Waandishi wa Habari na Bahasha: Sio Kila Bahasha ni Rushwa

Pasco mkuu, ukatae ukubali siku hizi waandishi bila bahasha hawatoi habari/pichaz..maslahi yamewekwa mbele kuliko taaluma..
 
Tena waandishi huwa wanaambiana wapi watoa bahasha na wapi hawatoi na sehemu wasizotoa bahasha huwa hawaziandiki habari za kutoka hapo, na sehemu kama ubalozini TRA na mashirika mengine yenye pesa huwa wanaenda wahariri maana huko wanajua kuna bahasha zilizotuna zaidi.
 
Mkuu Ngambo Ngali, kujua nini ni rushwa na nini sii rushwa hauhitaji kuisoma definition, rushwa ni fedha inaotolewa kwa malengo ya kuifluence the natural course of action, sasa hizi bahasha za usafiri, chakula au vikao, ni kwa lengo la kuwezesha, empowering na sio ku influence positive coverage!. Kama uwezeshaji wowote ni rushwa, then Tanzania yote tukula rushwa maana kufuati umasikini wetu, makusanyo yote hayatoshelezi uendeshaji wa nchi, hivyo kuna budget deficit ambayo inakuwa covered the general budget support fung inayotolewa na mataifa ya ulaya, hivyo nchi yetu nzima tunahongwa!.

Pasco, corruption is not a term of art, it is not an agricultural term, it's not a medical term. It is purely a legal term. Legal terms are defined in accordance with the statutes which create them, as you may be aware, since you are a lawyer, most of the statutes have an interpretation section which normally define some words which may bring difficulties in understanding them. If there is no definition then recourse is on the dictionaries legal or ordinary.

That being the position, for your benefit corruption has been defined by section 15 (1) of the Prevention and Combating of Corruption Act act no 13 of 2007. You are at liberty to read and understand it.

Pasco, you find it difficult to agree that what you have been doing constitutes corruption, this is because you the accused in this case. As a lawyer you have to know that you can never be a judge of your own case.

This is a very elementary rule, in case it skipped your mind I take this opportunity to refresh your memory to the effect that this is a cardinal rule which you should not ignore.In such a situation it would be proper for you to take all the arguments in here and ask someone to opine as to whether or not the acts constitute corruption.
 
Usianzishe Jihad vs Crusade, walioanzisha tangu enzi za Continapole wameshindwa itakuwa wewe?. Si unaona jinsi Mazayuni wanavyowatesa ndugu zenu kule Mashariki ya Kati?, si umeona ana wanaopigania Uislamu wanafanywa nini?, amekiona kilichompata Saadam, Osama na juzi juzi Ghadafi?!, bado unataka kutangaza vita?.

Naomba tutafungua thread nyingine tufanye vita kati ya Uislamu na Ukristu, ipi ni dini ya kweli ya Mwenye Enzi Mungu tuone nani atashinda, au hata tuwashindanishe Mtume Mohammed (SAW) na Nabii Issa Bin Maryam (AS) tuone nani ndio mwenye darja ya juu kwa Mwenyenzi Mungu, (Allah subhana wa ta'ala). kwa sasa hebu tujadili hizi bahasha bila kuingiza udini!.

Usitafute pakutokea, umelianzisa mwenyewe, na hayo ya dini ulipoyaanzisha nilijuwa unatafuta pakuchomokea kwani umejuwa FF hata kaa kimya. Wewe ni mla rushwa hata useme nini> hata Yesu kwa hili haji kukusaidia. Kila mmoja atabeba msalaba wake!, wako umeanza kukuwakia moto, maana mpaka uanze kubwabwaja namna hii? vibahasha hivyo unavyovipokea na kuvigawa ni moto huo unakuwakia, dhulma huanza kulipwa hapa duniani.
 
Mkuu Mzalendo80, Pasco wa jf ni mwandishi wa kujitolea wa jf, silipwi chochote na yeyote

Mkuu Lunyungu kwanza pole kwa hii, yote usemayo ni kweli mimi kama mwanahabari, nimeisha vipokea sana hivyo vibahasha na mpaka hapa nilipofika sasa mimi ndio navigawa hivyo vibahasha.

Sasa wapi kwenye ukweli hapo? Unajitolea na ulipwi na huku unapokea vibahasha na kuvigawa. Wapi tukuelewe?
 
Usitubabaishe kwa maneno, hizo bahasha unalipwa na nani?



Mpaka hapa nimeshaelewa mtoa vibahasha mzuri kwa Pasco


Mkuu Mzalendo80, Pasco wa jf ni mwandishi wa kujitolea wa jf, silipwi chochote na yeyote!. Hata utetezi wangu kwa Lowassa, wale mnaoamini nalipwa, kutokana na uwezo wenu wa kufikiri, endeleeni kuamini hivyo maana huo ndio uwezo wa fikra zenu!. Lakini wanaofikiri kwa kutumia logic zaidi, nadhani watakubaliana na mimi kuwa namtetea Lowassa for a reason, na kupitia hiyo reason behind, Lowassa hawezi kunilipa mimi nimpigie debe humu jf!.
 
FF naona leo umeamua kufa na Pasco
sio rahisi kwake kukubali. angalia wote wanaofanya ufisadi tanzania watakuambia
ni juhudi zao binafsi na akili huku wakijua wazi wanalipipana na kutuibia hata visivofaa kulipana
kina pasco wao wameshahalisha bahasha kama stahili zao
kwao haingii akilini kama ni dhambi au hawapaswi kupewa au ni nje ya maadili ya kazi
bila kuwabana kwa sheria kazi bado tunayo.
 
5. Jee ni bahasha zipi ni rushwa?.

Baada ya kuzitaja bahasha ni bahasha genuine, sasa nitaziorodhesha bahasha ambazo ni rushwa.
Bahasha ya Kushinikiza Positive Covarage.
Hii ndio bahasha ya kwanza ya rushwa, hutolewa na source ili kuwa entice waandishi wawafanyie favourable covarage. Kwa kawaida bahasha hii inakuwa nene fulani, bahasha hii huandamana na obligation kuwa lazima story itoke. Bahasha hizi za shinikizo la story kutoka hazitolewi kwa waandishi wote, bali to only few selected, na kwa vile bahasha hizi ni rushwa, hutolewa kwa kificho!. Zile bahasha za halali kama za usafiri husainiwa wazi wazi na hukawiwa kila mtu akiona kwa sababu there is nothing to hide, lakini hizi hutolewa kwa kificho, no one will know nani amepokea bahasha na nani hajapokea kutokana mazingira ya usiri. Watoaji wa bahasha hizi wanajua ni rushwa na wapokeaji wanajua ni rushwa!. (to avoid conflict of interest, nawaombeni msiniulize zaidi kuhusu hizi!).

Najiuliza kwa muda na kupata jibu nusu la kile watu wanashindwa kuelewa. Nijuavyo mimi magazeti huwa yanatafuta habari zenye mvuto ili yapate soko na wasomaji kwa wingi. Sidhani kama unaweza kupeleka habari ya kweli na yenye ushahidi katika chombo cha habari halafu wakudai pesa wewe mleta habari. Isipokuwa, unaweza kutokewa na mazingira ya kudaiwa pesa endapo kama habari unayotaka itolewe ina maslahi yako binafsi. Ama imekaa ki matangazo tangazo, hapo lazima mpunga ukutoke .
 
Waandishi na wana siasa wakiongopa hutumia rule ya "proverbial lies wrapped on truth", Pasco wewe unatumia "proverbial lies wrapped on lies".

Hata aje nani hapa huwezi kumkubalisha!

Pasco anataka kuhalalisha Ufisadi wa Vibahasha kuwa sio rushwa. Pasco huna tofauti na Mafisadi au Polisi anayepokea rushwa au mtoaji
 
Nataka tufike mahali tukubaliane kuwa ili bahasha iwe ni rushwa, lazima iwe na malengo ya kuimfluence, lakini bahasha genuine yenye malengo ya uwezeshaji, sio rushwa!.
Pasco,
Nadhani tumekwishafika hapo. Kupewa grant au usafiri kukuwezesha kufanya kazi yako bila kuambiwa useme hiki na usiseme kile si rushwa. Lakini kama nitaitwa na Wassira, au Nyalandu anataka nifuatane naye kuonyesha kuwa anafanya kazi makini pale Kariakoo kuwaondoa machinga wa Kichina, huku akinipa bahasha, na Wassira ananiambia niripoti nini juu ya shughuli zake, au anakupa tu press release na wewe kama kasuku unaitumia hiyo press release kumpamba Wassira kwenye gazeti kuwa ni kiongozi makini, hicho ni kinyume cha maadili yetu. Naelewa hali ngumu ya kifedha kwa vyombo vyetu vya habari, kwamba Mengi hana slash fund ya kuwawezesha waandishi kulipia usafiri na matumizi mengineyo katika kazi hii, lakini tukiendekeza kupokea bahasha ndipo tufanye kazi yetu tunajilemaza wenyewe. Mfano mzuri ni yule jamaa wa Business Times. Unless kama wewe ulimkatia chochote kama anavyodai dada yetu FF, huo ni mfano wa kuigwa. Alifika pale kwenye press conference yenu akajiondokea na kuandika ripoti yake before deadline. Hivyo ndivyo tunavyotakiwa tuwe.
 
Maridadi sana, hapa napata somo kuwa pengine rushwa japo ni kosa kwa sheria za nchi. Lakini kwa upande mmoja wa shilingi inaweza kuwa na faida pia. Hapa tunaona waandishi wa habari za uchunguzi wanaweza kuhatarisha maisha yao kwa ajili ya kusaka habari nyeti na mara nyingine hulazimika kutoa bahasha ili wapate habari kwa wepesi. Lakini pia hapa kuna jambo dogo nitahitaji msaada kidogo kuhusu matokeo ya faida ya rushwa atoayo mwandishi wa habari za uchunguzi . Kwa mfano: "Ikiwa mimi ni mwandishi wa habari za uchunguzi, nimepata fununu kuhusu taarifa ambazo pengine zinahusu njama zinazotishia usalama wa Taifa. Lakini kwa bahati mbaya yule mtoa taarifa anahitaji apewe bahasha kwanza ndipo anipe habari hiyo. Kwa bahati mbaya wakati nampa rushwa hiyo, jamaa wa Takukuru wananiweka kati na kunifungulia mashitaka ya kutoa rushwa. Mambo yatakuwaje hapo kwa upande wangu ikiwa nilikuwa natoa rushwa ili nipate habari kwa ajili ya maslahi ya Taifa? Je hii ni mfano wa rushwa halali? Samahani japo nimeuliza swali la kisheria, lakini naimani kwa uzoefu wako katika tasnia ya uandishi wa habari bila shaka umewahi kukumbana ama kushuhudia kesi ya aina hii. Nipe japo kwa ufupi.
Mkuu.
Mkuu Juma Kidogo, kama nilikuambia mpaka serikali na maufisa usalama, wapelelezi wanatembeza bahasha za rushwa halali ili kupata habari!. Hata katika baadhi ya matukio ya uhalifu, uhaini, kuna mshitakiwa katika kundi la wahalifu atakayekubali kukiri na kuwageuka wenzake, anapewa rushwa ya kutoshitakiwa na hivyo kugeuzwa shahidi number moja wa serikali PW1!.

Hao maofisa usalama wanaotoa rushwa hawakamatiki na hata ikitokea ukamchomea hawashitakiki!. Kama wewe ni mwandishi wa habari wa investigative sifa yako kuu ni having sharp nose for news na strong curiosity, ukivichanganya utakuwa na uwezo wa machale kukucheza kama unakutana na mtego!. Hata katika mahusiano tuu na mwezi wako kama unadanganywa, (being cheated) lazima utakuwa na uwezo wa kujua, kazi itabaki ni kuthibitisha tuu, na huko kuthibitisha ndio essence ya investigative!
 
Bahasha za Matangazo ya Biashara Kugeuzwa Habari nayo ni rushwa Mbaya inayoua Taaluma ya Habari!

Wanabodi,
Kwa vile hapa nchini hatuna sheria ya kugharimia vyombo vya habari vya umma, hii inamaana vyombo vyote vya habari Tanzania, vinalazimika kutegemea matangazo ili visurvive!. Serikali ndiye mtangazaji mkubwa kuliko mtangazaji mwingine yoyote wa matangazo. Vyombo vya habari vya serikali, gazeti la Daily News na TBC, vyenyewe vina advantage ya ziada over and above vyombo vingine vyote, kwa sababu, japo sina ushahidi wa uthibitisho, but trend inaonyesha kuna "waraka wa siri", unaoelekeza matangazo yote ya serikali, lazima kwanza yaende vyombo vya habari umma na ya ziada ndio ndio yaende vyombo binafsi!, hii ni kinyume cha ushindani huru wa kibiashara!. Advantage ya pili ya vyombo hivi, licha ya kupata preference ya matangazo ya serikali, pia mishahara yao inatoka hazina!, hivyo tunaviendesha vyombo hivi kwa kodi zetu!.

Kufuatia hali hii, vyombo vingine vyote vya habari ambavyo navyo ni utitiri, vinasurvive kwa matangazo hayo hayo, hali inayopelekea kusurvive kwa kugawana umasikini wetu as a result, media zote, zina survive katika lindi la umasikini!. Umasikini huu ndio unaopelekea media zenyewe kushindwa kuwagharimia waandishi wake katika kila assignment na ku compromise ama kukubali kukosa baadhi ya habari, ama kukubali kusaidiwa "bahasha" ili waweze kupata kila habari!.

Media zote haziwezi kulipa mishahara inayotosheleza angalau kujikimu kwa zile basic needs, let alone saving!. Kama mishahara ya serikali ndio hiyo mnayoisikia na wafanyakazi wa serikali wana survive, mishahara ya kwenye media zetu binafsi ni half ya ile ya serikali, ukiondoa IPP Media na Mwananchi!, nayo pia haitoshelezi, hivyo wana habari naweza kusema wote, wanaishi kwenye njaa kali!.

Baadhi ya wanahabari haswa wale ma senior editors wa magazeti wanamiliki vyuo vya uandishi wa habari, wale wapiga picha wanamili vyuo vya picha au photo studios na wale wa Redio na TV wanamiliki production houses na ma senior journalists kibao ama wana survive kwa membership kwenye press clubs, majukwaa ya wahariri, au underground advertising companies na PR companies ili to make both ends meet!. Shughuli zote hizo za pembeni wahariri/ waandishi na watangazaji wanazozifanya sio rushwa ila ni kinyume cha maadili kwa sababu zina cut accross the line of conflict of interest!. At this jancture, naomba nikiri wazi, bado wako waandishi wachache makini ambao wamesimama imara katika maadili, na hawa utawajua ile siku wanapoondoka duniani, wanakuwa wamekuja with nothing, wanaondoka with nothing na wanaacha nothing!.

Kufuatia survival ya media ni matangazo, na kusema ukweli matangazo ni ghali, tangazo la 60 sec prime ya ITV ni 800,000 na TBC ni 600,000 wakati full page ya Daily News/Guardian na Citizen ni 4,000,000 plus!. Baadhi wa maofisa masoko wa makampuni mbalimbali, ambao wameishajua njaa ya vyombo vyetu vya na hivyo ku devise mbinu ya kugeuza matangazo ni habari. Kama unatangazo lako unataka litoke inside news ya ITV utalipia 800,000!, lakini badala ya tangazo ukiwaita waandishi pale moven pick na kuwapiga lunch ya nguvu kwa kisingizio chochote, mwisho wa siku uawapatia kale ka bahasha ka "usafiri" ndani umewakea 100,000 then tangazo lako lita sail inside news for less na with more time!. Ndio maana mnaona kila siku ni habari za makampuni ya simu, makampuni ya bia, na biashara mbali mbali na vihabari vyao na picha magazeti, mara wamezindua hiki na hiki, mara washindi wa bahatinasibu hizi na zile mara wanatoa donation hii na ile etc, hayo yote ni matangazo kuyageuza habari, hii ni rushwa mbaya!.
 
Nataka tufike mahali tukubaliane kuwa ili bahasha iwe ni rushwa, lazima iwe na malengo ya kuimfluence, lakini bahasha genuine yenye malengo ya uwezeshaji, sio rushwa!.
Pasco,
Nadhani tumekwishafika hapo. Kupewa grant au usafiri kukuwezesha kufanya kazi yako bila kuambiwa useme hiki na usiseme kile si rushwa. Lakini kama nitaitwa na Wassira, au Nyalandu anataka nifuatane naye kuonyesha kuwa anafanya kazi makini pale Kariakoo kuwaondoa machinga wa Kichina, huku akinipa bahasha, na Wassira ananiambia niripoti nini juu ya shughuli zake, au anakupa tu press release na wewe kama kasuku unaitumia hiyo press release kumpamba Wassira kwenye gazeti kuwa ni kiongozi makini, hicho ni kinyume cha maadili yetu. Naelewa hali ngumu ya kifedha kwa vyombo vyetu vya habari, kwamba Mengi hana slash fund ya kuwawezesha waandishi kulipia usafiri na matumizi mengineyo katika kazi hii, lakini tukiendekeza kupokea bahasha ndipo tufanye kazi yetu tunajilemaza wenyewe. Mfano mzuri ni yule jamaa wa Business Times. Unless kama wewe ulimkatia chochote kama anavyodai dada yetu FF, huo ni mfano wa kuigwa. Alifika pale kwenye press conference yenu akajiondokea na kuandika ripoti yake before deadline. Hivyo ndivyo tunavyotakiwa tuwe.

Wala sijadai mimi, mimi nimesherehesha tu, hayo ni maungamo ya mwenyewe Pasco, ushahidi huu hapa:

...mimi nikamwambia bosi, nitamlipa mimi!. ...

...kuja kumaliza jamaa wa Bussiness Times akaniaga, fasta, nikamlinda, akaondoka zake!. Wale wengine wakasubiria bahasha nene, by the time zimetoka ni saa 10 jioni!. Tukaondoka zetu.
.
 
Mkuu mimi si mwandishi wa habari lakini siamini kama kazi ya uandishi wa habari haina maadili yanayozuia kupoke chochote kutoa kwa mtu unayechukua taarifa toka kwake
Pamoja na sababu lukuki za uchovu wa vyombo vyetu vya habari ambapo nakubaliana na wewe lakini je maadili ya kazi yana ruhusu?
Naamini umesomea kazi hii na unajua naongelea nini
Mkuu Paulss, waandishi wa habari kama ilivyo professionals nyingine zote, tunazo code zetu of ethis ambazo tunatakiwa tuzifuate, lakini kama zilivyo amri kuu za Mungu zipo na watu wanazivunja, itakuwa ethics?.

Sio tuu vyombo vyetu na waa ndishi wengi wanakiuka ethics, vingi ya vyombo vyetu hata kufuata professionalism ni sifuri!. Mfano kwenye TV news fulani, unakuta taarifa ya habari ya kwa lugha ya Kiswahili, kunawekwa insert mtu anazungumza Kiingereza, hakuna anya translation na new inaisha!. Standard Radio news item ni 60 sec ikizidi 90 sec, Standard TV news item ni 90 sec mpaka 180 kwa big news ukiondoa developing story life coverage!, kuna TV fulani, news za mwenye TV sometime mpaka 6 min!. TV clip ikifika 5 min hicho ni kipindi tosha!, sometimes huwa najiuliza hawa wamesomea wapi habari!. Juzi juzi wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru, nimetengeneza news clip fulani ya Mhe. Lowassa, (mimi nasambaza ready made news clips za kampuni fulani) nikawaita waandishi, nikawapatia na bahasha zao genuine za usafiri!, baadaye nikapigiwa simu na mhariri wa kituo fulani cha TV na kuniambia sorry, news clip yako ya Lowassa, hatutaitumia!, nikauliza ni kwa nini?, nikajibiwa "Mhe huyu ni marufuku kuonekana kwenye TV yetu!". Kusema ukweli mhariri ana mamlaka ya mwisho kuamua news ipi atumie na ipi asitumie, hiyo news ya Lowassa ingewezekana isitumiwe kwa uamuzi wa mhariri tuu kuwa its not worth it, nisingejali, lakini hilo la Lowassa haruhusiwi kuonekana kwenye TV fulani kwa amri kutoka juu?!, nikajiuliza juu kwa nani?, jibu ni moja tuu kwa "wamiliki". Hii inamaanisha baadhi ya wamiliki wanaingilia editorial freedom za vyombo vyao, na wamiliki wengine wanavitumia vyombo vyao for their advantage!.

Sikuishia hapo, mimi pia ninasambaza ready made radio na TV programs za kampuni fulani kwa kuzilipa hizo TV na Radio malipo halali ya program hizo on purely comercial basis!. Hivyo program yenye insert ya Lowassa ndani ya kipindi ambacho ni pre paid kikaenda, baada ya wenyewe kukipreview kipindi wakamuona, nikapigiwa simu kuwa kipindi kile hakitarushwa na ikibidi fedha zilizokilipia zirudishwe!. Nilikubali yaishe, nikawaruhusu insert ya Lowassa iondolewa ili kipindi kiendelee!

Ethics ni kitu kimoja, utekelezaji ni kitu kingine!. Kwa wenye kumbukumbu mnajua Dr. Salim Ahmed Salim alifanyiwa nini na magazeti ya Rai na Mtanzania!, ile inaitwa "concoction" ingekuwa ni nchi nyingine, mhariri yule angeny... debe!, au China anganyongwa!. Hapa kwetu ndio kwanza amekuwa rewarded kwa kazi nzuri!.

Hii ndio Tanzania bwana, ziko bahasha safi na bahasha chafu!
 
Pasco mkuu, ukatae ukubali siku hizi waandishi bila bahasha hawatoi habari/pichaz..maslahi yamewekwa mbele kuliko taaluma..
Rafiki Belinda Jacob (wewe ndie uliyekuwa rafiki yangu wa kwanza nilipojiunga tuu hapa jf!, ila hii lips yako rafiki!, usitutie majaribuni!).
Sio kweli Belinda, habari bado ni bure, habari nyingi media inazozotoa ni za bure, sio kweli ni mpaka bahasha ndipo utoe habari! ila ukweli unabaki kuwa kuna baadhi ya habari media haziwezi kuzifikia mpaka ziwezeshwe!.
Wiki iliyopita nilialikwa Morogoro JK alikuwa anazindua Ofisi mpya ya CAG, kesho yake rais alikuwa anazindua daraja fulani, nikaloby ka usafiri kangu kakaingizwa kwenye msafara!, ile safari kuanza, msafara unakwenda speed 140-160kph!, mbona nilijikalia pembeni na habari ikanipitia kando!. Kwenye ule msafara kuna magari maalum yamebeba waandishi, hapo wamewezeshwa kwa kupewa physical transport ili waweze kucover. Bila uwezeshaji huo, ni TBC na Daily News tuu ndio peke yao wangeweza kucover hiyo news kwa sababu ni media zao pekee ndizo zenye usafiri unaweza kwenda 140-160kph, media nyingine zote zina vigari tuu vinaweza kuzunguka hapa mjini pekee, na labda ITV kama wangetumia zile Vogue za Mmiliki.

Nawaombeni sana mkubaliane na mimi habari ni bure na zinatoka bila kulipiwa, ila bila vyombo vya habari na waandishi kuwezeshwa, pia hatuwezi!
 
Nataka tufike mahali tukubaliane kuwa ili bahasha iwe ni rushwa, lazima iwe na malengo ya kuimfluence, lakini bahasha genuine yenye malengo ya uwezeshaji, sio rushwa!.
Pasco,
Nadhani tumekwishafika hapo. Kupewa grant au usafiri kukuwezesha kufanya kazi yako bila kuambiwa useme hiki na usiseme kile si rushwa. Lakini kama nitaitwa na Wassira, au Nyalandu anataka nifuatane naye kuonyesha kuwa anafanya kazi makini pale Kariakoo kuwaondoa machinga wa Kichina, huku akinipa bahasha, na Wassira ananiambia niripoti nini juu ya shughuli zake, au anakupa tu press release na wewe kama kasuku unaitumia hiyo press release kumpamba Wassira kwenye gazeti kuwa ni kiongozi makini, hicho ni kinyume cha maadili yetu. Naelewa hali ngumu ya kifedha kwa vyombo vyetu vya habari, kwamba Mengi hana slash fund ya kuwawezesha waandishi kulipia usafiri na matumizi mengineyo katika kazi hii, lakini tukiendekeza kupokea bahasha ndipo tufanye kazi yetu tunajilemaza wenyewe. Mfano mzuri ni yule jamaa wa Business Times. Unless kama wewe ulimkatia chochote kama anavyodai dada yetu FF, huo ni mfano wa kuigwa. Alifika pale kwenye press conference yenu akajiondokea na kuandika ripoti yake before deadline. Hivyo ndivyo tunavyotakiwa tuwe.
Mkuu Jasusi, nakubaliana na wewe 100 kwa 100!. Hatua hii, Nataka tufike mahali tukubaliane kuwa ili bahasha iwe ni rushwa, lazima iwe na malengo ya kuimfluence, lakini bahasha genuine yenye malengo ya uwezeshaji, sio rushwa!.
Pasco,
Nadhani tumekwishafika hapo. Kupewa grant au usafiri kukuwezesha kufanya kazi yako bila kuambiwa useme hiki na usiseme kile si rushwa

Tunatatafuta hapa ni the deviding line kati ya uwezeshaji waandishi kutimiza wajibu wao bila influence na uwezeshaji waandishi ili kupata positive covarage nahadi nitafikia kwenye waandishi wanaoendekeza njaa na ile pettycash journalism!.
 
Mkuu Jasusi, nakubaliana na wewe 100 kwa 100!. Hatua hii, Nataka tufike mahali tukubaliane kuwa ili bahasha iwe ni rushwa, lazima iwe na malengo ya kuimfluence, lakini bahasha genuine yenye malengo ya uwezeshaji, sio rushwa!.
Pasco,
Nadhani tumekwishafika hapo. Kupewa grant au usafiri kukuwezesha kufanya kazi yako bila kuambiwa useme hiki na usiseme kile si rushwa

Tunatatafuta hapa ni the deviding line kati ya uwezeshaji waandishi kutimiza wajibu wao bila influence na uwezeshaji waandishi ili kupata positive covarage nahadi nitafikia kwenye waandishi wanaoendekeza njaa na ile pettycash journalism!.

Ikiwa wewe ndio unafundisha waandishi, tutegemee nini? Uozo tu.
 
Mkuu Wacha1, hivi ulidhani wale waandishi wanaosafiri na Obama wanasafiri bure, wanakula bure na kulala bure?. Si wanapewa bahasha nene huko makazini kwao! Wanaotoa hizo pesa za hizo bahasha nene ni kina nani?.

Au unatazama na kusikiliza BBC ukijua ni bure tuu kama sadaka?!. Kila aliye Uingereza anakatwa pesa za kusikiliza na kuangalia BBC, usikilize, usisikilize, utazame, usitazame, unakatwa!.

Naona umekurupuka tena kukurupuka kwenyewe ni asubuhi uko kama ulivyozaliwa na binadamu wanakushangaa. Hiyo Wingereza unayoiongelea ni ya kusadikika hakuna kitu kinachoitwa kodi kwa ajili ya BBC. kuna leseni ya kuangalia TV, kama hutaki kuangalia TV hakuna atakayekuuliza pesa yoyote tena hiyo ni kwa house hold. Hatuwezi kufanya mjadala na mambo ya majungu, wafanyakazi wa BBC wanalipwa mamillioni na wanalipa kodi kama hulipi utakuwa kama huyu jamaa hapa chini ambaye hivi sasa ana kesi.
article-2091085-116C8AF2000005DC-886_634x677.jpg



Fuatilia kesi hii ... ...

Usikurupuke Pascali hata wezi wa RADA waliohongwa na BA kesi ilikuwa cha moto, si uliona moto wake. Kama unataka kufahamu mambo ya Uingereza jaribu kupata habari sahihi sio kukurupuka ama kurukaruka na kudanganya jamii hizo hadithi peleka kwenye vijiwe vya migahawa. Ongea yale unayoyafahamu kwa undani utaheshimika.

FYI Nchi yenye vyuo vikuu zaidi ya 300 vinavyoheshimika ulimwenguni pote ambayo ina wakazi takriban million 60 haiwezi kuendeshwa kama unavyofikiria.
 
Back
Top Bottom