Wafanyakazi mwaka huu hamkuwa na matatizo hadi mkaamua kumfanyia Kampeni Rais Samia?

Wafanyakazi mwaka huu hamkuwa na matatizo hadi mkaamua kumfanyia Kampeni Rais Samia?

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Wakuu,

Katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), yaliyofanyika kitaifa mwaka huu mkoani Singida, ujumbe uliobebwa na mabango ya wafanyakazi kutoka Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) umenisikitisha sana kama mdau wa ajira.

"Uchaguzi Mkuu 2025 utuletee Viongozi wanaojali Haki na Maslahi ya Wafanyakazi, Sote tushiriki."

IMG_4675.jpeg
Kauli hii inaonekana kama ishara ya wazi ya kumuunga mkono Rais Samia kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao, jambo linaloibua maswali mengi kuhusu nafasi ya vyama vya wafanyakazi kwenye mchakato wa kisiasa.

1746705013819.png

1746705065377.png

1746705087050.png

1746705120850.png

1746705142141.png
Kwa maoni yangu, ujumbe huo unaashiria mwelekeo wa kisiasa usiostahili kujitokeza katika jukwaa la Mei Mosi, siku ambayo kwa kawaida hujikita katika kushughulikia changamoto za wafanyakazi, si kutoa taswira ya kisiasa.

Je, ni kweli kwamba mwaka huu wafanyakazi hawakuwa na malalamiko yoyote ya msingi, hadi wakaamua kutumia jukwaa la Mei Mosi kumfanyia kampeni Rais Samia?

Je, bado tuna uhuru wa kuhoji na kushinikiza maboresho ya haki na maslahi yetu kama wafanyakazi bila kuingiza siasa?

Ni vyema tufikiri kwa makini kuhusu mustakabali wa vyama vya wafanyakazi na wajibu wao wa kweli katika kutetea maslahi ya wanachama wao.

1746705183360.png

1746705207895.png

1746705238431.png


1746705254408.png


1746705270672.png


1746705637410.png
 

Attachments

  • 1746705285002.png
    1746705285002.png
    2.2 MB · Views: 16
mfanyakazi wa bongo ni kama beki tatu tu akishaona kila kitu kipo japo sio vyake akhaaaaaaaaaaaa ananenepeana tu kama broiler , hasa wale wapiga saluti yaani wameridhika utadhani hawana matatizo na ndio wakwanza kukopa kwa mangi vijidagaa na unga.
 
Back
Top Bottom