Waepuke wanawake masikini

Hii mada ni pana sana.. tukianza kuichambua tutapata vimada vidogo vidogo kibwena mzee mwenzangu.
MIe naamini mwanaume ni provider zaidi, mwanamke kwangu aje anitulize mahangaiko ya nafsi na mengineyo, ikitokea ana kipato hiyo ni nyomgeza na kipato chake kisiniharibie yale mahitaji yake kwangu.

Ukisema hivyo mzee mwenzangu tutaangukia kule kule vijana wanaposemaga tutafute pesa, ukiwa na pesa nzuri hata umaskini wa familia yake haukuumizi...
Kuna msenge m1 mtaani alienda kuoa huko mkoani, ile kupeleka mahari kukubaliwa tu, akapigia simu mafundi toka dar, wakapima ghorofa ikaanza kushushwa.. yupo na mkewe wanakula maisha
 
Bora wewe umeongea la maana,
Wanaume wa kizazi hiki no wonder wanaolewa wazazi sijui walikosea wapi!?
Wanawake wa sasa mnajiita strong women, independent women, wapambanaji na majina mengine mengi ya kishujaa cha kushangaza mkiondolewa kwenye kunufaika na pesa au mali za mwanaume mnaamisha goli.

Katika hali ya kawaida strong and independent woman atakubaliana na wazo la mwanaume na mwanamke wote kuanza wakiwa na kitu cha kuweka mezani bila mmoja kutarajiwa kuwa elevator wa mwenzake. Lakini kinachotokea ni tofauti. Uko wapi huo u-independent woman wenu mnaojinasibu nao.
 
Hela ya mwanamke hauhitaji wewe, anahitaji yeye. Mwanamke kuwa na kipato hamfanyii favor mtu yoyote, ni kwa ajiri yake. Tuache kuwaaminisha wanawake kwamba wanastahili noble prize kwa kubeba majukumu yao binafsi kama watu wazima.

Masuala kama mama bora na utulivu wa nafsi ni subjective hakuna guarantee kwamba utayapata kwa mwenye kipato au masikini. Lakini masikini ni liability kwa sababu anakuja ku-consume tu bila kuchangia chochote
 
ndio maana nikasema mada pana, inabidi tudadavue kila sehemu..
Ukiweka vyote costant, kasoro mali na akili, mwanamke mwenye akili anaejitambua ni bora kuliko mwenye kipato asiejielewa
 
Suala la mwanaume kuwa provider naliamimi pia, lakini lazima tukubaliane kwamba ni provider kwa mke sio kwa girlfriend. Wajibu wa ku-elevate maisha ya girlfriend ni wa wazazi wake

Pesa tutafute kwa sababu inatupa uhuru na access ya mambo mengi. Bado ukijumlisha hayo yote haiondoi ukweli kwamba masikini ni liability especially kwa kijana ambae bado yupo kwenye building stage. Ukisema wewe hauna shida na hiyo liability haimaanishi kwamba haipo.
 
Kitakwimu 80% ya watanzania ni masikini wanaotegemea kilimo kisichokuwa na tija kuendesha maisha.

Kama wote tutafata hicho ulichokiandika unaweza kukuta hata kwenye familia yenu au ukoo hakuna atakaeolewa.
Swala la mahusiano ni pana asee sio pesa ,au uzuri au tabia kuna mengi zaidi ya hayo.
 
Hapa mie nilikuwa nazungumzia mke, sio girlfriend...
 
ndio maana nikasema mada pana, inabidi tudadavue kila sehemu..
Ukiweka vyote costant, kasoro mali na akili, mwanamke mwenye akili anaejitambua ni bora kuliko mwenye kipato asiejielewa
Kitendo cha kuwa mtu mzima, hasomi hana kipato wala chochote kinachoendelea kwenye maisha yake that's means she failed even to figured out her life, sasa hiyo akili yake iko wapi. Ili kudhihirisha ana hiyo akili inatakiwa umkute kuna kitu ashaanza kukifanya otherwise una-gamble tu
 
Aahh, kwahiyo akili yako inakwambia wasiofanikiwa wote ni wajinga?
 
Umasikini wa kushindwa hata kujitafutia mahitaji binafsi katika mahali unapoishi haufiki hiyo 80%.
 
Aahh, kwahiyo akili yako inakwambia wasiofanikiwa wote ni wajinga?
Sio wajinga mkuu. Exception ipo kwenye kila kitu. Nachoongolea ni probability. Kwenye kundi la watu ambao tayari washa-figure out maisha yao kuna uwezekano mkubea wa kukutana na werevu wengi kuliko kundi ambalo bado halina uelekeo wowote kimaisha. Kipimo cha kwanza kujua akili ya mtu ni namna anavyoweza kuya-handle maisha yake.
 
Umeongea kama mwanaume.

Hii mambo sijui ya kutaka kushea na mwanamke ndo inaleta shida kwenye ndoa nyingi sasa hivi. Ile dhana ya mwanaume kuwa mmiliki na kiongozi inapotea sana kwa mawazo kama ya mleta mada.
 
Umeongea kama mwanaume.

Hii mambo sijui ya kutaka kushea na mwanamke ndo inaleta shida kwenye ndoa nyingi sasa hivi. Ile dhana ya mwanaume kuwa mmiliki na kiongozi inapotea sana kwa mawazo kama ya mleta mada.
Maisha yanabadilika dhana za kuishi haziwezi kuwa vilevile. Mwanamke wa leo kapewa access za elimu na kipato. Ukipewa elimu maana yake unajengewa uwezo wa kuyatafsiri mazingira ili kupata majibu ya changamoto zinazokunguka. Ukiwa na kipato maana yake automatically unaondolewa kwenye kundi la watu tegemezi.

Embu niambie kuna maana gani ya kuwasomesha mabinti zetu na kuwawezesha wawe na kipato kama mwishoe tutakuja kumbebesha mwanaume mzigo wa kutafuta majibu ya changamoto za mwanamke pamoja na kumtatulia matatizo yake kifedha.

Nini faida ya kumsomesha na kumwezesha mtoto wa kike ikiwa mwisho wa hayo yote ni sharti awe tegemezi kwa mwanaume?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…