Wadada, jifunzeni kuwa wasiri

Wadada, jifunzeni kuwa wasiri

Mie si-unfollow. Namfollow hadi rafiki yake @Kiranga mmoja hivi, ananikumbusha jinsi gani nimebarikiwa na nisijilalamishe kwa changamoto zinazonikabili 😛😛
Ni ulimbukeni tu na kutojielewa,kama huko Insta siwezi hata kuvumilia nawaunfollow tu...mtu mzima sasa sijui anashow off nini
 
Insta kumejaa watoto tu nashangaa kwanini hata wewe upo kule!
Nipo Insta kwa sababu zangu nyingine kabisa,usikariri na wewe.... au hujui Insta pia watu wafanya biashara,hizi social networks unaweza kuzitumia kwa faida yako take it positive hata kama wengine wanazitumia kihasara
Faida ya pili ni kupata umbea wa bongo muvi,insta sihami ng'oo ila nachagua vya kufatilia
 
Afu wanawake tunajuaga kurushana roho jamani. Kuna mtu anaweza akakusimulia mambo yake Eg, boyfriend wake anavyomtreat kumbe muongo mkubwa. Ndo wale wanaojinunulia hadi zawadi afu anadanganya wenzie kanunuliwa na baby. Aonekane tu yeye ndo anapendwa sana, yeye ndo anaenjoy mapenzi sana mmh, akili kumkichwa. Unaanzaje kusimulia ulivyolala na mtu mmh? What for?

Jamani Kuna wanaojinunulia zawadi??

And yes, kuna tofauti kati ya kupeana ujuzi na kuanza kusimuliana ya private.

Mkuu hii tabia haina ujana wa siku hizi wala zamani....Mi nakaa na watu wazima sana na wadogo kuliko mimi....Naweza kukwambia hao watu wazima ndio wanaongoza kuonyesha picha za faragha na mabinti wadogo kama watoto wao na hao ndio vijana wa zamani,hawafai kabisa.

Trust me wazee wa siku hizi nao whatsapp imewaharibu wanarusha picha za ajabu huwezi amini,tena wana ma group yao kabisa ukiona wanachorusha huwezi amini kama ni watu over 50yrs huko.

Hii ni tabia binafsi tu na ulimbukeni ambao hata wazee watu wazima wanao.

Saluni..... Wanawake watu wazima hizo story sasa!

Sikujua Kuna hadi magroup ya watu umri huo LOL .......labda rahatupu ya Nancy....nishawahi ona wababa mule.

Watu watokwe na ushamba wa media jamani.


Nahisi wameambukizwa na wanaume wa siku hizi....unakuta kijana kapata faraga jana na dada mrembo ...ana mfotoa naikibidi anategesha video kesho yake ana onyesha kwa washirika wake na hata kushea namba ya simu ya mdada na bazazi wengine wakapite huko..
Sasa amongst audience wahabari hizo hata wadada wanakuwepo nahata kuchangia ukosoaji na usifiaji wa hiyo habari na picha.....na aibu ilivyopotea sikuhizi....ndio hao ulosema mleta mada.....ila nahisi ni season tu kama fadhion ..
..hii generation ya millenials ikifika age ya 40. Sidhani kama yatakuwepo yote haya....
Uzuri wa haya maisha kila generation huona wazazi wao ni washamba na kwahiyo kamwe ma teenager wamiaka 20 ijayo hawatafanya upuuzi wowote tunaushuhudia hivi sasa God forbid
Nilisahau version ya wanaume.

Kweli labda watatuona washamba. Au labda ndo itakuwa norm!!! Manake siku hizi picha za couple wamelala kitandani ni nyingi.

Me shida yangu ni kutukanwa tu kwa hawa wadada.
 
Mmh utadhani wanaopendana kweli wanapigaga makelele sasa + kujionyesha. Wao ni mahaba tu na Kila mtu unajua kabisa pale daah, raha tupu

angalau mkionyana nyinyi kwa nyinyi mtaelewana lugha

Tutaambiwa tunaona wivu.... Lakini me sijali.... Kuonyesha uonyeshe mwenyewe, kuachana muachane wenyewe, baadae watu wakikuangalia vibaya u Deal nayo mwenyewe
 
Back
Top Bottom