Wachache (minority) humiliki uchumi mkubwa duniani

Wachache (minority) humiliki uchumi mkubwa duniani

komasalonde

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2024
Posts
2,742
Reaction score
3,520
Hii dunia imethibitika kabisa kuwa Ina rasilimali za kutosha kuwawezesha watu wote duniani kula, kusoma, kutibiwa, kutalii, kujenga/kupanga na kufurahia maisha.

Bahati mbaya sana, ubinafsi, ubabe na uchoyo ama wa kisiasa au kuitawala umehodhisha rasilimali zote kwa vikundi au watu binafsi, huku waliobaki wakiteseka, wakiugua, wakishindwa kusoma, wakikosa matibabu na hata kufa.

Nchini Marekani, asilimia 10 tu ya idadi yao, humiliki asilimia 60% ya pesa zote za nchi. Na asilimia 90 ya watu waliobaki wanaambulia asilimia 40 ya mali zote.

Hapa Tanzania kwa mfano, jarida la African Wealth report la 2022 linasema kuwa watu karibu 2357 wanamiliki mali/pesa za thamani ya usd bil 5 plus. Yaani kati ya watu milioni 60 Tanzania,, watu 2,357 asilimia ndogo sana wanamiliki mali kubwa.

Kumiliki mali sio tatizo. Tatizo ni njama za watu hao wachache/kikundi kutumia chama, dola, nguvu za giza na hila ili kupora mali zote za nchi.



Wachache/kikundi hawa, ni makatili, wababe na roho ngumu kupora kila rasilimali bila kujali waliobaki wanaishi au wanakufa.

Bahati mbaya, wengi wanaobaki maskini hawana namna ya kutetea, kulinda na kudai ama mgawanyo wa rasilimali au kuwezeshwa kupata nao sehemu ya urithi wao halali wa nchi.
 
Wachache/kikundi hawa, ni makatili, wababe na roho ngumu kupora kila rasilimali bila kujali waliobaki wanaishi au wanakufa
Kwa mfano wa nchi ulio utumia, hayo juu ni ukweli usiopingika.
 
...Lakini kitu usichokijua utajiri hautokani na kufanya kazi kutwa au kwa bidii.

Utajiri ni spiritual matter, wengi wanausubiri, wachache wanaufatilia Sana ila baadi ndo wanauchukua.

Kwa lugha nyepesi ni kwamba wengi wanautafuta utajiri, Lakini watu wachache huupata kwa utoshelevu wote 100%
 
Watu wengine wanajitoa muhanga sana aise kwa mfano Chief Godlove anayeuza jicho la tatu ambapo watu wenye hela humkunja kama kambalena kumwachia visenti anavyotumia kuwatambishia vijana wa TikTok.
 
Kwa hiyo na wewe unataka kujiunga naye siyo?
Sitaki kujiunga naye, sikumkubali lakini wabongo mna story nyingi juu ya watu ambao hamjui pesa wanapata wapi. Hii yote ni asiye na pesa kujaribu kujustify kutokuwa na pesa kwake kwa kusema aliye na pesa kazipata kwa njia mbaya sana.
 
Sitaki kujiunga naye, sikumkubali lakini wabongo mna story nyingi juu ya watu ambao hamjui pesa wanapata wapi. Hii yote ni asiye na pesa kujaribu kujustify kutokuwa na pesa kwake kwa kusema aliye na pesa kazipata kwa njia mbaya sana.
Tatizo yule jamaa ana mdomo sana na ninaijua michezo yake. Ingekuwa namwonea wivu basi ningeanza kuwatuhumu akiona Mo dewji , Rostam, Shabibi n.k.
 
Mbona wataalam wanasema utajiri ni siri bac hao watu 2k watakua na hizo siri
 
Tatizo yule jamaa ana mdomo sana na ninaijua michezo yake. Ingekuwa namwonea wivu basi ningeanza kuwatuhumu akiona Mo dewji , Rostam, Shabibi n.k.
Mo unajua biashara zake, rostam unajua, shabiby unajua, huyo haijulikani ndio maana anawadanganya mara freemasons mara sijui nini. Na wabongo wasipojua unafanya kitu gani wao watakuja na majibi yao.
Mimi nina ela ya kubadilisha mboga, mtaani hawajui kazi yangu basi wao wanasema eti mimi ni mwanajeshi. Ningekuwa tajiri sana wangesema labda muuza madawa, au freemasons. Hii ni tabia ya wabongo hasa wabongo masikini sana.
 
Mo unajua biashara zake, rostam unajua, shabiby unajua, huyo haijulikani ndio maana anawadanganya mara freemasons mara sijui nini. Na wabongo wasipojua unafanya kitu gani wao watakuja na majibi yao.
Mimi nina ela ya kubadilisha mboga, mtaani hawajui kazi yangu basi wao wanasema eti mimi ni mwanajeshi. Ningekuwa tajiri sana wangesema labda muuza madawa, au freemasons. Hii ni tabia ya wabongo hasa wabongo masikini sana.
Wewe unajigamba kama dogo godlove?
 
Wewe unajigamba kama dogo godlove?
Godlove yule atakuwa anawatapeli hivyo ukitaka kuwatapeli wabongo lazima ujigambe. Yani make them believe una pesa.
Si nasikia ana magroup ya whatsapp ya kuwafundisha watu utajiri kiingilio lak 3 na yanajaa.
Haki wewe tafta pesa uanze kodi magari, uende south upge pcha kidogo. Uanze tukana watu kuwa watafte pesa, basi wajinga watakuletea pesa wenyewe.
Ni formula wanaitumia wengi akiwemo sir jeff
 
Godlove yule atakuwa anawatapeli hivyo ukitaka kuwatapeli wabongo lazima ujigambe. Yani make them believe una pesa.
Si nasikia ana magroup ya whatsapp ya kuwafundisha watu utajiri kiingilio lak 3 na yanajaa.
Haki wewe tafta pesa uanze kodi magari, uende south upge pcha kidogo. Uanze tukana watu kuwa watafte pesa, basi wajinga watakuletea pesa wenyewe.
Ni formula wanaitumia wengi akiwemo sir jeff
Na mimi namtukana kama yeye anavyowatukana vijana na kuwadanganya.
Nawaambia vijana kuwa jamaa anajiuza ili waache tabia za kipuuzi.
 
Godlove yule atakuwa anawatapeli hivyo ukitaka kuwatapeli wabongo lazima ujigambe. Yani make them believe una pesa.
Si nasikia ana magroup ya whatsapp ya kuwafundisha watu utajiri kiingilio lak 3 na yanajaa.
Haki wewe tafta pesa uanze kodi magari, uende south upge pcha kidogo. Uanze tukana watu kuwa watafte pesa, basi wajinga watakuletea pesa wenyewe.
Ni formula wanaitumia wengi akiwemo sir jeff
Au kama sio tapeli basi madini yatakuwa yanampa hela chunya huko pengine ana MIGODI mbona kawaida sana vijana siku hizi kuwa na noti..sema yule tatizo ndo hivo sifa
 
Back
Top Bottom