unamaanisha wanaume hawana hii nature au? Jana tu nimetoka kumshangaa mkaka kapost picha ya sebule yake facebook. Kwa kuwa picha haikuambatana na maneno nikafikiri ni interior designer, nikaipenda sana; nilivyoendelea kusoma comments nikagundua ni sebule yake, ndo amehamia dar! Wengine wanapost magari, nyumba na sehemu za starehe wanazotembelea, aina za pombe walizo nazo ndani au walizokunywa... Show off kama ni nature basi ipo kwa jinsi zote ila tofauti inaweza kuwa aina ya vitu wanavyo-show off. Wanawake wata-show off vitu kama hivyo vya wanaume pamoja na mahusiano yao - waume/wapenzi na watoto pamoja na muonekano - nguo, viatu, mitindo ya nywele na mapambo. Lakini pia kama ni nature basi kuna wengine wana matatizo maana hawa-show off chochote ingawa wana vingi. Wao hupost mada za michezo, nukuu za watu mashuhuri na maandiko mbalimbali. Hoja ya msingi hapa nadhani ni mtu anaonyesha nini kwa lengo gani. Kuna ambavyo havitakiwi kuonyeshwa; na vinavyofaa kuonyeshwa basi iwe kwa malengo ya maana siyo mtu anaonyesha nyumba halafu anaandika "na bado!". Mwingine anapost picha ya mtoto wake mchanga wa siku moja anaandika "asiye na mwana aeleke jiwe..". SHOW-OFF HAZINA ME WALA KE ila mleta mada kachagua kuongea na wanawake.