Mi nashangaa sana mtu mzima mwenye elimu anapokuja na hoja za ubaguzi wa watanzania huku amesoma na anaijua historia ya nchi yetu vizuri. Tanzania ina makabila 120 na zaidi. Hivi kila kabila tukisema lazima litoe waziri na katibu mkuu nchi itatawalika? Mi ni mhangaza na kabila langu halijawahi kutoa waziri mbona sisemi nimebaguliwa. Tuache ukabila na ukanda nchi yetu ni moja. Hakuna makabila ya watawala wala makabila ya watawaliwa. Kiongozi anaweza kutoka kabila lolote, dini yoyote, mkoa wowote na kanda yoyote ilimradi tu ana sifa stahiki. Hongera sana Dr Magufuli, HAPA KAZI TU