Msaada: Namna ya kumsikiliza English native speaker wa kizungu

Anonymous Caller

JF-Expert Member
Sep 8, 2016
480
571
Wadau wa lugha,

Na Mimi bwana nimebahatika kupata kashahada fulani kutoka moja ya vyuo vyetu vikongwe.

kwahiyo ka-english ka hapa na pale kakuombea maji huwa ninako. Masomo ya english secondary nilipa daraja B.

Tatizo kuu langu ni moja;

Ukiongea wewe kiingereza (mswahili mwenzangu) huniteti chochote,
nitakuelewa vizuri sana.

Akiongea kiingereza mwafrika mwenzangu(mkenya,mnigeria,msauz nk&)
haniteti pia nitamwelewa anavyoniongelesha.

Akiniongelesha mzungu yeyote asiyekuwa mmarekani,mwingereza,au yeyote ambaye kwake english sio mother tongue, huyu nae hanisumbui sana.

Shida ipo kwny kumwelewa mzungu au mweusi ambaye kwake ENGLISH ni mother tongue au native language.

Naomba niwe muwazi, huwa siambulii kitu.

Sijui midomo ya hawa jamaa ikoje.
wanaongea micharango mno.

Cha ajabu sasa, yale anayonisemesha YAKIANDIKWA mahali ni kiingereza chepesi sana.

Kuna nyimbo nzuri sana za kizungu mfano akina usher raymond, nelly, etc
wakiimba ndio hamna kabisa.

Ila zile lyrics za nyimbo wanazoimba akina rihanna ukipewa ni english changa kabisa.

Mwaka Juzi, nikiwa naangalia mechi fulani ya liverpool, Michael owen alikuwa mchambuzi siku ile.

Nilitamani sana kujua nini owen anasema lakini kutokana na tatizo hili sikutoka na kitu.
utafikiri sikusoma.

Tulikuwa tunaangalia movie fulan nyumbani, ka-wife si kakaomba nikatafasirie! Nilibumbabumba uongo.

Drogba alipokuwa akihojiwa kwenye interview namuelewa. Aongee lampard sasa!

Kujua kiingereza jambo moja, kumsikiliza na kumwelewa English native speaker ni jambo jingne.

Sasa hebu tushaurianeni.
 
Tatizo lako ni kwamba unamsikiliza sana mtu wa native English ulitegenea Kila neno ulisikie , Sasa hiyo unakusababisha kukuondolea utulivu wa ufahamu (confidence).

Cha kukusaidia tafuta watu wa Native English uwe unaongea nao mara Kwa mara
 
Nkuu, ulisoma lugha ya kingereza yenyewe au umesoma mambo ya Uongozi mana kusoma ulaya si kweli ndo umejua English lg
 
Bro complete communication skills ni
1. Kuongea
2. Kuandika
3. Na kusikia/kuelewa

Sasa ndugu kama umekosa listening skills maana yake hukuwa vizur huko, sasa basi jitahid sana kusikiliza sana bbc broadcasting, especially England mother tongue slowly it will come up na ubongo wako utaweza kuidentify maneno yale kwa maneno ya kawaida, neno la kawaida unaweza usilisikie sababu ubongo wako unaona ni geni kabisa lakn likiandikwa unajiona mjinga, sikiliza kwa wingi redio za nje
 
Uwa ninapita pita kwenye forums ya wanaija nikagundua wao pia wanakumbwa na tatizo ili, Zaid ya nyuzi mbili nimewai kutana nazo katika forums wakilalamika kuwa haweawezi angalia taarifa ya Habari kwa media kama CNN etc.
 
Huko chuoni Mkuu itakua ulikua wale jamaa waliokua room wakiangalia movies ulikua unawaona kama mafala flani hivi. Movies ndio njia rahisi kuimprove listening skills na chuoni ndio kuna opportunity kubwa ya kuangalia movies zinapatikana kwa urahisi na una muda.
 
Huko chuoni Mkuu itakua ulikua wale jamaa waliokua room wakiangalia movies ulikua unawaona kama mafala flani hivi. Movies ndio njia rahisi kuimprove listening skills na chuoni ndio kuna opportunity kubwa ya kuangalia movies zinapatikana kwa urahisi na una muda.
ooh! labda zile movies ambazo chini yanapita maneno ya kile kilichotamkwa.
 
Wadau wa lugha,

Na Mimi bwana nimebahatika kupata kashahada fulan kutoka moja ya vyuo vyetu vikongwe...
Native English Speaker wanaoongea kiingereza vizuri sana na kwa speed ya hali ya juu, ni wa-Australia. Nashauri ukakae kwao mwaka mzima, au uende ukafanye nao kazi pale mgodi wa Kabanga Nickel, Ngara, wapo wamejaa wengi tu.

I admire Australians, ongea yao. Wanaongea kiingereza kizuri mno. Watu ambao huwa wanaongea kiingereza ambacho mimi huwa hakinifurahishi sana ni waingereza wenyewe. The next wanaofuata kwa Australians, ni Mmarekani, halafu baadaye Canadians.
 
Huko chuoni Mkuu itakua ulikua wale jamaa waliokua room wakiangalia movies ulikua unawaona kama mafala flani hivi. Movies ndio njia rahisi kuimprove listening skills na chuoni ndio kuna opportunity kubwa ya kuangalia movies zinapatikana kwa urahisi na una muda.

Yeah uko sahihi, Msingi wa kuelewa kiingereza unaanza toka pale mdogo ukiwa mtu mzima na haufahamu utahitaji nguvu zaid na kwa alivyosema I doubt hata kam atakuwa ni muongeaji mzuri pia apige mazoezi aachane na kingereza cha chuoni na shulen Tz, ukijua kile obvious huwez kumuelewa Native english speaker

Msingi wa kuelewa English ni Kuwasikiliza wenyewe wenye lugha yao mfano Mm toka mdogo nilianza na katuni, nkaja Movies, Tv shows, reality shows, documentaries na sku hizi kuna hizi audiobooks pamoja na podcasts yaani hivyo vyote lazima uelewe native speaker akiongea unamsikia kama anaongea kishwahili vile
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom