Vurugu mitaani Mwanza kati ya wamachinga na polisi

Vurugu mitaani Mwanza kati ya wamachinga na polisi

mkuu kareti unaziweza? Au ndio soja mzembe
we ukija kwangu nahakikisha unarud kiuno kimeteguka

Miongoni mwa vitu nnavyozingatia siku hizi ni kuvunja matofali kwa kichwa. Be very afraid ukiniona niko mstari wa mbele....frontline...huwa natoa ile ballistic helmet ndo nakubandika ndoo ya utosi! Tena nyie madogo mabishoo wa siku hizi na milegezo yenu hamna adabu hata kidogo na jamhuri.

Stay alert ukiniona front.ova!?
 
Halafu 2015 wataichagua CCM. Vijana mnaaswa sasa siasa za kishabiki za kuhongwa tshirt na kofia acheni. CCM haijawahi kuwasaidia zaidi ya kufilisi hata kle kidogo mlicho nacho
 
Huyu wenje aache kutuhadaa wananchi kwa kuomba muongozo kwa spika kuhusiana na hili sakata la machinga FFu.alikua anafaham kinachoendelea kuhusiana na hii operesheni ya kuondoa machinga vikao vilifanyika na alisaini manake haliwezifanyika jambo lolote kwenye jimbo bila mbunge kufahamishwa kwahiyo anafaham kila kitu hiyo ya kuomba muongozo kwa spika ni danganya toto ili tuone anatetea watu wa jimbo lake

Umenena kweli kweli kabisa
 
Machinga wanaathiri nini hapo makoronoi?au maduka makubwa hawauzi!!!!
Machinga wanafanya wenye maduka wasiuze kwasababu kila siku wao wanakuja na bidhaa zinazofanana na za kwenye maduka wanapanga kwenye uwanja njee ya maduka hayo!Kwasababu wao ni watu wakuja kila siku inakuwa vigumu kuwadhibiti walipe kodi.Kwakutolipa kodi kwao bidhaa zao zinakuwa bei poa,hivyo ushindani halali kibiashara unakuwa haupo!Japo jiji ndiyo linapaswa kulaumiwa kwa kutojishulisha na utaratibu uliobora toka mwanzo walipoanza kuitana hapo makoroboi!
 
Machinga wanauza bidhaa za haohao maduka makubwa

Huu utetezi sijui mnautoa wapi?? Neno makoroboi maana yake wafanyabiashara wauza koroboi ndio walikuwa hapo miaka nenda rudi sasa hao wafanyabiashara wenye utajiri walikuwa wapi?? Tuwape haki yao wanyonge.
 
Mapolisi ya Tanzania ni kama maroboti, yakiamrishwa yanaenda tu. Poor Polices.
 
Mapolisi ya Tanzania ni kama maroboti, yakiamrishwa yanaenda tu. Poor Polices.

wewe ndio poor kabisa, majeshi yote duniani ukubali amri za wakuu sasa sijui unamaanisha Mapolisi ya Tanzania hipi
 
Huu utetezi sijui mnautoa wapi?? Neno makoroboi maana yake wafanyabiashara wauza koroboi ndio walikuwa hapo miaka nenda rudi sasa hao wafanyabiashara wenye utajiri walikuwa wapi?? Tuwape haki yao wanyonge.

Neno makoroboi linatokana kweli na mafundi koroboi waliokuwa hapo miaka mingi nyuma, baadaye walianza kuingia wafanyabiasahara wa nguo za mitumba ambao walihamishiwa eneo la Mlango mmoja (Langolango) miaka ya 90 (1990s). Eneo linalozunguka maeneo hayo kumekuwa na maduka miaka yote hiyo. Kwa sababu ambazo mimi naziita ni za kisiasa Wenje alianza kuwatetea wafanyabiashara wamachinga wauze bidhaa zao bila kubughudhiwa ndipo kidogo-kidogo wakaongezeka na sasa wamefurika wakiuza bidhaa mbalimbali zikiwemo zile zinazouzwa na wenye maduka kuzungukia eneo hilo. Kama miezi mitatu au miwili hivi kulitangazwa kuwa wafanyabiashara wenye vibanda kandokando ya barabara na wale wa makoroboi waondoe biashara zao kwa vile sio biashara rasmi yaani hazijasajiriwa. Wenje amekuwa akisisitiza kuwatetea kupitia chama chake na ubunge wake. Lakini kinachoonekana ni unafiki ni kujifanya hajui kinachoendelea ilhali yeye ni mbunge na maamuzi ya jiji anayafahamu, lkn anajiinua mbele ya hadhara na kusema anawatetea n kuwa wanaonewa. Wenje anafahamu jinsi Eneo la makoroboi lilivyokuwa halina msongamano wa ajabu kabla hajawa mbunge na kutoa kauli zake. Wenje anapaswa kujua lile sio eneo la soko kama anavyotaka kuwaaminisha watu. Wamachinga wamepewa maeneo ambayo Wenje anajua wamekataa kuhamia ikiwemo eneo la Kiloleli, Sabasaba, nk. Watanzania tuwe wakweli tusiangalie upande wa kujidai kutetea Wamachinga wakati ukweli ni kuwa tunawadanganya na hatuwapi mbinu sahihi za kufanya.Kama waliokuwepo Makoroboi walihamishiwa Langolango, na wamejaa wengine wanataka watengewe eneo, hatuoni sasa utakuwa ni mchezo wa kujikusanya hapo na kudai watengewe eneo?
 
Mapolisi ya Tanzania ni kama maroboti, yakiamrishwa yanaenda tu. Poor Polices.

Wangekataa kwa sababu ipi? Yaani wangekataa kwa kutoa sababu gani? Yaani, kwa nini wakatae? Nadhani huelewi kwa nini kikundi fulani huitwa JESHI na taratibu zao . Pole sana ndugu yangu!
 
Neno makoroboi linatokana kweli na mafundi koroboi waliokuwa hapo miaka mingi nyuma, baadaye walianza kuingia wafanyabiasahara wa nguo za mitumba ambao walihamishiwa eneo la Mlango mmoja (Langolango) miaka ya 90 (1990s). Eneo linalozunguka maeneo hayo kumekuwa na maduka miaka yote hiyo. Kwa sababu ambazo mimi naziita ni za kisiasa Wenje alianza kuwatetea wafanyabiashara wamachinga wauze bidhaa zao bila kubughudhiwa ndipo kidogo-kidogo wakaongezeka na sasa wamefurika wakiuza bidhaa mbalimbali zikiwemo zile zinazouzwa na wenye maduka kuzungukia eneo hilo. Kama miezi mitatu au miwili hivi kulitangazwa kuwa wafanyabiashara wenye vibanda kandokando ya barabara na wale wa makoroboi waondoe biashara zao kwa vile sio biashara rasmi yaani hazijasajiriwa. Wenje amekuwa akisisitiza kuwatetea kupitia chama chake na ubunge wake. Lakini kinachoonekana ni unafiki ni kujifanya hajui kinachoendelea ilhali yeye ni mbunge na maamuzi ya jiji anayafahamu, lkn anajiinua mbele ya hadhara na kusema anawatetea n kuwa wanaonewa. Wenje anafahamu jinsi Eneo la makoroboi lilivyokuwa halina msongamano wa ajabu kabla hajawa mbunge na kutoa kauli zake. Wenje anapaswa kujua lile sio eneo la soko kama anavyotaka kuwaaminisha watu. Wamachinga wamepewa maeneo ambayo Wenje anajua wamekataa kuhamia ikiwemo eneo la Kiloleli, Sabasaba, nk. Watanzania tuwe wakweli tusiangalie upande wa kujidai kutetea Wamachinga wakati ukweli ni kuwa tunawadanganya na hatuwapi mbinu sahihi za kufanya.Kama waliokuwepo Makoroboi walihamishiwa Langolango, na wamejaa wengine wanataka watengewe eneo, hatuoni sasa utakuwa ni mchezo wa kujikusanya hapo na kudai watengewe eneo?

Shida kubwa hapa ni nguvu ya pesa! lakini pia pamoja na huyo Wenje kutuhumiwa na hao wasio watanzania ambao wanatakiwa kuwa nje ya mji! Je, kwa nini Lowasa alipokuja Mwanza walikusanyana hapo hapo makoroboi!! Au faida yake imekwisha na sasa waondoke!??
 
Mlio Mwanza poleni sana na matukio yanayoendelea huko sisi tupo na nyie pamoja kwa dua zetu.

Poleni sana, natumai vurugu zitatulia na mtazidi kutujuza kinachoendelea
 
Naomba unisaidie kujua ni polisi wa nchi gani wakiamrishwa huwa hawaendi au hawafuati amri?
mkuu utachoka bure kuelezea,saa ingine ujue hapo unahangaika na mtu wa kidato cha kwanza,kwahiyo anakua hana exposure na mambo yanavyoenda,maadamu yeye amesikia wenje anasema hivi na yeye anakariri hapo hapo,ujue elimu imeshuka sana siku hizi.
 
Back
Top Bottom