“I wanted to but I couldn’t.”
“Why?”
“Well you said it might get you into trouble if the police get involved in this!” Winnie alinijibu huku ananiangalia kwa macho ya huruma.
Moyoni niliumia kweli kweli. Binti huyu japo tumejuana kwa siku chache tu lakini alikuwa anajali usalama wangu kiasi hiki. Alikuwa anahatarisha maisha yake kwa kutotoa taarifa hii ya kufuatiliwa na watu wasiojulikana polisi na anafanya hivyo ili tu kunilinda nisiingie kwenye matatizo na polisi. Na sasa mimi ndiye mtu pekee ambaye ni tegemeo lake kumnasua kwenye kizaazaa hiki ambacho amejikuta yumo. Moyo ulikuwa unaniuma kwa kuwa nilikuwa sijui nifanye nini, nilikuwa bado sijui hata adui yetu halisi alikuwa ni nani.
Nikiwa nawaza hivi ghafla mlango wa mgahawa ulifunguliwa na aliingia binti mrembo wa kizungu. Alikuwa amevalia kigauni kifupi sana cha rangi nyekundu. Kigauni kilikuwa kifupi kiasi kwamba sehemu kubwa ya mapaja yake yalibakia wazi. Chini alikuwa amevalia viatu virefu vya rangi nyekundu pia. Shingoni alikuwa amevalia mkufu wenye kumeremeta kwa vito vya thamani ambao ulionyesha ulikuwa wa bei ghali si kidogo. Nilipomtazama usoni macho yetu yaligongana, akatabasamu. Naama ndipo hapa ambapo niling’amua, nimewahi pia kumuona huyu binti… yes, nimewahi kumuona. Nilibakia nimemkodolea macho tu… binti alitembea kwa mwendo wa madaha kama mwanamtindo na kwenda kukaa kwenye kiti pale ambapo yule kijana wa kizungu ambaye Winnie alisema kuwa alikuwa anamfutilia alikuwa ameketi. Naam, sasa kumbukumbu yangu ilinijea sawia kabisa, niwahi kuwaona hawa watu… ni siku ile pale Radisson Blu Hotel… siku ile ambapo nilikuwa nabishana yule muhudumu Erica, pale kwenye eneo la kupumzika pale mapokezi kulikuwa na mama mwenye mtoto, alafu kulikuwa na yule jamaa mwenye kuvaa kofia ya pama na koti refu jeusi na pia kulikuwa na hawa wapenzi wawili. Ni hawa hawa ambapo nilipochukua taxi na kuondoka nao walichukua taxi nyingine na kunifuatilia kwa nyuma. Kisha nilipomuamuru dereva asimamishe gari nao walimama kwa muda wa kama dakika moja hivi na kisha kuamua kuondoka wakitupita kwa kasi pale tuliposimama. Naam, ni hawa hawa. Mapigo ya moyo yalinienda mbio.
“What is it?” Winnie aliniuliza.
Alikuwa ameona namna ambavyo nilibadilika mara baada ya yule binti wa kizungu kuingia humu mgahawani na kwenda kuketi pale kwa yule kijana wa kizungu.
“I know them!” nilimjibu bila kumuangalia. Macho yangu bado nilikuwa nimeyakaza kuwatazama wale vijana wa kizungu.
“Who are they?” Winnie aliniuliza kwa shauku.
“I don’t know who they are but this is not the first time I see them!”
Nikiwa najiuliza kichwani ni nini kilikuwa kinaendelea na watu hawa ni akina nani, mara yule kijana wa kiume alimuita muhudumu na kisha kumlipa. Wakainuka yeye na mwenzake yule binti aliyekuja hapa dakika chache ziliopita na kisha wakatoja nje ya mgahawa na kuondoka.