Wabunge wanaoshauri vijana wajitolee ili wapewe kipaumbele kwenye ajira, onyesheni mfano wa ninyi kujitolea kwanza!

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,664
18,040
Kuna wabunge wanatoa mawazo ya hila hadi wanakera!! Ni unafiki mkubwa sana!! Lengo lao ni kutaka kuwapitisha watu wao kwenye ajira ya utumishi wa umma kwa mlango wa nyuma wa "kujitolea". Hii itatesa sana wale watakaoingia kichwa kichwa kujitolea wakati wako nje ya kundi hili la wateule!! Watajitolea miaka nenda rudi na ajira wasipate!! Kuna vijana wengi sana walijitolea hadi wakanyoosha mikono!!

Hawa wabunge tunawataka na wao wajitolee kwenye bunge hili la bajeti!! Wasipate posho wala mshahara!! Zile walizokwisha chukua zihesabike mkopo na wazirejeshe!! Waonyeshe huu uzalendo hadi mwisho wa mwaka, halafu ndio watufundishe utamu wa kujitolea!!

Hawana hata aibu, hebu watuambie huyo anayejitolea atakula nini?, atavaa nini? atatibiwa vipi? hadi siku atakapopata ajira!! Halafu hatuzungumzii kujitolea kwa mwezi mmoja au miwili bali mwaka au miaka!! Hii ni kutumia shida ya mtu kumfanya mtumwa!! HATUTAKI!! Jitoleeni kwanza nyie wabunge na mawaziri kwa mwaka mmoja!!
 
Riz-one Kik*ete onesha mfano wa kujitolea kipindi chote kilichobakia hadi uchaguzi mkuu!. Usichukue mshahara wala posho!! Kama itakuwa ngumu kwako pamoja na kusheheni vitega uchumi kibao, kwa nini unakomalia wengine wasiokuwa na kitega uchumi chochote wajitolee!!
 
Hawa wabunge wa miaka huu wanaongea mambo mazito kinadharia sana.Ajabu wengi wao ni magraduate lakini Kishimba akipewa nafasi ya kuichambua hoja anaonekana yuko vizuri upstairs kuliko wao.Kuna haja ya kurecheck vyeti vya hawa waishiwa
 
Tuambieni wakati vijana wanajitolea watapata wapi mahitaji yao ya kila siku? Najua watoto wenu mtawahudumia wakati "wanajitolea" kwa matumaini ya uhakika wa kuajiriwa kwa michongo, je wale mnaotaka kuwaingiza mkenge nao wajitolee kiukweli bila matumaini ya uhakika wa ajira nani atawapa mahitaji yao na ya wategemezi wao wakati wanajitolea? ONENI AIBU?
 
Hawa wabunge wa miaka huu wanaongea mambo mazito kinadharia sana.Ajabu wengi wao ni magraduate lakini Kishimba akipewa nafasi ya kuichambua hoja anaonekana yuko vizuri upstairs kuliko wao.Kuna haja ya kurecheck vyeti vya hawa waishiwa
Nakuunga mkono!!
 
Wakubwa hawana hamu na uwanja sawa wa ajira kupitia PSRS!! Waacheni watoto wenu wakapambane na watoto wa wakulima kwenye usaili!! Kama mlivyowapeleka watoto wenu huko kwenye shule za binafsi lakini wakapambana na watoto wa wakulima na wajasiliamali kwenye mitihani ya necta na vyuo bila kupewa kipaumbele, hali kadhalika wapelekeni watoto wenu "wakajitolewe" lakini msiwakwepeshe kupambana na vijana wanaofanya vibarua kila siku kupambana kwenye usaili wa PSRS kwa kuwapa kipaumbele eti "wamejitolea".

Hivi hamjui kuwa wakati watoto wa wakubwa hupewa nauli na wazazi wao ili wahudhurie usaili wa PSRS lakini watoto wa watanazina walio wengi hufanya vibariua ili wapate nauli za kuwawezesha kuhudhuria saili za PSRS. Sasa kama wakijitolea nauli na malazi wakati wa usaili watapata wapi?
 
Wanafiki hao aishi kwa hofu juu ya Ulinzi wa kazi zao.
Wacheleweshewe mishahara au waminywe posho ht kwa siku nne uone timbwili.
 
Hivi ni lini mara ya mwisho tumesikia BOT wakitangaza ajira kupitia PSRS? Ina maana huko watu huwa hawastaafu au? Nina wasi wasi huko ndiko kumejaa hao watoto wa wakubwa wanakodai "wanajitolea"
 
Mnaotaka watoto wenu wajitolee sawa lakini jueni lazima wakumbane na usaili wa PSRS!! Mbeleko kwa "waliojitolea" HAKUNA
 
Kuna wabunge wanatoa mawazo ya hila hadi wanakera!! Ni unafiki mkubwa sana!! Lengo lao ni kutaka kuwapitisha watu wao kwenye ajira ya utumishi wa umma kwa mlango wa nyuma wa "kujitolea". Hii itatesa sana wale watakaoingia kichwa kichwa kujitolea wakati wako nje ya kundi hili la wateule!! Watajitolea miaka nenda rudi na ajira wasipate!! Kuna vijana wengi sana walijitolea hadi wakanyoosha mikono!!

Hawa wabunge tunawataka na wao wajitolee kwenye bunge hili la bajeti!! Wasipate posho wala mshahara!! Zile walizokwisha chukua zihesabike mkopo na wazirejeshe!! Waonyeshe huu uzalendo hadi mwisho wa mwaka, halafu ndio watufundishe utamu wa kujitolea!!

Hawana hata aibu, hebu watuambie huyo anayejitolea atakula nini?, atavaa nini? atatibiwa vipi? hadi siku atakapopata ajira!! Halafu hatuzungumzii kujitolea kwa mwezi mmoja au miwili bali mwaka au miaka!! Hii ni kutumia shida ya mtu kumfanya mtumwa!! HATUTAKI!! Jitoleeni kwanza nyie wabunge na mawaziri kwa mwaka mmoja!!
 
Tuambieni wakati vijana wanajitolea watapata wapi mahitaji yao ya kila siku? Najua watoto wenu mtawahudumia wakati "wanajitolea" kwa matumaini ya uhakika wa kuajiriwa kwa michongo, je wale mnaotaka kuwaingiza mkenge nao wajitolee kiukweli bila matumaini ya uhakika wa ajira nani atawapa mahitaji yao na ya wategemezi wao wakati wanajitolea? ONENI AIBU?
 
Mtoa mada fuata utaratibu. Hutakiwi utoe mada afalafu uendelee kuchangia mwenyewe na kujijibu. Kama kuna hoja katika Uzi wako wadau watotoa michango na maoni yao. Ukiona uzi umedoda ujue hakuna hoja.
 
Kuna wabunge wanatoa mawazo ya hila hadi wanakera!! Ni unafiki mkubwa sana!! Lengo lao ni kutaka kuwapitisha watu wao kwenye ajira ya utumishi wa umma kwa mlango wa nyuma wa "kujitolea". Hii itatesa sana wale watakaoingia kichwa kichwa kujitolea wakati wako nje ya kundi hili la wateule!! Watajitolea miaka nenda rudi na ajira wasipate!! Kuna vijana wengi sana walijitolea hadi wakanyoosha mikono!!

Hawa wabunge tunawataka na wao wajitolee kwenye bunge hili la bajeti!! Wasipate posho wala mshahara!! Zile walizokwisha chukua zihesabike mkopo na wazirejeshe!! Waonyeshe huu uzalendo hadi mwisho wa mwaka, halafu ndio watufundishe utamu wa kujitolea!!

Hawana hata aibu, hebu watuambie huyo anayejitolea atakula nini?, atavaa nini? atatibiwa vipi? hadi siku atakapopata ajira!! Halafu hatuzungumzii kujitolea kwa mwezi mmoja au miwili bali mwaka au miaka!! Hii ni kutumia shida ya mtu kumfanya mtumwa!! HATUTAKI!! Jitoleeni kwanza nyie wabunge na mawaziri kwa mwaka mmoja!!
ZIKITOKA AJIRA WABUNGE WANATUMA VIMEMO ili WATOTO NA NDUGU ZAO WAAJIRIWE ILA WATOTO WA MASIKINI wao WAJITOLEE
 
Back
Top Bottom