lamalu
JF-Expert Member
- Jan 6, 2014
- 611
- 766
Nilikuwa nasikia tu kwa wengine leo nimehakikisha kuwa hawa Voda kweli ni wezi. mimi ni mteja ninayetumia mtandao wa voda namba 0762749205,jana usiku saa nne nilinunua solio la sh.1000 kupitia m-pesa na kupata sms "BR04DY593 Imethibitishwa umenunua Tsh1,000 ya muda wa maongezi saa 10:02 PM Tarehe 11/7/15 Salio lako jipya la akaunti ya M-PESA ni Tsh19,670" kuonyesha kwamba nimepata salio hilo la sh 1000,na nikapata sms nyingine kutoka voda "Umepokea Tsh 1000.00. Salio lako jipya ni Tsh 1000.00. Kumb. 444323401339996668. Time: 7/11/2015 10:00:36 PM" hivyo nikajiunga na kifurushi cha siku internet bila kikomo na kupata ujumbe kua ombi langu linashughulikiwa lakini sikupata sms yoyote kunijulisha kuwa nimeunganshwa kwenye kifurushi hicho. nipoangalia salio la maongezi nikakuta zero ,ilipofika saa tano yaani saa moja baadae ndipo nikapata sms "Salio lako halitoshi kununua kifurushi cha Data.Tafadhali ongeza salio lako na kisha jaribu tena au nunua kifurushi kidogo cha data. Time: 7/11/2015 11:02:46 PM" siku yapili yake jumapili saa 1.30PM nikampigia mhudumu wa wateja na kunijibu kwa kwa maneno rahisi tu kuwa internet ni ghali sana na salio langu limeshatumika ingawa nilimuleza kuwa nilikuwa off-line imekuwaje salio litumike.lakini aling'ang'ania maeleo yake ya awali.
Nichogundua kuwa hawa VODA ni WEzI na wahudumu wao kwa wateja wana uelewa mdogo wa mambo ya internet
ingawa nitatoa taarifa kwa Tume ya mawasiliano lakini pia nawashauri wadau mhame mtandao huu kwa kuwa si salama tena
21/7/2015
hawa voda kweli wezi ili kudhibitisha wizi wao wameifungia account yangu ya M-pesa baada ya kutoa malalamiko haya mtandaoni!!!.
Daaah..hata Mimi imenitokea juzi,ila tofaut ni kwamba Mimi niliingiza 1000 sikununua kwa mpesa,kila nikiunga inakataa kuja kuangalia salio nakuta 0 has wameamua kuiba kwa njia hiyo