Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

vodacom m pesa mnahuduma mbovu sana. leo nilikuwa najaribu kutoa pesa kwa wakala chakusikitisha wakala ananiambia hakupokea msg kutoka makao makuu.

ikabidi nikae zaidi ya masaa 6 ndo wakamtumia msg wakala ili atoe pesa. huduma zenu mbovu sana hapa wilaya ya hanang eneo la cmsc
 
Minara yenu IPO tu huku visiwa vya ziwa Victoria lakini mawasiliano ni shida mno, internet ndiyo taabu kabisa Sikh zote network busy.

Nazungumzia mnara wa MAISOME ISLAND, Mbona mnazidiwa na Airtel ambao kwayo nyote minara yenu na yao IPO eneo hilo hilo, hata hapa natumia airtel, Voda yenu imebuma!!!
 
Mimi Niko wilayani Rombo hususan mnara wa Hakwe. Siku za nyuma internet ilikuwa nzuri sana lakini baada ya voda kuongeza mnara wa Ngoyoni imekuwa ya shida na ya kuoteaotea. Shida ni nini?
 
Samahani nilipumzika kwa mda kutumia Till yangu ya mpesa baada ya kuibiwa. Haikufanya muamala wowote kwa Muda WA mwezi moja lkn ilikuwepo hewani na ina salio ndani.

Sasa nilihitaji kuitumia tena nakuta haina menu ya m-pesa nikaenda Voda shop naambiwa imefungwa mpaka niende Dar es salaam makao makuu na mm nipo mkoani. Mtanisaidiaje kutatua tatizo langu?
 
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

  • Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
  • Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
  • Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
  • Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
  • Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.

Karibu

Vodacom Tanzania
Hivi Voda mna matatizo gani kuchukua pesa mko fasta ktk akaunti yangu lakini Huduma sifuri, Jana nimenunua umeme wa luku kupitia M-PESA lkn hadi sasa naandika SMS hii sipata token na pesa mmechukua huu ni WIZI iweje sms za matangazo yenu ziwe zinafika fasta mara app sijui jiunge na miito

ila kila nikipiga Huduma kwa Wateja mnasema pesa yangu iko hewani mbona hayo mabango yenu hayakai hewani yanafika fasta, mna bore si mara ya kwanza, rudisheni pesa yangu huko mnaiona,..
 
Hivi Hua mnajibu Maswali kweli???


Haya mimi swali langu ni hivi ubao wa DSE Tanzania hampo mpaka sasa na tarehe 12 June 2017 ndio ilikua ck ya nyie kuwepo at first time baada ya kuuza share zenu, tupeni feedback kwanini hampo hadi leo???
 
Hivi Hua mnajibu Maswali kweli???


Haya mimi swali langu ni hivi ubao wa DSE Tanzania hampo mpaka sasa na tarehe 12 June 2017 ndio ilikua ck ya nyie kuwepo at first time baada ya kuuza share zenu, tupeni feedback kwanini hampo hadi leo???
Ukitaka wakujibu hawa. Leta mada kuwa wanahusika na makinikia labda.
 
Najua hakosekani mtu wa hii kampuni humu. Kama hamjui basi nawaambia hiviii,"tangu siku ya jumatatu na jumanne inapofika saa sita usiku network inatoweka kabisa! Simu inageuka toy!"
Kwa siku ya jumatatu tangu saa sita network ilivyotoweka sikumbuki ilirejea muda gani, maana hadi napitiwa na usingizi saa tisa, simu haikuwa na network. Nilivyoamka asubuhi ndio nikaikuta!
Jumanne hivyo hivyo ilivyofika mida ya saa sita mkapita nayo tena, ila ikajitahidi kurudi saa nane bando langu likikaribia kuisha!
Leo hii nimeandika hii taarifa kwa kuweka na Kigogo sababu ya hiyo network kusumbua, ila leo angalau ilikuwa inakata "viuno" yaani inatoweka na kurudi.
Pamoja na kero zote hizo, hata kuomba radhi au kutoa taarifa hakuna! Aiseee!! Mngefidia hata huo muda mliopita na bando zetu basi!
Au mnajifanya hamjui kuwa Mkulu kameza funguo za kibubu?! Morogoro.
wanasumbua ila Sio kama tigo
 
Kuna - sijui niite ni "ujanja" - nadhani kwa kweli. Simu yangu ina laini 2 tu. Voda na Tigo. Niliweka internet ya wote wawili. Lakini hivi sasa upande wa Tigo siwezi kuaccess internet. Nahisi kuna kimchezo ka ku-hack simu za watu hapa. Kama ni kweli, mnaonaje nikiwashitaki kwa mamlaka ya mawasiliano?
shitaki kama una evidence
 
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

- Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
- Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.

Karibu

Vodacom Tanzania
Kwa nini mnatuuzia tablet kwa bei kubwa halafu hamna spea zake?

Mfano,mtu bahati mbaya amevunja kioo cha tablet,kwa nini vioo vyake hamuuzi/kwanini vioo vyake havipatikani? Je mnatuuzia kwa makusudi?
 
Ndg Mteja una deni la 805 Tshs kutokana na huduma za Nipige Tafu. Tafadhali ongeza salio ili kulipia huduma hii. Vodacom Kazi ni Kwako
 
Back
Top Bottom