Vyama vya Siasa havijui au vimesahau wajibu wao?

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,823
35,829
Vyama vya siasa si ajira kwamba ni mahali pa kwenda kujipatia riziki.

Vyama vya siasa vina wajibu. Wajibu wake si mdogo.

Siasa ni kama mchezo wa mpira kuchukua na kuzitumia lose balls zote Ili kujipatia magoli.

Kumekuja kukapita mambo ya tozo. Kumekuja panya road. Kunafukuta ya bima ya afya. Kuna katiba mpya ambayo mbele na nyuma yake wala hakujulikani tena. Mauaji ya kiholela yanaendelea, nk nk.

Vyama vyetu viko kimya. Zaidi sana tunasikia pongezi eti kuwa mwendo sasa uwe huo unaoitwa wa kususa, ati hadi akili ziwakae watu sawa!

Mbatia ndiyo hivyo tayari yamemfika, alipo maji ya shingo. Hata pa kusemea tu amekosa kwa maelekezo pendwa kutoka juu.

IMG_20220925_194301_981.jpg


Enyi vyama vya siasa, agenda zenu ni za kusubiri kupewa ushindi mezani na walio washindani wetu?

Hatupaswi kuchezeshwa ngoma na washindani wetu. Hawa tuna haki ya kuwachezesha yetu.

NInakazia: Aluta continua, mikutano ya siasa ni haki yetu. Twende kazi. Mengine tutayaona mbele kwa mbele.
 
Vyama vya siasa si ajira kwamba ni mahali pa kwenda kujipatia riziki.

Vyama vya siasa vina wajibu. Wajibu wake si mdogo.

Siasa ni kama mchezo wa mpira kuchukua na kuzitumia lose balls zote Ili kujipatia magoli.
Kwa Tanzania, its very unfortunately hatuna any serious and credible opposition, hivyo tuna chama kimoja tuu, the one and only na kitatawala milele!. Kupata maendeleo ya kweli, Watanzania ni lazima tujifunze kuukubali ukweli!. Hili la CCM kutawala milele ni kweli!.

P
 
Tatizo la ukosefu wa ajira limeenda mbali sana, siku hizi wengi wanaojiunga kwenye hivyo vyama wanaenda kujitafutia ajira huko, kwasababu wengi wana wategemezi.

Matokeo yake hili linasababisha wanasiasa wengi hasa wa upinzani wawekwe mfukoni na CCM, wanajikuta wanashindwa kuwasemea wananchi, wanaobaki na ujasiri wao wanakuwa wachache sana ambao sauti zao hazitoshi kuleta impact.
 
Hapa kwetu kuanzia juzi kulikua na chaguzi za CCM aisee hiki chama kweli kitatawala milele ni kijani na njano tu mji mzima. Hivi vyama vya siasa ni kama Saccos tu hawajui waendako na wanatakiwa kufanya nini hawana hata mashina kwenye majimbo wao wanasubiria uchaguzi mkuu waanze kutafutana
 
Kwa Tanzania, its very unfortunately hatuna any serious and credible opposition, hivyo tuna chama kimoja tuu, the one and only na kitatawala milele!. Kupata maendeleo ya kweli, Watanzania ni lazima tujifunze kuukubali ukweli!. Hili la CCM kutawala milele ni kweli!.

P

Ila mkuu bandiko hili linahusu vyama vyote. Si CCM, Tadea au ACT iaweza kudai inatimiza wajibu wake kama chama kujivika uhalali mbele ya watu.

Chama gani kinawasemea nani kwenye Tozo, mauaji ya kiholela, katiba mpya, bima ya afya nk

Chama kipi kinasimama wapi kwa dhati Yao kwenye haya?
 
Tatizo la ukosefu wa ajira limeenda mbali sana, siku hizi wengi wanaojiunga kwenye hivyo vyama wanaenda kujitafutia ajira huko, kwasababu wengi wana wategemezi.

Matokeo yake hili linasababisha wanasiasa wengi hasa wa upinzani wawekwe mfukoni na CCM, wanajikuta wanashindwa kuwasemea wananchi, wanaobaki na ujasiri wao wanakuwa wachache sana ambao sauti zao hazitoshi kuleta impact.

Hivi vyama vinahitaji mageuzi au mapinduzi kwa maana ya strategic transformation:

Muda wa mapinduzi vyamani ni sasa
 
Bila kufanyiwa kazi tatizo la msingi, ukosefu wa ajira, hayo mageuzi vyamani sioni kama yatakuwa na tija endapo hao wapya watakuwa bado wametawaliwa na njaa.

Msingi wa mageuzi siyo kuhusiana na watu. Hapa zaidi ni kuwekana sawa wazi wazi: nini malengo na madhumuni. Watu wakachagua kusuka au kunyoa.

Hii ni across the board si upinzani tu bali hata huko CCM.

Kwani kina Pascal Mayalla karata wanazotupa huko ni kwa ajili ya kuifanyia nini hasa nchi hii? Yanapaswa kuwa wazi vyamani.

Ni lazima tuwekane wazi ili ijulikane nini hatufanyi au nini tunafanya na hadi wapi.

Ukimya wa vyama hivi katika yanayotokea hata na kina Ruge hauna afya.
 
Msingi wa mageuzi siyo kuhusiana na watu. Hapa zaidi ni kuwekana sawa wazi wazi: nini malengo na madhumuni. Watu wakachagua kusuka au kunyoa.

Hii ni across the board si upinzani tu bali hata huko CCM.

Kwani kina Pascal Mayalla karata wanazotupa huko ni kwa ajili ya kuifanyia nini hasa nchi hii? Yanapaswa kuwa wazi vyamani.

Ni lazima tuwekane wazi ili ijulikane nini hatufanyi au nini tunafanya na hadi wapi.

Ukimya wa vyama hivi katika yanayotokea hata na kina Ruge hauna afya.
Naunga mkono hoja
P
 
Back
Top Bottom