Wadau wa kilimo hivi mwaka huu kuna maonyesho ya kilimo nanenane?

HOPEfull

JF-Expert Member
Apr 8, 2021
1,726
2,082
Habari humu.
Kichwa cha habari chahusika.Sioni shamrashamra za hii sikukuu pia hata matangazo sisikii.Je inawezekana na mwaka huu maonesho yakapotezewa na ukizingatia kuna kazi ya sensa na makazi.

Ni maonesho muhimu sana kwa wakulima na wafugaji na huwa yanatoa fursa kubwa za kibiashara kwa watu wengi kutoka sehemu mbalimbali.

Mwaka jana kulikuwa na sababu zilitolewa za kutofanyika kwa maonesho haya sasa sijui mwaka huu.
Kilimo ndio sehemu ya ajira kwa watanzania wengi milioni 60 na zaidi sasa itakuwa kitu cha ajabu kutoyawekea umuhimu haya maonesho.

Naona kama kuna danadana kuhusu kitu hiki muhimu
Nchi yetu haina uwezo wa kutoa ajira kwa watu wake wengi hatuna viwanda vya kutosha na vingi vimekufa hivyo kilimo ndio kiwanda pekee kilichobaki cha kutoa ajira kwa wananchi walio wengi.

Nchi za ulaya na asia zinajivunia uwezo wao wa viwanda vingi vya uzalishaji na kupunguza tatizo la ajira tofauti na nchi zetu za kiafrika vijana hawana kazi wasomi wanazunguka na bahasha kutwa.. panya rodi mtaani wanaibuka kila siku hii ni kutokana na kutokuwa na ajira na kazi ambazo zinatokanana viwanda vya uzalishaji bidhaa.

Juzi nimesikia kuna kiwanda cha sukari cha mfanyabiashara mmoja kinatarajia kufunguliwa ni taarifa nzuri hiyo kwa taifa letu vijana watapata ajira kwa kiasi angalau ingawa bado tatizo ni kubwa.

Hayati JPM alisisitisa sana suala la viwanda aliona umuhimu wake kwa watanzania basi serikali nayo isisitize suala la kilimo kama ajira ya watu wengi naona kama hakuna nguvu kubwa huku.
 


Walisema Yatakuwepo

Ila Morogoro Naona Ukarabati Unaendelea Lakini Dodoma Kimya
 
Ndio yapo, na kitaifa yanafanyika Mbeya kwenye viwanja vya John Mwakangale.
Huyo hapo chini ni mkuu wa mkoa Juma Homera anakukaribisha.
Anasema Karibuni sana
Screenshot_20220716-103426_Instagram.jpg
 
Naibu Waziri wa kilimo bashe wakati yupo bungeni kama mbunge alikuwa ni mmoja wa wabunge wenye michango yenye tija sana hasa kwenye kuishauri wizara ya fedha na mipango nakumbuka mheshimiwa mpango wakati akiwa waziri wa fedha alikuwa akimsikiliza kwa makini sana, sass sijui baada ya kupewa unaibu uwaziri wa kilimo sijui huko anatusaidiaje wakulima yale mawazo yake kule bungeni na ule ushauri aliokuwa anatoa sijajua bado anayo au amesahau tayari shida.
 
Habari humu.
Kichwa cha habari chahusika.Sioni shamrashamra za hii sikukuu pia hata matangazo sisikii.Je inawezekana na mwaka huu maonesho yakapotezewa na ukizingatia kuna kazi ya sensa na makazi.
Ni maonesho muhimu sana kwa wakulima na wafugaji na huwa yanatoa fursa kubwa za kibiashara kwa watu wengi kutoka sehemu mbalimbali.

Mwaka jana kulikuwa na sababu zilitolewa za kutofanyika kwa maonesho haya sasa sijui mwaka huu.
Kilimo ndio sehemu ya ajira kwa watanzania wengi milioni 60 na zaidi sasa itakuwa kitu cha ajabu kutoyawekea umuhimu haya maonesho..
Naona kama kuna danadana kuhusu kitu hiki muhimu.
Nchi yetu haina uwezo wa kutoa ajira kwa watu wake wengi hatuna viwanda vya kutosha na vingi vimekufa hivyo kilimo ndio kiwanda pekee kilichobaki cha kutoa ajira kwa wananchi walio wengi.

Nchi za ulaya na asia zinajivunia uwezo wao wa viwanda vingi vya uzalishaji na kupunguza tatizo la ajira tofauti na nchi zetu za kiafrika vijana hawana kazi wasomi wanazunguka na bahasha kutwa.. panya rodi mtaani wanaibuka kila siku hii ni kutokana na kutokuwa na ajira na kazi ambazo zinatokanana viwanda vya uzalishaji bidhaa.

Juzi nimesikia kuna kiwanda cha sukari cha mfanyabiashara mmoja kinatarajia kufunguliwa ni taarifa nzuri hiyo kwa taifa letu vijana watapata ajira kwa kiasi angalau ingawa bado tatizo ni kubwa.
Hayati Jpm alisisitisa sana suala la viwanda aliona umuhimu wake kwa watanzania basi serikali nayo isisitize suala la kilimo kama ajira ya watu wengi naona kama hakuna nguvu kubwa huku.
Yapo, kitaifa yatafanyika Mbeya, nenda kauze chips, mishikaki na bia.
 
Naibu Waziri wa kilimo bashe wakati yupo bungeni kama mbunge alikuwa ni mmoja wa wabunge wenye michango yenye tija sana hasa kwenye kuishauri wizara ya fedha na mipango nakumbuka mheshimiwa mpango wakati akiwa waziri wa fedha alikuwa akimsikiliza kwa makini sana, sass sijui baada ya kupewa unaibu uwaziri wa kilimo sijui huko anatusaidiaje wakulima yale mawazo yake kule bungeni na ule ushauri aliokuwa anatoa sijajua bado anayo au amesahau tayari shida.
Mkuu, amka.
Hussein Bashe ni waziri wa kilimo, sio naibu waziri tena. Naibu wake anaitwa Anthony Mavunde.
 
Mkitaka maonesho yenu yawe na attention waalikeni wakina shilole,stevenyerere waimba singeli konde waiteni hapo muwape airtime
Wakina lokole kuwepo na umbeaumbea,hapo mtatiliwa jichoo

Ova
 
Back
Top Bottom