Habari wapendwa,
Wadada leo naomba tujikumbushe kitu kidogo hapa :- Ni kuhusu kuchagua watu wa kuwa nao kwenye mahusiano mf: -kumezuka wimbi la wasichana kupenda kutembea na waume za watu kisa wapate pesa za kujikimu kimaisha kwa upande wangu mimi naona tunakosea sana hiyo tabia na kwanza utachelewa sana maisha kwa kupenda vya dezo mwisho wa siku vitakutokea puani wewe msichana mdogo umeng'ang'ana na mizee isiyojiheshimu kisa anakupa hela na bora hata iwe hela sasa 50000 huoni kama ni dharau?
Yani kakuona jalala la kumwagia taka mwili wake puu! Kwanini wadada tusijikite katika kutafuta maisha? Mume wa mtu akikutongoza ujue kakuona wewe ni dastibini zile za barabarani ambazo kila mpita njia anatupia taka na kwenda zake, yani limtu na mauchafu yake wewe unalikubali maana hakuna malengo yoyote kawashwa huko kaona aje kwako ni bora utulie upate wako asiye na mke ukipenda vya dezo utatumika hadi utakuwa unatembea upande upande.
Tuacheni jamani.