Hajui ni kwanini hayo mataifa yanaitwa first world...
Watu kama hawa, wakati watanzania walio wengi wanahangaika na umeme wa kuchombeza, wao wanayo majenereta waliyoyanunua kwa pesa za kifisadi, wakati watanzania walio wengi hawana miundo mbinu rasmi ya maji safi na salama, wao wanatumia maji ya kununua kwa pesa za kifisadi, wakati watazania walio wengi wanatibiwa magonjwa makubwa kwenye vituo vya afya na zahanati, wao wanakwenda huko "first world" kutibiwa mafua... Hajui kwamba hayo mataifa yamepewa status ya "u-first world", sio kwasababu kuna watu wachache wametusua kimaisha, bali ni kwasababu taifa zima limetusua kwa ajili ya wananchi wake wote.
Alafu huyu mtu utamkuta yuko hapa jf busy kutetea makitu ya uovu na ya ajabu kabisa yanayotendeka kwenye hili taifa lenye uchumi na watu maskini...