Wabaya wa Lowassa wazidi kuumbuka

Wabaya wa Lowassa wazidi kuumbuka

Na yeye ni mwanadamu hawezi kuwa mkamilifu kwa kila nyambo

Ni andiko lake mkuu,kimsingi anastahili kuvuliwa hiyo PHd aliyopata kutokana na kuandika asichokiamini mkuu ,ni aibi kubwa mno afadhali angekua ameropoka mtaani mkuu ,kukana andiko la Phd ni dhambi kubwa mno
 
MANTIKI HAPA NI NINI? KUMSAFISHA MAMVI? Pengine mwishowe mtafanikiwa
 
utter stupidity! thesis ya doctorate yake inahusiana nini na Dr kama Waziri na msimamo wa serikali na chama chake..kingine hii connection ya lowassa, katiba mpya, serikali 3 na mwakyembe umeshindwa kuijenga, eti fisadi wa kalamu..Fisadi kwaambie maboss wako atabaki kua yule wa pesa kwa sababu economc crimes zinadidimiza uchumi na kuathiri siasa, uongozi, na maendeleo ya jamii kwa ujumla...wapuuzi kama nyie mko wengi sana na jamii mara nyingi uongozwa na mpuuzi mkuu miongoni wa wapuuzi kama huo boss wako
 
Prezdaa LOWASA,..mungu amjaalie maisha marefu!naamini katika ndoto zake..
Stuttgart,Germany
 
PhD nyingi za Bongo ni FEKI.

Msiamini kwamba waliandika wao baada ya utafiti..

Thesisi na Disertation wanaandikiwa kwahiyo wenyewe wanapresent tu...wala hawajui yaliyomo...na wala mawazo siyo yao.

wacha uwongo!! PhD ya ujerumani ile sio ya Bongo au ya Online. linganisha quotation ya Kigwangala na Tundu Lisu - mmoja wapo atakuwa mwongo kama alivyotaka kulivuruga Bunge wakati mwongozo ulikuwa very premature.
 
Wadau Dr Harrison Mwakyembe aliyeongoza mashambulizi kwenye sakata la Richmond lililomchachafya Lowasa naye ameumbuka,Kuumbuka kwake ni kutokana na kubeba msimamo wa chama chake wa serikali 2 na kupuuza maoni ya wananchi tuliyoyatoa na zaidi ya yote kuyaasi maandishi yake kwenye Thesis yake yanayoelezea msimamo wa serikali 3 ndiyo jibu la matatizo yote.SWALI LANGU NI JE,Nani ni mnafiki zaidi kati ya FISADI WA KALAMU (MWAKYEMBE) NA FISADI WA FEDHA(LOWASA)? Note:Ikumbukwe kwenye suala la ufisadi ndani ya CCM hakuna mwenye uthubutu wa kumnyooshea mwingine kidole!MWAKYEMBE TUNAHITAJI MAJIBU YAKO,AU ULIKUWA HUKIJUI ULICHOKUWA UNAKIANDIKA KWENYE THESIS YAKO? Huku mtihani wa kipimo cha unafiki wa SITTA utatokana na jinsi atakavyoliendesha bunge la katiba hadi mwisho wa mchakato!

Wabaya wa Lowasa kwa sababu walisema ukweli ama? Kama wao wana matatizo hiyo siyo nyenzo ya kusema walikosea kumkosoa EL. The guy is a thief period. Mengine haya ni maloloso tu. Kama asingekuwa mwizi asingejiuzulu.
 
wacha uwongo!! PhD ya ujerumani ile sio ya Bongo au ya Online. linganisha quotation ya Kigwangala na Tundu Lisu - mmoja wapo atakuwa mwongo kama alivyotaka kulivuruga Bunge wakati mwongozo ulikuwa very premature.

Chuo kilichomtunuku ndo kiko ujerumani..ila Amefanya utafiti bongo. Ndo maana kuna mashaka kama kweli mtu umefanya utafiti wa jambo mwenyewe na kupata jawabu itakuwaje adisprove aliyoyafanyia utafiti bila utafiti mwingine!!???

CCM wanawatumia vibaya wasomi,wanafanya Academicians wa Tanzania waonekane kundi la watu wasiyo na thamani.

Mtu kama Shivji sasa hivi anatumika kwa nyuma ya pazia kupotosha wakati hapo kabla alikuwa mstari wa mbele kutumia elimu yake kukomboa fikra za wengine.
 
Ninaamini kama huujuu ukweli halisu juu ya Lowassa utamshambulia vilivyo, lakini naamini pia cku ukweli juu yake utakapo mature egnough kuwa constructive, wapo watakao jilaumu kwa machozi kwa kunena yasiyo juu yake...its matter of time.kitakacho mharibia Lowassa ni kimoja tu kama hatokidhibiti...ni iwapo atashindwa kujizuia asilipe kisasi kwa watesi wake, othwise no one like him
....we trust EL
 
Hivi unawelewa kuwa misimamo hubadillika?

Wakati anaandika thesis yake alikuwa anatafuta ukweli ili nchi ifaidike na utafiti wake. Sasa hivi anaficha ukweli ili chama chake kifaidike na unafiki wake. Msimamo wa kisomi na kitafiti hauwezi kubadilika bila ya kuwa na utafiti mwingine wa kuonyesha yaliyoandikwa mwanzoni yalikuwa na walakini.
 
mwakyembe njaa tu,alimwandama fisadi lowassa ili apate uwaziri,ile sumu haiishagi mwilini,it' just a matter of time
 
Wakati anaandika thesis yake alikuwa anatafuta ukweli ili nchi ifaidike na utafiti wake. Sasa hivi anaficha ukweli ili chama chake kifaidike na unafiki wake. Msimamo wa kisomi na kitafiti hauwezi kubadilika bila ya kuwa na utafiti mwingine wa kuonyesha yaliyoandikwa mwanzoni yalikuwa na walakini.
Thesis zingine huwa ni za kutafutia degree tu...

hapo ndipo tujifunze aina ya maprofesa tulionao hawasimamii wakitoacho bali kiingiacho tumboni.
 
"Ni kweli,mwakyembe baada ya kupewa uwaziri misimamo yake ikabadilika,Shivji baada ya kwenda kwenye kongamano la vijana Dar lililoandaliwa na wizara ya habari,utamadun na michezo pia misimamo yake ikabadilika" ONLY IN TANZANIA

Kukuongezea je unafahamu msimamo wa katibu mku wa cuf maalim seif wa mwaka 1984 kuhusiana muungano ? Na msimamo wake wa sasa ?
 
Kwanini Lowassa ameingizwa hapa? kuna agenda gani na Lowassa? tufikirie kwa mapana jamani,
Huku kwenye JF kuna mtu alishawahi kuni PM akaniambia mimi nazubaa huku wakati watu wanachangamkia mahela kwa Lowassa...Nilimtolea uvivu palepale kuwa Lowassa hawezi kununua utu wangu.
Kwa hiyo jamani tuwe makini na watu wanaotaka kumsafisha Lowassa kwa kutumia njia mbalimbali huku
. Lowassa akitubu kwa Mungu na kuwaomba Watanzania Masamaha halafu akurudisha mali zote kwa watanzania alizozipora kwa njia haramu mbona atasafishika lakini siyo kwa ujanjaujanja anaoutumia
 
Kwa kawaida wasomi ndio wanaoiangusha na kuiangamiza nchi, sio wakulima wala wafanyabiashara. Angalia Shivji na Dr. Mwakwembe ni wanasheria waliobobea lakini unafiki ndio unawaponza.
 
huu ujinga siwezi kujizuia kusema neno..uliyeandika thread mapenzi yako kwa lowassa yamekufanya mtumwa
 
Back
Top Bottom