kwenda na report zaform one na form two nikiwa nimekuwa wa kwanza,lakini wale jamaa waliishia kunikejeli na kunidharau kwasababu ya dini yangu.

Na yule second master naye alifanya hivyo hivyo.

Kwa hakika watu hawa walitaka niwe muuza dagaa pale feli kama mama yangu kisha waesma waislamu hawataki kusoma ni vilaza,acha niuchukie mfumo kristo maana ni hatri sana kwa taifa hili.Asante Mungu,asante mama kwa kunifikisha hapa nilipo,maana mama pamoja na ufukura wake wote lakini alijua mwanae nina kipawa lazima nisome ndio maana alinirudisha shule baada ya kukaa nyumbani mwaka na nusu.
 
Kwa maelezo yako basi pendekezo la nini kifanyike namba 4 lirekebishwe na kuongeza Serkali iwachunguze na viongozi wa Serkali ambao wanachochea udini waziwazi au kwa kificho - na au hata kwa kutofanya chochote kuzuia gonjwa hili. tatizo ni nani katika Serkali atafanya hii kazi?

mimi nadhani tatizo lipo kwa uongozi uliopo madarakani leo. kwanini tofauti hizi zote hazikuwahi kujitokeza katika awamu zingine.mimi nadhani ninaulaumu uongozi wa sasa na hata kama haya yatakuja kudevelop na kutupelekea kuwa kama Rwanda(Mungu aepushilie mbali) and if i will manage to survive washtakiwa wangu namba moja watakuwa ni uongozi uliopo madarakani leo. sababu najiuliza usalama wa taifa siku hizi upo wapi?? unafanya nini?? mashushu wako wapi na wanafanya nini? majeshi yetu vipi? serikali na mihimili yake wanafanya nini? by the way mimi ninaona hawa ndiyo wachochezi wa vuguvugu hili la kidini namba moja. sijawahi kuwa na wasiwasi na maisha yangu na familia yangu kama wakti huu, ninajua tunavyoendelea hivi kwa sasa isipopatikana suluhu ya ukweli isiyo ya kinafiki mdomoni itakuja kulipuka tu nooo way.hawa wachochezi wetu hawatakuwepo na familia zao, watakuwa wanaangalia kwenye screen tu na kusikiliza kwenye redio. mimi with a certain time to come nafikiria niikimbie hii nchi na familia yangu.haitakalika unless watu fulani muhimu watakapokuwa sincere kulisimamia hili kwa ukweli.

imetokea sehemu napokuwaga inanikutanisha na watu tofauti tofauti, yaani kwa yale ninayoyasikia sasa yakitoka mioyoni mwa watu ninaona ile mbegu iliyopandwa imeshaota mizizi na sasa inachepua, inahitaji mvua moja kubwa kuufanya huu mmea uonekane vizuri.

kwa imani yangu (natambua kila mtu ana imani yake na jinsi wanavyofanya)huwa kabla hatuchagua viongozi katika uchaguzi huwa tunafanya maombi kwa muda mrefu tu before, na nia ni kuwa tunamwomba Mungu atuelekeze mtu sahihi wa kumchagua. we even fast for that issue. wakati tunafanya maombi haya before sana uchaguzi wa 2005 God answered to one of the person and he said to him ni nani hasa watakaokuwa viongozi for that time, na hakuishia hapo tu alionyesha ni kwa jinsi gani kipindi hichi cha uongozi kitakavyokuwa. alisema katika kipindi cha kwanza vitu vingekuwa hivi na hivi, and then the next period things will be more like this and this.anyway at the time sikuwa na haja ya kucomment sababu yawezekana haikuwa ni Mungu ni hisia zake tu, and niliacha hivyohivyo. lakini kwa ukweli nilipiga kura na kumchagua ambaye niliona angefaa.l thank God amenipa uhai hata sasa ambapo ninakumbuka maono ya yule mtu mwaka 2005 katikati, ambapo nimeona kila alilolisema limekuwa kama alivyosema, nimeogopa coz yule aliyeona na kusema hakuishia hapo alitoa na solution to do.so kwa upande wangu ninaona watanzania tunakoelekea si kuzuri.heri hawa waadhiri wanaojikosha leo na matamko yao mazuri sababu wanaweza kuokoka na tribunals.lakini ukweli nadhani unabaki palepale ni viongozi wetu walioko madarakani ambao wanaweza kukomesha hili na sisi vikundi kwa vikundi, imani tofauti hatutakuwa na jinsi zaidi ya kufuata yale wenye meno wametaka.
 
1.Mkoloni alikuwa mkristo hakujenga shule maeneo ya waislamu,maeneo haya waislamu walijikitika katika elimu ya dini.Kumbuka muarabu aliwafundisha watu kiarabu na kuandika lugha ya kiarabu kwa kutumia herufi za kirumi,hivyo kabla ya mjerumani waislamu ndio walikuwa wasomi katka nchi hii.Alipokuja Mjerumani akasema watu wote waliokuwa wanajua kusoma na kuandika kiarabu hawajuai kusoma na kuandika,dunia ikabadilika kama vile kutoka mfumo wa analojia kwenda digitali
hakika huu ndio msingi wa yote, mkuu unajua kujenga hoja ila mwanzoni ulitawaliwa na hasira kiasi kwamba ilikuwa ni ngumu kuamini zimetoka kwa mtu msomi..umeeleweka vizuri sana.[/QUOTE]

Ni kweli msingi wa yote ulikwa hapo ndio hata mababu zetu waligundua hilo ndio maana >95% ya walikuwa mbele katika harakati za kudai uhuru wa nchi hii,so baada ya uhuru serikali ya Nyerere ilibidi ichukue hatua kuondoa upogo huu,lakini badala yake Nyerere akaja na mfumo kristo,soma vitabu vilivyoandikwa na Maaskofu na Mapadri wa kikatoliki
 
mimi nadhani tatizo lipo kwa uongozi uliopo madarakani leo. kwanini tofauti hizi zote hazikuwahi kujitokeza katika awamu zingine.mimi nadhani ninaulaumu uongozi wa sasa na hata kama haya yatakuja kudevelop na kutupelekea kuwa kama Rwanda(Mungu aepushilie mbali) and if i will manage to survive washtakiwa wangu namba moja watakuwa ni uongozi uliopo madarakani leo. sababu najiuliza usalama wa taifa siku hizi upo wapi?? unafanya nini?? mashushu wako wapi na wanafanya nini? majeshi yetu vipi? serikali na mihimili yake wanafanya nini? by the way mimi ninaona hawa ndiyo wachochezi wa vuguvugu hili la kidini namba moja. sijawahi kuwa na wasiwasi na maisha yangu na familia yangu kama wakti huu, ninajua tunavyoendelea hivi kwa sasa isipopatikana suluhu ya ukweli isiyo ya kinafiki mdomoni itakuja kulipuka tu nooo way.hawa wachochezi wetu hawatakuwepo na familia zao, watakuwa wanaangalia kwenye screen tu na kusikiliza kwenye redio. mimi with a certain time to come nafikiria niikimbie hii nchi na familia yangu.haitakalika unless watu fulani muhimu watakapokuwa sincere kulisimamia hili kwa ukweli.

imetokea sehemu napokuwaga inanikutanisha na watu tofauti tofauti, yaani kwa yale ninayoyasikia sasa yakitoka mioyoni mwa watu ninaona ile mbegu iliyopandwa imeshaota mizizi na sasa inachepua, inahitaji mvua moja kubwa kuufanya huu mmea uonekane vizuri.

kwa imani yangu (natambua kila mtu ana imani yake na jinsi wanavyofanya)huwa kabla hatuchagua viongozi katika uchaguzi huwa tunafanya maombi kwa muda mrefu tu before, na nia ni kuwa tunamwomba Mungu atuelekeze mtu sahihi wa kumchagua. we even fast for that issue. wakati tunafanya maombi haya before sana uchaguzi wa 2005 God answered to one of the person and he said to him ni nani hasa watakaokuwa viongozi for that time, na hakuishia hapo tu alionyesha ni kwa jinsi gani kipindi hichi cha uongozi kitakavyokuwa. alisema katika kipindi cha kwanza vitu vingekuwa hivi na hivi, and then the next period things will be more like this and this.anyway at the time sikuwa na haja ya kucomment sababu yawezekana haikuwa ni Mungu ni hisia zake tu, and niliacha hivyohivyo. lakini kwa ukweli nilipiga kura na kumchagua ambaye niliona angefaa.l thank God amenipa uhai hata sasa ambapo ninakumbuka maono ya yule mtu mwaka 2005 katikati, ambapo nimeona kila alilolisema limekuwa kama alivyosema, nimeogopa coz yule aliyeona na kusema hakuishia hapo alitoa na solution to do.so kwa upande wangu ninaona watanzania tunakoelekea si kuzuri.heri hawa waadhiri wanaojikosha leo na matamko yao mazuri sababu wanaweza kuokoka na tribunals.lakini ukweli nadhani unabaki palepale ni viongozi wetu walioko madarakani ambao wanaweza kukomesha hili na sisi vikundi kwa vikundi, imani tofauti hatutakuwa na jinsi zaidi ya kufuata yale wenye meno wametaka.

Mutakuwa na wasiwasai mpaka pale mutakapokuwa tayari kuuvunja mfumo kristo.

Udini haukuanza katika uongozi huu,udini ulizaanza tokea enzi za Baba wa Kanisa Nyerere.

Tatizo lenu ni moja zamani mulizoea kuamrisha vyombo vya dola,na vyombo vya dola vilitii amri za maaskofu bila kuhoji,kwa hivi sasa hiyo hali kidogo imeanza kupungua,hawezi Askofu akaamuka tu kuamrisha vyombo dola vikamate waislamu na vyombo vya dola vikatii mara moja,viatatii lakini kwa kuchelewa kidogo

Shame up on you munaotaka Maaskofu waendelee kuiamrisha serikali.
 
Bado tunakumbuka Baba wa Kanisa nyerere alivyopambana na waislamu baada ya uhuru mpaka akafanikiwa kuanzisha kitengo cha usalama wa taifa cha kuwadhibiti na kurudisha nyuma maendeleo ya waislamu a.k.a BAKWATA.
 
mimi nadhani tatizo lipo kwa uongozi uliopo madarakani leo. kwanini tofauti hizi zote hazikuwahi kujitokeza katika awamu zingine.mimi nadhani ninaulaumu uongozi wa sasa na hata kama haya yatakuja kudevelop na kutupelekea kuwa kama Rwanda(Mungu aepushilie mbali) and if i will manage to survive washtakiwa wangu namba moja watakuwa ni uongozi uliopo madarakani leo. sababu najiuliza usalama wa taifa siku hizi upo wapi?? unafanya nini?? mashushu wako wapi na wanafanya nini? majeshi yetu vipi? serikali na mihimili yake wanafanya nini? by the way mimi ninaona hawa ndiyo wachochezi wa vuguvugu hili la kidini namba moja. sijawahi kuwa na wasiwasi na maisha yangu na familia yangu kama wakti huu, ninajua tunavyoendelea hivi kwa sasa isipopatikana suluhu ya ukweli isiyo ya kinafiki mdomoni itakuja kulipuka tu nooo way.hawa wachochezi wetu hawatakuwepo na familia zao, watakuwa wanaangalia kwenye screen tu na kusikiliza kwenye redio. mimi with a certain time to come nafikiria niikimbie hii nchi na familia yangu.haitakalika unless watu fulani muhimu watakapokuwa sincere kulisimamia hili kwa ukweli.

imetokea sehemu napokuwaga inanikutanisha na watu tofauti tofauti, yaani kwa yale ninayoyasikia sasa yakitoka mioyoni mwa watu ninaona ile mbegu iliyopandwa imeshaota mizizi na sasa inachepua, inahitaji mvua moja kubwa kuufanya huu mmea uonekane vizuri.

kwa imani yangu (natambua kila mtu ana imani yake na jinsi wanavyofanya)huwa kabla hatuchagua viongozi katika uchaguzi huwa tunafanya maombi kwa muda mrefu tu before, na nia ni kuwa tunamwomba Mungu atuelekeze mtu sahihi wa kumchagua. we even fast for that issue. wakati tunafanya maombi haya before sana uchaguzi wa 2005 God answered to one of the person and he said to him ni nani hasa watakaokuwa viongozi for that time, na hakuishia hapo tu alionyesha ni kwa jinsi gani kipindi hichi cha uongozi kitakavyokuwa. alisema katika kipindi cha kwanza vitu vingekuwa hivi na hivi, and then the next period things will be more like this and this.anyway at the time sikuwa na haja ya kucomment sababu yawezekana haikuwa ni Mungu ni hisia zake tu, and niliacha hivyohivyo. lakini kwa ukweli nilipiga kura na kumchagua ambaye niliona angefaa.l thank God amenipa uhai hata sasa ambapo ninakumbuka maono ya yule mtu mwaka 2005 katikati, ambapo nimeona kila alilolisema limekuwa kama alivyosema, nimeogopa coz yule aliyeona na kusema hakuishia hapo alitoa na solution to do.so kwa upande wangu ninaona watanzania tunakoelekea si kuzuri.heri hawa waadhiri wanaojikosha leo na matamko yao mazuri sababu wanaweza kuokoka na tribunals.lakini ukweli nadhani unabaki palepale ni viongozi wetu walioko madarakani ambao wanaweza kukomesha hili na sisi vikundi kwa vikundi, imani tofauti hatutakuwa na jinsi zaidi ya kufuata yale wenye meno wametaka.

Tatizo la Watanzania tuna uhonjwa wa kulalamika na kutoambiana ukweli. Ukiangalia tamko la hawa Wahadjhiri linazungukazunguka kidiplomasia lakini hawausemu ukweli waziwazi. Kwa wanaofaamu unajua wanachokikusudia. Kwa sababu hii walengwa wanaendelea kufanya mambo yanayolalamikiwa. Lakini mimi nawaza tukiwa na utamaduni wa kuambiana moja kwa moja matatizo ya namna hii yatapungua.

Ndugu yangu huwezi kukimbia. Sijui wewe familia yako inaishia wapi kwa sababu sidhani kuwa utawahamisha wote. Mbaya sana familia zetu zina mchanganyiko wa imani, sijui tukiingia katika mtafaruku huu ni familia ipi haitaguswa!
 
Issue sio ''kusoma sana'' kama unavyotaka kuniwekea maneno mdomoni (hakuna mahali nimesema nimesoma sana ila kama uliota). Issue ni kusoma na kufanya kazi kwa bidii.

Watu wengine bana,wepesi kuwaambia wenzao hawakusoma,wakiambiwa wanaruka juu elimu sio muhimu.

Utawasikia Ilunga na Ponda hawakusama hivyo waislamu wanaongozwa na vilaza,lakinia wakiambiwa Mbowe hakusoma,Sugu hakusoma.Lema hakusoms na wengine wengi,pia muongezi Mnyika aliyeshindwa shule baada ya kupta A zake tisa za kupewa za maua seminari,watakuja juu hoo tunaangalia uwezo wa mtu kiutendaji,watu wa ajabu hawa!!!!!!!!!!!!!!!
 
Tatizo la Watanzania tuna uhonjwa wa kulalamika na kutoambiana ukweli. Ukiangalia tamko la hawa Wahadjhiri linazungukazunguka kidiplomasia lakini hawausemu ukweli waziwazi. Kwa wanaofaamu unajua wanachokikusudia. Kwa sababu hii walengwa wanaendelea kufanya mambo yanayolalamikiwa. Lakini mimi nawaza tukiwa na utamaduni wa kuambiana moja kwa moja matatizo ya namna hii yatapungua.

Ndugu yangu huwezi kukimbia. Sijui wewe familia yako inaishia wapi kwa sababu sidhani kuwa utawahamisha wote. Mbaya sana familia zetu zina mchanganyiko wa imani, sijui tukiingia katika mtafaruku huu ni familia ipi haitaguswa!

Watakufa kwanza Maaskofu na Padri waliondaa na kuuendeleza mfumo kristo,nyinyi makabwela wenzetu tunaoishi pamoja kwenye nyumba za kupanga na kuombana chumvi na moto hatuna shida na nyinyi.
 
Asante.
Lakini nikukumbushe tu kwamba sikuweka matokeo yangu hapa hili munisifie,nimeweka matokea yangu hapa hli kuonesha namna gani vijana wakiislamu tunavyosumbuliwa na mfumo kristo,maana wale mawakala wa mfumo kristo kule wilayani kwangu pamoja na kujua niliongoza mtihani wa darasa la saba kiwilaya,na kwenda na report zaform one na form two nikiwa nimekuwa wa kwanza,lakini wale jamaa waliishia kunikejeli na kunidharau kwasababu ya dini yangu.

Na yule second master naye alifanya hivyo hivyo.

Kwa hakika watu hawa walitaka niwe muuza dagaa pale feli kama mama yangu kisha waesma waislamu hawataki kusoma ni vilaza,acha niuchukie mfumo kristo maana ni hatri sana kwa taifa hili.Asante Mungu,asante mama kwa kunifikisha hapa nilipo,maana mama pamoja na ufukura wake wote lakini alijua mwanae nina kipawa lazima nisome ndio maana alinirudisha shule baada ya kukaa nyumbani mwaka na nusu.
Kwanza nishukuru kwa kunikumbusha kwamba rais aliyekuwa madarakani mwaka 96 ni Mkapa..nimerekebisha kwa faida ya watakaopitia.
lakini bado nna matatizo na imani yako kwa unachoita mfumo kristo. Hebu nisaidie, kama aliyekufukuza shule alikuwa second master headmaster alikuwa wapi? Huyo headmaster alikuwa dini gani?
Hebu tuambie kuhusu wanafunzi wa kikristo walikuwa wanapendelewa na second master au nao walikuwa wanakutana na madhila kama yako?

Mwisho, naomba nikwambie mimi O' level na A' level nimerudishwa nyumbani mara nyingi kwa kukosa ada,, tena kwa viboko kwamba tunawasumbua walimu kutufuata madarasani, nawafahamu na wenzangu wengi waislam na wakristo waliokutwa na mambo hayo sasa wewe unaposema kwa kuwa wewe ni muislam na aliyekurudisha ni mkristo basi unaamini alifanya hivyo kwa sabbu ya tofauti ya dini zenu mimi unasikitisha.
 
Ndio maana nilisema tamko hili la wasomi halijakaa kisomi.
Baada ya kufuatilia michango ya kwenye thread hii imedhihirika. Unaona hata kwenye mjhadala wa tamko la wasomi badala ya kuwa chanzo cha utatuzi ndio kwanza tamko hili linachochea kutokuelewana zaidi.
 
Kwanza nishukuru kwa kunikumbusha kwamba rais aliyekuwa madarakani mwaka 96 ni Mkapa..nimerekebisha kwa faida ya watakaopitia.
lakini bado nna matatizo na imani yako kwa unachoita mfumo kristo. Hebu nisaidie, kama aliyekufukuza shule alikuwa second master headmaster alikuwa wapi? Huyo headmaster alikuwa dini gani?
Hebu tuambie kuhusu wanafunzi wa kikristo walikuwa wanapendelewa na second master au nao walikuwa wanakutana na madhila kama yako?

Mwisho, naomba nikwambie mimi O' level na A' level nimerudishwa nyumbani mara nyingi kwa kukosa ada,, tena kwa viboko kwamba tunawasumbua walimu kutufuata madarasani, nawafahamu na wenzangu wengi waislam na wakristo waliokutwa na mambo hayo sasa wewe unaposema kwa kuwa wewe ni muislam na aliyekurudisha ni mkristo basi unaamini alifanya hivyo kwa sabbu ya tofauti ya dini zenu mimi unasikitisha.

Mzee mbana mgumu sana kuelewa,sijalalamika kurudishwa nyumbani kwa ajili ya ada,hiyu second master alitoa maneno ya kejeli na dharau kwangu na mama yangu,kumbuka kipindi hicho tulikwenda na ada na barua kutoka wizarani ili wanipokokee kwasababu nilikaa nyumbani mwaka na nusu.

Mzee mbona ofisi nyingi tu zimejaa mawakala wa mfumo kristo,acha kupiga porojo hapa inawezekana hata wewe mwenyewe ni wakala wa mfumo kristo kama alivyo mkuu wa chuo ninachofundisha.

Yule headmaster,ameshafariki mung amlipe anachostahiki tulikuwa tunatoka mkoa mmoja na mimi,alikuwa anijua nilivyokuwa nafanya vizuri darasani form one na form two,pia alimuonea huruma dada yake(mama yangu) wa mkoa mmoja alivyokuwa analia ndio akamwambia muache kijana afanye mtihani mwka huu na atafaulu na kuwa daktari mzuri,mama na mimi tunayakumbuka san maneno ya yule mzee ni kweli nimekuwa daktari.

Form six semister ya mwisho nilifukuzwa tena shule kwa kukosa ada nikakaa nyumbani hata mock sikufanya nikaenda kufanya mtihani wa taifa PCB nikapata division point 10,hapa sina wa kumlaumu zaidi ya ufukara wa mama yangu uliosababisha na mfumo kristo ulioasisiwa na Baba wa Kanisa Nyerere
 
Nikiwa mwaka nilikuja kubadilisha pasipoti yangu,pale uhamiaji walisumbua nikakapelekakila kitu walichohotaji,usumbufu ukaendelea mpka zikabaki siku mbili tiketi yangu ihishe muda wake ndio wakaniambia unahitwa na bosi.

Nikaenda kwa Bosi,basi nikakutana na wakala wa mfumo kristo akinambia hutapewa pasport kwasababu wewe sio raia wa nchi hii,nakamuangalia usoni kisha nikamuuliza kuan mtu aliyedhaliwa kilwa akawa sio raia,akaniambia nimeshakuambia wewe sio raia,nikamuuliza tena mbona mwanzo mulinpa pasport,akataka kunifukuza,nikagoma na kumuambia nimekugundua wewe ni wakala wa mfumo kristo unataka nishinde kurudi chuo hili nikauze dagaa kisha musema waislamu hatupendi kusoma.

Nikamuambia usiponipa pasport leo utaenda kujibu kesi hii kw bosi na utanikatia pasport,na nikichelewa chuo utanifutia chuo wewe,kasha nikatoka nje ya ofisi yake,mara akamtuma mtu aje kuniita niakenda kule akaniambia unajua nilishachafua faili lako hivyo itabidi uandike barua kwa mkurugenzi wa uhamiaji ili tuweze kukupa pasport leo.Nikamwambia siandiki barua kisha nikatoka,akamtuma tena yule akaja kuniambia unajua ndugu yangu mzee ameshakwama kwa hiyo wewe andika tu barua tumsaidie,nikaandika baraua kwa mkurunze,wakaniambia nifuate pasport saa nane.

Nilipoenda saa nane nikaikuta pasport ya moto imetoka kwenye mtambo muda huo huo,jamaa likaniambia umetusumbua wewe maana imebidi tuvunje utaratibu hili tukutengezee pasport leo,sikumjibu nikasaini na kutimka zangu.

Nchi imejaa mawakala wa mfumo kristo hii,we acha tu
 
Nikiwa mwaka nilikuja kubadilisha pasipoti yangu,pale uhamiaji walisumbua nikakapelekakila kitu walichohotaji,usumbufu ukaendelea mpka zikabaki siku mbili tiketi yangu ihishe muda wake ndio wakaniambia unahitwa na bosi.

Nikaenda kwa Bosi,basi nikakutana na wakala wa mfumo kristo akinambia hutapewa pasport kwasababu wewe sio raia wa nchi hii,nakamuangalia usoni kisha nikamuuliza kuan mtu aliyedhaliwa kilwa akawa sio raia,akaniambia nimeshakuambia wewe sio raia,nikamuuliza tena mbona mwanzo mulinpa pasport,akataka kunifukuza,nikagoma na kumuambia nimekugundua wewe ni wakala wa mfumo kristo unataka nishinde kurudi chuo hili nikauze dagaa kisha musema waislamu hatupendi kusoma.

Nikamuambia usiponipa pasport leo utaenda kujibu kesi hii kw bosi na utanikatia pasport,na nikichelewa chuo utanifutia chuo wewe,kasha nikatoka nje ya ofisi yake,mara akamtuma mtu aje kuniita niakenda kule akaniambia unajua nilishachafua faili lako hivyo itabidi uandike barua kwa mkurugenzi wa uhamiaji ili tuweze kukupa pasport leo.Nikamwambia siandiki barua kisha nikatoka,akamtuma tena yule akaja kuniambia unajua ndugu yangu mzee ameshakwama kwa hiyo wewe andika tu barua tumsaidie,nikaandika baraua kwa mkurunze,wakaniambia nifuate pasport saa nane.

Nilipoenda saa nane nikaikuta pasport ya moto imetoka kwenye mtambo muda huo huo,jamaa likaniambia umetusumbua wewe maana imebidi tuvunje utaratibu hili tukutengezee pasport leo,sikumjibu nikasaini na kutimka zangu.

Nchi imejaa mawakala wa mfumo kristo hii,we acha tu

Ukiogopa mamba hata ukiona ujiti usiku utasema mamba.

Watu wakikwambia hapo palikuwa na tatizo la rushwa tu, watu walikuwa wanataka rushwa, hayo ya mfumokristo ni yako utasemaje?

Kipi kinachokufanya uamini hapo tatizo lilikuwa ni mfumokristo na wala si rushwa?

Unataka kusema wakristo hawasumbuliwi uhamiaji?

Unajua tangu uhuru mawaziri wangapi waislamu wamepita hapo?

Kama kuna mfumokristo, mfano wako wa hapo juu haujaumulika bado.
 
Tatizo kubwa lililokuwepo Tanzania ni kuwa na wanasiasa wanaojijali wenyewe kuliko wanao waongoza,wanasiasa walioweka maslahi mbele kuliko kazi zao

Serikali inatakiwa iwe sawa kwa dini zote zilizokuwepo katika nchi,Haya matatizo ya dini yamekuja kwasabu wanasiasa wanashindwa kuwakemea viongozi wa dini kwa kuogopa kutopata kura kwa waumini wa dini fulani

kwasababu mwanasiasa anajijali yeye tu sio anaowaongoza, maamuzi yake yanakuwa "linalotokea na llitoke yangu yananiendea",na maamuzi haya si kwenye Dini tu bali kwenye elimu kwenye matibabu nk
 
Back
Top Bottom