Wabunge wataka Condester Sichwale aliyetolewa nje kisa mavazi aombwe radhi

Mwendazake alijipambanua kama mzalendo, lakini kwa maoni yangu mimi naona hakuwa Mzalendo, ila alikuwa na ajenda yake ambayo alitaka kuipitisha kupitia neno la uzalendo.
Badala kujadili mambo muhimu ya kitaifa, watumishi wanaiba kwa kujilipa posho hadi 300m kwa wiki. Bunge la ccm linajadili mavazi, afu mtu anasema Magufuli (aliewaleta hawa bungeni) ni shujaa

Sent from my vivo 1611 using JamiiForums mobile a
 
Sakata la kutolewa nje kwa mbunge wa Momba Condester Sichwale (CCM) kuhusu mavazi, limeibuka tena leo jioni katika kikao cha Bunge baada ya wabunge wanawake kutaka aombwe radhi na aliyetoa hoja.

Hata hivyo mbunge Hussein Amar amesema hawezi kuomba radhi kwa sababu alichosema alikuwa sahihi kwakuwa mavazi aliyovaa mbunge mwenzake hayakuwa na staha ndiyo maana Spika wa Bunge Job Ndugai aliridhia hoja aliyoitoa yeye (Amar).

Katika kikao cha leo jioni wabunge Jacqueline Ngonyani na Stella Manyanya waliomba mwongozo wa Spika kwa madai mbunge aliyetolewa nje alionewa.

Mapema leo Sichwale alitolewa nje kwa amri ya Spika baada ya Amar kuomba mwongozo kwa kutumia kanuni 170 kuhusu mavazi ya staha.

Ngonyani amesema kilichotokea ni kwamba mbunge huyo alionewa kwani alikuwa na vazi la staha ambalo halikuwa na shida lakini akasema huenda Spika hakuona.

"Mimi ni mjumbe wa Baraza Kuu la wanawake wa CCM, ninapoona kuna uonevu lazima niseme na hili sikiungi mkono huyu mwanamke mwenzetu ameonewa,"amesema Ngonyani.

Mbunge huyo amesisitiza kuwa uonevu wa namna hiyo haupaswi kuvumiliwa kwakuwa umemdhalilisha mbunge huyo na wapiga kura wake jimboni.

Kwa upande wake Manyanya amesema tangu asubuhi alikuwa anafuatilia kwenye mitandao na amebaini kuwa Sichwale hakuwa na vazi baya.

Hata hivyo Manyanya amesema haiwezekani wabunge vijana wavae mavazi kama wanayovaa wabunge wanawake watu wazima.

Amesema katika siku za karibuni limeibuka suala la kutoa lugha za kuwadhalilisha wabunge wanawake ndani ya ukumbi ambako wakati mwingine hutamkwa kiungo cha mwanamke halafu wengine wanafurahi.

Naibu Spika Dkt. Tulia Akson amesema atatoa mwongozo baada ya kufuatilia jambo hilo.

View attachment 1805646
Wamempaisha, wengine ambao tulikuwa hatumfahamu tunaanza kumfuatilia
 
Ulikua uonevu na uzalilishaji mkubwa sana na usiovumilika, huyu mzee asilete sheria na maoni ya nyumbani kwake kwenye public, Huyu mzee lazıma ashitakiwe kwa uzalilishaji na spika amuombe razi huyu Mama na wanawake wote, kwani kitendo hiki na Katika chombo hiki ni kimezalilisha Wanawake wote, na huyu Mama hakuwa na kosa Nguo zake zilimsitiri vizuri bila shaka yeyote.
Hivi unafahamu Unachokiongea ?!!

Mbunge anashtakiwa vipi kwa kuongea mawazo yake ndani ya bunge ?!!!

Tena mawazo Yake yalipokelewa na kutafsiriwa kikanuni na MKUU WA SHUGHULI ZA BUNGE(mh.Spika).......

Na bahati iliyoje alikuwepo mh.Spika Mwenyewe kwani kinyume chake labda "uamuzi usingekuwa ulivyokuwa"....

#KaziIendelee
 
Wazee wa siku hizi bana asije kuwa aliomba mzigo kanyimwa sasa akabakia na lake moyoni..!!
 
Sisi tulishauri wabunge washonewe uniform kama student wavae sare Ili kuepusha haya awakusikia
 
Ulikua uonevu na uzalilishaji mkubwa sana na usiovumilika, huyu mzee asilete sheria na maoni ya nyumbani kwake kwenye public, Huyu mzee lazıma ashitakiwe kwa uzalilishaji na spika amuombe razi huyu Mama na wanawake wote, kwani kitendo hiki na Katika chombo hiki ni kimezalilisha Wanawake wote, na huyu Mama hakuwa na kosa Nguo zake zilimsitiri vizuri bila shaka yeyote.
Job anayejinasibu kuwa mtetezi wa wanawake mbona ameshiriki udhalilishaji huu? au yeye kapewa kazi ya kuwatetea covid-19 pekee!! yetu macho mwaka huu kila jambo linakwenda against huyu jamaa !!
 
Hivi unafahamu Unachokiongea ?!!

Mbunge anashtakiwa vipi kwa kuongea mawazo yake ndani ya bunge ?!!!

Tena mawazo Yake yalipokelewa na kutafsiriwa kikanuni na MKUU WA SHUGHULI ZA BUNGE(mh.Spika).......

Na bahati iliyoje alikuwepo mh.Spika Mwenyewe kwani kinyume chake labda "uamuzi usingekuwa ulivyokuwa"....

#KaziIendelee
Na spika anatakiwa amuombe msamaha kwani amekosea, huwezi kutoa hukumu kutokana na macho yako, toa makosa yaliyokua kwenye nguo aliyovaa na taja sifa za mavazi ya wanawake ambayo yanaruhusiwa. na Je spika na yule mzee aliyetoa hoja ni wataalamu wa mavazi? kwanini wasiajiri wataalamu kwa ajili ya kuwashauri na wengine kukaa mlangoni kwa ajili ya ukaguzi? usikubali uzalilishaji kwenye chombo kikubwa kama kile, kwani italeta mazara makubwa kwenye jamii, watoto wa kike watazalilishwa kila mahali kwa sababu ya maumbo Yao tu. lazima hawa watu wawajibike kwa uzalilishaji ulitokea kwenye chombo kama kile.
 
Na spika anatakiwa amuombe msamaha kwani amekosea, huwezi kutoa hukumu kutokana na macho yako, toa makosa yaliyokua kwenye nguo aliyovaa na taja sifa za mavazi ya wanawake ambayo yanaruhusiwa. na Je spika na yule mzee aliyetoa hoja ni wataalamu wa mavazi? kwanini wasiajiri wataalamu kwa ajili ya kuwashauri na wengine kukaa mlangoni kwa ajili ya ukaguzi? usikubali uzalilishaji kwenye chombo kikubwa kama kile, kwani italeta mazara makubwa kwenye jamii, watoto wa kike watazalilishwa kila mahali kwa sababu ya maumbo Yao tu. lazima hawa watu wawajibike kwa uzalilishaji ulitokea kwenye chombo kama kile.
Sasa nani awajibike ?!!!

Awajibike kwa nani ?!!

Mh.Spika atolewe uspika kwa jambo hilo ?!!

Mbunge wa Nyang'wale afukuzwe bungeni kwa jambo hilo ?!!

Hayo yote usemayo yana sheria nyuma yake kuyafanikisha ?!!
 
Ningekuwa spika...ingawa siwezi kuwa spika...ningeamuru wote wanaoendeleza huu mjadala watoke nje kabisaaaa....hivi hakuna changamoto za wananchi wao majimboni mpaka hili liwe Jambo serious HIVI?
Hili jambo ni muhimu sana kwani linaleta uzalilishaji kwa watoto wa kike na kuwaweka kwenye hatari, na heshima ya chombo kama kile kama kuna tatitizo wangetumia njia ya staha kumjulisha mhusika, na watoe sababu sio kwa kuangalia na macho tu na kutoa maamuzi. ili kufuta huo uzalilishaji ni lazima waombe msamaha hazarani
 
Back
Top Bottom