Wafanyakazi wa TANESCO!!!!!

Katavi

Platinum Member
Aug 31, 2009
41,983
12,702
Enzi nikiwa mdogo hawa jamaa walikuja kuweka nguzo katika nyumba yetu, lakini cha kushangaza baba siku hiyo alitufukuza watoto wote pale nyumbani.......tuliporudi tukakuta nguzo imesimamisha.
Nilibaki nikijiuliza kwa nini tuliondolewa pale nyumbani, lakini siku moja nilipata jibu baada ya kushuhudia jamaa wakisimamisha nguzo sehemu moja jirani na pale nyumbani......dah!!! Jamaa nyimbo wanazoimba ni balaa, yale matusi ya nguoni yanageuzwa nyimbo nzuri sana za kuvutia kusikiliza............sasa najiuliza sijui zile nyimbo ndio zilikuwa zinawapa nguvu!! Au walikuwa wanafundishwa huko vyuoni kwao kuwa bila matusi yale kazi haziendi..
Sijui kama mpaka sasa wanaendelea na utaratibu ule!!
 
Mkuu siyo siri si kwamba nakopi ila nakumbuka nilikuwa nasoma shule ya msingi na enzi hizo shule ilikuwa ni sa moja hadi sita na nusu mchana kisha tunarudi home kula na tunarudi shule saa nane kwa ajili ya masomo hadi kumiunusu. Nimekumbuka waliwahi kuja kusimamisha nguzo saa sita na ndo kwanza tulikuwa tumerudi siku hiyo mama alitwambia chakula kimeungulia so turudi shule mapema tutakula saa kumi akatupa hela ya andazi moja moja. Kumbe shida ilikuwa ni hii? Wazazi bwana!
 
Mdau nikiwa Sumbawanga miaka ya 80-82 mitaa ya Regional Block kwa wale wanaoijua Sumbawanga miaka hiyo ndo walikuwa wanapitisha nguzo za umeme kule na kuweka umeme niliwashuhudia live na tulikuwa tunaimba sana nyimbo zao na misemo yao ni matusi makubwa sana ya nguoni lkn kuna misemo hii ya Ali fum fum mwanaume fum fum wanapandisha mlingoti juu na alijuu juu mwanaume juu juu hahahaa wale jamaa nuksiiiiiii
 
Mkuu siyo siri si kwamba nakopi ila nakumbuka nilikuwa nasoma shule ya msingi na enzi hizo shule ilikuwa ni sa moja hadi sita na nusu mchana kisha tunarudi home kula na tunarudi shule saa nane kwa ajili ya masomo hadi kumiunusu. Nimekumbuka waliwahi kuja kusimamisha nguzo saa sita na ndo kwanza tulikuwa tumerudi siku hiyo mama alitwambia chakula kimeungulia so turudi shule mapema tutakula saa kumi akatupa hela ya andazi moja moja. Kumbe shida ilikuwa ni hii? Wazazi bwana!
Ahahahaah wale jamaa nuksi, kuna jamaa mmoja aliwahi mwambia mama yake aondoke nyumbani aliposikia jamaa wanakuja kubadili nguzo hapo!
 
Mdau nikiwa Sumbawanga miaka ya 80-82 mitaa ya Regional Block kwa wale wanaoijua Sumbawanga miaka hiyo ndo walikuwa wanapitisha nguzo za umeme kule na kuweka umeme niliwashuhudia live na tulikuwa tunaimba sana nyimbo zao na misemo yao ni matusi makubwa sana ya nguoni lkn kuna misemo hii ya Ali fum fum mwanaume fum fum wanapandisha mlingoti juu na alijuu juu mwanaume juu juu hahahaa wale jamaa nuksiiiiiii
Mitaa hiyo naipata sana mkuu!
 
Nimefanya kazi kidogo kwenye sehemu za ujenzi na hizi ni kwa Tanzania na bara la Ulaya miaka ya 90.

Nikiwa huko, nilifikiri Wazungu hawatukani, mhhhh.....

Jamaa walikuwa wakijenga Drinage System kubwa mjini na ilikuwa kama wanajenga line ya Metro. Nikashuka hadi chini na kwenda hadi sehemu wanayochimba na kuweka zile kuta kwa juu na chini na kukausha maji. Kuna Zee la Kizungu, lilikuwa kila likikata udongo, maji yanaruka na lenyewe linaweka tusi. Basi kila action ilikuwa ni K..., mb......, Mb.. ndani ya Ma..... Na kila kitu kibaya basi wanakilinganisha na Mb....
Kwa Tz nilishawahi kufanya kazi pale Interchick...... Mhhh wale wabeba zege hasa kijana mmoja aitwaye Kuti akikaa Kawe.... Huyu alikuwa na tabia akiwa nyumbani, haongei kabisa na wabeba zege wenzake kwa kuhofia watamkumbushia aliyoyasema kazini.

Kiboko ni Mkurugenzi mmoja wa Interchick aitwaye Makongoro (Nyerere family). Jamaa na shule yake swaafi USA, akarudi zake Bongo. Wakati akijenga nyumba yake, akakubaliana na wabeba zege kiasi cha Sh.60,0000 ya miaka ya 80. Jamaa wamekula mzigoooo wakaona hela mbuzi na wakagoma kufanya kazi. Kufika usiku kama saa sita, Makongoro kaingia na msosi kwenye Pajero lake na anakuta kazi imesimama. Wakadai walipwe Tsh 80,000 wamalizie kazi. Jamaa likawaangalia na kuwaambia " mkitaka hiyo hela, sawa ntakupeni ila nikuf*** kwanza nyote." Jamaa wakajua leo wamekutana na mtoto wa kihuni na wakamalizia tu kazi na kujiondokea.

Siku iliyofuata wakaja wenyewe wanasema "hili li Makongoro halifai, jana limetutukana kishenzi....."

Wabeba zege, Makuli wa bandari, wafanyakazi wa Tanesco, Dawasco nk nk matusi ni kama MAFUTA yao. Wakisharusha matusi ni kama wamejiwekea petrol.

Matusi huwa yanasaidia sana kupandisha morali ya mtu na kumpa nguvu na kujiamini.

Kama hujaingalia film ya KING'S SPEECH, basi nenda humo ndani uone Baba yake Queen Elizabeth akiporomosha matusi.
 
enzi nikiwa mdogo hawa jamaa walikuja kuweka nguzo katika nyumba yetu, lakini cha kushangaza baba siku hiyo alitufukuza watoto wote pale nyumbani.......tuliporudi tukakuta nguzo imesimamisha.
Nilibaki nikijiuliza kwa nini tuliondolewa pale nyumbani, lakini siku moja nilipata jibu baada ya kushuhudia jamaa wakisimamisha nguzo sehemu moja jirani na pale nyumbani......dah!!! Jamaa nyimbo wanazoimba ni balaa, yale matusi ya nguoni yanageuzwa nyimbo nzuri sana za kuvutia kusikiliza............sasa najiuliza sijui zile nyimbo ndio zilikuwa zinawapa nguvu!! Au walikuwa wanafundishwa huko vyuoni kwao kuwa bila matusi yale kazi haziendi..
Sijui kama mpaka sasa wanaendelea na utaratibu ule!!

mafundi magari..pikipiki..nao wamo mkuu.
 
ha hahaaaaa!!!!
mie nilishuhudia nguzo ya jirani yangu ilidondoka wakaja, ghafla nikaona kina mama wamejazana wanacheka sana, nikatamani nichungulie dirishani, huwezi amini, sikubanduka pale mpaka nguzo ilivyosimamishwaaaa, ilikua balaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!

Tanesco ni nuksi naona wamefundishwa kutukana wale!!
 
Nimefanya kazi kidogo kwenye sehemu za ujenzi na hizi ni kwa Tanzania na bara la Ulaya miaka ya 90.

Nikiwa huko, nilifikiri Wazungu hawatukani, mhhhh.....

Jamaa walikuwa wakijenga Drinage System kubwa mjini na ilikuwa kama wanajenga line ya Metro. Nikashuka hadi chini na kwenda hadi sehemu wanayochimba na kuweka zile kuta kwa juu na chini na kukausha maji. Kuna Zee la Kizungu, lilikuwa kila likikata udongo, maji yanaruka na lenyewe linaweka tusi. Basi kila action ilikuwa ni K..., mb......, Mb.. ndani ya Ma..... Na kila kitu kibaya basi wanakilinganisha na Mb....
Kwa Tz nilishawahi kufanya kazi pale Interchick...... Mhhh wale wabeba zege hasa kijana mmoja aitwaye Kuti akikaa Kawe.... Huyu alikuwa na tabia akiwa nyumbani, haongei kabisa na wabeba zege wenzake kwa kuhofia watamkumbushia aliyoyasema kazini.

Kiboko ni Mkurugenzi mmoja wa Interchick aitwaye Makongoro (Nyerere family). Jamaa na shule yake swaafi USA, akarudi zake Bongo. Wakati akijenga nyumba yake, akakubaliana na wabeba zege kiasi cha Sh.60,0000 ya miaka ya 80. Jamaa wamekula mzigoooo wakaona hela mbuzi na wakagoma kufanya kazi. Kufika usiku kama saa sita, Makongoro kaingia na msosi kwenye Pajero lake na anakuta kazi imesimama. Wakadai walipwe Tsh 80,000 wamalizie kazi. Jamaa likawaangalia na kuwaambia " mkitaka hiyo hela, sawa ntakupeni ila nikuf*** kwanza nyote." Jamaa wakajua leo wamekutana na mtoto wa kihuni na wakamalizia tu kazi na kujiondokea.

Siku iliyofuata wakaja wenyewe wanasema "hili li Makongoro halifai, jana limetutukana kishenzi....."

Wabeba zege, Makuli wa bandari, wafanyakazi wa Tanesco, Dawasco nk nk matusi ni kama MAFUTA yao. Wakisharusha matusi ni kama wamejiwekea petrol.

Matusi huwa yanasaidia sana kupandisha morali ya mtu na kumpa nguvu na kujiamini.

Kama hujaingalia film ya KING'S SPEECH, basi nenda humo ndani uone Baba yake Queen Elizabeth akiporomosha matusi.
Kumbe ni sehemu zote tu wanakotumia nguvu lazima matusi yawepo!
 
ha hahaaaaa!!!!
mie nilishuhudia nguzo ya jirani yangu ilidondoka wakaja, ghafla nikaona kina mama wamejazana wanacheka sana, nikatamani nichungulie dirishani, huwezi amini, sikubanduka pale mpaka nguzo ilivyosimamishwaaaa, ilikua balaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!

Tanesco ni nuksi naona wamefundishwa kutukana wale!!
Ahahahahaaah!! Huenda ulijifunza maneno mengi sana.
 
Back
Top Bottom