Yaani ni kweli kabisaaa......
Ilaa...... mimi ilishanitokea tofauti.....
Well ni miaka lukuki huko nyuma....
Tulikuwa wapenzi halafu tukaachana sababu ya kuchuniana, (our ego). Wakati huo wote tuko chuo, ila kila mtu anachukua fani tofauti, mimi chuo cha sanaa yeye cha sayansi.
Siku ya siku yeye ndo akanitumia ujumbe amenikumbuke nikamtembelee chuo.....
Nikaenda hadi chuoni kwao mbaliii.....
Kufika pale nikaingia hadi chumbani kwake alikuwa kalala kitandani na pensi pekeyake, mimi niko na mgauni wangu mrefuu hadi kisiginoni ila umenichonga mwili, akaniambia njoo ukae kitandani nikakataa....
Nikakaa kwenye kiti, na yeye hakuamka pale kitandani tukaongeleshana kivivu hivohivo nikaona jau nikamwambia mi naondoka....
Nikajua ataamka anibembeleze nisiondoke, akaniambia haya safari njema....😐😐😐
Nikajiambia mama amka uende hata sikusindikizwa hadi kituoni.....
Nilichukia kwanini nilipoteza muda wangu kwenda hadi Kibaha kutokea Bagamoyo....😑😑
Hata sijui inahusiananje na nilichokwoti, nimejikuta tuu nasimulia...😉