Wabeba mabox vs wala vumbi: Chuki ya nini??

Wabeba mabox vs wala vumbi: Chuki ya nini??

alafu mkimaliza kubeba hayo maboksi mrudi na hela muwekeze nyumbani kwenu!CLEAR?
kwa hili nawatetea wabeba maboksi........kuliko uwekeze tz bora ukawekeze Somalia....
 
Nafikiri tatizo ni kwamba watu wanashindwa kuelewa mbeba maboksi ni mtu wa aina gani na yule mla vumbi pia. Ni yule mtu ambae "by chance" ameingia Ughaibuni na anachakarika.

Mbeba maboksi ni yule mtu ambae yupo Ulaya (hasa kwa UK) ama kwa muda mfupi (mwanafunzi) au mrefu (wale wenye ukaazi wa kudumu na wanashindwa kupata kazi nzuri kutokana na sifa haba) na anafanya kazi katika maeneo mbalimbali kwa mfano kwenye maghala, viwandani, ujenzi, uyaya, utunzaji wazee na wasiojiweza na hulipwa ujira kulingana na masaa anayofanya (worker) iwe ni GBP kuanzia (kwa sasa) 5.73 hadi 11 kwa saa.

Malipo kwa vibarua huchukua kati ya wiki au wiki mbili na unaweza kuishia na kati ya 250 au 350 GBP hizi ukiangalia na uchumi wa Tanzania utajua ni kiasi gani mtu anapata.

Mla au wala vumbi sijui ni walio katika kundi gani kwa hio sitaingia sana huko mpaka pale mtu yeyote atakaponipa maelezo kwamba ni watu wa aina gani.

Sasa tukirudi kwa mbeba maboksi utaona kwamba ukipata pesa ya ujira wa kazi yako hapo inabidi uzingatie vitu muhimu kama pango la chumba au nyumba ambayo utakuwa unachangia na wabeba maboksi wenzio, nauli ya kusafiria au kulipia mafuta ya gari kama unalo, bills za simu, gesi na umeme na kama ulichelewa kuwaambia watu wa halmashauri kwamba wewe ni mwanafunzi basi itabidi ulipe Council Tax.

Pamoja na mambo mengine mengi tu ukifika mwisho wa mwezi kulingana na kipato chako, ndio unaangalia masuala kama Western Union kwa ndugu nyumbani TZ na projects zozote kama utakuwa nazo huko.

Sasa kwa wale wenye ukaazi wa kudumu au "indefinite leave to remain" kama inavyojulikana au uraia kabisa, mambo ni mazuri kiasi kwenye masuala fulanifulani kama vile shule ambako utakwenda kwa hiari yako na fee haitakusumbua kwa maana kwamba itabidi uchukue mkopo.

Pia kwenye masuala ya nyumba kidogo kuna unafuu kwa kuzingatia kwamba sheria kwa sasa inawaangalia sana wale wenye ILR na raia wa UK kuliko wale wenye "time limit".

Sisi binadamu tunapofanya kitu chochote chenye kuwa na "positive impact"
naona kuna vitu vitatu ambavyo kwa kiingereza naviita motive, means and opportunity.

Kwa hio aidha uwe ughaibuni au Tanzania ukiweza kuangalia motive au dhamira yako ni nini je ni kuishi Ughaibuni na kutengeneza maisha ya Tanzania na utakuwa na nyenzo gani iwe ni elimu, au ajira na pia kama kuna "opportunity" au nafasi ya kufanya hayo au utaendelea kuishi katika mazingira ambayo hayamnufaishi kila mtu basi utakuwa na matokeo mazuri au mabaya.

Ukiangalia wale watanzania ambao wamesomeshwa na serikali katika nchi mbalimbali duniani ingawa ni kwa shida sana, wengi wao wameweza kurudi nyumbani na kuingia katika mazingira yaleyale walioyaacha ya ukiritimba wa kupita kiasi, rushwa na madudu mengine na wao kuwa sehemu ya "system" ileile. Ila kwa watanzania wengine tuishio ughaibuni tunaamini kwamba maendeleo yataletwa kwa kuonesha mfano na baadhi yetu wamekwishaonesha hayo.

Kwa hio nikihitisha maoni yangu hapa naona kwamba ni kheri mtu anaeishi Ughaibuni akitengeneza dorali au paundi huku akijenga nyumbani kwa kuwekeza na kuwa na vitega uchumi ingawa anakuwa na barriers kibao ambazo zinajulikana.

Beef haitakuwa kubwa baina ya makundi haya kwa kuangalia impact itakayokuja kutokana na mwamko wa mheshimiwa mtarajiwa Mwakalinga ambae ameonesha njia na sie wengine tupo nyuma kuwekeza Tanzania katika nyanja mbalimbali na mwishoe kuisimamisha nchi yetu kutoka katika dimbwi la ujinga uliotukuka.

Nnapenda kuona kwamba wale waliopo nyumbani Tanzania wanaelewa kwamba Ughaibuni mambo ni mswano tu kama utajitahidi kusoma au kwenda professional na ili ulipwe si chini ya GBP 1500 kwa mwezi kwa kazi za kawaida tu.

Pia tusisahau kwamba wale waishio ughaibuni wana exposure kubwa sana, na ukiangalia mfumo mzima wa kodi unavofanya kazi, mfano tu kwenye suala la kodi ya maendeleo huwa napenda sana.
 
Last edited:
Jamanie tuache husda na fii, sababu mbali mbali zinapelekea watu kuishi nje ya nchi zao, ikiwa ni pamoja na ndoa, afya, kazi, elimu, ulinzi na kadhalika. Mtu kama anabeba box, daktari, developer au vyovote vile shida iko wapi? Kwa njia moja au nyingine nao wanachangia kwenye uchumi wa taifa letu: investments mbali mbali, ajira zinazotokana na project zao, na pesa wanazotuma kutoka huko waliko.

Kabla hatujarusha mawe kuwapiga wenzetu kwenye hili la kujenga nchi kila mmoja wetu ajiangalie yeye binafsi ni vipi anachangia kwenye ujenzi wa taifa. Watumishi wa uma serikali na mashirika yake wengi uwajibikaji hakuna. Watu wanajiendea wanavyotaka, hujui mtu kaingia saa ngapi au katoka saa ngapi kazini. Wengi wakienda lunch ama wanaextend muda au kibaya zaidi wanaishia. Unakuta mtu anaexcuse kibao asiende kazini, mara kafiwa na jirani, mara anauguliwa au analeta ed kutoka kwa daktari asiende kazini, ukifuatilia amekwenda Zenji. Je kuna appraisal za kupima utendaji wa watumishi na uwajibishwaji? Watu wanalipwa mishahara kwa kazi wasizofanya huu ni wizi na huku ni kubomoa nchi, nchi inajengwa na wananchi wake wenyewe.
 
Nina njozi. Siku moja wabeba maboksi wote watarudi nyumbani. Naam watarejea kujenga Taifa. Mungu ibariki Tanzania. Wabariki na watu wake waliosambaa ughaibuni!

I have a dream. One day all box lifters will come back home. Behold they will return to build the nation. God bless Tanzania. Also bless its people who are scattered abroad!
 
alafu mkimaliza kubeba hayo maboksi mrudi na hela muwekeze nyumbani kwenu!CLEAR?

Ungewashauri haya waTZ waliopo bongo waliokusanya over 50 billions in a short time kwa njia ya DECI. Wengekuwa makini na serikali makini huo ni mtaji murwa kabisa wangeweza hata kununua HISA Wallstreet ya Charlotte kwa akina Mashaka..he he he..
 
kwanin unasema hivyo mkuu?

Watu siku hizi wanaangalia wawekeze wapi watakapopata faida yenye akili. Hii ndio inayoitwa nguvu ya masoko na opportunity costs optimization. Sasa wewe kalaghabaho!
 
Nina njozi. Siku moja wabeba maboksi wote watarudi nyumbani. Naam watarejea kujenga Taifa. Mungu ibariki Tanzania. Wabariki na watu wake waliosambaa ughaibuni!

I have a dream. One day all box lifters will come back home. Behold they will return to build the nation. God bless Tanzania. Also bless its people who are scattered abroad!

Wewe ombea mafisadi watoweke. Achana na wana ughaibuni. Kula sahani moja na mafisadi ambao ndio wanaibomoa nchi.
 
Nina njozi. Siku moja wabeba maboksi wote watarudi nyumbani. Naam watarejea kujenga Taifa. Mungu ibariki Tanzania. Wabariki na watu wake waliosambaa ughaibuni!

I have a dream. One day all box lifters will come back home. Behold they will return to build the nation. God bless Tanzania. Also bless its people who are scattered abroad!
Mie naombea wabaki huko huko ughaibuni, maana kila aliyokuwa ughaibuni aseme arudi home, soko la ajira litakuwaje? Hivi sasa mtu ukimaliza chuo kupata ajira kimbembe, je wakija wa kutoka ughaibuni itakuwaje? Maana hivi sasa hapa bongo kuna baadhi ya sehemu kama kuna nafasi za kazi wa kwanza kupata ni yule aliyotoka na vyeti ughaibuni ndio wanapewa priority hawaangalii kasoma chuo gani wala nini, hao ilimradi kasoma majuu na english inapanda.
 
Mie naombea wabaki huko huko ughaibuni, maana kila aliyokuwa ughaibuni aseme arudi home, soko la ajira litakuwaje? Hivi sasa mtu ukimaliza chuo kupata ajira kimbembe, je wakija wa kutoka ughaibuni itakuwaje? Maana hivi sasa hapa bongo kuna baadhi ya sehemu kama kuna nafasi za kazi wa kwanza kupata ni yule aliyotoka na vyeti ughaibuni ndio wanapewa priority hawaangalii kasoma chuo gani wala nini, hao ilimradi kasoma majuu na english inapanda.

Wakirudi watatutengenezea ajira milioni 1 za kubeba maboksi!
 
Mimi nadhani kuna jelousy fulani watu walio bongo wanaifeel kwa watu ambao wapo nje, nasema hivyo kwa sabu hiyo term Mbeba Boxi inatumika TU kwa watu wanaofanya kazi nje.
Hata siku moja sijawahi kuona mtu anayefanya manual labour bongo akaitwa maneno ya kejeli, lakini ukifanya nje taabu! Hiyo Mla Vumbi inatokana ni defensive response ya wabeba box, na wao si lazima wapate cha kusema bwana!
sahihi kabisa
 
Mitundiko 72 kwenye hii maada ila ni yaleyale mivutano kati ya walio ughaibuni na wale walio Tanzania. Waliochangia bila unazi (objective) ni wachache sana. Suala hapa ni uchaguzi(choice) , mtu kaona akiwa nyumbani maisha hayamuendei sawa kama alivo ughaibuni kaamua kukaa huko tatizo nini kama mtu huyo anafurahia maisha yake? Mwingine nae kaona yakukaa ughaibuni kubeba box hayawezi kaamua kujikalia nyumbani na anaona ni afadhali kuliko ng'ambo safii hakuna shida!

Wengine wameng'ang'ana tu ooh rudini nyumbani muwekeze! dah we unafikirri suluhisho hilo linaweza kua la tija kwa kila mtu? au ndo yale mambo ya TZ mama mmoja anaanzisha biashara ya kupika vitumbua basi ukiamka asubuhi inayofuata ni wamama wote wanachoma vitumbua? tuwe wabunifu kidogo watanzania jamani! na tukubali mitindo, njia tofauti za kujitafutia riziki! tusiwe na mawazo mgando!
 
hadi kufikia hatua ya kuitwa wabeba mabox ujue ni idadi kubw aya wabongo wanafanya shughuli hiyo huko nje. nadhani hiyo chuki imekuja baada ya baadhi yetu sisi tunaoitwa wala vumbi kugundua kuwa hao wabeba mabox wanapokuja bongo wanakuja kwa mbwembwe nyingi na nyodo ilhali kazi wanazofanya huko nje ndio kama hivyo. maadam tumeshajuana basi hizo chuki zife tu tubaki kufarijiana na kupeana mawazo mapya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom