VIPEPEO WEUSI
SEASON 2 – FROM ZURICH WITH RULES
EPISODE 03
Sikujua kwanini lakini nilijikuta nasita kupokea simu ya Kaburu. Nilibaki naitazama tu jinsi ambavyo ilikuwa inaita. Kichwani nilikuwa najiuliza hii ilikuwa bahati mbaya au kulikuwa na muunganiko kati ya simu ya kaburu na bahasha iliyo mkononi mwangu ambayo niliikuta pale sakafuni. Kuna wazo fulani kichwani lilikuwa linaniambia kuwa nisipokee ile simu ya Kaburu lakini pia upande mwingine kuna wazo lilkuwa linanijia kwamba hakukuwa na uhusiano wowote kati ya simu ya Kaburu na bahasha iliyo mkononi mkwangu.
“haloo..” nilijikuta nimepokea simu bila kufikiri mara mbili mbili.
“uko wapi Ray?” Kaburu aliniuliza bila hata kujibu salamu yangu.
“bado niko Dodoma Eric…”
“Nahitaji uje Dar leo hii kwa namna yoyote ile!” Kaburu aliongea kwa sauti ya chini kama vile kuna watu ambao alikuwa hataki wasikie anachozungumza.
Nilijikuta nashindwa kuongea neno lolote. Kama kuna kitu ambacho nilikuwa natamani muda huu basi ilikuwa ni kutopata habari ambayo ingenIongezea kitendawili kingine kichwani mwangu. Kwa sauti hii na jinsi ambavyo Kaburu alikuwa anaongea ilikuwa ni dhahiri kabisa kwamba kulikuwa na kila dalili ya kichwa changu kuvurugika tena kutokana na habari mbaya nyingine ambayo ingeongeza sintofahamu ambyo tayari ilikuwa imenielemea kichwani.
Nilifumba macho kwa nguvu na kutazama juu.
“kuna nini Dar?” nikamuuliza huku bado nimefumba macho.
“Ray nahitaji uje haraka iwezekanavyo… vitu vingine vyote nitakueleza huku… si sawa tukionge kwenye simu.” Aliongea kwa sauti ya kunong’ona zaidi safari hii.
“Kaburu natakiwa pia niwe Morogoro leo hii kwa dharura maalumu… kwa hiyo ni vyema unieleze ni nini hasa ambacho kinaendelea huko Dar.!” Nikapngea kwa kufoka.
“Nimeletewa ujembe kwenye bahasha ambao nadhani unakuhusu.!”
Sikushituka kwa sababu ya kunieleza kuwa kuna ujumbe ameletewa, bali lilikuwa ni neno bahsha ndilo ambalo lilinishitua. Kuna muda unatamani kama uwezo kupotea na usiwepo kwenye maisha haya au kwenye dunia hii. Na kuna muda unatamani labda ubadilishane na mtu mwingine maisha yako. Ndivyo ambavyo nilikuwa najisikia muda huu. Japo bado nilikuwa sifahamu ujumbbe huo alioletewa ulikuwa unahusu nini lakini lakini tayari akili tyangu na kichwa changu kilikuwa kimevuruhika na nilikuwa sitamani kusikia zaidi. Sintofahamu ambayo ilikuwa kichwani mwangu ilikuwa imenielemea tayari, nilikuwa sihitaji sintofahmu nyoingine tena kichwani.
“Ray.., bado hewani?” kabru aliongea. “Ray.. Ray..”
“Niko hapa Eric.!” Nilijibu kwa sauti ya unyonge kabisa.
“Unakuja ama vipi?”
“Hiyo Bahasha ina ujmbe gani?” niliuza kwa sauti ya unyonge.
“Sidhani kama ni sahihi kuongea hili kwenye simu!”
”Eric huo ujumbe unahusu nini?” nikamuuliza kwa hasira.
“ok… ok.!! Umeandikwa ‘December 19, 7712/LH ZURICH, CITIBANK’..” Kaburu aliusoma ujumbe kwa taratibu.
Niligundua kuwa kwenye ujumbe huu ambao Kaburu alikuwa ananisomea japo ulikuwa unafanana kabisa na ule ujumbe ambao nililetewa na Siwatu muda mfupi uliopita lakini ulikuwa hauna vitu kadhaa.
“Umenisomea huo ujumbe kwa usahihi?” nikamuuliza.
“Yes! Umeandikwa hivyo… ‘December 19, 7712/LH ZURICH, CITIBANK’..” akarudia tena kunisomea.
Safari hii niliamini kuwa hakuwa amesahau kitu chochote kukisoma. Ujumbe ambao alikuwa amepelekewa ulikuwa tofauti na huu ambao nilikuwa nao ulioletwa kama lisaa limoja lililopita. Ujumbe wake huu alionisomea ulikuwa hauna neno ‘A+. A+’. pia katika ujumbe wangu neno ‘Citibank’ lilitangulia kabla ya neno ‘Zurich’ tofauti na ujumbe ambo Kaburu alinisomea, neno ‘Zurich’ lilikuwa limetangulia. Nilijua fika kwamba hii haikuwa bahati mbaya, yeyeyote ambaye alikuwa anajaribu kucheza na akili yangu alikuwa na maana kutofautisha jumbe hizi mbili.
“Uliandaa kile kikao nilichokwambia?” nikamuuliza Kaburu.
“Ray hivi umesikia kitu ambcho nimekueleza?” Kaburu aliongea kwa sauti ambayo japo niliku
“Ray hivi umesikia kitu ambcho nimekueleza?” Kaburu aliongea kwa sauti ambayo japo nilikuwa simuoni lakini nilijua kuwa alikuwa kwenye mshangao.
“Siwezi kuja Eric… andaa kikao na Waziri Mkuu!” niliongea kisha nikakata simu.
Kuna mtu ameijua siri kubwa kuhusu mimi na likuwa anajaribu kunichezea akili. Sikujua lengo lake hasa lilikuwa ni lipi lakini ilionekana dhahri kuwa alikuwa na lengo mahususi kabisa kuhus hiki ambacho alikuwa anakifanya.
Nikajirusha kitandani na kulala kuangalia juu ya dari. Nilhisi dunia yangu ilikuwa inataka kupasuka vipande vipande kabla hata azma yangu kutimia. Nikajaribu kuwaza na kuwazua. Ni nini ambacho kilikuwa kinaendelea? Ni nani ambaye alikuwa ananichezea akili?
Niliwaza tena na tena kuhusu kuachwa kwa herufi A+,A+ kjatika ujube ambao Kaburu alikuwa amepelekewa. Kwa ambao tunafahamu suala hili na maana yake, ambao nilikuwa naamini tulikuwa watu watatu tu yaani mimi, marehemu baba yangu na Rais wa Citibank.. A+ ilikuwa inamaanisha kundi langu la damu.
Miaka mitatu iliyopita, siku ya kwanza ambayo nilipelekwa kwenye ghorofa la PPF house waliponitoa damu na kuondoka nayoo sikuelewa walikuwa wanaifanyia nini. Ni mpaka siku ambayo nilifika Zurich ndipo ambapo nilielewa kwa nini wanachama wote wa jumuiya ya siri ya The Board walikuwa wanachukuliwa damu siku ya kwanza tu wanapojiunga na jumuiya hiyo.
Kila ambavyo nilikuwa nafikiria kichwani nilikuwa nakosa jibu la kwanini herufi hizo zinazowakilisha kundi langu la damu, A+ zilikuwa zimeachwa katika ujumbe ambao kaburu alikuwa amepelekewa. Na ni nani hasa alikuwa anafanya mchezo huu?
Kwa upande fulani nikaanza kuhisi labda kuna mtu au kikundi fulani cha watu ambacho kilikuwa kinajaribu kukwamisha juhudi zangu zilizonileta hapa Dodoma… nilianza kuhis labda kuna watu ambao walikuwa hawataki nifanikiwa kukamilisha kitu ambacho kilikuwa kimenileta hapa Dodoma. Na kama kuliuwa na mtu au watu ambao walikuwa hawataki nifanikiwe kukamilisha kilichonileta hapa ni nani au akina nani?
Walau sasa kidgo nikaanza kuona kuna taa ilikuwa inawaka kichwani mwangu. Hili ndilo swali ambalo nilikuwa natakiwa kujiuliza muda wote huu. Ni nani ambaye anaweza kuwa na mslahi ya kutotaka kuona nilichokuja kukifanya hapa Dodoma kilikuwa hakifanikiwi.
Ili niwe kwenye muelekeo sahihi wa kupata jibu la swali ambalo nilikuwa najiuliza kichwani nilikuwa napaswa kutembea hatua kwa hatua kichwani mwangu na kuhusu lengo langu hasa la kuwa hapa Dodoma.
Nikaanza kuwaza kuanzia mwanzo kabisa wa dhamira yangu…
Kutokana na safari yangu ya Zurich miaka miwili iliyopita, licha ya mambo mengi na siri nzito ambazo nilikutana nazo huko kutokana na kufuata maelezo niliyoyakuta kwenye nyaraka ambazo nilikabidhiwa na maraehemu baba yangu siku ambayo alijipiga risasi mbele yangu, nilijikuta kwa namna moja au nyingine nilichokiona zurich kilipandikiza kusudi la kimaisha ndani yangu, a purpose. Kusudi ambalo nisingeweza kumueleza mtu yeyote. Kusudi ambalo nisingeweza kulieleza kwa mtu akanielewa, kusudi ambalo lilikuwa ni vyema zaidi nikibaki nalo mwenyewe moyoni mwangu.
Japokuwa nilijua dhahri kwamba kuna uwezekano mkubwa wa kuijenga tena upya jumuiya ya siri ya The Board ili niweze kutimiza kusudi hili, lakini sikuwa na jinsi nyingine ya kufanya.
Swali ambalo sasa nilihisi nilikuwa napaswa kujiuliza, ni nani ambaye kwa namna yeyete ile asingekuwa tayari kuona dhumuni langu hili linafanikiwa? Au nikijiuliza swali mahususi zaid, ni nani ambaye asingependa kuona The Board inarejea tena kama akihis kuna mazingira ya jumuiya hiyo kuundwa upya?
Jibu ambalo lilikuwa linaninjia kichwani nilikuwa sitaki kuliamini, nilihisi niendelee kutafakari labda nipata jibu mbadala. Lakini kila mbavyo nilikuwa natafakari zaidi nipate jibu mbadala ndivyo ambavyo nilikuwa nazidi kuona kichwani mwangu kuwa jibu ambalo nilikuwa nalo tayari ndilo ambalo lilikuwa jibu sahihi zaidi.
Kwa namna ambavyo nimeishi miaka miwili iliyo pita au miaka mitatu kwa kuwa sahibhi zaidi, na kwa mambo ambayo niliyaona na siri ambazo nimefanikiwa kuzing’amua, ni
The Bold: , nilkuwa na hakika bila shaka yeyote kichwani mwangu kuwa kama kuna mtu au watu ambao kwa gharama yeyote ile wasingeweza kukubali kuona The Board inarejea basi walikuwa ni Rais wa nchi na mke wangu mpenzi Cheupe.
Kama ningemueleza mtu jibu hili nina amini kabisa anenihis labda nimechanganyikiwa. Lakini uhalisia ulikuwa ni kwamba hili ndilo jibu ambalo kichwani mwangu lilikuwa linaleta maana zaidi. Kama kuna mtu alikuwa anafanya huu mchezo basi alikuwa ni Rais wa nchi au mke wangu Cheupe.
Nikainuka kitandani na kuchukua taulo kwenda bafuni. Nilidhamiria kuwa kwa namna yyote ile, ni lazima nitimize kilichonileta hapa Dodoma na kwa namna yeyeote ile lazima nifahamu ni nani yuko nyuma ya ii sintofahamu niliyokuwa nayo kichwani.
Niliona huu ndio ulikuwa muda sahihi wa kuweka mtego ili walau nianze kupata mwanga wa sintofahamu ambayo nilikuwa nayo kichwani. Kabla sijaingiabafuni nilichukua simu na kuandika ujumbe mfupi.
“Mueleze mke wangu kuwa sitaweza kurudi Moro leo..”
Nikamtumia ujumbe huu Issack na kisha nikaingia bafuni.
Nawezekana kuwa mwendawazimu kumtilia mashaka mkewangu, lakini baada ya safari yangu ya Zurich na vitu ambavyo niliviona huko. Nilijiwekea kanuni tatu za kuongoza maisha yangu. Kanuni namba mbili, Second Rule….HAKUNA JAMBO LILILO DHAHIRI MAISHANI. KILA JAMBO NI FUMBO. EVERYTHING IS A SECRET. NOTHING IS AS IT SEEMS.
Nikazima simu baada ya kutuma ujumbe na kuingia bafuni.
Itaendelea…..
THE BOLD