Katavi
Platinum Member
- Aug 31, 2009
- 41,983
- 12,702
Enzi nikiwa mdogo hawa jamaa walikuja kuweka nguzo katika nyumba yetu, lakini cha kushangaza baba siku hiyo alitufukuza watoto wote pale nyumbani.......tuliporudi tukakuta nguzo imesimamisha.
Nilibaki nikijiuliza kwa nini tuliondolewa pale nyumbani, lakini siku moja nilipata jibu baada ya kushuhudia jamaa wakisimamisha nguzo sehemu moja jirani na pale nyumbani......dah!!! Jamaa nyimbo wanazoimba ni balaa, yale matusi ya nguoni yanageuzwa nyimbo nzuri sana za kuvutia kusikiliza............sasa najiuliza sijui zile nyimbo ndio zilikuwa zinawapa nguvu!! Au walikuwa wanafundishwa huko vyuoni kwao kuwa bila matusi yale kazi haziendi..
Sijui kama mpaka sasa wanaendelea na utaratibu ule!!
Nilibaki nikijiuliza kwa nini tuliondolewa pale nyumbani, lakini siku moja nilipata jibu baada ya kushuhudia jamaa wakisimamisha nguzo sehemu moja jirani na pale nyumbani......dah!!! Jamaa nyimbo wanazoimba ni balaa, yale matusi ya nguoni yanageuzwa nyimbo nzuri sana za kuvutia kusikiliza............sasa najiuliza sijui zile nyimbo ndio zilikuwa zinawapa nguvu!! Au walikuwa wanafundishwa huko vyuoni kwao kuwa bila matusi yale kazi haziendi..
Sijui kama mpaka sasa wanaendelea na utaratibu ule!!