Vipepeo weusi season 2: From Zurich with rules

Vipepeo weusi season 2: From Zurich with rules

VIPEPEO WEUSI



SEASON 2 - FROM ZURICH WITH RULES



EPISODE 04



Mikaka mitatu iliyopita nilipoisambaratisha jumuiya ya siri ya The Board moja ya mwanachAma wa jumuiya hiyo ambaye alitakiwa kwenda gerezani alikuwa ni Zephania Zuberi, kipindi hicho akiwa ni mbunge wa jimbo la Nkasi. Moja kati ya maajabu ya maisha niliyowahi kuyaona ni namna ambavyo Mhe. Zephania Zuberi aliweza kushinda ile kesi dhidi ya jamuhuri na hatimaye chama chake kufanikiwa kushika dola na yeye kuchaguliwa kuwa Waziri Mkuu na yote haya yamefanyika ndani ya miaka mitatu pekee.



Japokuwa kwa sasa likuwa ameshikilia nafasi hii nyeti ndani ya nchi lakini kutokana na vitu nilivyokuwa navifahamu nay eye alikuwa bado havifahamu na alihitaji kuvijua kutoka kwangu ndicho hasa ambacho kilikuwa kinamfanya ashindwe kunidhuru au kunifanyia lolote baya licha ya kutamani kufanya hivyo.



Kwa siku mbili zilizopita nilikuwa nimehama kutoka Dodoma Hotel na kuhamia Samali Lodge iliyoko mtaa wa Kiwanja cha ndege hapa Dodoma, sehemu ambayo miaka mitatu iliyopita mimi na Cheupe tulifikia pia tulipokuwa tunawakimbia watu wa jumuiya ya siri ya The Board.



Asubuhi ya leo nilikuwa nimepokea simu kutoka kwa Kaburu kunieleza kuwa kikao changu nilichokiomba na Waziri Mkuu Zephania Zuberi kilikuwa kimefanikiwa na siku ya leo ndio tunatakiwa kuonana. Mahala ambapo tulikubaliana kuonana ilikuwa ni nyumbani kwake eneo la Mlimwa, muda wa usiku baada ya saa tano kamili.



Mbele yangu yalikuwa yamebakia masaa mawili tu kufika saa tano kamili usiku, nilikuwa natembea kwenye barabara ya vumbi yenye kuzungukwa na kijimsitu kidogo ambayo ilikuwa inatokea Kiwanja cha ndege. Barabara hii ndio ilikuwa inaenda kukutana na barabara nyingine ndogo ya Lami ambayo ndiyo hasa ilikuwa inaelekea moja kwa moja mpaka Mlimwa hapa Dodoma ambako kuna makazi ya Waziri Mkuu. Kichwani mwangu nilikuwa nafikiria ni kwa sababu gani mpaka muda huu wawakilishi wa Citibank na LE BLOC walikuwa hawajawasiliana nami ilhali walikuwa wanatakiwa wawepo kwenye kikao hiki. Kwa upande fulani kichwani mwangu nilikuwa nahisi kuwa wale mabinti wawili, yule mzungu na mwenzake wa Kinyarwanda walikuwa ndio wawakilishi nilikuwa nawategemea. Lakini kila nilipowaza hili nilijikuta najikosoa mimi mwenyewe kwamba yawezekana si wao kutokana na mwenendo wao wa kunichunguza kwa siri na kutojitambulisha kwangu.



Karatasi ambazo SIwatu aliziacha pale chumbani kwangu Dodoma Hotel siku mbili zilizopita hazikuweza kunisaidia sana, kwani hazikuonyesha hasa mabinti hao walikuwa ni akina nani, bali zilionyesha mwenendo wa mabinti hao kwa muda wa siku nne ambazo walikuwa pale Hotelini. Yaani walikuwa wanaamka saa ngapi, wanatoka Hotel saa ngapi kwenda kutembea mtaani, wanarejea saa ngapi, wanakula chakula saa ngapi, wanakula nini na kadhalika na kadhalika.

Japokuwa taarifa hizi hazikunisaidia chochote kwenye kujua hasa wale mabinti walikuwa ni akina nani, lakini ziliniachia swali kichwani Siwatu alizipata wapi zile taarifa? Kama alizikusanya yeye mwenyewe, je alikuwa anazikusanya na kufanya hivyo kwa dhumuni gani hasa? Huyu Siwatu kwa uhalisia wake alikuwa ni nani?



Sikutaka kujichosha sana akili yangu kwa maswali na vitendawili vingi ambavyo nilikuwa naviwaza kichwani mwangu. Nilidhamiria kuelekeza akili yangu kichwani kuwaza kikao kilichopo mbele yangu. Kikao changu na Waziri Mkuu Zephania Zuberi. Japokuwa mpaka muda huu, masaa mawili kabla ya kikao bado hakukuwa na dalili yoyote ya muwakilishi wa Citibank au LE BLOC, lakini Kaburu alinieleza kwamba, wamemuhakikishia kuwa watakuwepo kwenye kikao na wawakilishi wao tayari wako Dodoma.



Kichwani nilijiaminisha zaidi kuwa ni wale mabinti wawili. Lakini swali bado lilinaki kichwani, kwanini walikuwa hawajitambulishi kwangu? Na kwa nini walikuwa wananifuatilia kwa siri siri?





Nikiwa bado natembea kwa mguu tayari nikiwa nimekamata barabara ndogo ya lami ambayo inaenda moja kwa moja mpaka Mlimwa… ghafla gari aina ya Range Rover nyeusi, ilinipita kwa kasi kubwa sana huku vioo vyake vyeusi visivyoonyesha ndani vikiwa vimefungwa. Kwa fikira ya haraka haraka niliamini kuwa gari hii ilikuwa inaelekea nyumbani kwa Waziri Mkuu.

Pale Mlimwa mahala ambako kuna nyumba ya Waziri MKuu, imejengwa kwenye muinuko fulani hivi kama mlima. Kutoka hapa ambako nimesimama mpaka nyumbani kwa Waziri Mkuu kulikuwa na kama kilomita tatu au mbili na nusu hivi. Kabla ya kufika kwenye makazi hayo, kutoka hapa nilipo kulikuwa na kona moja ya mwisho ambayo nayo inapita kwenye kijimsitu kidogo. Kwa hiyo kama gari likitangulia mbele yako kwa mita kadhaa, labla mita mia mbili au mita mia tatu, kisha likakata kona hii, mara moja linapotea kwenye upeo wa macho yako lakini unakuja kuliona tena kwa mbali sana lianza kukaribia kwenye Makazi ya Waziri Mkuu kutokana na kuwa mlimani.



Kwa hiyo gari hii aina ya Range Rover iliponipita tu na kukata kona ilipotea kwenye upeo wa macho yangu na kwa kuzingatia kasi ambayo ilikuwa inaendeshwa, nilitegemea ndani ya kama dakika mbili hivi au tatu nianze kuiona kule mlimani ikikaribia kwenye nyumba ya Waziri Mkuu. Lakini zilipita mpaka dakika tano nzima bila kuona gari ile ikitokea kule mbele mlimani. Kwa haraka nikang'amua kwamba gari hii baada ya kukata kona na kuingia kwenye kijimsitu kidogo kilichopo mbele yangu, kuna mahala ilikuwa imesimama. Ni kwasababu gani ilikuwa imesimama, sikuweza kujua kwa haraka, lakini 'machale' yalikuwa yameanza kunicheza.



Nikatembea kama mwendo wa dakika tano nikaiona gari ile imeegeshwa pembezoni mwa barabara mbele yangu. Bila shaka yoyote nilijua kabisa kuwa yeyote yule ambaye alikuwa anaendesha gari hili alikuwa na malengo fulani na mimi.

Nilipoifikia gari pale ilipo, licha ya kiza kinene ambacho kilichopo hapa kwenye hiki kijimsitu, nilijitahidi kuchungulia ndani ya gari na kugundua mkuwa kulikuwa hakuna mtu. Aliyekuwa anaendesha hii gari alikuwa ameshuka na sikuweza kumuona kokote pale karibu na gari hii. Taa za mbele za gari zilikuwa zimeachwa zinawaka mwanga mkali kabisa.



Kitu cha kwanza ambacho nilikifanya ni kupeleka mkono wangu mpaka kiunoni ambako nilikuwa nimeficha silaha yangu, bastola aina ya glock 19 na kisha kuichukua na kuishikilia mkononi. Kisha kwa makusudi kabisa niliendelea kutembea kuelekea mbele huku ule mwanga wa taa za gari ukinimulika. Yeyote yule ambaye alikuwa anafanya mchezo huu nilitaka afahamu fika kwamba nilikuwa na silaha na nilikuwa tayari kuitumia endapo itanibidi kufanya hivyo.



Niliendelea kutembea kuelekea mbele kufuata barabara hii ya kuelekea kwa Waziri Mkuu kwa takribani dakika nyingine kumi na nikahisi kwambu kulikuwa na mtu au watu ambao walikwa wananifuatilia nyuma yangu kwa kujificha. Hivyo kwa haraka sana nikafanya uamuzi wa kuchepuka na kuingia vichakani. Baada nya kuingia vichakani, nikaanza ukimbia kuelekea mkono wa kulia badala ya kuelekea mbele nilikokuwa naenda. Nilikimbia kuelekea kulia kwa kama dakika tatu nzima na kisha nikaanza kukimbia tena kurudi nyuma nilikotoka bila kutumia barabara, yaani nilikimbia vichaka kwa vichaka. Nilikimbia kwa takribani dakika tano nyingine. Kicha nikatembea mpaka bararabari na kuhama upande wa bara bara, yaani mwanzo nilikuwa upande wa kushoto, na sasa nikahamia vichaka vya upande wa kulia.



Baada ya hapo nikaanza kutembea kuelekea mbele kuifuata muelekeo wa nyumba ya waziri mkuu. Mpaka hapa nilijua kabisa kuwa yeyote yule ambaye alikuwa ananifuatilia, kwa kitendo hiki cha ghafla nilichokifnya kwa kukimbia kwenye mzunguko wa mvurugiko pamoja na giza hili lazima atakuwa nimempoteza na hakuwa anafahamu niko wapi. Tumaini langu sasa lilikuwa ni kutafuta na nianze kumfuatilia yeye au wao.



Nilitembea kuelekea mbele kama dakika saba au nane ndipo nikaanza kuona vivuli vya watu wawili mbele yangu kama mita mia moja kutoka nilipo nao wakiwa vichakani wanatafuta kitu. Walikuwa wananitafuta mimi.



Niliwafuatilia kwa kama dakika tano nyingine, nikagundua kuwa walikuwa wanazunguka hapo hapo tu, hawaelekei mbele nilikokuwa nataka. Kwa hesabu ya haraka nilijua kuwa nimebakiwa na kama chini ya saa moja mbele yangu kufikia mihadi yangu na kikao changu na Waziri Mkuu, kama nitaendeleza huu upuuzi unaoendelea hapa tunaweza kujikuta tunawindana mpaka asubuhi kunakucha.



Japokuwa wote tulikuwa gizani, lakini kwa madakika yote haya ambayo tumekaa hapa gizani, nilijikuta macho tayari yamezoea giza na nilianza akuona kwa usawia. Kwahiyo nikainua bastola yangu kwa kujiamini kabisa na kumlenga mmoja wa wale watu akiwa kama mita thelathini mbele yangu, nililenga pajani kwa ke kwa makusudi kabisa ili nimjeruhi tu bila kumsababishia jeraha linaloweza kusababisha kifo.



"Baaaaaaaaannnggg.!!"



Nilifyatua risasi na ilimpata barabara nilipokua ninapataka. Nilitegemea nao watajibu mapigo ya risasi, hivyo baada ya kufyatua risasi hii nilijificha nyuma ya mtu. Dakika nzima ilipita bila kusikia majibu yoyote yale ya riasi kutoka kwao. Nilichokuwa nasikia ni kelele za malalamiko ya maumivu tu kutoka kwa yule ambaye nilimdungua na mwenzake alikuwa anaonekana kama alikuwa anamsaidia kumnyanyua au kumburuza kutoka pale walipo.



Kwa kuwasikiliza tu sauti zao, niligundua kuwa waliuwa ni wanawake na wote wawili walikuwa wanazungumza kifaransa. Niljikuta ghafla nimeshikwa na bumbuwazi baada ya akili yangu mara moja kung'amua kuwa hawa watakuwa ni wale mabinti wawili ambao walikuwa wananifuatilia kwa wiki nzima iliyopita pale Dodoma Hotel. "hawa mabinti wanataka nini?" nilijikuta najiuliza tena na tena kichwani.



Nilianza kusikia sauti zao sasa zinasikika kutoka barabarani, na nikahisi kuwa walikuwa wanataka kupakiana kwenye gari lao na kuondoka hapo kabla sijafanya madhara makubwa zaidi. Bila kupoteza muda mara moja nikatimua mbio kuelekea barabarani walipo.



"simameni hapo hapo mlipo kabla sijawapasua vichwa.!!" Nilikuwa naongea kwa kufoka huku nawafuata pale walipo.



"put the gun down you idiot.!" Moja ya wale akina dada aliongea kwa kingereza chenye lafudhi ya kifaransa.



"I say no body moves!" nikafoka zaidi huku nimewakaribia kabisa.



"Ray nimekwambia weka silaha yako chini!" yule binti mmoja ambaye alikuwa ni yule wa Kinyarwanda aliongea kwa kishwahili fasaha huku amenikazia macho.



Macho yetu yalikuwa yamezoea giza tayari, kwahiyo tulikuwa tunaonana kwa usahihi kabisa. Tulikuwa umbali wa kama mita mbili tu hivi, alipotamka jina langu na kunikazia macho alionekana dhahiri kabisa alikuwa ananifahamu na hawakuwa na nia mbaya dhidi yangu japokuwa nilijua pasina shaka kabisa kulikuwa na jambo fulani hivi la siri ambalo litawawia vigumu sana kuniambia ukweli.



"whoa re you guys? And what the hell do you want? You guys have been following me for the whole week.!! What the hell do you want?" nikang'aka kwa umombo.



"you know exactly who we are… so stop playing around!"



"who is playing around!! I don't know who you are… so I'm going ask you one last time… who are you?"



Ukapita ukimya wa kama dakika mbili nzima tukiwa tumekaziana macho. Bado nilikuwa nimewanyooshea bastola huku kidole kikiwa kwenye 'trigger'. Yule mwenzake pale chini alikuwa anagugumia bad na maumivu ya jeraha la risasi.



"Representatives from LE BLOC and Citibank!" yule binti akaongea kwa hasira kwa kifupi tu akiwa bado amenikazia macho.



"and why didn't you just approach me and say so, all these days ?" nikauliza huku nimeanza kushusha chini bastola yangu.



"we have our reasons!" yule binti wa Kinyarwanda alinijibu bila kuniangalia huku anamuinua mwenzake na kumuweka kwenye siti ya nyuma ya gari.



"like what?" nikamuuliza huku narudisha tena bastola yangu kiunoni.



"..Lets see… unh for 'starters', we don't trust you and may be I could say we don't know you..!" aliongea huku anaanza kufungua mlango wa mbele wa gari wa siti ya dereva.



"…what the hell are talking about! How can you say that you don't know me while you said my name a few seconds ago?"



"its complicated! Lets get the hell out of here before someone find us!"



Akawasha gari na kukata kona kushoto kutoka barabarani kuelekea vichakani. Aliendsha kwa mwendo wa taratibu wa tahadhari kutokana na miti miti mingi hivyo niliweza kulifuatia gari kwa nyuma kwa miguu. Tuliingia ndani ya vichaka kama mwendo wa dakika tatu kutoka barabarani na kisha akasimamisha gari na kisha kufungua mlango wa nyuma aliko mwenzake ili apate hewa safi ya kutosha.

Nikapiga tena hesabu haraka haraka kichwani, itakuwa imebakia kama nusu saa tu ili kufika saa tano kamili ambapo tunapaswa kuonana na Waziri Mkuu.



Yule binti wa Kinyarwanda akachukua begi la mgongoni kutoka katika siti ya nyuma ya gari na kuanza kutoa vifaa vya kurekodia. Nilielewa ni nini alikuwa nataka tufanye. Alikuwa anataka rekodi ya uthibitisho kuhusu uhalali wangu… aikuwa anataka recording namba 004W22 katika mfululizo wa recording nilianza kuziwasilisha LE BLOC na Citibank tangu mwaka na nusu uliopita. Mwezi mmoja uliopita niliwasilisha recording namba 004W21 na sasa ilikuwa ni recording ya tatu kutoka mwisho, 004W22. Kilichoukuwa kinanikera rohoni kwangu ni kwamba kazi hii ya kurekodi tulitakiwa kufanya siku kadhaa zilizopita, lakini ajabu walikuwa wananipiga chenga mabinti hawa. Nilijisikia kukereka haswa kila nikizingatia kwamba pia tulikuwa na dakika chache sana mbele yetu tunatakiwa kuwa mbele ya kikao.





"ok! We are all set.. lets do this quickly" binti wa Kinyarwanda aliongea huku amewasha camera iliyo juu ya stendi yake na kunimulika na taa ya kurekodia.



Sikutaka kupoteza muda… moja kwa moja nikaenda kwenye zoezi lililo mbele yetu.



"Jina langu naitwa Rweyemamu Kajuna, hii ni recording namba 004W22 kuthibitihs nina password ya sanduku 7712/LH"



Yule binti alikuwa amenikazia macho ya kukereka nilipomaliza kujieleza sentesi hii.



"Nini?" Nikamuuliza.



"not good enough!" aliongea kwa lafudhi yake ya kifaransa.



Rohoni nilikereka zaidi. Kwanza nilikereka kwa kunitaka nifanye zoezi hili leo lakini nilikereka pia nikijua wazi kabisa binti huyu hakuwa hata akijua ni nini hasa nilikuwa naongea. Niliamini kabisa alikuwa hata hajua hiyo 'recording namba 004W22' ilikuwa na maana gani. Niliamini tu kuwa alikuwa amekaririshwa natakiwa nijieleze vipi kwenye recording hii. Nilikereka zaidi kila nilipokumbuka kwamba tulikuwa tunachelewa kwenye kikao na Waziri Mkuu, na si hivyo tu nilihofia juu ya uhai wa mwenzake ambaye alikuwa pale kwenye gari anaugulia maumivu.



"..hivi tutarudia hii kwa mara ngapi ili uridhike.!" Nikajitahidi kumuuliza kwa kujifanya kukereka haswa, lakini ukweli ni kwamba akili yangu na macho yangu vyote vilikua kwenye mlango wa gari ulio wazi kama mita tano kutoka pale tulikosimama.



"…tutarudia mara nyingi kadiri ambavyo utaendelea kunizungusha.!" Yule dada naye akaongea kwa ukali kiasi na safari hii kunifanya nihisi hisia ya kukereka kwenye sauti yake.



Sikumjibu chochote moja kwa moja, akili yangu na macho yangu bado vilikuwa kwenye ule mlango wa gari mbele yetu. Nikaanza kuhisi labda huyu binti hajui mwenzake yuko katika hali tete kiasi gani. Lakini kwa kadiri nilivyomsoma juu ya weledi wake wa matumizi ya silaha ilinifanya niondoe hisia za kudhania kuwa labda binti huyu alikuwa hajui hali tete aliyonayo mwenzake pale kwenye gari. Silaha ambayo nilitumia kufyatua risasi aliiona na ilikuwa pale ndani ya gari, bastola aina ya glock 19 na nilikuwa na uhakika kabisa alikuwa anajua madhara ambayo bastola hii inafanya kwenye mwili wa binadamu ikifyatuliwa umbali wa karibu kaka ambavyo mimi niliifyatua.



"…mwenzako kama hatutampatia huduma ya kwanza ndani ya dakika chache zijazo tutampoteza.!" Nikaongea tena kwa mara nyingine huku bado macho yangu nimekaza kuelekea kule ambapo mlango wa gari ulikuwa umefunguliwa.



Hakunijibu chochote kile. Aliendelea tu kunikazia macho. Endapo kama tutaendelea na huu mchezo, ni dhahiri kwamba tutakosa kikao na Waziri Mkuu na pia mtunaweza kumpoteza yule binti wa kizungu ambaye niliamini alikuwa na taarifa nyeti ninazohitaji. Nikakata shauri nijieleze kwa ufasaha kwa kadiri anavyotaka.



"Jina langu naitwa Rweyemamu Charles Kajuna, watu wa karibu wanapendelea kuniita Ray na marafiki zangu wanapendelea kuniita jina la utani 'Kichwa'… hii ni recording namba 004W22 kuthibitisha kuwa ninayo mkononi mwangu password ya sanduku 7712/LH lililopo Union Bank Of India, jijini Mumbay nchini India. Narudia hii isomeke kama recording namba 004W22.!"



Nikamaliza na kumuangalia usoni yule binti huku nimeamkazia macho, "Umeridhika?" nikamuuliza nikiwa nimekereka haswa.



"Angalau inaridhisha kwa utambulisho.!" Akanijibu huku kwa mara ya kwanza nikimuona akitabasamu.





********



SASA HIVI (KWENYE MAKAZI YA WAZIRI MKUU - MLIMWA, DODOMA)





Wote wanne, mimi, Giselle, Ilana na PM Zephania tulikuwa tumekaa kwenye mukimya wa kama dakika mbili nzima pale sebeleni.



PM Zephania alikuwa anitazama huku usoni kama vile ana tabasamu la mbali sana kuashiria kama vile amepata ushindi fulani hivi.



"Ray, nahisi nafahamu ni kwanini uko hapa, na nahisi nafahamu hiki kikao kina lengo gani haswa… lakini kwa faida yetu sote nadhani unieleze kinagaubaga kabisa kila kitu kuhusu lengo la hiki kikao na ni nini hasa kimekusukuma mpka mkufikia hapa leo kwenye kikao hiki.!"



PM zephania aliongea kwa kujiamini na kisha kuinua kikombe cha kahawa alicholetewa muda si mrefu na kunywa kidogo.





Nilielewa ni nini hasa napaswa kueleza… japokuwa nilijua mengi tayari atakuwa anayafahamu lakini nilitakiwa nimueleze kila kitu kuanzia safari yangu ya Zurich miaka mitatu iliyopita, nimueleze kuhusu nilichokikuta kwenye sanduku la siri la mwenyekiti wao lilikuwa linahifadhi nyaraka huko Zurich kwenye tawi la bank ya Citibak, nimueleze pia matukio yote yaliyotokea kwa miaka miwili iliyopita na kunifanya nichukue maamuzi haya ambayo niko nayatekeleza na ambayo yanaweza kabisa kupelekea kuunda upya jumuiya ya siri ya 'The Board'… na mwisho kabisa nimueleze kwa nini nimekuja kuonana naye.



Kwa haraka haraka, naweza kuonekana mwendawazimu kwa kutaka kuunda tena upya jumuiya ambayo nilipambana kufa na kupona kuisambaratisha miaka mitatu iliyopita. Na kwa adui yangu kama PM Zephania anaweza kuhisi labda amenishinda kwa kitendo changu cha kuja kuonana naye.

Lakini kitu ambacho hakijui ni miaka mitatu iliyopita, baada ya safari yangui ya Zurich, nilijiwekea kanuni tatu kuongoza maisha yangu. Three Rules. Na kanuni ya tatu, nilijiapiza kuwa… NITAISHI KILA SIKU YANGU KIMKAKATI… AS A BORN TACTICIAN… KILA HATUA NITAKAYOPIGA INA MAANA TOFAUTI NYUMA YA PAZIA. .. "EVERY MOVE MEANS SOMETHING."







Itaendelea….









THE BOLD
 
The bold, asante lkn hapa kwenye hii episode 4 naona kuna baadhi ya vitu vimekuwa marudio saana ! kuna episode ilielezea mengi sana kuhusu hii ya leo!

Asante ni nzuri!
 
The bold, asante lkn hapa kwenye hii episode 4 naona kuna baadhi ya vitu vimekuwa marudio saana ! kuna episode ilielezea mengi sana kuhusu hii ya leo!

Asante ni nzuri!
Paragraph kadhaa za mwisho zinaungana na Episode 1...

Ukisoma Episode 1 utagundua kuwa kinachoelezwa na Ray kimeanzia katikati... That's why kwenye ile episode 1 pale mwishoni mwishoni Ray anaanza kuelezea movement zake "Wiki moja iliyopita" akiwa Dodoma Hotel...

So basically Episode 2, 3 & 4 zinaonyesha movement za Ray for one week akiwa Dodoma Hotel mpaka kufika pale mlimwa nyumbaji kwa Waziri mkuu... Ndio maana unaona hizo haya za mwisho hapo zina kichwa cha habari "Sasa hivi (Mlimwa, nyumbqni kwa PM)"... Kwa maana ya kwamba stori inarudi katika muda husika aliopo Ray sasa hivi...


Umenipata hapo mamito??
 
Paragraph kadhaa za mwisho zinaungana na Episode 1...

Ukisoma Episode 1 utagundua kuwa kinachoelezwa na Ray kimeanzia katikati... That's why kwenye ile episode 1 pale mwishoni mwishoni Ray anaanza kuelezea movement zake "Wiki moja iliyopita" akiwa Dodoma Hotel...

So basically Episode 2, 3 & 4 zinaonyesha movement za Ray for one week akiwa Dodoma Hotel mpaka kufika pale mlimwa nyumbaji kwa Waziri mkuu... Ndio maana unaona hizo haya za mwisho hapo zina kichwa cha habari "Sasa hivi (Mlimwa, nyumbqni kwa PM)"... Kwa maana ya kwamba stori inarudi katika muda husika aliopo Ray sasa hivi...


Umenipata hapo mamito??
Nimekupata The bold, shukrani kwa ufafanuzi muruwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom