Nina marafiki zangu waislam, marafiki hasa, ambao naujua upendo wao kwangu, tunashirikiana kwa upendo usioelezeka.
Hata mfanye nini, mimi hata siku moja siwezi kuwachukia hawa waislam marafiki zangu ambao hawajawahi kunitendea ubaya wowote. Hata wale nisio kuwa jirani nao, kamwe siwezi kuwachukia kwa sababu ya imani yao. Mtu achukiwe kwa matendo yao. Yaani mnataka hata nikimwona jambazi akisema ni mkristo, nimpende kwa sababu ya ukristo wake, nisaha ujambazi wake? Na mwingine ni mtu mwema, mwenye uoendo, lakini kwa sababu ni muislam, nimchukie. Ni kiapo mbele ya Mungu wangu, kamwe siwezi kufanya hivyo. Mimi naamini kuwa awe muislam, mkristo au mbudha, Mungu huyatazama matendo yao, na siyo dini yao.
Ayatollah ametangulia mbele za haki, sikuwahi kumchukia kwa sababu ya imani yake, lakini nilimchukia kwa matendo yake ya kikatili, kama lile tendo la kumwua mwanamke ambaye hakuvaa ninja, halafu wanawake wengine walipoandama, nao akawaua, akina mama zaidi ya 70! Hiyo siamini kama ni imani, bali ni ushetani.
Habari mbaya kabisa nimeipokea jana, watoto wadogo, wasio na maamuzi yoyote, zaidi ya 100, wameuawa nchini Iran. Kwa kweli hiyo ilinishtua na kunisikitisha sana kwa kiasi ambacho siwezi kuelezea. Miili ya watoto waliouawa imepangwa kwenye mstari, msululu wa maiti.
Tulio wakubwa, tuna jukumu mbele za Mungu, kuwalinda watoto hawa wasio na hatia, na sio kuwaangamiza. Hata kama ni vita, si sahihi kabisa kuwaangamiza watu wasio na hatia, wasio na uwezo wala kuwa na maamuzi yoyote.
Kama mauaji ya Ayatollah kwa wasio na hatia yalikuwa mabaya, basi ya mwingine yeyote dhidi ya wasio na hatia hayawezi kuwa mazuri
Ingependeza kama Dunia ingeungana kusaidia kuwalinda watoto wa Iran, na wale walio wagonjwa, kwa kuwatengea maeneo maalum, hata ndani ya mataifa jirani.