Aegon Targaryen
Member
- Sep 1, 2017
- 24
- 21
Watu wengi wakisikia Clouds ina beef na msanii au mtu yeyote akili zao moja kwa moja zinawatuma kwa Ruge na Kusaga. Ukweli ni kwamba anaefanya kila kitu kinachohusu utendaji ndani ya Clouds Media Group ni mwanadada Fauzia. Huyu ndiye mastermind wa kila kitu kinachofanyika mjengoni kuanzia uajiri, nani atangazwe, nani apate udhamini, ajira nk.
Fauzia cheo chake kwa haraka utadhani ni msaidizi wa Ruge na aliwahi kuwa msaidizi wa Kusaga mwanzoni, baada ya muda kutokana na uchapakazi wake majukumu yameongezwa anafanya kazi za operation anahakikisha kila kinachofanyika kina mkono wake.
Ukichukiwa na Fauzia kama ni mtangazaji jua maisha yako ni magumu, waulize Asmah Makau, Regina Mwalekwa, Doreen Andy, Anorld Kayanda na wengine walioishia kukalishwa benchi au “kupangiwa kazi nyingine”
Msanii ukizinguana na Fauzia habari yako ndo imefikia mwisho, mfano mzuri ni Ruby ambaye wengi wanadhani ugomvi wake na Zamaradi ndio ulisababisha lakini ukweli ni kwamba Fauzia ndiye kampiga pini. Kuna orodha kubwa ya wasanii ambao wamekuwa blacklisted nyimbo zao hazipigiwi kwa sababu walitaka kumpanda kichwani. Hata Diamond majuzi alipoanzisha bifu na Kiba alijikuta wimbo wake mpya wa Zilipendwa hauchezwi sana kulinganisha na ule wa Kiba, akanyimwa interview ya kuutambalisha katika XL kwa sababu tu alitofautiana lugha na Fauzia.
Kama ni event organizer wa bongo unataka udhamini wa Clouds kama media partner hakikisha uko vizuri na Clouds. Muulize muandaaji wa nyamachoma festival ambavyo mara kadhaa alijikuta akikwaa kisiki kutokana na kuzinguana na Fauzia.
Na mwisho kabisa usiwaze hata siku mmoja kwenda kwa Ruge au Kusaga unaposhindwa kuelewana na mwanadada Fauzia, tafuta mtu awapatanishe maana bila hivyo sahau kufanya kazi na Clouds.
Huyu ndiye Fauzia Kurane, the woman who leads from behind and make things happen.