Jolebatawi
JF-Expert Member
- Dec 10, 2011
- 549
- 230
Wadau Dr Harrison Mwakyembe aliyeongoza mashambulizi kwenye sakata la Richmond lililomchachafya Lowasa naye ameumbuka,Kuumbuka kwake ni kutokana na kubeba msimamo wa chama chake wa serikali 2 na kupuuza maoni ya wananchi tuliyoyatoa na zaidi ya yote kuyaasi maandishi yake kwenye Thesis yake yanayoelezea msimamo wa serikali 3 ndiyo jibu la matatizo yote.SWALI LANGU NI JE,Nani ni mnafiki zaidi kati ya FISADI WA KALAMU (MWAKYEMBE) NA FISADI WA FEDHA(LOWASA)? Note:Ikumbukwe kwenye suala la ufisadi ndani ya CCM hakuna mwenye uthubutu wa kumnyooshea mwingine kidole!MWAKYEMBE TUNAHITAJI MAJIBU YAKO,AU ULIKUWA HUKIJUI ULICHOKUWA UNAKIANDIKA KWENYE THESIS YAKO? Huku mtihani wa kipimo cha unafiki wa SITTA utatokana na jinsi atakavyoliendesha bunge la katiba hadi mwisho wa mchakato!