Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Nilikuwa nasikia tu kwa wengine leo nimehakikisha kuwa hawa Voda kweli ni wezi. mimi ni mteja ninayetumia mtandao wa voda namba 0762749205,jana usiku saa nne nilinunua solio la sh.1000 kupitia m-pesa na kupata sms "BR04DY593 Imethibitishwa umenunua Tsh1,000 ya muda wa maongezi saa 10:02 PM Tarehe 11/7/15 Salio lako jipya la akaunti ya M-PESA ni Tsh19,670" kuonyesha kwamba nimepata salio hilo la sh 1000,na nikapata sms nyingine kutoka voda "Umepokea Tsh 1000.00. Salio lako jipya ni Tsh 1000.00. Kumb. 444323401339996668. Time: 7/11/2015 10:00:36 PM" hivyo nikajiunga na kifurushi cha siku internet bila kikomo na kupata ujumbe kua ombi langu linashughulikiwa lakini sikupata sms yoyote kunijulisha kuwa nimeunganshwa kwenye kifurushi hicho. nipoangalia salio la maongezi nikakuta zero ,ilipofika saa tano yaani saa moja baadae ndipo nikapata sms "Salio lako halitoshi kununua kifurushi cha Data.Tafadhali ongeza salio lako na kisha jaribu tena au nunua kifurushi kidogo cha data. Time: 7/11/2015 11:02:46 PM" siku yapili yake jumapili saa 1.30PM nikampigia mhudumu wa wateja na kunijibu kwa kwa maneno rahisi tu kuwa internet ni ghali sana na salio langu limeshatumika ingawa nilimuleza kuwa nilikuwa off-line imekuwaje salio litumike.lakini aling'ang'ania maeleo yake ya awali.
Nichogundua kuwa hawa VODA ni WEzI na wahudumu wao kwa wateja wana uelewa mdogo wa mambo ya internet
ingawa nitatoa taarifa kwa Tume ya mawasiliano lakini pia nawashauri wadau mhame mtandao huu kwa kuwa si salama tena

21/7/2015
hawa voda kweli wezi ili kudhibitisha wizi wao wameifungia account yangu ya M-pesa baada ya kutoa malalamiko haya mtandaoni!!!.

Daaah..hata Mimi imenitokea juzi,ila tofaut ni kwamba Mimi niliingiza 1000 sikununua kwa mpesa,kila nikiunga inakataa kuja kuangalia salio nakuta 0 has wameamua kuiba kwa njia hiyo
 
0754916840 nimeisajili ila napokea ujumbe kuwa line yangu imefungiwa,kwenda kwa wakala natakiwa kulipia 1000 ili nisajiliwe upya na nipigwe picha hapo hapo kwa wakala,vodacom mnaenda kupoteza wateja! Juz nimeweka elf moja kila nikijiunga na kifurushi bila kikomo inakataa baadae nakuja kuangalia salio nakuta balance ni zero! Na data nilizima,
 
Hiiiii...Mimi ni msichana mrembo,unaweza kuchat na...! Hapo hapo nikaamua kukata simu yenu,niliwaambia mimi nina shida na msichana mrembo? Mbona kila kukicha hamkosi kubuni njia za kusumbua wateja wenu? Hakika mnakera sana mat*k* yenu nyie,kuanzia leo sitaki mnipigie wala kunitumia ma sms yenu yasiyo na kichwa wala miguu,mkome kabisa kama mlivyokoma ku...
 
Yani nimechoka meseji kila dakika mara niwezeshe mara salio halitoshi.

Yani mpaka zimefika 50 zinaingia kwa mfululizo.

Nawauliza nyinyi Vodacom kwani ni lazima kuweka salio na kama natumia internent tu.

Naomba msitume meseji zenu kila mara zinachosha!

Donatila
 
Mbona kuna ubabaishaji katika upatikanaji wa uwakala wa M-pesa? Hata kama umekabidhi documents zote?
 
Hii si support thread? Sasa mbona hamwajibu wajumbe wanaolalamikia ubovu wa huduma zenu? Vodacom Tanzania


hapa naona ni ubabaishaji tu kama huduma zao zilivo, wameona waweke wasikie tunalalamika kuhusu nn halafu watuone kama wajinga. Maana sioni kama post zikijibiwa??!!
 
Last edited by a moderator:
Hii yote ni sababu ya kukosa upinzani wa kweli sambamba na mamlaka husika kutojali watu wake. Bila hivyo wasinge kuwa na jeuri kiasi hiki kwa wateja wao.
Wena wizi mwingine usio rasmi unao kufanya utumie paspo ridhaa yako,ukinunua kifurushi cha data iwe maalmu ama kitokanacho na kifurushi cha maongezi likabakia salio kwenye akaunti yako,ukitumia mb zikaisha hawatoi taarifa mpaka watumie na salio lililomo kwenye akaunti yako. Likiisha ndiyo unaona SMS ya kukutaarifu kuisha kwa kifurushi chako.
 
Nilikuwa naikubali sana huduma ya M PAWA, mpaka pale ilipopotea line ya voda ikiwa na deni lao na mawakala wao wanasema hawawezi kurudisha line mpaka uende voda shop.
sijui itakuwaje na hilo deni lenu.
 
Kifurushi cha internet kwa mwezi bila kikomo maana yake nini? Mbona ukitumia 5gb kinaminywa?
 
Mwezi huu mmeniibia 14000 yangu bila hata sababu. Namba yangu ni 0767210396. Nimepiga customer care na wanadai kuripoti ili kushughulikiwa tatizo langu, siku ya tano hii hakuna lolote. Kwa nini mnatukata pesa zetu bila sababu? Nitasubiria siku 2 kupata majibu, nisipoyapata nitaanzisha thread kabisa kuhusiana na wizi wenu huu...
 
tatizo langu nimesajili lain ya voda
sasa miezimitatu nabiwa nikasaji tena nashindwa kujua nilipo sajili
nimefika nambiwa kuwa umesajiliwa sasa kwanini
 

Attachments

  • 1439266658115.jpg
    1439266658115.jpg
    26.1 KB · Views: 184
Voda nataka kuwalipa deni lenu na line imepotea niwalipe vipi?
na mawakala wenu wanasema hawawezi kuirudisha.
 
Mimi nimeanza na vodacom since inaanza kazi hpa tz bt nimeanza kuichoka mpaka jamaa zng wana niulize ww uko nahisa naibiwa sna
 
Back
Top Bottom