Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Zamani ilikuwa 24 hrs sasa ikaonekana wafanyakazi wengi wana access ya kufanya reversal ,ikaja changamoto ya security ya pesa ,walichofanya kuimarisha security ya pesa ya mtumiaji ni Huduma wakapunguza idadi ya watu wa kuingia kwenye system ndiyo kiss cha kuweka muda wa Masaa 72, huyo aliyekujibu kuwa nisiku saba alikuwa ana stress zake tu,ila wewe make sure kuwa jina linaloonyesha kabla ya kutuma ni la mlengwa acha uzembe unapo tuma pesa.
 
Siwatetei Voda, hata mimi nimeshakua muhanga wa hili jambo zaidi ya mara moja.

Nafikiri ni kutokana na haya mambo mawili, kwanza kabisa, uaminifu, kuna ile mtu anakutumia pesa kisha anapiga simu kusingizia amekosea namba wakati ki ukweli ameghairi au kuahirisha adhma yake, hapo inabidi kampuni ya simu wajirishe kabla ya kuugeuza muamala.

Pili, kuibuka kwa utapeli kwa baadhi ya wafanyakazi wasio waaminifu wa kwenye makampuni ya simu, hii imesababisha uimarishaji wa mchakato na uhakiki wa kurudisha hiyo miamala ili kupunguza kampuni kupigwa.
 
Kuna wizi mkubwa kwa fedha za salio za wateja unaoendelea sasa hivi katika mtandao wa Vodacom.
Kwa vile hili si jungu bali ukweli nimisha report wizi huo katika kitengo cha malalamiko TCRA kwa hatua zaidi.

Nimeweka salio la Tsha 10,000 mchana wa leo kwa Mpesa ref Y23SY687 na baada ya muda mfupi nikakuta salio langu la maongezi ni sifuri.

Nikanunua vocha na kutumiwa tshs 10,000 na hela yote imekatwa tena.

Wateja wa Vodacom jihadharini, kuna mwizi kaingia mtandaoni Vodacom

UPDATE
=====
VODACOM wamefanya ustaarabu wa kunipigia baada ya kuona detail ya transaction hapo juu, na kuiona kwenye mtandao wa Jamiiforums.
Kimsingi wameapologise kwa mtafaruku uliotokea lakini wamenieleza nifike ofisini kwao kuona aian ya simu ninyotumia isije ikawa data apps ziko wazi.
Na kweli baada ya maongezi ya kuchunguza, mobile data setting ilikuwa ON, na mimeizima sasa.

Hata hivyo ni vema nitaenda kupata maelezo ya kuyeyuka kwa salio langu , karibu 20,000, kwa siku moja.
Wanabodi mtajulishwa inawezekana kuna wenye tatizo kama langu.

UPDATE
=====
Nimeonana na waheshimiwa sana wa Customer Care pale Block 4 Mlimani City.
Cha kusikitisha ni wao kushindwa kuchukua malalamiko yangu na kuyafanyia kazi, na hii ni licha ya kuwaelewesha kuwa hili tukio nalijawahi kunitokea na hii kuwa ni mara ya kwanza.

Hawa jamaa wa Customer Care ni kama mabalozi waliopewa jukumu la kusafisha kampuni ya VODACOM hata kama inanuka kwa wizi uliodhahiri.
Kitu ambacho hawajui ni kuwa nilifanya due diligence kupitia wafanyakazi ndani ya VODACOM walionidhihirishia kuwa kuna wafanyakazi wasio waaminifu ambao wana access na personal security settings za wateja.

Na wafanyakazi hao huwa "wapiga kishenzi" fedha za wateja.

Kwa kifupi mtu wa Customer Care ameshindwa kuniconvince na maelezo yake ya upotevu wa Tshs 20,000 katika mtandao wa VODACOM.
VODACOM

Wezi sana nimejaribu kuwafuata kwenye page yao , wananiambia huo ndo utaratibu wao , niko na rafiki yangu mumoja hapa alikosea pesa ofcoz ni uzembe lakini ilikaa wiki mbili, ukipiga simu wanongea ongea, mimi nafikili cha msingi this time naenda kuleft huduma hii
 
Juzi tu hapa nimekosea wamerudisha within 24hrs [HASHTAG]#Pesa[/HASHTAG] ni mpesa


Mimi niliwahi kusimuliwa na mtu kuwa VODOCOM sio watu wazuri wanachelewesha reversal , nilikataa na nikamwambia mimi nikipiga simu huwa hawachukuwi muda mrefu, masaa 72 yalikuwa hayafiki napata muamala na kuna siku nakumbuka nilifanyiwa reversal within the day, Ndungu yangu kama vile niliomba na mimi nikosea nipate uzoefu....

Hii inaitwa isije kukupata ukawaelewa Hatariiiiiiiiiiiiiiii alfu unaitaka hio pesa
 
Ni aibu sana kwa mtandao mkubwa wa mawasiliano kama Vodacom kutusumbua na kutujazia matangazo yenu kwenye inbox text zetu haswa Mimi ni mwasilika wa hizi text toka Vodacom , sijawahigi kujiunga au kuomba kuunganishwa kwa ajili ya kupata infoz updates za huu ujinga mnaonitumia kila lisaa.
Pls stop this shit om.
Sample text za hawa Jamaa wanituamizo ni kama hizi
42fc5be7d4f3a0eb5790cd5e6b40c485.jpg

Vodacom kama ni brand mnayo hamna haja ya kuendelea kunijazia matangazo yenu haya. Hamnilipi kwa chochote hicho kwa ajili ya hiz promo zenu ispokuwa mm ndo nawaweka mjn hapa kwa kununua vocha zenu.
Acheni huu upuuzi.
Jamaa nia yko ni kuuza sura ili upate mademu ama!!!!!
 
Ni aibu sana kwa mtandao mkubwa wa mawasiliano kama Vodacom kutusumbua na kutujazia matangazo yenu kwenye inbox text zetu haswa Mimi ni mwasilika wa hizi text toka Vodacom , sijawahigi kujiunga au kuomba kuunganishwa kwa ajili ya kupata infoz updates za huu ujinga mnaonitumia kila lisaa.
Pls stop this shit om.
Sample text za hawa Jamaa wanituamizo ni kama hizi
42fc5be7d4f3a0eb5790cd5e6b40c485.jpg

Vodacom kama ni brand mnayo hamna haja ya kuendelea kunijazia matangazo yenu haya. Hamnilipi kwa chochote hicho kwa ajili ya hiz promo zenu ispokuwa mm ndo nawaweka mjn hapa kwa kununua vocha zenu.
Acheni huu upuuzi.
Cheki sasa wanaume washalike you're lips
 
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

- Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
- Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.

Karibu

Vodacom Tanzania

nimesikia mnauza vocha za Tsh 50 ,100 na 200 kwenye vituo vya mabasi ya mwendo kasi , je ni kweli mna vocha za aina hii?
 
Vodacom na mitandao mingine embu boresheni mifumo yenu haswa pale mtu anapotuma hela kimakosa mtandao mwingine.masaa 72 kusubiria hela irudi ilipotoka ni inshu.halafu sasa hela kule ilipoenda kimakosa kama imeshatolewa rudisheni basi majibu hata kwa sms.

Nilituma hela kimakosa kwenda voda kutoka tigo sijajibiwa na tigo hela haikukutwa kwenye hiyo voda iliyotumiwa hela.ingawa nimewapigia tigo five times.mara tu nilipotoa taarifa just 2-5 minutes nilishatoa taarifa tigo.

lakini hela haikurudi nabaki tu naambiwa tatizo lako tunalipatia ufumbuzi.halafu hizi kampuni customer care line ina matangazo mengi sana.punguzeni.nafaham ningeipata ile hela isingekuwa matangazo lukuki na ushirikiano wenu mbaya
 
Back
Top Bottom