Wafanyabiashara mnaofanya biashara kimazoea jiandaeni kisaikolojia na ujio wa kina "Niffer" wengi zaidi

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Mar 29, 2012
10,223
22,301
Kwa wiki iliyopita mitandaoni hasa Instagram na Twitter kuliibuka mjadala mkali ikiwemo vita ya maneno miongoni mwa wafanyabiashara wa mjini Dar es Salaam. Baadhi ya wafanyabiashara walimtupia lawama Bi Niffer ambaye ni mfanyabiashara mdogo anayekuwa kwa kasi ya ajabu. Wanamtuhumu Niffer kurukia kila biashara huku akivunja miiko mingi ya biashara hizo. Wanadai Niffer amekuwa akiharibu bei za soko kwa makusudi huku akiponda bidhaa za wafanyabiashara wengine.

Hili suala limekuwa na mitazamo mingi. Watu wengi wamesema Niffer yuko sahihi kwa sababu ni mbunifu na hakuna sheria anayovunja. Upande mwingine unadai sio vema Niffer kuanika bei zake ndogo hadharani kwa sababu zinawaharibia wenye maduka ambao wanalipa kodi nyingi sana. Binafsi baada ya kufuatilia hili sakata nimeona ni sahihi 100% Niffer kuendelea kuwapelekea moto hao wakongwe wasiotaka kubadilika. Pia yeye kuuza vitu kwa bei ya chini ni msaada kwa wananchi wengi. Niffer ni mjasiriamali kamili anayetatua changamoto za raia huku raia wakiweka pesa kwenye wallet ya Niffer.

Ukitoa wauza nguo kwa bei ya jumla hao wafanyabiashara wengine ni wapigaji kwa kuweka bei za juu kupitiliza. Nina ushahidi usiotia shaka. Kwa mfano raba za AirForce zinazouzwa 35 - 50k... ila kuziagiza hadi kukufikia haizidi 15k kila kitu. Sasa kuna sababu zipi za kuuza kwa bei mara 2 au 3? Wanyabiashara wakongwe jueni kabisa kutatokea kina "Niffer" wengi sana na sokoni kutachafuka mno. Mjiandae kisaikolojia.

Ninamshauri Niffer naye asifanye kosa la kuponda bidhaa za wenzake. Apromoti tu bidhaa zake bila kutamka shombo kuhusu wengine. Wafanyabiashara wakongwe wana mbinu nyingi safi na chafu kwahiyo awe makini asije akazimishwa. Ni HATARI. Pia yule boyfriend wa Niffer awekeze zaidi kwenye kukata viuno kitandani maana kwa hali ilivyo Niffer anaenda kuwa mkubwa zaidi na kuna mabaradhuli wenye hela hawawezi kuona mtoto mkali kama yule wakaacha apite hivihivi.
 
Wamemkalia kooni tu dada wa watu bure,, sidhani kama mtu kua na biashara zaidi ya moja ni makosa maana kila mtu anaangalia kwa wakati huo fursa zinapatikana upande upi.. Halafu wanaomsema wenyewe ni watu wazima kiasi kwamba ilibidi tu wajiangalie waone dogo anawapita kwenye kitu gani ( kama ni kwenye kutangaza biashara yake au bei) na wao waone wanakuja na mbinu gani ya ushindani kwenye biashara...

But kwenye biashara kukiwa na hekaheka kama hivi ndio soko linachangamka biashara zinatembea.. Aendelee tu kuwannyoosha ila asiharibu na za wenzake ( kama wanavyodai lakini)
 
Kwa wiki iliyopita mitandaoni hasa Instagram na Twitter kuliibuka mjadala mkali ikiwemo vita ya maneno miongoni mwa wafanyabiashara wa mjini Dar es Salaam. Baadhi ya wafanyabiashara walimtupia lawama Bi Niffer ambaye ni mfanyabiashara mdogo anayekuwa kwa kasi ya ajabu. Wanamtuhumu Niffer kurukia kila biashara huku akivunja miiko mingi ya biashara hizo. Wanadai Niffer amekuwa akiharibu bei za soko kwa makusudi huku akiponda bidhaa za wafanyabiashara wengine.

Hili suala limekuwa na mitazamo mingi. Watu wengi wamesema Niffer yuko sahihi kwa sababu ni mbunifu na hakuna sheria anayovunja. Upande mwingine unadai sio vema Niffer kuanika bei zake ndogo hadharani kwa sababu zinawaharibia wenye maduka ambao wanalipa kodi nyingi sana. Binafsi baada ya kufuatilia hili sakata nimeona ni sahihi 100% Niffer kuendelea kuwapelekea moto hao wakongwe wasiotaka kubadilika. Pia yeye kuuza vitu kwa bei ya chini ni msaada kwa wananchi wengi. Niffer ni mjasiriamali kamili anayetatua changamoto za raia huku raia wakiweka pesa kwenye wallet ya Niffer.

Ukitoa wauza nguo kwa bei ya jumla hao wafanyabiashara wengine ni wapigaji kwa kuweka bei za juu kupitiliza. Nina ushahidi usiotia shaka. Kwa mfano raba za AirForce zinazouzwa 35 - 50k... ila kuziagiza hadi kukufikia haizidi 15k kila kitu. Sasa kuna sababu zipi za kuuza kwa bei mara 2 au 3? Wanyabiashara wakongwe jueni kabisa kutatokea kina "Niffer" wengi sana na sokoni kutachafuka mno. Mjiandae kisaikolojia.
Uyo niffer sio wa kwanza kufanya biashara ya hivyo hata wakina faiza walianza hivyo siku nyingi tu na sasa hawasikiki na wapo wengine wengi tu wanaagizia watu bidhaa nje tena kwa bei nafuu mfano Haika yule dada wa businesseagle, chidd mapenz, kim china na wengineo wengi.

Shida ya niffer ni kutangaza bidhaa za wengine ni FAKE ilihali yeye mwenyewe anaenda nunua bidhaa hizo hizo anazoziita fake na kuziuza kwa bei yake.
 
Uyo niffer sio wa kwanza kufanya biashara ya hivyo hata wakina faiza walianza hivyo siku nyingi tu na sasa hawasikiki na wapo wengine wengi tu wanaagizia watu bidhaa nje tena kwa bei nafuu mfano Haika yule dada wa businesseagle, chidd mapenz, kim china na wengineo wengi.

Shida ya niffer ni kutangaza bidhaa za wengine ni FAKE ilihali yeye mwenyewe anaenda nunua bidhaa hizo hizo anazoziita fake na kuziuza kwa bei yake.
Niffer anawazidi hao wengine kwa mbali sana kwenye marketing skills. Naunga mkono yeye kutorusha shombo kuhusu biashara za wengine.
 
Wamemkalia kooni tu dada wa watu bure,, sidhani kama mtu kua na biashara zaidi ya moja ni makosa maana kila mtu anaangalia kwa wakati huo fursa zinapatikana upande upi.. Halafu wanaomsema wenyewe ni watu wazima kiasi kwamba ilibidi tu wajiangalie waone dogo anawapita kwenye kitu gani ( kama ni kwenye kutangaza biashara yake au bei) na wao waone wanakuja na mbinu gani ya ushindani kwenye biashara...

But kwenye biashara kukiwa na hekaheka kama hivi ndio soko linachangamka biashara zinatembea.. Aendelee tu kuwannyoosha ila asiharibu na za wenzake ( kama wanavyodai lakini)
Niffer kawazidi mbinu
 
Hamna akili yoyote ya ziada aliyo nayo niffer kwenye biashara ya uagizaji zaidi ya makelele tuu ambayo yatamletea shida, watu wanalipa Kodi, OCs na tozo za kutosha kuendesha biashara hawezi kufanana na huyo niffer anaechukua vi order kadhaa wanaingiza kimagumashi kisha wanauza bila efd, ajitafakari
 
Hamna akili yoyote ya ziada aliyo nayo niffer kwenye biashara ya uagizaji zaidi ya makelele tuu ambayo yatamletea shida, watu wanalipa Kodi, OCs na tozo za kutosha kuendesha biashara hawezi kufanana na huyo niffer anaechukua vi order kadhaa wanaingiza kimagumashi kisha wanauza bila efd, ajitafakari
Wakati unasema hivyo tayari binti mdogo anasukuma ndinga kali sana. Kuhusu efd na kodi zingine anaweza elekezwa na mambo yakamwendea fresh tu. Yule binti kwa sasa anakimbiza sana.
 
Biashara ni vita kila mtu apambane na yake sioni kosa la Niffer kabisa kwanza amesaidia maana wengi huweki bei za ajabu,huyo Rest kafanya biashara ngapi au ana biashara ngapi?? Mnataka mtu afanye biashara mnavyotaka nyie Khaa!
Niffer aachwe aisee auze kila kitu tutamsapoti tu Ndio ashakuwa mwamposa wa kike
 
Tukizungumzia biashara tena biashara za Tanzania ni vurugu mechi patashika nguo kuchanika yani fouls za kutosha hakuna haki kwenye angles zote, Kwaiyo Bi niffer azidi kupambana tu kwa upande wake na KILA MTU ASHINDE MECHI ZAKE.

vita ni vita Muraaah!
 
Wakati unasema hivyo tayari binti mdogo anasukuma ndinga kali sana. Kuhusu efd na kodi zingine anaweza elekezwa na mambo yakamwendea fresh tu. Yule binti kwa sasa anakimbiza sana.
Kuhusu kusukuma ndinga kali sioni shida ni mafanikio yake na hata mimi supendi umasikini. Shida yangu ni kuwaponda wafanyabiashara wengine kuwa wanauza fake na bei ghali, ndio nnapopingana nae wakati huo huo operation zao ziko tofauti, bei haziwezi kufanana
 
Kuhusu kusukuma ndinga kali sioni shida ni mafanikio yake na hata mimi supendi umasikini. Shida yangu ni kuwaponda wafanyabiashara wengine kuwa wanauza fake na bei ghali, ndio nnapopingana nae wakati huo huo operation zao ziko tofauti, bei haziwezi kufanana
Kuhusu kuwaponda wafanyabiashara wenzake hata mimi siungi mkono kabisa kwasababu kitakachofuata sio kitu kizuri. Nimemshauri binti apromoti biashara yake bila kuweka pua yake kwenye biashara za wengine.
 
Wakati akipambana na vita ya kimwili awe makini pia na vita ya kiroho vinginevyo soon atalamba mchanga.
Haya maneno nilishaambiwa kipindi ninaanza biashara.

Na nimeendelea kuambiwa zaidi ya mara elfu,
Biashara ni sayansi, yaani zama hizi watu wenye maduka makubwa wanatengeneza Apps za ku locate bidhaa zilipo na zimebaki kiasi gani ndani ya duka wewe unaendelea kusema mambo ya kiroho.

wacha mapambano yaendelee.
 
Back
Top Bottom