Waandishi wa Habari na Bahasha: Sio Kila Bahasha ni Rushwa

The Boss,
Mwaka 1998 niliendesha semina ya waandishi wa radio na TV pale DSM na Arusha. Tulipofika katika mada ya ethics nikazusha hili suala la kupokea bahasha kutoka kwa mawaziri au watu wakubwa. Waandishi wote pale walikuwa na msimamo kwamba bahasha ni essential kwa kazi zao, nikasema hapana. Tulibishana mpaka nikaona heri tukubaliane kutokukubaliana. Lakini niliwakumbusha kuwa huwezi kuwa partial unaporipoti juu ya mtu anayekupa bahasha. Utatoa ripoti nzuri tu juu yake. Ni kweli kama usemavyo wenzetu Tanzania, na nchi nyingine zinazoendelea ambazo zimeendekeza mtindo huu, zinajiundia utaratibu wa kipekee, na ndio maana Pasco amekazana kuziweka hizo bahasha katika mafungu mbalimbali. Ningepata fursa nyingine ningependa kukutana na wale wanaomiliki magazeti, radio na tv niwaambie kuwa lazima watenge fungu la expenses za waandishi wa habari kwa sababu kuendekeza hii tabia ya kutegemea vibahasha ndiko kulikopelekea waandishi wetu wawe wavivu, wasiwe critical, na washindwe kutimiza wajibu wao kama fourth estate.

asante aisee
nilianza kushangaa mno....
 
Mkuu pasco nakuunga mkono kweli kabisa
vingine ni """"vibahaaaaaaashaaaaaaaaaaaa""""" tu wanapiga kelele
 
Mkuu Mzalendo80, kwa vile ndio kwanza niko kwenye mada ya bahasha zipi ni halali na zipi sii halali, kwenye bahasha halali, pia naelezea uhalali wake, lengo la hizo biashara halali, ni ama usafiri, "transport", ama chakula "lunch" ama posho "allowance", ama ni masurufu "per diem", ama ni maduhuli "imprest" etc. Matumizi ya posho na marupurupu ni halali!, sasa wanaotoa hayo marupurupu wanapata nini, jibu ni nothing, kama wa wabunge wanavyolipwa posho ya laki 200,000 kwa siku, anayewalipa anapata nini?.

Je kampuni yako iliyokuajiri haikulipii hizo expenses? Kama wanashindwa basi hiyo Kampuni ni uchwara, Huwezi kwenda kutafuta habari halafu mtu akulipe wakati kampuni yako inakulipa mshahara. Hiyo ni rushwa kwa sisi walalahoi tunajua ni rushwa hata uibadili jina unalolita lakini ni Rushwa na bahati yenu PCCB ni kitengo cha Kusafisha Mafisadi lasivyo mbona mngeishia Lupango.

 
Mkuu Ndallo, waandishi uchwala ni wale wanaojifanya waandishi lakini sii waandishi chochote si lolote na wapo wa aina mbili. Aina ya kwanza ni wale waliovamia fani baadaye wakajikuta hawawezi bali wanang'ang'ania uandishi huku wanachoandika hakina mashiko. Waandishi uchwala wa pili ni wale ambao walikuwa waandishi wakajikuta hawana kazi hivyo kuvizia matukio mbalimbali kuwinda bahasha for survival, hawa ndio huitwa makanjanja!.
Mkuu Pasco, wakati nasubiri kusikia habari za bahasha halali na haramu naomba nianzie kwa hoja yako hapo juu.

Uandishi ni taaluma kama zingine tena imefikia mahali pa kuitwa mhimili wa nne. Nadhani si rahisi kukuta kila mtu anajiita Mwanasheria, Daktari au Engineer. Makundi haya yanalinda taaluma zao kwa manufaa yao na ya taifa kwa ujumla. Sasa waandishi wa habari wanafanya nini kuzuia makanjanja!!!! Hivi huoni kuwa waandishi wenye kalamu ndio walitakiwa waongoze na wengine wafuate na sio kinyume chake!

Pili, kuna kitu tukubaliane na nawaomba radhi waandishi watakao kereka lakini siombi radhi kwa hoja. Ni wazi kuwa waandishi wetu wamedumaa katika kujifunza ima kutoka kwa wenzao au kwa wao wenyewe. Ukifuatilia uandishi wa habari wa nchi za wenzetu utagundua sisi bado kabisa. Mfano, habari zinaandikwa kama taarifa ya karani na hakuna analysis, details au observation. Ni habari tu fulani kasema fulani amekwenda wapi. Yaani ni reporters na sio journalist.

Tatu hakuna ufuatailiaji wa habari na wala kutoa usuli (feedback). Leo nikiwauliza waandishi wa habari wa Tanzania yule mtoto aliyeokotwa akilelewa na nyani amefikia wapi hakuna jibu.

Hakuna anayefuatailia kujua kile aliachoandika juzi kimefikia wapi.
Hata hizo habari sensational basi hawazifuatilii. Ukimuuliza mwandishi wa habari nchini, ile tume ya kikwete iliyohusu IGP, AG, PCCB chief imetoa taarifa au imefikia wapi hakuna mwenye jibu n.k

Mnadhani watu wanataka kusikia siasa tu bila kujua kuwa yapo mambo mengi madogo madogo lakini yanaigusa jamii sana.
Kuna mwandishi waliwahi kaundika kuhusu kufuliwa kondomu kunakoitwa 'kifanyio' kule shinyanga tena kwa biashara.
Kwangu mimi ilikuwa ni habari kubwa sana kuliko data za IMF ambazo mwananchi hawezi kuzitafsiri achilia mbali kuwa anaishi nazo kila uchao akipigika na njaa. Hili la kondomu ni muhimu kwake kwani halisubiri mwaka 2030 Tanzania itakapoipuku Kenya Kiuchumi

Niseme tu kuwa waandishi wa Tanzania sio creative na hili mnatakiwa mlifanyie kazi. Ninashangaa mzungu anakuja kutoka marekani na kuniandikia habari za maisha ya manzese au bustani ya mungu kule Iringa wakati kila siku watu wanapita na kuona maua.
Lakini pia lazima muwe na curiosity ya mambo. Waandishi wangapi wanajua kuhusu umuhimu wa mbuga ya Tarangire na chatu wanaopanda miti au simba wanaopanda miti?

Mngekuwa makini, mashirika kamaTANAPA wangewapa kazi za kuandika documentary n.k na siku kusubiri bahasha zisizo na uhakika.
Sehemu ya matatizo yenu ni kutotaka kujifunza, kutokuwa na passion na professional kunakopelekea kukosa curiosity.
 
Hivi mnafikiri mwandishi wa habari ni mjinga kufanya kazi mwananchimkulipwa laki tatu
mnahisi atakula wapi jamani vile ni vijibahasha tu kama vijisenti ambavyo kila mtanzania
aliviidhinisha
 
bahasha ni bahasha tu hata ukiipambaje!
Mkuu BADILI TABIA, naungana na wewe mia kwa mia kuwa bahasha ni bahasha, hilo halina ubishi ila sio kila bahasha ni hongo au rishwa!.

Ndio maana kuna kuanzia bahasha ya posa, bahasha ya rambirambi, bahasha ya sadaka kanisani etc.

Hata hizi bahasha za waandishi, zipo bahasha za usafiri, bahasha za lunch, bahasha za masurufu, bahasha za maduhuli, bahasha za posho za vikao, bahasha za marupurupu ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi, bahasha za usumbufu, bahasha za uwajibikaji, zote hizi ni bahasha halali ambazo waandishi wa habari wanapaswa kulipwa!. Hizi sio favours ni stahili zao ambazo wa wanastahili kulipwa!.
 
ni vyema hii taaluma ikawa na board km board za wahindisi au madokta (mf. AQRB, ERB) ili kwamba mtu akimaliza digrii ya kwanza aingie kwenye field walau kwa 2years labda itasaidia kupunguza mabahasha ya pasco.
 
Mkuu Pasco, wakati nasubiri kusikia habari za bahasha halali na haramu naomba nianzie kwa hoja yako hapo juu.
.................................................
Mngekuwa makini, TANAPA wangewapa kazi za kuandika documentary n.k na siku kusubiri bahasha zisizo na uhakika.
Sehemu ya matatizo yenu ni kutotaka kujifunza, kutokuwa na passion na professional kunakopelekea kukosa curiosity.

kwa tz nadhani hilo tatizo halipo kwa waandishi tu, loh!
 
Mi sikubaliani na Pasco hata kidogo..
Hata kama mabosi wako wana njaa ya namna gani.. Huwezi ukanunuliwa,ukakubali na ukanunulika wote,na ukawa satisfied na bei ama price tag,yet ukahalalisha kuwa ni essential...
 
Mkuu Ndallo, waandishi uchwala ni wale wanaojifanya waandishi lakini sii waandishi chochote si lolote na wapo wa aina mbili. Aina ya kwanza ni wale waliovamia fani baadaye wakajikuta hawawezi bali wanang'ang'ania uandishi huku wanachoandika hakina mashiko. Waandishi uchwala wa pili ni wale ambao walikuwa waandishi wakajikuta hawana kazi hivyo kuvizia matukio mbalimbali kuwinda bahasha for survival, hawa ndio huitwa makanjanja!..

Wewe Pasco upo kundi lipi hapo?
 
Mkuu Pasco, wakati nasubiri kusikia habari za bahasha halali na haramu naomba nianzie kwa hoja yako hapo juu.

Uandishi ni taaluma kama zingine tena imefikia mahali pa kuitwa mhimili wa nne. Nadhani si rahisi kukuta kila mtu anajiita Mwanasheria, Daktari au Engineer. Makundi haya yanalinda taaluma zao kwa manufaa yao na ya taifa kwa ujumla. Sasa waandishi wa habari wanafanya nini kuzuia makanjanja!!!! Hivi huoni kuwa waandishi wenye kalamu ndio walitakiwa waongoze na wengine wafuate na sio kinyume chake!

Pili, kuna kitu tukubaliane na nawaomba radhi waandishi watakao kereka lakini siombi radhi kwa hoja. Ni wazi kuwa waandishi wetu wamedumaa katika kujifunza ima kutoka kwa wenzao au kwa wao wenyewe. Ukifuatilia uandishi wa habari wa nchi za wenzetu utagundua sisi bado kabisa. Mfano, habari zinaandikwa kama taarifa ya karani na hakuna analysis, details au observation. Ni habari tu fulani kasema fulani amekwenda wapi. Yaani ni reporters na sio journalist.

Tatu hakuna ufuatailiaji wa habari na wala kutoa usuli (feedback). Leo nikiwauliza waandishi wa habari wa Tanzania yule mtoto aliyeokotwa akilelewa na nyani amefikia wapi hakuna jibu.

Hakuna anayefuatailia kujua kile aliachoandika juzi kimefikia wapi.
Hata hizo habari sensational basi hawazifuatilii. Ukimuuliza mwandishi wa habari nchini, ile tume ya kikwete iliyohusu IGP, AG, PCCB chief imetoa taarifa au imefikia wapi hakuna mwenye jibu n.k

Mnadhani watu wanataka kusikia siasa tu bila kujua kuwa yapo mambo mengi madogo madogo lakini yanaigusa jamii sana.
Kuna mwandishi waliwahi kaundika kuhusu kufuliwa kondomu kunakoitwa 'kifanyio' kule shinyanga tena kwa biashara.
Kwangu mimi ilikuwa ni habari kubwa sana kuliko data za IMF ambazo mwananchi hawezi kuzitafsiri achilia mbali kuwa anaishi nazo kila uchao akipigika na njaa. Hili la kondomu ni muhimu kwake kwani halisubiri mwaka 2030 Tanzania itakapoipuku Kenya Kiuchumi

Niseme tu kuwa waandishi wa Tanzania sio creative na hili mnatakiwa mlifanyie kazi. Ninashangaa mzungu anakuja kutoka marekani na kuniandikia habari za maisha ya manzese au bustani ya mungu kule Iringa wakati kila siku watu wanapita na kuona maua.
Lakini pia lazima muwe na curiosity ya mambo. Waandishi wangapi wanajua kuhusu umuhimu wa mbuga ya Tarangire na chatu wanaopanda miti au simba wanaopanda miti?

Mngekuwa makini, TANAPA wangewapa kazi za kuandika documentary n.k na siku kusubiri bahasha zisizo na uhakika.
Sehemu ya matatizo yenu ni kutotaka kujifunza, kutokuwa na passion na professional kunakopelekea kukosa curiosity.
Mkuu Nguruvi3, mambo uliongea yamenigusa na nitakujibu kwa kituo nikitulia.

Uandishi sio tuu ni kazi ya wito bali pia ni kipaji. Uandishi wa Tanzania unakabiliwa na utapia mlo wa vipaji na ukata wa kupindukia. Hatuna specialization hivyo ukiondoa the Citizen hata bajeti yetu inachambuliwa vizuri zaidi na The East African kuliko magazeti yetu!. Zile picha zote za wanyama na vivutio vyetu vya utalii unazoziona kwenye post cards na kalenda mbalimbali zimepigwa na wazungu!. Hata zile movie zote za wanyama wetu ni kazi ya wazungu kwa sababu ya ukata!.

Tatizo la waandishi wetu sio tuu ukosefu wa creativity bali pia lack of aggreviness kufuatilia issues ndio maana tunaishia kwenye reportage tuu sio analysis wala hakuna folloup wala feedback!.

Naendelea na bahasha za halali zikiwemo za kufuata habari za vijijini na kufanya investigative journalism bila uwezeshaji mwandishi hawezi kufanya lolote la maana na kuwezeshwa ndiko huko kwa kupewa bahasha ambazo ndizo nataka kuzijengea hoja kuwa ni bahasha halali!.
 
asante
ndo maana nimeuliza huu utamaduni ni wa kimataifa au la?
taaluma ya uandishi wa habari ni taaluma universal....haiwezekani waandishi wa TZ
wakajiundia utaratibu wao wa kipekee
naoja hakuna anaenijibu hilo swali.....

Ukiona swali halijibiki inamaanisha haka ni kautaratibu ketu hapa Tz na kama alivyosema mwana Jf Mmoja kuwa kwa upande wa USA na UK alikokuwa akifanyia kazi mambo ya vibahasha havipo,tena mimi nadhani hari hii sio TZ peke yake ni hata nchi nyingine za kiafrika tatizo tu hatuna mofano halisi,ngoja tuingie mtandaoni tunakuja na majibu
ona hii
Tunisian Newspapers Scrutinized for Ties to Ben Ali

The Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same time
The Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same time


The corruption of journalism BRITISH politicians and journalists have vied to use the strongest possible adjectives to condemn the behaviour of phone-hackers paid by the News of the World.

This newspaper shares their revulsion at practices at the Sunday tabloid owned by News International, a British subsidiary of News Corporation, which publishes The Australian.


[h=1]Curing Journalism of Corruption is Needed in Post-split
Sudan
Sudanese newspapers need an overhaul to restore credibility by putting a stop
to unethical practices.[/h]kumbe kila sehemu bwana,tatizo ni kwamba waandishi wa Tz wanazifukizia na kuzisaka popote pale bahasha zilipo huo ndio utofauti uliopo
 
Kwani Pasco,source analazimika au anapaswa amlipe au amkirimie mambo gani mwandishi?
Una maana mi nikiwa Mtwara,nikitoa taarifa kwenye ofisi yako..sina budi kuandika pia kwamba,wakionyesha tiketi za ndege watarudishiwa nauli zao,na nitawalipa per diem sh kadhaa kwa siku?? Yaani ni wajibu wangu?
Haya umetaja TBC,na wao wakipokea barua ya namna hiyo wana act vipi?
Asante Pasco......
 
Mkuu Nguruvi3, mambo uliongea yamenigusa na nitakujibu kwa kituo nikitulia.

Uandishi sio tuu ni kazi ya wito bali pia ni kipaji. Uandishi wa Tanzania unakabiliwa na utapia mlo wa vipaji na ukata wa kupindukia. Hatuna specialization hivyo ukiondoa the Citizen hata bajeti yetu inachambuliwa vizuri zaidi na The East African kuliko magazeti yetu!. Zile picha zote za wanyama na vivutio vyetu vya utalii unazoziona kwenye post cards na kalenda mbalimbali zimepigwa na wazungu!. Hata zile movie zote za wanyama wetu ni kazi ya wazungu kwa sababu ya ukata!.

Tatizo la waandishi wetu sio tuu ukosefu wa creativity bali pia lack of aggreviness kufuatilia issues ndio maana tunaishia kwenye reportage tuu sio analysis wala hakuna folloup wala feedback!.

Naendelea na bahasha za halali zikiwemo za kufuata habari za vijijini na kufanya investigative journalism bila uwezeshaji mwandishi hawezi kufanya lolote la maana na kuwezeshwa ndiko huko kwa kupewa bahasha ambazo ndizo nataka kuzijengea hoja kuwa ni bahasha halali!.

Unadhihalalisha hata kama sio halali, Mkuu hiyo ni Rushwa hata kama utairemba kwa majina bado ni rushwa
 
Mkuu BADILI TABIA, naungana na wewe mia kwa mia kuwa bahasha ni bahasha, hilo halina ubishi ila sio kila bahasha ni hongo au rishwa!.
Ndio maana kuna kuanzia bahasha ya posa, bahasha ya rambirambi, bahasha ya sadaka kanisani etc.
Hata hizi bahasha za waandishi, zipo bahasha za usafiri, bahasha za lunch, bahasha za masurufu, bahasha za maduhuli, bahasha za posho za vikao, bahasha za marupurupu ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi, bahasha za usumbufu, bahasha za uwajibikaji, zote hizi ni bahasha halali ambazo waandishi wa habari wanapaswa kulipwa!. Hizi sio favours ni stahili zao ambazo wa wanastahili kulipwa!.
Mkuu Pasco nakubaliana nawe kabisa kuwa waandishi wa habari ni fani kama nyingine na wanadamu kama wengine. Kuna stahiki zao kama wengine na haki zao kama taaluma nyingine.

Nikutahadhirishe tu kuwa unapoweka mpaka wa hiki ni halali na hiki sio unaweza kujifunga na kamba yako mwenyewe.
Kuna kitu kinaitwa Law, halafu Regulations. Hivi ni vitu ni 'binding' ya kuwa mwandishi anapaswa kufanya ABC au hapaswi kufanya ABC.
Nadhani umesahau kitu kinaitwa 'ethics' ambacho ukikiangalia haki 'bind' moja kwa moja lakini kinaweza kuwa chachu ya kuumua mkate wakati Regulations na Law zinafanya kazi.

Waandishi mna ethics zenu kama alivyo mwanasheria au Daktari.
Nitashangaa kama utanikuta saa 6 mchana nipo mahali na Hakimu tunapata Lunch halafu saa nane anasikiliza kesi yangu.
Lunch ni haki ya hakimu kama mlo na hakuna mahali imesemwa itoke wapi.
Kinachomsuta hakimu ni ethics(maadili) , kwamba atatenda ilivyokusudiwa? Lunch imeleta kitu kingine kinaitwa conflict of interest kati ya mimi mshtakiwa anayenifahamu tukiwa katika lunch na sheria anazozijua na hiyo ime compromise integrity ya hakimu lakini haina maana kuwa ni haramu.

Nimetoa mfano huo ili kujenga hoja kuwa hizo bahasha unazosema ni halali ni kweli yaweza kuwa ni halali, lakini je huoni kuna ambazo zinaleta conflict of interest, zina violate principle, values and ethics za uandishi?

Labda pia nionyeshe wapi kamba inaweza kukufunga. Bahasa za usumbufu ni zipo hizo Pasco? nielimishe hapa.
 
Ukiona swali halijibiki inamaanisha haka ni kautaratibu ketu hapa Tz na kama alivyosema mwana Jf Mmoja kuwa kwa upande wa USA na UK alikokuwa akifanyia kazi mambo ya vibahasha havipo,tena mimi nadhani hari hii sio TZ peke yake ni hata nchi nyingine za kiafrika tatizo tu hatuna mofano halisi,ngoja tuingie mtandaoni tunakuja na majibu
ona hii
Tunisian Newspapers Scrutinized for Ties to Ben Ali

The Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same timeThe Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same time
The Tunisian press has found itself under increasing scrutiny for the lingering presence of ties to the old regime. The National Union of Journalists announced plans to publish a "blacklist" of names of journalists known by the group to be corrupted by involvement with ex-leader Zine El Abidine's propaganda ministry. At the same time


The corruption of journalism BRITISH politicians and journalists have vied to use the strongest possible adjectives to condemn the behaviour of phone-hackers paid by the News of the World.

This newspaper shares their revulsion at practices at the Sunday tabloid owned by News International, a British subsidiary of News Corporation, which publishes The Australian.


Curing Journalism of Corruption is Needed in Post-split
Sudan
Sudanese newspapers need an overhaul to restore credibility by putting a stop
to unethical practices.


kumbe kila sehemu bwana,tatizo ni kwamba waandishi wa Tz wanazifukizia na kuzisaka popote pale bahasha zilipo huo ndio utofauti uliopo

Njaa zitawauwa hawa waandishi habari uchwara wa Tanzania, wanafanyika kazi matumbo sio fani. Wanaiaibisha fani ya uandishi wa habari.
 
Kwa kuanzia wanabodi, naomba tukubaliane kuwa bahasha za usafiri ni genuine kama zinatolewa kwa malengo ya kuwawezesha waa ndishi wafike mahali pa tukio na kurudi. Media zetu ni masikini za kutupwa!, Pamoja na kuwa na vituo vya TV lukuki na vingine viko kwa zaidi ya miaka 10, vituo vyote hivi viko hoi bin taaban kiuchumi na kuna vingine vina survive kwa kudra ya mwenyeenzi Mungu!. Ukiondoa TBC ambayo ni spoon fed, vituo vingine vyote vinavyo survive God knows!. Umasikini wa vituo hivi utaujua kwa kuangalia amount of local programing na quality of creativity na quality of production ni very poor!. Hatuna local series hata moja!. Series zote 100% kwenye TV zetu zote, ni foreign!. Hakuna media yoyote nchini yenye budget ya invetigative stories, Jerry Mura alipoondoka ITV, Usiku wa Habari ukajifia natural death!. Ukiondoa talk show ya Kiti Moto enzi zile, bado sijaona talk show ambayo inaniwahisha nyumbani never to miss it, Dakika 45 ya ITV sasa ni angalau angalau. Jeneral on Monday alitaka kujitahidi lakini wapi!. Talk show zote za studio ni cheap stuff ambazo ndizo only we can afford, redio na magazeti ndio msiseme kabisa!.

Kufuatia umasikini huo, whoever mwenye news yake ambayo iko mbali, lazima awafacilitate waandishi wafike, the easiest facilitation ni kupitia bahasha. Media zote dunia nzima ili ziweze kutimiza wajibu wake ni lazima ziwezeshwe ili ziwawezeshe waandishi wake watimize wajibu wao!. Uwezeshaji wowote wa media, hizi ndizo bahasha zenyewe!. Rais wetu afanyapo ziara za mikoani na hata nje ya nchi, husafiri na pool of journalits ambao lazima wewezeshwe kwa bahasha!. Mkisikia ripota wa ITV, TBC, Chanel Ten au Star TV anaripoti ziara ya rais akiwa nje ya nchi, ukae ukijua chombo chake pekee hakija jeuri ya kumpeleka kuripoti Marekani bila kuwa facilitated na Ikulu!. Kwa maana hiyo mpaka Ikulu inakata panga!.

Mtu asikutanganye eti CNN na vyombo vya habari vya Marekani wanaosafiri kwenye Airforce One na rais Obama, wanasafiri bure!. Wanakatiwa bahasha za nguvu kutoka vyombo vyao na labda hivyo vyombo vyao vinachangia gharama, lakini hizo fedha za vyombo vyao ni mibahasha minene toka ma multanational na matlilateral companies/organizations, lakini the bottom line ni bahasha!.

Kuna watu wanaweza kuleta hoja kuhusu BBC ambacho ndicho chombo pekee cha habari ambacho hakipokea matangazo, hivyo hakipokei bahasha ya mtu!. Kwa wasio jua watafikiri BBC ndio chombo malaika hakipokei bahasha!, No!. BBC wanapokea bahasha kupitia kodi ambayo inakatwa kwa kila mtu aliyeko Uingereza, haijalishi unaisikia au husikilizi redio yake au huangalii tivi yake, unailipia utake usitake!. Hizi ndizo bahasha ambazo BBC inakiburi cha kuwakatia waandishi wake watimize wajibu wao!.
 
Iwe fedha ya usafiri, au malazi au chakula kama anakupa kwa kutaka umuandike, hiyo ni rushwa tu. Hauna ujanja hapo.

Dahh, mpokea rushwa na mgawa rushwa unataka kujitetea? nilikuwa sijui lakini leo umeweka wazi mwenyewe. Acha hiyo ni dhambi kubwa sana, si kidini tu hata ki uzalendo.

Kuanzia leo hii ni vita rasmi, mimi na wewe na sitokubali au kuamini chochote unachokiandika. Wewe unafanya dhulma kubwa sana kwa watanzania na kukiri kwako hapa inabidi uchukuliwe hatua kali sana za kisheria, iwe ni fundisho kwa wengine.

Kwa kuwa umekiri mwenyewe sasa tuelezee na vibahasha hivyo umeshapokea kutoka kwa nani na nani na umesha vigawa kwa nani na nani.

Kama inabidi utengeneze fedha kwa uandishi wako kuna njia nyingi sana za kutengeneza pesa za halali, kwa kuanzia unaweza kuwa muandishi wa scripts na si wa habari.

Nkusikitikia sana na hapo hapo nakushangaa sana tena na hapo hapo nakusifu kwa kueleza ukweli lakini ukweli haukuondelei dhambi ya kupokea na kugawa rushwa kama ulivyokiri mwenyewe hapo juu.
 
Yaani na hotuba yotealioandika unauliza yuko upande gani jamani
si wabahasha...ama unataka awe upande wa kubahashiwa hayo mambo ayataki ndio maana wanaamua kupokea bahasha kua avoid kubahashiwa..mkiona mwandishi masikini ama kakaa na mtu ananyweshwa ooohh bwabwa lake sasa pasco kawapa mbinu mpya mambo ya kuchafuana kisa mtu kapewa ofa tu atutaki ukija na wewe rosegarden tunakupa ofa
 
Back
Top Bottom