Wabunge Mafisadi wamwinda Dr Slaa

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Dk. Slaa awindwa bungeni

• Waziri Kombani, Ghasia waongoza mkakati

na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MWENENDO wa mambo katika mkutano wa 15 wa Bunge, unaoendelea mjini hapa, unazidi kuwa na utata mara baada ya kuwapo taarifa kuwa serikali imeanza mkakati maalumu wa kummaliza kisiasa na kumfungulia kesi ya jinai, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa.

Habari za uhakika zilizolifikia Tanzania Daima Jumatano kutoka kwa baadhi ya wabunge, zimedai kuwa, kwa siku kadhaa sasa, mawaziri wawili wamekuwa wakipanga mkakati huo wakishirikiana na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na baadhi wa kutoka kambi ya upinzani.


Mawaziri wanaotajwa kuendesha mkakati huo ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi, Hawa Ghasia na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Celina Kombani.

Habari hizo zinadai kuwa, mawaziri hao wamekuwa wakipita kwa wabunge wakiwaeleza kuwa serikali imetambua kuwa ni jambo la hatari kuendelea kuwa na mtu wa aina ya Dk. Slaa bungeni, akiwa na wadhifa wa unyekiti katika Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa.

Mbunge mmoja aliyefuatwa na mmoja wa mawaziri hao na kushawishiwa kushiriki katika mpango wa kumshughulikia Dk. Slaa na kufanikiwa kuzungumza na Tanzania Daima Jumatano kwa sharti la jina lake kutotajwa gazetini, alieleza kuwa, Waziri Kombani anasimamia mpango wa kumuondoa Dk. Slaa katika wadhifa wake wa Uenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, huku Waziri Ghasia akiwa ameweka watu maalumu wanaochunguza maofisa wa serikali anaozungumza nao, wanaodhaniwa kuwa ndio wanaompatia nyaraka za siri za serikali zinazohusu ufisadi.

“Mimi nilifuatwa na Waziri Kombani mwenyewe, kwa mdomo wake akaanza kunishawishi niisaidie serikali kumshaghulikia Dk. Slaa, kwa sababu ni mtu hatari anayeinyima usingizi. Aliniambia kuwa ni vigumu kujua watu wanaompatia nyaraka za siri za serikali, hasa zile zinazohusu ufisadi, kwa sababu Waziri Ghasia ameweka watu maalumu wanaofuatilia maofisa wa serikali alio karibu nao, lakini mpaka sasa hakuna mafanikio.

“Waziri Kombani aliniambia kuwa, Waziri Ghasia alifikia uamuzi huo ili kujua maofisa wa serikali anaowasiliana nao kwa sababu hao ndio wanaompatia nyaraka za siri za serikali, na kwamba kama akikamatwa nazo safari hii, hatapona,” alisema mbunge huyo.


Mmoja wa viongozi wa kambi ya upinzani aliyezungumza na gazeti hili na kutaka jina lake lihifadhiwe kwa sababu ameteuliwa kuongoza timu ya kuchunguza madai hayo dhidi ya Dk. Slaa, alisema kambi ya upinzani inazo taarifa hizo na inazifanyia kazi kwa siri, kwa sababu baadhi ya wabunge wa kambi hiyo wamenunuliwa ili kumuangamiza.

Alisema uchunguzi wa timu yake umebaini kuwa, Dk. Slaa alianza kuingia katika mgogoro na wabunge baada ya kuzuia posho ambazo wajumbe wa kamati walikuwa wakilipwa na halmashauri mara wanapokwenda kuzikagua.

“Hali ni mbaya, lakini tunafanya kazi na tutalipua bomu ili wananchi wajue kuwa vita hii inapiganwa pia na mawaziri na si wabunge peke yao.

“Uchunguzi wa timu yangu umebaini kuwa, Dk. Slaa alianza kuchukiwa na wabunge wenzake alionao katika kamati moja ambayo yeye ni mwenyekiti wake, baada ya kuzuia malipo ya posho kutoka halmashauri walizokuwa wakifika kuzikagua kwa sababu ni kinyume cha taratibu.

“Lakini Dk. Slaa, alikuwa na sababu ya msingi ya kuzuia posho hizo, kwa sababu Bunge linawalipa wabunge kila wanapokuwa katika shughuli halali za Bunge. Kulipwa na halmashauri ni kinyume cha taratibu, kwa sababu wanakuwa wamelipwa posho mara mbili kwa kikao kimoja. Sasa alipozuia kwa sababu walikuwa wamezoea, chuki ikaanza,” alisema kiongozi huyo wa upinzani ambaye pia ni mbunge.


Akizungumzia wabunge na mawaziri wanaoongoza mkakati huo wa kummaliza Dk. Slaa, alisema taarifa za uhakika alizonazo ni pamoja na Waziri Kombani na Mbunge wa Kibakwe (CCM), George Simbachawene, ambao wamekuwa wakipita kwa wabunge wakiwataka kuungana kwa pamoja kupinga hatua za upotoshaji zinazofanywa na Dk. Slaa kwa lengo la kulichafua Bunge.

Alisema Waziri Kombani tayari amekwishakutana na Mbunge wa Viti Maalumu, Grace Kihwelu (CHADEMA) na kumshawishi akubali kuchukua wadhifa wa Dk. Slaa wa uenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa mara tu atakapoondolewa, na kwamba alimuahidi kuwa serikali itakuwa pamoja naye katika shughuli zake zote zinazohusu ubunge.

Kuhusu Waziri Ghasia, alisema baadhi wa wabunge wameishasikika wakieleza kuwa wamepewa kazi maalumu na waziri huyo ya kuchunguza na kumpatia taarifa iwapo Dk. Slaa ana nyaraka mpya za serikali na mahali alikozihifadhi ili akamatwe na kushughulikiwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

Alipoulizwa kuhusu madai hayo, Waziri Kombani alilieleza gazeti hili kuwa, hana ugomvi na Dk. Slaa, hivyo hana sababu yoyote ya kushiriki katika mpango wa kumuangamiza kisiasa au kumfikisha katika vyombo vya dola.

Aliongeza kuwa, alichokisema Dk. Slaa hakihusiani na wizara yake na kwamba tangu alipoingia katika utumishi wa umma, hajawahi kuhusika katika tuhuma au kashfa yoyote na jambo hilo hataruhusu litokee.

Tanzania Daima Jumatano lilipowasiliana na Kihwelu na kumuuliza kuhusu madai hayo, alisema hana taarifa hizo, lakini lilipomueleza kuna ushahidi kuwa alikutana na Waziri Kombani na akashawishiwa kukubali kuchukua nafasi ya Dk. Slaa katika kamati yake atakapoondolewa, alinyamaza kwa muda kisha akasema ni jambo la kweli, lakini hapendi kulizungumzia.

“Jamani hili jambo umelijuaje, sikiliza ndugu yangu, mimi Waziri Kombani alinifuata pale ofisi za benki bungeni, akaniambia jambo hilo, lakini nilikataa hapo hapo na nilimueleza wazi kuwa siwezi kumsaliti kiongozi wangu kwa sababu hana kosa na anachokitetea ni cha kweli. Sikuendelea kusikiliza maneno yake, nilimuacha hapo benki,” alisema Kihwelu.

Baadaye gazeti hili liliwasiliana tena na Kombani na kumueleza kuwa kuna taarifa alikutana na Kihwelu na kumshawishi awe tayari kushika nafasi ya Dk. Slaa, waziri huyo alikana, na kueleza kuwa katika maisha yake yote bungeni hajawahi kufika katika ofisi hizo.

“Naomba mniamini, simo katika mkakati huo, hapo benki ya Bunge mimi sijawahi kufika na hata leo nilikuwa sina hela kabisa, lakini nilimtuma mtoto wangu benki akaenda kunichukulia. Mimi ni msafi, simo katika kashfa hizo,” alisisitiza Waziri Kombani.

Naye Simbachawene alipoulizwa kuhusu madai ya kushiriki kwake katika mpango huo alikana na kueleza kuwa, Dk. Slaa ni shemeji yake, hivyo hawezi kushiriki katika mpango wowote wa kumuumiza.

Simbachawene alieleza zaidi kuwa, ingawa hakubaliani na vitendo vya Dk. Slaa, hasa kutangaza maslahi ya wabunge, lakini hata kama yeye na wenzake wana nia hiyo, hawawezi kufanikiwa kwa sababu suala hilo halihusiani na kamati.

“Dk. Slaa ni shemeji yangu, siwezi hata kidogo kushiriki mkakati wowote wa kumuumiza. Mimi sikubaliani naye anapotangaza maslahi ya wabunge, kwanza tunalipwa kidogo sana kulingana na wabunge wenzetu wa nchi nyingine. Lakini hata kama mimi na wenzangu tuna mpango wa kumshughulikia, naamini hatuwezi kufanikiwa kwa sababu suala hilo halipo katika kamati yake,” alisema Simbachawene.

Tanzania Daima Jumatano ilipowasiliana na Dk. Slaa kuhusu madai hayo, alikiri kuwa anazo taarifa za kuwapo kwa mikakati hiyo, lakini haimtishi kwa sababu uenyekiti wa kamati si uhai wake, bali ni sehemu ya majukumu ya kuwashughulikia wananchi.

Alisema hashangazwi na hatua ya mawaziri hao kuandaa hujuma dhidi yake, kwa sababu anatambua kuwa mtu yoyote anapokuwa mwiba kwa serikali, lazima ifanye mkakati wa kumshughulikia.

“Nina taarifa kuhusu mipango hiyo, lakini mimi ni mbunge ninayejua majukumu yangu, jambo hilo halinisumbui. Hawa mawaziri wamepoteza mwelekeo, hawamsaidii rais, wanamuumiza. Niwaambie kwamba nikiletewa nyaraka hizo wanazoita za siri lakini zinaeleza ufisadi, nitazichukua wanikamate. Wakinikamata nitafurahi sana kwa sababu tutakwenda mahakamani, tutapambana, huko kila kitu kitajulikana kuhusu siri za serikali,” alisema.

Alipoulizwa anavyojisikia baada ya kuzomewa na wabunge na hata kubezwa na Spika wa Bunge, Samuel Sitta kutokana na hatua yake ya kutaja mishahara na posho za wabunge alisema kwa kujiamini: “Hata Spika akiwa mkali ninapozungumzia mishahara na posho kubwa za wabunge, hanisumbui, kwani mara ngapi amenitaka nifute kauli zangu bungeni, kama sifuti au nafuta najua mimi. Mara ngapi ameniambia atanipeleka polisi? Muhimu afahamu kuwa jabali huwa halitikisiki.”

Tangu kuanza kwa mkutano wa 15 wa Bunge, Dk. Slaa amekuwa katika wakati mgumu kutokana na wabunge kumshambulia kwa maneno na kumzomea anaposimama kuzungumza bungeni, wakimtuhumu kuwa amefanya kosa kutaja kiwango cha mishahara na posho wanazolipwa wabunge.
 
michkp-1.jpg
[/IMG]
 

Msaliti wa Watanzania kazini. Usifikiri kila mtu anayepambana na mafisadi ni mwanachama wa CHADEMA. Wengi wetu tunafanya hivyo kwa mapenzi ya nchi yetu ambayo sasa imetekwa nyara na mafisadi ambao wanajilimbikizia utajiri wa kutisha wao na vibaraka vyao wakati asilimia kubwa ya Watanzania wakiendelea kuishi maisha ya dhiki kubwa. Ujue mwisho wa mafisadi waliokuweka mifukoni mwao hauko mbali.
 
Msaliti wa Watanzania kazini. Usifikiri kila mtu anayepambana na mafisadi ni mwanachama wa CHADEMA. Wengi wetu tunafanya hivyo kwa mapenzi ya nchi yetu ambayo sasa imetekwa nyara na mafisadi ambao wanajilimbikizia utajiri wa kutisha wao na vibaraka vyao wakati asilimia kubwa ya Watanzania wakiendelea kuishi maisha ya dhiki kubwa. Ujue mwisho wa mafisadi waliokuweka mifukoni mwao hauko mbali.
thread_sucks-3.jpg
 
Unastahili kupelekwa Mirembe maana naona hizo pesa za mafisadi zinakuharibu akili. Sasa unaonyesha kila dalili za punguani. Pole sana. Wahi Mirembe kabla hujaharibikiwa kabisa.
 
"kwanza tunalipwa kidogo sana kulingana na wabunge wenzetu wa nchi nyingine" alisema Simbachawene.

Hii inatosheleza kuwa wabunge wetu akili zao hazifanyi kazi, hawajiulizi kwa nini watu wao wanalipwa kidogo sana kuliko wananchi wenzao wa nchi nyingine. What is your GDP compared to Kenya's?
 
Haleluya! Mungu hamfichi mnafiki, chochote wanachopanga gizani kitawekwa nuruni!
 
GT ni msomi mzuri tu ; lakini VIJISENTI vya wakina Manji vinamtesa anakuwa punguani!!
 
GT ni msomi mzuri tu ; lakini VIJISENTI vya wakina Manji vinamtesa anakuwa punguani!!
:rolleyes:

Ana elimu gani hiyo ya kusema ni msomi? Kama ni ki-degree wengi wanazo. Kama ni ki-masters, nimeona wengi walizonazo lakini pumbuani tupu. Ka-Phd hawezi kuwa nacho hata siku moja. Pia kumbuka Elimu si akili.
Back to the real topic, yaani this is a serious matter. Hatuwezi kumpoteza Dk Slaa. Huyu jamaa ni mkombozi mpya. Hao wabunge wa upinzani wanaompinga watajwe majina na ishu ipelekwe majimboni mwao. Hatuwezi kukubali kuyumbishwa na wachache hata siku moja. Sisi sio makondoo. Nchi ni yetu sote, na kama inaleta matunda tule sote.
Yani hii post imenisikitisha sana sana, hasa kuona na wabunge wa upinzani wamo ndani. AIBU kwa BUNGE.
Tusije kusikia Sokoine nyingine hapa. Siku hiyo kutakuwa hakuna kulala.
 
Mhh. Kweli hii vita ya ufisadi si kwa kiwango nilichokuwa nakifikiria. Ni vita kali sana. So yaani anyways one day,.... one day...tutashinda. Acheni kumjadili huyo GT tuendelee kupambana na hawa mafisadi
 
ANALYSIS: What are these ministers up to?

NKWAZI MHANGO
St John's NL, Canada

THE other day I was at a pub quaffing liquor when the radio announced the rants of two ministers. They are thundering at Reginald Mengi for committing a sacrilege - touching the untouchable 'fisadis.'

Firstly, I thought liquor was taking its toll on my upstairs. I, thus, tried to ignore the whole brouhahas and bugaboos thinking it were but 'njaa.' But when the morning papers quoted these winos, I decided to send them these salaams.

You know what. It needs the courage of the mad. Who could believe that ministers of the same power-that-be could dress themselves down by standing by and with the fisadis as opposed to wananchi.

What fancy pants! Mr President, though you are left with a few days in office before the next poll, fire these guys. Records show they have always been chewing what they cannot swallow.

Going back to this despicable act, my heart asked me: Does it mean the 'fisadis' are now hiring ministers to intimidate and ultimately silence us. Do they know they're enjoying all those yum-yum, thanks to our taxes. In law, the conspirator is as guilty as the doer.

Let's look at it the other way. Why ministers always keep mum when it comes to pressing matters such as smoking out 'fisadis' but the same jump into the bandwagon of defending them. Once a 'fisadi' always a 'fisadi.' Jesus once said: ''You'll know them by their fruits.'' And verily he added: ''The one that?s going to betray me is the one with whom I share the table.'' And, indeed, Judas Iscariot did! How many 'Judas Iscariot' do we have out there.

There's this tendency of misconstruing and misuse of law. One of the said heartless ministers said. ''How can Mengi judge whilst he is not the court'' Folks, what is wrong up there? Mengi did not judge. He cannot be such goon. He reported what he knows would add up to President Jakaya Kikwete's calls that we give him the names of sharks so that he can deal with them as we did in albino indiscreet killings. Were we court to do the same as we were asked by the same government. 'Huu nao ni ufisadi' of its kind so to speak.

One thing dresses down all those 'fisadis' defending their colleagues. When one of the alleged sharks, Jeetu Patel, was approached by the media to reciprocate, he said: Mengi has constitutional right to say whatever he deems fit. If the alleged person sees it this way, what gears you to defend the person whose defence has already been heard.

Rostam Aziz said: ''..it is illogical to argue with Mengi.'' In other words, he had nothing to dispute. As for Yusuf Manji, he said Mengi is not civilized as if what was disputed was whether Mengi is civilized or not! If the alleged persons are looking into and taking the matter that way, where do these ministers scoop their standpoint? Who sent them.

The other minister said Mengi is abusively using his media empire to demolish others! What bullshit. What should he use if politicians can use their parties and ministers their office that belong to wananchi. For these myopic ministers, nobody has the say except politicians! This country does not belong to politicians but Tanzanians in the first place.

If others can use their media empire to trash Mengi why shouldn't he use his to fight graft instead of condoning it as others do. Mengi founded his media many years ago. Others found them to see to it that their masters are wheeled in power so as to defend and feed them. Refer to Dr Harrison Mwakyembe who contended that Rostam got his thanks to EPA monies by the way of Kagoda. Who is wrong in this case 'waheshimiwa'.

Let me emphasize it. Mengi is not stupid to usurp powers that he knows belong to the so-called extra debito judiciae or the fountain of justice. My foot! Mengi has never been such a charlatan like several everyone can name, so to speak.

If the said ministers stand to what they said, chances are fisadis' money is at work believe me! If any sane person can accuse Mengi of wrong doing by helping the government to get the sharks it's always wananchi to bring forth, this person must either be one of them or working for them. If Mengi can use his media to fight graft so be it even if this means to offend ?fisadis' - like those erroneously accusing him of wrong doing for taking on 'fisadis'.

I can?t just understand yet. How can a minister whose government has always made us believe is fighting corruption jump into the bandwagon of cheerleaders and conspirators? Why should we turn our country into that of the frogs? You know what happened when frogs misbehaved? God punished them heavily as they found themselves choosing between a stock and a stork.

I still can?t believe that some ministers supposed to be geared by the spirit of serving their country were, instead, driven by their stomachs and their master ?fisadis?. Let the guys defend themselves. For those that want to defend them, do it in the right manner. Let the lawyers defend them shall they prefer to institute charges against Mengi.

Joji and Sofi, what?s wrong with you before whom everything was put in the agora that the sharks are almost behind all stinking ?ulaji? Does it mean you?re the ones I said the other day, that prefer to use Indians simply because they?re?easy to get rid of and repatriate.

Let me wrap up this way. Being a minister does not make you a god or a person who knows all. Importantly, one can be a minister and still be ignorant and corrupt as it happened to others whose offices were used to burn our fingers.

Those who shack up with fisadis should put up or shut up instead of dreaming about dictating our wars against graft. Otherwise, 'mmechemsha' though you say Mengi is the one who boiled down. It?s you and shame on you.
nkwazigatsha@yahoo.com
 
Hivi, hawa mafisadi wakifanikiwa kumnasa Slaa, Watanzania watafanya nini?

Na hawawezi ng'o! Slaa ni mtu wa kipekee sana, Yaani i couldnt resist my self to be proud of him, kwamba alikataa na kukataza kupata posho mara 2 kwa kamati yake?

To be sincere, ni muaminifu kuliko hata mimi! huu ni uzalendo wa hali ya juu, ambao nimeushuhudia katika kizazi cha hivi karibuni!

Mungu akubariki sana Slaa na akuweze kuyashinda yote, hata ndoto yako ya kumkomboa mtanzania utakapo itimiza!
 
Kwa kweli Mawaziri wa serikali ya Kikwete wanasikitisha sana. Sijui ni saa ngapi wanakaa kupanga na kufatilia mikakati ya kumkomboa mwananchi maskini wa kule kirando, au uyuwi, au tandahimba au kibong'oto. Just imagine,
  • In the past week tumeambiwa Mawaziri Chikawe, Kamala na Masha walikua Monduli na "kikao" cha "mikakati" baada ya mengi kutoa tamko la mafisadi papa,
  • Mawaziri Sofia Simba na George Mkuchika wanahaha na waandishi kumtisha Mengi kwa "kuwachafua wananchi", bila shaka kuna bakshishi itafuata kwa juhudi zao hizo.
  • Huko bungeni mawaziri Kombani na Hawa Ghasia wanaweka mkakati wa "kumshughulikia" Dr Slaa.
Nauliza, hivi kwa mwendo huu kutakua na maisha bora kwa kila Mtanzania ifikapo 2010?... Ni saa ngapi hawa mawaziri wanaumia vichwa kutatua matatizo ya mwananchi wa kawaida?.....Kikwete namsikitikia kwakua hana watu wa kazi kwenye baraza lake, lakini namlaumu fully yeye mwenyewe kwa kuendelea kuilea hii mizigo ya walipa kodi kwenye baraza.
 
Kwa kweli Mawaziri wa serikali ya Kikwete wanasikitisha sana. Sijui ni saa ngapi wanakaa kupanga na kufatilia mikakati ya kumkomboa mwananchi maskini wa kule kirando, au uyuwi, au tandahimba au kibong'oto. Just imagine,
  • In the past week tumeambiwa Mawaziri Chikawe, Kamala na Masha walikua Monduli na "kikao" cha "mikakati" baada ya mengi kutoa tamko la mafisadi papa,
  • Mawaziri Sofia Simba na George Mkuchika wanahaha na waandishi kumtisha Mengi kwa "kuwachafua wananchi", bila shaka kuna bakshishi itafuata kwa juhudi zao hizo.
  • Huko bungeni mawaziri Kombani na Hawa Ghasia wanaweka mkakati wa "kumshughulikia" Dr Slaa.
Nauliza, hivi kwa mwendo huu kutakua na maisha bora kwa kila Mtanzania ifikapo 2010?... Ni saa ngapi hawa mawaziri wanaumia vichwa kutatua matatizo ya mwananchi wa kawaida?.....Kikwete namsikitikia kwakua hana watu wa kazi kwenye baraza lake, lakini namlaumu fully yeye mwenyewe kwa kuendelea kuilea hii mizigo ya walipa kodi kwenye baraza.

Hakuna waziri hapo. They are all political charlatans! Aibu tupu kuona jinsi nchi yetu ilivyogeuzwa kuwa banana republic na hii mijitu!!
 
Unastahili kupelekwa Mirembe maana naona hizo pesa za mafisadi zinakuharibu akili. Sasa unaonyesha kila dalili za punguani. Pole sana. Wahi Mirembe kabla hujaharibikiwa kabisa.

Mkuu Bubu you utterly nailed it. Tunaweza muona yupo ok kumbe ndio anadata kimtindo.
 
GT ni msomi mzuri tu ; lakini VIJISENTI vya wakina Manji vinamtesa anakuwa punguani!!

Kwi kwi kwi, hawezi kuwa msomi kwa argument kama hizo. It makes no difference, anyway I pity him
 
Back
Top Bottom