Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

Aibu..​

Unatoka sebuleni unaenda zako chooni, unaingia tu hivi, ghafla unakutana na mzigo wa kutisha sana wa KINYESI juu ya Choo!!!
Kwa kuwa hujabanwa sana, unaamua kurudi zako sebuleni...
Ile unatoka tu, unamuona demu mremboo uliyemtongoza jana anakuja kuingia Choo unakotoka wewe na kina mzigo wa haja🙄 Na ashakuona wewe ndo unatoka mle ndani..
Unaona isiwe shida, unaamua kurudi uka flash fasta. Duh, kumbe bahati mbaya maji hakuna kabisaaa..!!!

Hapo ndo utajua kwa nini kuku huoga udongo😳
 

Mchaga​

Mchaga alinunua mbuzi akamwambia mpishi Nyama nusu ipike pilau na ingine itie kwenye friza.​

Kichwa fanya supu, miguu fanya mchuzi chukuchuku.​

Ngozi usitupe tutafanya mswala, utumbo pikia ndizi na mifupa tutawauzia wenye mbwa.​

Kinyesi kihifadhi kwa mbolea ya bustani.​

Mpishi akamuuliza Hutaki na sauti ya mbuzi tufanye ring tone kwenye simu yako?​

Mchaga akajibu Yesuuuu! hivi inawezekana? bac fanya hivyo tuwauzie na wengine hiyo ringtone upesi😊​

 
IMG_20220805_104859_093.jpg
 

Kilichompata jamaa mroho wa nyama..​

Jamaa kaenda kumtembelea rafiki yake Levi, kule sehemu za milimani, akakaribishwa vizuri tu.
Muda si muda bonge ya ugali na nyama nyingi tu zikawekwa mezani., Wakati wanakaribia kumaliza kula, akagundua kuwa shemeji yake, mke wa rafiki yake hali nyama:

JAMAA: Aise hili ni bonge ya lanchi hii, lakini Levi mbona sisi tu tunakula nyama shemeji Gulo hagusi kabisa anaishia mchicha tu? Tabia gani hii?
LEVI: Hapana bestie, wala sijamkataza, ila shemeji yako Mngoni, halagi nyama ya FISI kama sisi😊
 

Mzunguko wa elimu..​

01.👉Wale wanafunzi walioongoza
Mashuleni, wanaenda kwenye
Engineering na Medical schools.

02.👉Wale waliokuwa wa pili, wanachukua MBA na LLB na kuja kuwa Mameneja wa wanafunzi walioshika nafasi ya kwanza.

03.👉Wale waliokuwa wa tatu, wanageukia
Siasa na kuwaongoza wote hapo juu.
Yaani wa kwanza na wa pili.

04.👉Wale waliofeli, wanaenda Jeshi, hawa wakigoma, basi hao wa juu
wote hawana amani..

05.👉Wale waliopata Zero na waliokataa
shule wanakuwa waganga wa kienyeji, na viongozi wa dini..
Wote hapo juu watamtafuta huyu, pale
mambo yao yanapokwenda kombo. Kweli kila mmoja ni bosi akiwa kwenye nafasi yake😊
 

Dogo na dada wa kazi..​

Dogo: mama hivi malaika si wanapaa?
Mama: ndiyo wanapaa, kwani vipi?
Dogo: nimesikia baba jana anamuita dada, malaika wangu, kwa hiyo nae atapaa?
Mama: ndiyo atapaa kuelekea kijijini kwao huko kesho mapema asubuhi.. umbwa kabisa huyu😳
 

Mke mpenda hela!​

Jamaa karudi toka kazini mpole na hana furaha!
MKE; Vipi leo mbona hivyo?!
MUME; Ofisi yetu imeungua na watu wote waliokuwemo wamekufa.
MKE; Duuh! Ilikuaje wewe ukapona?
MUME; Nilikua chooni jirani na ofisi najisaidia.
MKE; Loh maskini, familia zao itakuaje?
MUME; Watalipwa million 100 kila mfiwa.
MKE; (KWA HASIRA), Ona sasa na wewe kupenda kwako kwenda kwenda chooni umetukosesha mihela.. Bora Ungeenda kujisadia akhera huko😳
 

Visa vya Madenge​

Baada ya kumaliza form four babaake akamwambia achague zawadi yoyote aipendayo
MADENGE: naomba pesa nikamuoe bibi maana siku nyingi amekuwa akiniita mchumba wake.
BABA: Shenzi kabisa wewe. Yule ni mama yangu mzazi huwezi kumuoa.
MADENGE: Mbona wewe umemuoa mama yangu mzazi sijasema kitu? Lazima nilipize kisasi ikikuuma muache mama yangu ili kila mtu akae na mamayake😎
 
Back
Top Bottom