The Mockingjay
JF-Expert Member
- Jan 11, 2011
- 380
- 121
mie nipo hapa dodoma,
tangu waheshimiwa wabunge waanze kuja dodoma kwa kikao cha bunge la bajeti, kumekuwepo na ongezeko kubwa la mashangingi hasa nyakati za jioni kuja hapa chuo kikuu cha dodoma na kuwachukua watoto na kuondoka nao. Wabunge wanawatuma madereva tu, wao hawaonekani!
Je hii ndo kazi ambayo wametumwa na wapiga kura wao? Na je kwanini wanawaharibia maisha watoto wa watu wakati wao wameoa na kuwa na familia zao? Kama wanahusudu sana ngono kwanini wasije na wake zao?
Nawakilisha wadau!!!
there is a very simple solution for this my friend.
Tafuta camera nzuri. Piga picha hao mademu wakiingia kwenye hayo mashangingi.
Ikiwezekana, hakikisha na kupata ushahidi wa picha wakiwa hata pamoja kwenye hoteli wanakula.
Au hao mabinti wakiwa wanaingia kwenye vyumba au sehemu zozote wanazokutana.
Ukiweza kuwa-link pamoja then tutawafanya kama hawa wafuatao:
1. Arnold schwaznegger
2. Straus-kahn
3. John edwards
maana yake, watoto wao, wake zao, familia zao, wapiga kura zao wataona ufuska wao.
Mtu asiyeheshimu ndoa yake ana mapungufu ya uongozi, ina maana ana tamaa sana, kwa hiyo ni virahisi sana hata kupokea rushwa na kuwanyima watu wake haki yao. Viongozi wa hivi hawafai!!!!!!![/color][/size][/b]
[/list]