imhotep
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 61,236
- 98,404
Kama ingelikuwa ni kweli, basi angekuwa nyoka muoga kuliko wote duniani.Kwa kuongezea Black Mamba hutumia kasi yake ya ajabu kukimbia hatari,na si kwa ajili ya kukimbiza windo
Kama ingelikuwa ni kweli, basi angekuwa nyoka muoga kuliko wote duniani.Kwa kuongezea Black Mamba hutumia kasi yake ya ajabu kukimbia hatari,na si kwa ajili ya kukimbiza windo
Usije ukamchangaya na Boomslang maana wanafanana sana.Hao wanaitwa Spotted bush snake!! wanakua na rangi ya kijani lakin na vidoa doa vyeusi hawa HAWANA SUMU
Huyo jamaa anakamata koboko wadogo wadogo tena kila ukimuita unamlipa dola arobaini lakini koboko waliokomaa wako nchi ya Zimbabwe na Msumbiji.Kuna kipindi flani, kwenye channel ya 'Nat geo wild' kinaitwa 'snake in the city' jamaa mmoja na demu wake, wanawakamata hao akina black mamba 'kama hawana akili nzuri.
Nutnux1. TAIPAN WA ARDHINI:
Nyoka huyu ni wa kwanza kuwa na sumu kali duniani, anaeishi ardhini tu. aking'ata kitu chochote hutoa sumu kiasa cha milligram110 iliyo na uwezo wa kuua binadamu 100 au panya 250,000.
2. NYOKA WA BRAUNI KUTOKA MASHARIKI:
Nyoka huyu anayepatikana kwa wingi Australia anashikilia nafasi ya pili kwakuwa na sumu kali sana ambayo 1/14,000 ya tone la sumu humuua mtu mzima kwa muda mfupi, anasifika pia kwa kuwa na spidi sana ya kukimbia.
3. KRAIT WA BLUU
Nyoka huyu anayepatikana Kusini mashariki mwa bara la Asia na indonesia anashika nafasi ya tatu kwa kuwa na sumu kali, 50% ya kung'ata kwake husababisha kifo au kuparalyse na ni vigumu kupona hata kwa matumuizi ya dawa ya kumaliza makali sumu ya nyoka(Antivenin).
Nyoka huyu pia ana sifa ya kuwashambulia na kuwauwa nyoka wenzake hata wa jamii yake
4. TAIPAN
Nyoka huyu anaeshikilia nafasi ya nne anaptaikana nchini Australia, ana sumu kali iliyo na uwezo wa kuua nguruwe wa guinea 12,000, pia katika ung'ataji wake husababisha kifo ndani ya lisaa limoja.
5. BLACK MAMBA
Nyoka huyu anayepatikana sehemu nyingi ya Africa anashika nafasi ya tano huku akiwa anaogopeka sana kwa ukali wa sumu yake na ushambuliaji wake.
Ana uwezo wa kushambulia kwa kurusha sumu hadi mara 12 kwa wakati mmmoja ambayo huweza kuuwa binadamu 10 hadi 25 kwa wakati mmoja. Ung'ataji wake mmoja hutoa sumu kiasi cha milligram 100 hadi 120.
Huwa anasifika sana duniani kwa kuwa nyoka wa kwanza mwenye mbio ardhini akiwa na uwezo wa kukimbia kilometa 20 kwa lisaa limoja.
Nyoka huyu anapatikana pia Tanzania hivyo si vibaya tukimjua zaidi ili ukisikia yupo sehemu utafute namna ya kujihami nae...
MAMBAS ni aina ya nyoka wakali wapatikanao ktk dunia ya leo. Ni nyoka wenye sumu kali na wenye kasi ktk mwendo na wana sifa ya kutaga mayai (oviparous).
Kuna aina mbili za mambas :
1. GREEN MAMBAS.
2. BLACK MAMBAS.
Green mamba wanasumu aina ya NEUROTOXIC na HAEMOTOXIC. Wanaishi miaka 12 hadi 14 (makadirio kulingana na takwimu za sayansi) wanataga mayai na kuanguliwa kwa siku 80 hadi 90.
BLACK MAMBA pia wanauwezo wa kupanda miti wakati wakitafuta chalula na wanaurefu kati ya sentimita 220 hadi 320. Ni kati ya nyoka wenye sumu kali wapatikanao Afrika. Wanataga mayai kati ya 12 na 18,na kuangua kati ya siku 80 hadi tisini.
Mambas ni nyoka wakali na wenye kung'ata zaidi ya mara moja kwa sababu meno yao hayang'oki wakati wakigonga kitu. Meno yanayong'oka kwa nyoka yanaitwa FRONT FANGED MOVABLE na yasiyong'ooka yanaitwa FRONT FANGED FIXED.
Iwapo nyoka hawa wata kung'ata utaweza kuishi kati ya dakika 20 (kwa mujibu wa utafiti) Na kupoteza maisha...
Una bahati sana ungezubaa angekuja kukusimamia usoni huku amepanua mdomo wake mweusi.Nakumbuka nilikuwa natoka kuokota kuni porin huko kijijin (kwa wa dar kuni ni miti iliyokauka kwa ajil ya kupikia) nimejitwika kuni zangu nateremka kurudi mara naona nyasi zinatingishika kwa kas mara paaap naona nyoka mrefu anakimbia balaa kuja upande wangu sikutaka kujiuliza nikatupa mzigo chini hizo spidi nilizotoka nazo sikumbuk ila nikajikuta niko kulekule nilikookotea kuni kuwafuata wengine akiri haikuwa ya kawaida mpaka nikapewa togwa (juice ya mahindi na ulezi)
Black Mamba kamwe hakimbii Hatariii NEVER... Jamaa huwa anaikimbiza hatarii!! Afuu koboko mkubwa anaweza toa sauti kubwaa kama kufoka hivi... Wanyama wakiisikia mbioo... Ni nyokaa anaegongaa bila Kuacha meno soo anaweza gonga watu hata 100 kwa muda mchache sanaaa...Na speed yake sio ya nchi hiiKama ingelikuwa ni kweli, basi angekuwa nyoka muoga kuliko wote duniani.
Huyu anaweza kuwa kipalanonga huyu.
Shida yako unaangalia sana TV.koboko aliyekomaa anakugonga na utaalam wako ndio unsishia hapo hapo.Njia ulizotoa sio sahihi black mamba unamkamata nipe fimbo nakukamatia mamba bila kumjeruhi wala kumuua
Ndege wanamjuaView attachment 724533
Koboko huwa na miujiza fulani hivi,tazama huyo ndege anavyomshangilia.
Yo makoboko kweli(ni jina la utani la hcho kijiji)mayai ya black mamba ni matamu sana, ila upatikanaji wake ndio changa moto. mie kuna sehemu tulikua kambi maeneo ya tabora tukawa pale ambapo tunapumzika , kwa juu yake palikua ni makazi yake jioni, wakati anarudi nae kupumzika ibabi muiache njia kwa mda apite , tofauti na hapo ugovi unakua umeutafuta mwenyewe na mmoja tulimuua
Nyoka wa kijani wapo aina kadhaa,wengine hawana sumu kabisa. Ila huyo green mamba ni shida. Anahasira za hatari sana pia akipanua mdomo ndani utaona ni mweusi. Hyo ndo tofauti yake na hao wakijani wengineWee unamjuwa Green mamba lakini? Ni hatari sana
Hata waSouth wana kikosi cha special forces kinaitwa koboko.Sio huko tu hata hapa nyumban tanzania ndani ya JWTZ kuna kikosi maalumu( Special force) Kinaitwa BLACK MAMBA( KOBOKO) ndicho kilichowezesha kumuondoa Idd Amin na majeshi yake TZ na UG...na Pia ndicho kilichoongoza mapigano ya kukiondoa kikundi naweza kukiita cha wahauni (M23) huko Congo chini ya mwanaume Maj gen Mwakibolwa!!!