Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

Screenshot_20220828-180642.jpg
 

Mume na mke:​

Jamaa mmoja alizidiwa ghafla usiku wa manane akamwamsha mkewe..
Mume: amka haraka, piga simu hospitali kitengo cha dharura ambulance ije kunichukua nimezidiwa sana!
Mke: ohoo.. kumbe simu yangu haina salio, naomba password ya simu yako niifungue nipige..
Mume: Oohooo! Aah wapi... no, no, no.. wacha tu. Hata hivyo siyo kesi, kila nafsi itaonja mauti bhana..
 

Wadada:​

Mfalme Sulemani alikuwa na wake 700 na alichepuka (cheated) na vimada 300 . Mpenzi wako/Mume wako unamfumania na kimada mmoja tu ugomvi na amani inapotea ndani ya nyumba, unasimulia kuanzia padri, Mchungaji, ukoo wako mzima, mashoga, stress, vidonda vya tumbo, inapelekea mpaka unaokoka, eti kisa kamuonjesha mmoja.. Sasa akionjesha 700 si utapiga kambi Mirembe huko?!!! Wadada acheni HiZO😊
 

Mwaka juzi jamaa aliangalia mechi ya mpira na mkewe..​

WIFE: Baibie, yule ni nani? Ni Chris Brown??
HUSBAND: Yule ni Theo Walcott
WIFE: ile Yellow Card ni ya nini?

HUSBAND: ile ni ya Onyo, na Red Card inamaanisha mchezaji awache kucheza na atoke inje ya uwanja.
WIFE: Oooooh! Inakaa kama traffic light! Yellow- Ilani na Red – Simama
HUSBAND: Yeah yeah swity! Ndio hivyo.
WIFE: Na je Green Card??
HUSBAND: Aaaah! Hakuna kitu kama hicho.

WIFE: Nataka Arsenal ishinde world cup.
HUSBAND: [kimya]
WIFE: Ni nani yule mzee anakaa kama Mr. Bean??
HUSBAND: Yeees swity, yule ni kocha wa Arsenal, anaitwa Arsene Wenger.
WIFE: Oooooh! inamaanisha yule kocha mwengine ni Chelsea Wenger??
HUSBAND: [Kabadilisha channel]😁
 

Madhara ya kusinzia kwenye ibada​

Tukiwa kanisani majuzi, mdada mmoja alikuwa amesinzia , akaamka akasikia tu Pastor anasema:
” SIMAMA”
Yule dada akasimama akashangaa kanisa zima linamtizama kwa mshangao akiwemo mumewe, akaangalia kanisa zima akashtuka kujiona yeye peke yake ndiye aliyesimama..

Pastor akamwambia, wee dada endelea kusimama hivyo hivyo..,
Pastor: tumepata mmoja hadi sasa, huyo aliyesimama..

Pastor: Narudia kwa mara ya mwisho kwa ambaye hajaelewa..
” Kama wewe umewahi kumsaliti mwenza wako au bado unasaliti ndoa yako SIMAMA”
Binti akazima
 

Wadada:​

Mfalme Sulemani alikuwa na wake 700 na alichepuka (cheated) na vimada 300 . Mpenzi wako/Mume wako unamfumania na kimada mmoja tu ugomvi na amani inapotea ndani ya nyumba, unasimulia kuanzia padri, Mchungaji, ukoo wako mzima, mashoga, stress, vidonda vya tumbo, inapelekea mpaka unaokoka, eti kisa kamuonjesha mmoja.. Sasa akionjesha 700 si utapiga kambi Mirembe huko?!!! Wadada acheni HiZO
Mfalme Suleiman alifaidi sana aisee dooh mbususu 700, akifika ya 350 huku nyuma ya 200 si itakuwa ishaziba
 
Back
Top Bottom