Wafahamu nyoka hatari Zaidi duniani

Wafahamu nyoka hatari Zaidi duniani

mayai ya black mamba ni matamu sana, ila upatikanaji wake ndio changa moto. mie kuna sehemu tulikua kambi maeneo ya tabora tukawa pale ambapo tunapumzika , kwa juu yake palikua ni makazi yake jioni, wakati anarudi nae kupumzika ibabi muiache njia kwa mda apite , tofauti na hapo ugovi unakua umeutafuta mwenyewe na mmoja tulimuua
Huyu ni nyoka mwenye hadithi nyingi sana na anaegopwa kuliko wote kwa sababu tofauti na nyoka wengine ambao hujihami, Black Mamba hua anashambulia. kwa Tanzania nyoka hawa wapo sana katika mapori ya Tabora na Mwanza na jina lake la asili ni Koboko. Siku zote nasema nyoka huyu angekua anapatika ulaya wazungu wangempa promo sana ila sisi waswahili tunawaua sana kiasi ambacho sasa hivi ni nadra kumpata Black Mamba mwenye ukubwa wa chatu mkubwa
 
mayai ya black mamba ni matamu sana, ila upatikanaji wake ndio changa moto. mie kuna sehemu tulikua kambi maeneo ya tabora tukawa pale ambapo tunapumzika , kwa juu yake palikua ni makazi yake jioni, wakati anarudi nae kupumzika ibabi muiache njia kwa mda apite , tofauti na hapo ugovi unakua umeutafuta mwenyewe na mmoja tulimuua
Yanaliwa
 
Ni kweli, kwa mfano mie nilikua maeneo ya igombe kule tabora, makoboko ni mengi kweli sema watu wa maeneo ya pale hawawasumbui sana hao nyoka, kunakua kama na ka amani fulani ila sio 100%, mwanzo nilikuaga naogopa sana wananiambia wapo nyuma ya eneo ambalo hua nalala maana kulikua na kichunguu kikubwa sana na mti mkubwa ila badae nikazoe tu, ila kuna mda wanapo kua wanatoka kwenda kuota jua na mawindoni na wanapo rudi ni lazima kujiepusha na maeneo ya makazi yao na njia wanazo tumia.

Huyu ni nyoka mwenye hadithi nyingi sana na anaegopwa kuliko wote kwa sababu tofauti na nyoka wengine ambao hujihami, Black Mamba hua anashambulia. kwa Tanzania nyoka hawa wapo sana katika mapori ya Tabora na Mwanza na jina lake la asili ni Koboko. Siku zote nasema nyoka huyu angekua anapatika ulaya wazungu wangempa promo sana ila sisi waswahili tunawaua sana kiasi ambacho sasa hivi ni nadra kumpata Black Mamba mwenye ukubwa wa chatu mkubwa
 
ila tabora, ule mkoa una manyoka mengi sana. kipindi nimehama kutoka huko kuja huku, hadi nikikua na miss kuona nyoka, nilikua nimezoea haipiti siku bila kukimbizana na swila au manyoka mengine mengine... ila huku dar kimyaa kabisa hakuna kabisa oya oya za nyoka na mijoka

Huyu ni nyoka mwenye hadithi nyingi sana na anaegopwa kuliko wote kwa sababu tofauti na nyoka wengine ambao hujihami, Black Mamba hua anashambulia. kwa Tanzania nyoka hawa wapo sana katika mapori ya Tabora na Mwanza na jina lake la asili ni Koboko. Siku zote nasema nyoka huyu angekua anapatika ulaya wazungu wangempa promo sana ila sisi waswahili tunawaua sana kiasi ambacho sasa hivi ni nadra kumpata Black Mamba mwenye ukubwa wa chatu mkubwa
 
Black mamba si nyoka mkali Ni miongon mwa mamba wapole Sana lkn pale tu utakapo mletea usumbufu Hapo Hapo huwa ana react
Black mamba is a territorial snake brother, akiwa porini ukiingia katika orbit yake anatoka huko alipo anakufata, wameshaua ng'ombe na mifugo kadhaa sema siku hizi wale Black Mamba wakubwa hawapo tena au wapo wachache sana na hawa wadogo wanakua sio aggressive kiviile
 
Black mamba is a territorial snake brother, akiwa porini ukiingia katika orbit yake anatoka huko alipo anakufata, wameshaua ng'ombe na mifugo kadhaa sema siku hizi wale Black Mamba wakubwa hawapo tena au wapo wachache sana na hawa wadogo wanakua sio aggressive kiviile
N kwel mkuu ila minina experience nilipewa warning moja Matata af wakapita zao bila kunidhur walkuwa wawil
 
Tena tafiti zao wanazofanya wanaangalia tu ukali wa sumu lakini hawasemi kwa ukali (aggressiveness) wa nyoka yupi ni most deadly, wangemkuta Koboko ni nambari moja
Ni kweli kabisa, kutana na hao wengine wote Ila sio koboko, ukizisoma tafiti zao, hao nyoka wengine hujaribu kuepusha shari hata ukikutana nae.
Koboko yeye huepusha shari asikutane na wewe kabisa, Ila sasa akikuona tu, hajui kama uliingia anga zake kwa bahati mbaya ama la, yeye ni tifu kwa kwenda mbele. Kwa kifupi, tofauti na hao wengine, yeye ukikutana nae sali sala zako za mwisho.
 
1. TAIPAN WA ARDHINI:

Nyoka huyu ni wa kwanza kuwa na sumu kali duniani, anaeishi ardhini tu. aking'ata kitu chochote hutoa sumu kiasa cha milligram110 iliyo na uwezo wa kuua binadamu 100 au panya 250,000.

2. NYOKA WA BRAUNI KUTOKA MASHARIKI:

Nyoka huyu anayepatikana kwa wingi Australia anashikilia nafasi ya pili kwakuwa na sumu kali sana ambayo 1/14,000 ya tone la sumu humuua mtu mzima kwa muda mfupi, anasifika pia kwa kuwa na spidi sana ya kukimbia.

3. KRAIT WA BLUU

Nyoka huyu anayepatikana Kusini mashariki mwa bara la Asia na indonesia anashika nafasi ya tatu kwa kuwa na sumu kali, 50% ya kung'ata kwake husababisha kifo au kuparalyse na ni vigumu kupona hata kwa matumuizi ya dawa ya kumaliza makali sumu ya nyoka(Antivenin).
Nyoka huyu pia ana sifa ya kuwashambulia na kuwauwa nyoka wenzake hata wa jamii yake

4. TAIPAN

Nyoka huyu anaeshikilia nafasi ya nne anaptaikana nchini Australia, ana sumu kali iliyo na uwezo wa kuua nguruwe wa guinea 12,000, pia katika ung'ataji wake husababisha kifo ndani ya lisaa limoja.

5. BLACK MAMBA

Nyoka huyu anayepatikana sehemu nyingi ya Africa anashika nafasi ya tano huku akiwa anaogopeka sana kwa ukali wa sumu yake na ushambuliaji wake.
Ana uwezo wa kushambulia kwa kurusha sumu hadi mara 12 kwa wakati mmmoja ambayo huweza kuuwa binadamu 10 hadi 25 kwa wakati mmoja. Ung'ataji wake mmoja hutoa sumu kiasi cha milligram 100 hadi 120.
Huwa anasifika sana duniani kwa kuwa nyoka wa kwanza mwenye mbio ardhini akiwa na uwezo wa kukimbia kilometa 20 kwa lisaa limoja.
Nyoka huyu anapatikana pia Tanzania hivyo si vibaya tukimjua zaidi ili ukisikia yupo sehemu utafute namna ya kujihami nae...
MAMBAS ni aina ya nyoka wakali wapatikanao ktk dunia ya leo. Ni nyoka wenye sumu kali na wenye kasi ktk mwendo na wana sifa ya kutaga mayai (oviparous).
Kuna aina mbili za mambas :
1. GREEN MAMBAS.
2. BLACK MAMBAS.
Green mamba wanasumu aina ya NEUROTOXIC na HAEMOTOXIC. Wanaishi miaka 12 hadi 14 (makadirio kulingana na takwimu za sayansi) wanataga mayai na kuanguliwa kwa siku 80 hadi 90.
BLACK MAMBA pia wanauwezo wa kupanda miti wakati wakitafuta chalula na wanaurefu kati ya sentimita 220 hadi 320. Ni kati ya nyoka wenye sumu kali wapatikanao Afrika. Wanataga mayai kati ya 12 na 18,na kuangua kati ya siku 80 hadi tisini.
Mambas ni nyoka wakali na wenye kung'ata zaidi ya mara moja kwa sababu meno yao hayang'oki wakati wakigonga kitu. Meno yanayong'oka kwa nyoka yanaitwa FRONT FANGED MOVABLE na yasiyong'ooka yanaitwa FRONT FANGED FIXED.
Iwapo nyoka hawa wata kung'ata utaweza kuishi kati ya dakika 20 (kwa mujibu wa utafiti) Na kupoteza maisha...
Ebhana huyu black mamba nimesoma tips kadhaa kuwa ni nyoka hatari sana, kwanza ana sumu kali, pili ana uwezo wa kukimbia umbali mrefu sana, kuruka toka umbali mrefu na kusimama kwa kutumia mkia wake hivyo kuweza kugonga vitu vilivyo kimo cha juu mfano ng'ombe, mbuzi n.... Ni nyoka mkorofi sana na ambaye ukianzisha vita dhidi yake ni lazima ummalize la sivyo yeye anakumaliza..... Sumu yake ya Neurotoxin inaathiri mfumo wa never katika ubongo ndio maana akikung'ta within 20 you gone
 
Ni kweli kabisa, kutana na hao wengine wote Ila sio koboko, ukizisoma tafiti zao, hao nyoka wengine hujaribu kuepusha shari hata ukikutana nae.
Koboko yeye huepusha shari asikutane na wewe kabisa, Ila sasa akikuona tu, hajui kama uliingia anga zake kwa bahati mbaya ama la, yeye ni tifu kwa kwenda mbele. Kwa kifupi, tofauti na hao wengine, yeye ukikutana nae sali sala zako za mwisho.

Mkuu. Black mamba na Cobra mafia wakikutana face to face nani anasurrender kwake?
 
Back
Top Bottom