Wabeba box wengi wamerudi na ndoto...

Wabeba box wengi wamerudi na ndoto...

. ... Hahahaaa boxxxxxxx waludi bongo tu kuna maisha wakikomaa wanatusua tuu mwisho wa siku maisha hayagandi ... Jamani njoooni home!!!
 
wabongo majungu wanaongoza lkn me natambua maisha popote pale
 
mbona kama mna upendo hamtoi michongo kwa waliopo zaidi zaidi ya figisu figisu tuu hapa..
 
Maisha popote haijalishi una beba box.au unakula fumbi shika panapo shikika utusue.
 
Tatizo kubwa wabongo walilonalo ni "Inferiority complex"..sasa hapa ni udhaifu wao kwa wabeba mabox sijui tatizo ni nini, wakikaa huko EAC pia udhaifu kwa wakenya,waganda etc..you guys need to grow up and stop that shiit...time for change.
 
Hahaaa age. Inaelekea kibraaa.....jf bna! Ila wabonggo tunabaniana nakumbuka 2012 kuna gepu limetokea botswana kuhusu mambo ya wanyama (vetinary) washikaj wote walioko botswana nilipowachek no respond....anyway huu uzi umenikumbusha miaka hiyo
Sasa na wewe Botswana na vetinary yako ungeenda kufanya nini? Kule huwa wanatafutwa watu wa Veterinary mkuu ndo maana jamaa unasema walikubania, lakini ukweli ni kwamba walishindwa wakuweke wapi maana vetinary kwa kule haina deal labda hapa Bongo!
 
Ndugu zangu wawili wamesharudi nabanana nao hapa nyumbani kwangu,walichoambulia ni kengereza tu na stori za london hakuna la zaidi

Honestly, one can detect so much hate kwenye post za namna hii na kwenye comments kama hizi...

...is it possible labda kuna vitu unaviona wanavyo hao nduguzo na haikufarahishi, vinakufanya ujione inadequate and inferior? Au labda unaona hao ndugu zako hawa-deserve kuwa na hiyo experince/exposure ya uingereza na kuongea hiyo lugha ngeni? Au labda wewe kuongea vibaya kuhusu hao ndugu zako kunakufanya ujisikie vizuri?

Inamaana hao ndugu zako hawana namna kabisa ya maisha? Au ndio wamerudi kutoka masomoni na wako kwenye harakati za kuendelea kutafuta maisha? Maana wewe unavyoongea, ni kama vile hao ndugu zako walienda huko uingereza kwa kazi maalumu kujiharibia maisha, na sasa wamerudi wakiwa wameshatimiza azma yao.
 
Kwanza elewa maisha yako popote na hakuna elimu kubwa kama kutembea ukiwa na malengo chanya. Ninachofahamu Watz tuna roho ya kwanini kwani hata uzi wako unaonyesha kabisa kuwa hauwatakii mafanikio isipokuwa wafeli maisha na kulingana na wewe ama uwazidi kimaisha. Kwa kifupi ni hivi hata mimi niite mbeba box lkn tayari nina mpango wa kupeleka mdogo wangu kusoma ng'ambo baada ya kupewa offer hiyo kupitia mwenyeji wangu na kuzamia kwangu aka kubeba box. Ninachokiomba kwa mungu ni afya na anilinde kufikisha malengo yangu, nikifanikiwa asante mungu nikikosa pia asante mungu na sitakata tamaa japo sijutii na naona nilichelewa.
Mungu siyo mungu!!! Yote Kheri!!!
 
ukuta wa mafanikio Tanzania ni mgumu kuriko ukuta wa Leceister team..chuki na roho mbaya ndio iliyotawala..nenda jozi..thailand..hong kong..Vietnam hata Cambodia maisha yapo kuriko hapo mtabaki kuanzia nyuzi za kuchukia waliofanikiwa na kutoa mifano ya waliofeli mbona bongo hapo watu wamefeli maisha toka utotoni mpaka uzeeni..
 
Asikudanganye mtu,wengi choka mbaya.
Mtu anasota miaka kumi,ndio kwaanza ananunua kiwanja Chanika,wakati wewe una nyumba tayari.
Wengi wanaona aibu kurudi,lakini ukweli ni kwamba wanapoteza muda mwingi kwa kipato kikubwa na makato ya kodi makubwa na matumizi makubwa.
Bongo nouma wewe,Mama lishe anamiliki nyumba kwa mtaji wa laki moja,maisha ni kujipanga tu mkuu.
Waliotusua Majuu na South ni Zamani sana,ila kwa sasa hakuna issue kabisaaa.
 
Mleta hoja kuna kitu kimoja ngoja nikuambie ambao watu wengi hawakifahamu.

Maisha ya kutoka nje haina maana ndio utafanikiwa, hapana.

Wengi wanaofikiri hivyo nafikiri hawayajui maisha ya nje, au maisha kwa ujumla.

Maisha popote, usiogope kujaribu na usiogope kwa kuona kutoka kwa mwenzako, au unaemfahamu ambae kwa upande wako unaona hakufanikiwa kimaisha, au kushindwa kama unavyodai.

Ukweli ni kwamba pamoja ya kutoka nje na kutokufanikiwa kama unavyotaka wewe ukumbuke, mwenzio aliejaribu kutoka amejifunza mambo mengi sana, kiuchache kuanzia mazingira, mfumo wa maisha, na mengine mengi ambayo yule ambae hakuwahi kujaribu maisha ya nje kiasi kwamba anaweza danganyika kirahisi, kwa chochote atakachokisikia.

Na pia kuna mengi huwezi kuyafahamu mpaka pale utakapojaribu wewe mwenyewe, ndio utakutana nayo, huwezi kuhadithiwa/kusimuliwa.

Maisha ya kutoka ni Elimu tosha, na upeo wa alietoka (maisha ya nje) unakuwa mkubwa sana kulinganisha na yule ambae hakuwahi kujaribu maisha ya nje.

Changamoto za kimaisha ni nyingi iwe nje, au ndani ya nchi, nikiwa na maana hakuna maisha rahisi.

Kwahiyo bidii yako popote hapa Ulimwenguni utafanikiwa.

Nenda nje ya nchi, na uwe mtu wa bidii na kujituma nakuhakikishia utafanikiwa
 
Sasa na wewe Botswana na vetinary yako ungeenda kufanya nini? Kule huwa wanatafutwa watu wa Veterinary mkuu ndo maana jamaa unasema walikubania, lakini ukweli ni kwamba walishindwa wakuweke wapi maana vetinary kwa kule haina deal labda hapa Bongo!

umeona vetinary tuu, tena imewekwa kwenye mabano. mengne haukuona.?? busara muhimu.
 
Hivi hata kama mtu kalosti kivyake, maisha yake, tatizo kubwa litakalofanya pilipili ya shamba imuwashe mtu ni lipi?

Au ushambenga tu?
Mkuu watu wanajua kufanya generalization sana tu.... Mimi nimesafiri nje Mara nyingi Na kuonana Na watanzania huko wanaishi vyema tu. Tatizo wengine wanataka pa kuongea kuputia wachache waliorudi wakiwa na hali ambayo sio nzuri kifedha. Wanadahau wengine wamelizwa na ndugu zao when they were sending money kujenga na hakuna kilichofanyika....
 
Hivi bongo hakuna waliofulia na hawajawahi kwenda ng'ambo? Je hakuna wabongo wabeba box? No wonder wachina wanauza karanga kuongeza kipato!
 
Hivi hakuna bongo hakuna waliofulia na hawajawahi kwenda ng'ambo? Je hakuna wabongo wabeba box? No wonder wachina wanauza karanga kuongeza kipato!
Wapo wamejaa tele nakutana nao kila siku huku mitaani.
 
Back
Top Bottom