Vyakula vinavyobaki kwenye mighahawa huwa vinapelekwa wapi?

Ugali jaa,mchuzi juu,huuziwa wabeba zege na makuli,ila hata ww ukitaka,mwambie mama muuza,ugali jaa,mchuzi juu
 
Wali wa maji ukibaki, kesho utatiwa viungo na kuwa pilau. Maharage ya Leo, kesho yanatiwa tui la Nazi. Nyama iliyolala, kesho inakaangwa rost. Wali, ulioliwa na kubakizwa kwenye sahani, unaenguliwa na kurudishwa sufuriani. Maji ya kunywa wanachemsha ndoo moja ya Lita 20,wanachanganya na maji ambayo hayajachemshwa Lita 30,ili yanuke moshi, mnywaji ajue yamechemshwa, kumbe hola. Vijiko vinatumbukizwa na kutolewa kwenye maji na kurudiswa kwenye Huduma. Upo hapo brother?
 
wanapika kulingana na wateja wao,kama kubaki kinabaki kidogo sana watoto wao na wenyewe wanakula
kama hutaki basi huwa wanasafirisha wanapeleka ulaya,huko soko la viporo lipo sana
 
Heshima kwenu wakuu.

Kama kichwa kinavojieleza hapo juu, naomba kujua vile vyakula vinavyobaki baada ya mauzo ya siku kule kwenye mahoteli, migahawa na mama lishe huwa vinaenda wapi?
Msaada kwa anaejua maana nina wasiwasi huwa tunalishwa viporo.
Ukisikia wali jaa na mchuzi juu, jua tayari ushalishwa kiporo...
 
Wali wa maji ukibaki, kesho utatiwa viungo na kuwa pilau. Maharage ya Leo, kesho yanatiwa tui la Nazi. Nyama iliyolala, kesho inakaangwa rost. Wali, ulioliwa na kubakizwa kwenye sahani, unaenguliwa na kurudishwa sufuriani. Maji ya kunywa wanachemsha ndoo moja ya Lita 20,wanachanganya na maji ambayo hayajachemshwa Lita 30,ili yanuke moshi, mnywaji ajue yamechemshwa, kumbe hola. Vijiko vinatumbukizwa na kutolewa kwenye maji na kurudiswa kwenye Huduma. Upo hapo brother?


Aki umenitisha
 
Heshima kwenu wakuu.

Kama kichwa kinavojieleza hapo juu, naomba kujua vile vyakula vinavyobaki baada ya mauzo ya siku kule kwenye mahoteli, migahawa na mama lishe huwa vinaenda wapi?
Msaada kwa anaejua maana nina wasiwasi huwa tunalishwa viporo.

Si unauziwa tena siku zinazofata.

Ina maana wewe kwenu hujawahi kula kiporo cha jana kikawa kitamu zaidi ya chakula cha leo leo?

Uhifadhi wa vyakula ni kitu cha kawaida sana wala si kitu cha kushangaza.
 
Kama kimehifadhiwa vizuri bila kuharibika hamna tofauti mkuu. Kama umeshakula hotelini jua umeshakula kiporo mara nyingi tu.
Tatizo sio kuhifadhiwa vizuri, tatizo ni kwamba kwanini wasiweke wazi kwamba hiki ni kiporo ili mtu unaponunua unajua kabisa kuwa nanunua kiporo. Kwanini ununue kiporo kwa bei ya chakula cha leo?

Ni kweli nimeshakula kiporo (ndio maana siku hizi nimekuwa makini) ila nikila kiporo huwa najua kwa sababu ukila lazima ulale (kinaleta sana usingizi)...
 
Si unauziwa tena siku zinazofata.

Ina maana wewe kwenu hujawahi kula kiporo cha jana kikawa kitamu zaidi ya chakula cha leo leo?

Uhifadhi wa vyakula ni kitu cha kawaida sana wala si kitu cha kushangaza.
Duuh kiporo kiwe kitamu zaidi, mathalani ugali wa jana uwe mtamu kuliko wa leo?!!
 
Heshima kwenu wakuu.

Kama kichwa kinavojieleza hapo juu, naomba kujua vile vyakula vinavyobaki baada ya mauzo ya siku kule kwenye mahoteli, migahawa na mama lishe huwa vinaenda wapi?
Msaada kwa anaejua maana nina wasiwasi huwa tunalishwa viporo.
Kariakoo ukisikia wali jaa mboga juu sio kwamba wanakujazia, kakuona wakuja na hautagundua wali wa jana na mboga ya juzi.
 
Wanaweka viungo vya pilau ....mkija mdanganywa kua ni pilau ...kumbe likiporo la jana..........
 
Back
Top Bottom