kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,317
- 12,617
Kimsingi waafrika walikuwa wanawaona Wazungu kama watu wenye akili nyingi ma matajiri sana kuliko wao, lakini vita ya Ukraine imekanusha ujinga huu wa fikra hizi za inferiority/udhaifu dhidi ya Wazungu.
Mpango wa Uingereza kujitoa kwenye umoja wa Ulaya ulipangwa na Marekani kupitia Uingereza kwa maslahi yake baada ya EU kuikaba roho dollar ya Marekani kwa Euro Yao, uchumi wa Marekani ulikuwa unatishiwa na EU block. Uingereza ikachochewa na US kujitoa kwa ahadi kemkem kutoka US baada ya kujitoa.
Baada ya Uingereza kujitoa kwenye umoja wa Ulaya (Brexit) Uingereza ilitarajiwa ingekuwa na hali mbaya sana kiuchumi na kibiashara, Lakini, ili kuisaidiia UK Marekani na UK walipanga kuzisambaratisha Ujeruman, Ufaransa na Italy kiuchumi ambazo ndio wafadhiri wakubwa wa EU, hivyo EU itakufa na ushindani kwa US na UK dhidi ya EU utakoma.
Njia walioyotumia kuiua EU ni kubuni vita ya Ukraine-Urusi. Vita hii ilibuniwa siku nyingi hata kabla ya Uingereza kutangaza kujitoa EU kwa lengo la kuzinyima nchi za EU nishati kutoka Urusi ambayo ndio kichocheo Cha uchumi wa Ujeruman, Ufaransa na Italy na nchi nyingi za EU.
EU walikuwa wajinga kiasi Cha kutouona huu mtego wa wazi kabisa ambao hata kuku anauona. Baada ya vita kuanza hatua ya kwanza ya Uingereza n kaka yake Marekani ni kutangaza vikwazo vya nishati ya Urusi isikanyage Ulaya na Marekani Huku wakifahamu kuwa uchumi wa Ujeruman na Ulaya unategemea nishati na chakula kutoka Urusi, walifika mbali hadi kuyapasua kwa mabomu mabomba ya kupeka gesi Ulaya na hasa Ujeruman kiranja mkuu wa EU.
Watu walidhani waafrika ndio wenye akili za kuku lakini Sasa inadhihirika wazi kumbe tatizo sio akili mbovu za viongozi wa Afrika bali hata Wazungu akili zao zinaweza kufinyangwafinyangwa pia na kuonekana sio chochote.
Mgogoro huu umetufumbua macho na akili zetu kutambua kumbe Ulaya ni maskini sana kwa rasilimali kuliko Afrika, kumbe Ulaya wanatumia ujanjaujanja kuishi kwa jasho za wengine, kumbe Ulaya nao ni wajinga sana na kumbe bila kunyonya wengine hawawezi kuishi na kumbe ndio maana ilikuwa lazima kwa kutafuta makoloni. Ukweli huu unaonyesha kuwa vita ya kujaribu kutafuta makoloni tena haiko mbali. Hii pia inaonyesha kuwa viongozi wetu tunaowachagua wanakutana na vishawishi na vitisho vingi kutoka nchi za western, hawana kitu, kitu Chao lazima kitoka Africa na kwingineko hata kwa kutumia nguvu.
Mpango wa Uingereza kujitoa kwenye umoja wa Ulaya ulipangwa na Marekani kupitia Uingereza kwa maslahi yake baada ya EU kuikaba roho dollar ya Marekani kwa Euro Yao, uchumi wa Marekani ulikuwa unatishiwa na EU block. Uingereza ikachochewa na US kujitoa kwa ahadi kemkem kutoka US baada ya kujitoa.
Baada ya Uingereza kujitoa kwenye umoja wa Ulaya (Brexit) Uingereza ilitarajiwa ingekuwa na hali mbaya sana kiuchumi na kibiashara, Lakini, ili kuisaidiia UK Marekani na UK walipanga kuzisambaratisha Ujeruman, Ufaransa na Italy kiuchumi ambazo ndio wafadhiri wakubwa wa EU, hivyo EU itakufa na ushindani kwa US na UK dhidi ya EU utakoma.
Njia walioyotumia kuiua EU ni kubuni vita ya Ukraine-Urusi. Vita hii ilibuniwa siku nyingi hata kabla ya Uingereza kutangaza kujitoa EU kwa lengo la kuzinyima nchi za EU nishati kutoka Urusi ambayo ndio kichocheo Cha uchumi wa Ujeruman, Ufaransa na Italy na nchi nyingi za EU.
EU walikuwa wajinga kiasi Cha kutouona huu mtego wa wazi kabisa ambao hata kuku anauona. Baada ya vita kuanza hatua ya kwanza ya Uingereza n kaka yake Marekani ni kutangaza vikwazo vya nishati ya Urusi isikanyage Ulaya na Marekani Huku wakifahamu kuwa uchumi wa Ujeruman na Ulaya unategemea nishati na chakula kutoka Urusi, walifika mbali hadi kuyapasua kwa mabomu mabomba ya kupeka gesi Ulaya na hasa Ujeruman kiranja mkuu wa EU.
Watu walidhani waafrika ndio wenye akili za kuku lakini Sasa inadhihirika wazi kumbe tatizo sio akili mbovu za viongozi wa Afrika bali hata Wazungu akili zao zinaweza kufinyangwafinyangwa pia na kuonekana sio chochote.
Mgogoro huu umetufumbua macho na akili zetu kutambua kumbe Ulaya ni maskini sana kwa rasilimali kuliko Afrika, kumbe Ulaya wanatumia ujanjaujanja kuishi kwa jasho za wengine, kumbe Ulaya nao ni wajinga sana na kumbe bila kunyonya wengine hawawezi kuishi na kumbe ndio maana ilikuwa lazima kwa kutafuta makoloni. Ukweli huu unaonyesha kuwa vita ya kujaribu kutafuta makoloni tena haiko mbali. Hii pia inaonyesha kuwa viongozi wetu tunaowachagua wanakutana na vishawishi na vitisho vingi kutoka nchi za western, hawana kitu, kitu Chao lazima kitoka Africa na kwingineko hata kwa kutumia nguvu.