LINGWAMBA
JF-Expert Member
- Sep 30, 2023
- 419
- 946
Kwa mujibu wa IRNA, katika mashambulizi hayo kambi na vituo vya kijeshi vya utawala wa Kizayuni na askari wa utawala huo katika eneo la kaskazini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu wamelengwa mara kadhaa na mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani.
Aidha, Hizbullah ya Lebanon ilitangaza jana Jumapili kwamba imevilenga kwa makombora vituo vya Roysat al-Alam na Zabadin katika mashamba ya Shabaa ya ardhi za Lebanon zinazokaliwa kwa mabavu na utawala huo ghasibu.
Sambamba na kuanza operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa iliyotekelezwa na makundi ya muqawama ya Palestina Oktoba 7, 2023, harakati ya Hizbullah ya Lebanon imekuwa nayo ikitekeleza oparesheni kali kila siku dhidi ya ngome za utawala wa Kizayuni ili kuzidi kuwashughulisha askari wengi wa jeshi la Kizayuni kaskazini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu na kupunguza mashinikizo dhidi ya muqawama katika eneo la Gaza.
Operesheni za Hizbullah zilianza siku moja tu baada ya kuanza operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa sambamba na uvamizi wa utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza.
Kuhusiana na suala hilo, vyombo vya habari vya Kizayuni vimekiri mara kadhaa kwamba Hizbullah ingali ina nguvu kubwa zaidi za kijeshi katika eneo la kaskazini mwa ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na kwamba jeshi la Israel limenasa kwenye mtego wa eneo hilo.../