Wadada, jifunzeni kuwa wasiri

Wadada, jifunzeni kuwa wasiri

Basi nisaidie kuelewa..Kama haujaongea kwa niaba ya watu flani,ina maana umejiongelea mwenyewe ?
Keep your secret to yourself and tell it to God,very common saying....hapo hujaelewa nini?
Nikamalizia kwa kusema maisha ya usiri ni mazuri,sababu unakua na amani...hapo bado hujaelewa,its not my fault sasa kama bichwa lako linajielewesha utakavyo....
 
raha ya mapenzi kuhadithiana we vip, unakaa nayo moyoni kwani ni kiapo hicho?

Nasikitishwa na haya majina nayosikia wadada wanaitwa kila siku; Especially Malaya.

Lunch leo Nimekaa na wanaume wanamsema mrembo flani, mwenye BAHATI ya kuvuta mashine za ukweli, $$$, you know.

Unfortunately bado jamii yetu inakandamiza mwanamke na kumFavour mwanaume. Bado watu wanaona ngono ni kwa ajili ya mwanaume. Mwanamke akutwe bikra lakini mwanaume haijalishi. Hatoulizwa!

Najua wanawake siku hizi wana uhuru kuliko zamani lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa hata zamani wadada walikuwa wanajipa good time tu.

Tatizo wadada sikuhizi hamna siri!

We kila kitu kuhadithia mashosti. Kila utakayetoka naye unaonyesha watu. Kila utakachopewa kila utakapopelekwa(i.e hotels) tutaona picha. Mmoja akianza kusifia game la alilochezewa na fulani na we umo kutaja kina fulani...

Sio tu unasababisha watu ambao bado hawaelewi uhuru wako wakuone vibaya na kukuita majina, Bali hata mwenyewe unakuwa tu mtu wa hovyo. Ukipewa hela unadunduliza ubadilishe smart phone ili tuone shem ni anaKuspoil/mtunzaji, hufikirii maisha baada ya huyo mtu.

Wengine mnapelekwa guest tu lakini tutaona picha ya dinner na breakfast za kizaramo. Mbona wenzenu wanapelekwa 4 stars wamekausha!!

JIFUNZENI USIRI.

Acha love/sex life yako iwe private. Utatuonyesha mumeo. Usihadithie mashosti,ndo wabaya wako hao. Ukipitia/Ukilala hotelini wakati unajua unaishi kwenu/hostel, au unajua unataka kuonekana mtu wa dini, achana na hiyo camera.

Hupungukiwi kitu. Zoea kusema Sina mtu esp. Nyie wadada wa chuo mlio na pressure za kushow off mabwana. Itawasaidia hata kuacha kutumia pesa hovyo.

***Nisije kuambiwa nahamasisha uasherati. Iko chini ya mtu Binafsi kushikilia viwango alivyojiwekea. Kama hayo maandiko hayako akilini mwa huyo dada, hamna utakachoweza kufanya kuzuia...

***you wanna be "that" good lady at 30? Don't get caught at 20.
 
Keep your secret to yourself and tell it to God,very common saying....hapo hujaelewa nini?
Nikamalizia kwa kusema maisha ya usiri ni mazuri,sababu unakua na amani...hapo bado hujaelewa,its not my fault sasa kama bichwa lako linajielewesha utakavyo....
Teh teh..Kumbe huo ni msemo..Basi sawa
 
Tuna EXPECT ukiwa umri fulani u behave kiaina fulani ndio maana tuna discuss hili......
Kweli mkuuu, ndio maana watu sikuhiz tunashangaa umri hauendani na rika
 
We ulijua ni mstari kutoka kwa bible au...sio lazima uelewe kila kitu...teh punguza uzito..
Teh teh..Inabidi nianze diet ya ubongo..Sijakuelewa hata..Nimekubali yaishe tu
 
Kuna mtu haamini kama anaweza kuingia Ramada Resort, akala na akalala bila kucheck in fb. Halafu huu ugonjwa umewapata hadi wanaume, inasikitisha sana.
 
Usiwasingizie wanawake. Kuna baba 40yrs old namuona anarusha picha 30 kwa mpigo fb natamani kumuuliza labda ana simu mpya inapost automatically?
Watu wameamua kuishi maisha yao yote kwenye media. Vitu vya ajabu sana!
Ningeshauri lianzishwe jukwaa la Wanawake humu JF ili mambo kama haya yafanyike humoo


Nanyi wadada kuweni wasili bhana mtu mmefanya mambo yenu huko then unakuja tangaza kwa shogayo , unataka uibiwe au

be smart bhana
 
Kuna mtu haamini kama anaweza kuingia Ramada Resort, akala na akalala bila kucheck in fb. Halafu huu ugonjwa umewapata hadi wanaume, inasikitisha sana.
Ila kuna uhusiano wa karibu sana kati ya camera na jinsia ya kike!
 
kwa muonekano huwa wa jf tutawapoteza wengi sana.. Mpaka watakapokuja kuzoea nadhani itakuwa march Mwakani.. Tunza Siri Yako.. Ibaki kwako na Mungu Wako
 
Teh teh..Inabidi nianze diet ya ubongo..Sijakuelewa hata..Nimekubali yaishe tu
Teh,mwalimu wako wa vidudu alipata shida kwakweli...
Mimi pia sina kipaji cha kumwelewesha mtu bahati mbaya..
 
Usiwasingizie wanawake. Kuna baba 40yrs old namuona anarusha picha 30 kwa mpigo fb natamani kumuuliza labda ana simu mpya inapost automatically?
Watu wameamua kuishi maisha yao yote kwenye media. Vitu vya ajabu sana!
Ni ulimbukeni tu na kutojielewa,kama huko Insta siwezi hata kuvumilia nawaunfollow tu...mtu mzima sasa sijui anashow off nini
 
Ni ulimbukeni tu na kutojielewa,kama huko Insta siwezi hata kuvumilia nawaunfollow tu...mtu mzima sasa sijui anashow off nini
Insta kumejaa watoto tu nashangaa kwanini hata wewe upo kule!
 
Back
Top Bottom