Habibu B. Anga
JF-Expert Member
- May 7, 2013
- 6,557
- 25,757
- Thread starter
- #421
Winnie alibakia ametumbua macho asielewe kile ambacho kilikuwa kinaendelea. Hakuelewa kuhusu hili neno la fumbo ambalo nilipewa siku yangu ya kwanza tu kuingia Zurich ambapo nilitakiwa kufika kwenye mgahawa huu na kuwaambia wahudumu waniletee ‘dragon wings’. Siku ambayo hapa hapa mgahawani baada ya kuwaambia neno hilo la siri nilikutanishwa na yule mzee wa kichina ambaye alinichoma sindano ya kemikali na kupoteza fahamu na kujikuta nimeamka kwenye lile jengo mtaa wa Hardstrasse.
Yule kijana wa miraba mine alisogea pale mlangoni na kutupisha tuingie jikoni. Lilikuwa ni jiko la kisasa la ukubwa wa wastani. Kulikuwa na wapishi kama watano hivi wakiwa na ‘apron’ zao za upishi kila mmoja akioneakana kuwa ‘bize’ kuandaa chakula. Katika wapishi hawa watano mmoja wao alikuwa yule mzee wa kichina ambaye nilikutana naye hapa nilipokuja siku ile ya kwanza.
“Give us some privacy!” yule mzee aliongea na wapishi wengine na wote kwa haraka na heshima kubwa walitoka jikoni.
Yule kijana wa miraba mine ambaye awali alikuwa ametuzuia tusiingie pale mlangoni alifunga mlango kwa ndani. Kwa hiyo ndani ya jiko tulibakia mimi, Winnie, yule mzee na kijana huyu wa miraba minne. Winnie taharuki iliongezeka usoni mwake baada ya mlango wa jiko kufungwa.
“PUUUUUUUUHH.!!!” Nilikuwa nimegeuka nikimuangalia yule kijana akifunga mlango na ghafla nilishitukizwa kwa ngumi nzito ya uso iliyonifanya nijiinamie nikishikilia mdomo na kugugumia kwa maumivu.
“That’s for Ivanka!” yule mzee wa kichina aliongea huku nikimuona akivuta kasi ili kunidondoshea ngumi nyingine.
“PUUUUUUUUHH.!!!” Alinidondoshea ngumi ya pili ambayo ilinipata tumboni.
Nilidondoka chini na kujinyongorota kwa maumivu.
“That’s for Luke…” mzee aliongea kwa kukereka.
“what…the ***…are you doing!” niliongea kwa taabu nikijinyongorota kwa maumivu pale chini sakafuni.
“stupid kid… get up!” mzee alifoka na kuja kuninyanyua mzobe mzobe na kunikalisha kwenye moja ya kiti pale jikoni. Alikuwa ni mzee wa makamo lakini nilishangaa namna ambavyo alikuwa mkakakamavu.
Nilikaa kwenye kitu huku nikiwa kama niko ‘disorriented’. Nilikuwa naona maluweluwe tu. Alikuwa amenishambulia kwa kunishtukiza na sikuwa namuelewa maana ya kile ambacho alikuwa anakisema.
“I told you to go back to the hotel and wait motherfucker! Is that hard?” mzee alifoka huku amenikwida shati uso wake akiwa ameusogeza karibu kabisa na wa kwangu.
Nilibakia nimetumbua macho tu nisijue ni kitu gani hasa niongee. Nakumbuka mara ya mwisho tulipoonana alinipa maagizo hayo. Siku ile ambayo nilikuta mgahawa umefungwa na kuzunguka mlango wa nyuma. Kijana wake wa ulinzi aliponikamata nilimueleza kuwa nimetumwa na ‘melchizedek’. Baadae aliniuliza swali la mtego ambalo nililijibu kwa usahihi. Na kisha akanieleza “go back to the hotel and wait”. Lakini nilipofika hotelini na kukuta chumba kizima kinanukia harufu ya windex na pia kukuta kopo hilo la dawa ya windex imesahauliwa chumbani kwangu niliamua kuondoka na kuhamia kwenye jengo la Hardstrasse. Ni kweli sikufanya kama vile ambavyo alikuwa amenieleza, lakini sikuelewa hiki kipigo chote na kunitajia majina ya Ivanka na Luke alikuwa na maana gani hasa.
“do you know what you have done you son of bitch!! You killed them both..!” mzee alifoka huku akiniachia kwa nguvu shati ambalo alilkuwa amenikwida na kunifanya nisukumwe nyuma nusura nidondoke tena ardhini.
“I don’t understand!” niliongea kwa sauti ya kutetema kwa hasira na uoga.
Yule mzee alienda mpaka upande mmoja wa jiko ambako kulikuwa na makorokoro akapekua pekua na kisha kutoka na bahasha mbili za kaki.
Akatembea haraka haraka kwa hasira mpaka pale nilipo. Kwa hasira kubwa aliweka zile bahasha mbili kwenye meza ya karibu yangu. Kisha nikamuona anafunua lile apron lake la upishi na kisha anapeleka mkono wake kiunoni. Alipotoa mkono alikuwa ameshikilia bastola mkononi.
Sikujua kama nikimbie au nifanye nini. Wote wawili, mimi na Winnie tulibakia tumetumbua macho huku tukitetemeka kwa hisia ambayo tulikuwa nayo kichwani yule mzee alichokuwa anataka kukifanya.
Lakini ajabu ni kwamba aliigeuza ile bastola na kuishika mdomoni huku mshikio akiuelekeza kwangu kwa maana ya kwamba alikuwa ananikabidhi ile bastola. Niliipokea huku mikono inatetemeka. Akachukua na zile bahasha mbili ambazoa likuwa ameziweka pale mezani awali nazo pia akanikabidhi.
“this is the package that I delivered for you at Radison Blue but you were not there.!” Mzee aliongea kwa hasira huku amenikazia macho.
“I don’t understand!” nilimjibu huku bado nikiwa natetemeka.
“Now you are on your own Ray! Don’t ever come back here… if I ever see you here again I swear to God I’m gonn’ skin you alive!” mzee aliongea kwa hasira na kwa msisitizo akionekana kumaanisha kila neno ambalo alikuwa analiongea.
Nilibakia nimemkodolea macho kwa karibia nusu dakika. Niligeuka kumuangalia Winnie, alikuwa ananiangalia kwa woga kama vile ameona kifo mbele yake.
Nikageuka kumuangalia tena yule mzee.
“I don’t understand!” nikamweleza tena.
“Get the *** out of here before I cut off your haed!” mzee aliongea huku ameanza kupiga hatua za taratibu kunifuata tena.
“Let’s go Ray!” Winnie aliongea kwa upole huku ananishika mkono kuniondosha. Nahisi alikuwa amegunduka kwamba kutokana na kilichokuwa kimetoka hapa haraka haraka, akili yangu ilikuwa imesizi ghafla na sikuwa nawaza sawasawa, nilikuwa kama niko kwenye bumbuwazi na uwepo wangu hapa ulikuwa unaendelea kumtia hasira huyu mzee.
Tulitoka jikoni na moja kwa moja kutokea sehemu ya mbele ya mgahawa ambayo tulikuwa tumekaa awali. Tulitembea haraka haraka na kutoka nje mpaka kwenye gari ya Winnie ambayo alikuwa amekuja nayo na kuingia ndani haraka.
Yule kijana wa miraba mine alisogea pale mlangoni na kutupisha tuingie jikoni. Lilikuwa ni jiko la kisasa la ukubwa wa wastani. Kulikuwa na wapishi kama watano hivi wakiwa na ‘apron’ zao za upishi kila mmoja akioneakana kuwa ‘bize’ kuandaa chakula. Katika wapishi hawa watano mmoja wao alikuwa yule mzee wa kichina ambaye nilikutana naye hapa nilipokuja siku ile ya kwanza.
“Give us some privacy!” yule mzee aliongea na wapishi wengine na wote kwa haraka na heshima kubwa walitoka jikoni.
Yule kijana wa miraba mine ambaye awali alikuwa ametuzuia tusiingie pale mlangoni alifunga mlango kwa ndani. Kwa hiyo ndani ya jiko tulibakia mimi, Winnie, yule mzee na kijana huyu wa miraba minne. Winnie taharuki iliongezeka usoni mwake baada ya mlango wa jiko kufungwa.
“PUUUUUUUUHH.!!!” Nilikuwa nimegeuka nikimuangalia yule kijana akifunga mlango na ghafla nilishitukizwa kwa ngumi nzito ya uso iliyonifanya nijiinamie nikishikilia mdomo na kugugumia kwa maumivu.
“That’s for Ivanka!” yule mzee wa kichina aliongea huku nikimuona akivuta kasi ili kunidondoshea ngumi nyingine.
“PUUUUUUUUHH.!!!” Alinidondoshea ngumi ya pili ambayo ilinipata tumboni.
Nilidondoka chini na kujinyongorota kwa maumivu.
“That’s for Luke…” mzee aliongea kwa kukereka.
“what…the ***…are you doing!” niliongea kwa taabu nikijinyongorota kwa maumivu pale chini sakafuni.
“stupid kid… get up!” mzee alifoka na kuja kuninyanyua mzobe mzobe na kunikalisha kwenye moja ya kiti pale jikoni. Alikuwa ni mzee wa makamo lakini nilishangaa namna ambavyo alikuwa mkakakamavu.
Nilikaa kwenye kitu huku nikiwa kama niko ‘disorriented’. Nilikuwa naona maluweluwe tu. Alikuwa amenishambulia kwa kunishtukiza na sikuwa namuelewa maana ya kile ambacho alikuwa anakisema.
“I told you to go back to the hotel and wait motherfucker! Is that hard?” mzee alifoka huku amenikwida shati uso wake akiwa ameusogeza karibu kabisa na wa kwangu.
Nilibakia nimetumbua macho tu nisijue ni kitu gani hasa niongee. Nakumbuka mara ya mwisho tulipoonana alinipa maagizo hayo. Siku ile ambayo nilikuta mgahawa umefungwa na kuzunguka mlango wa nyuma. Kijana wake wa ulinzi aliponikamata nilimueleza kuwa nimetumwa na ‘melchizedek’. Baadae aliniuliza swali la mtego ambalo nililijibu kwa usahihi. Na kisha akanieleza “go back to the hotel and wait”. Lakini nilipofika hotelini na kukuta chumba kizima kinanukia harufu ya windex na pia kukuta kopo hilo la dawa ya windex imesahauliwa chumbani kwangu niliamua kuondoka na kuhamia kwenye jengo la Hardstrasse. Ni kweli sikufanya kama vile ambavyo alikuwa amenieleza, lakini sikuelewa hiki kipigo chote na kunitajia majina ya Ivanka na Luke alikuwa na maana gani hasa.
“do you know what you have done you son of bitch!! You killed them both..!” mzee alifoka huku akiniachia kwa nguvu shati ambalo alilkuwa amenikwida na kunifanya nisukumwe nyuma nusura nidondoke tena ardhini.
“I don’t understand!” niliongea kwa sauti ya kutetema kwa hasira na uoga.
Yule mzee alienda mpaka upande mmoja wa jiko ambako kulikuwa na makorokoro akapekua pekua na kisha kutoka na bahasha mbili za kaki.
Akatembea haraka haraka kwa hasira mpaka pale nilipo. Kwa hasira kubwa aliweka zile bahasha mbili kwenye meza ya karibu yangu. Kisha nikamuona anafunua lile apron lake la upishi na kisha anapeleka mkono wake kiunoni. Alipotoa mkono alikuwa ameshikilia bastola mkononi.
Sikujua kama nikimbie au nifanye nini. Wote wawili, mimi na Winnie tulibakia tumetumbua macho huku tukitetemeka kwa hisia ambayo tulikuwa nayo kichwani yule mzee alichokuwa anataka kukifanya.
Lakini ajabu ni kwamba aliigeuza ile bastola na kuishika mdomoni huku mshikio akiuelekeza kwangu kwa maana ya kwamba alikuwa ananikabidhi ile bastola. Niliipokea huku mikono inatetemeka. Akachukua na zile bahasha mbili ambazoa likuwa ameziweka pale mezani awali nazo pia akanikabidhi.
“this is the package that I delivered for you at Radison Blue but you were not there.!” Mzee aliongea kwa hasira huku amenikazia macho.
“I don’t understand!” nilimjibu huku bado nikiwa natetemeka.
“Now you are on your own Ray! Don’t ever come back here… if I ever see you here again I swear to God I’m gonn’ skin you alive!” mzee aliongea kwa hasira na kwa msisitizo akionekana kumaanisha kila neno ambalo alikuwa analiongea.
Nilibakia nimemkodolea macho kwa karibia nusu dakika. Niligeuka kumuangalia Winnie, alikuwa ananiangalia kwa woga kama vile ameona kifo mbele yake.
Nikageuka kumuangalia tena yule mzee.
“I don’t understand!” nikamweleza tena.
“Get the *** out of here before I cut off your haed!” mzee aliongea huku ameanza kupiga hatua za taratibu kunifuata tena.
“Let’s go Ray!” Winnie aliongea kwa upole huku ananishika mkono kuniondosha. Nahisi alikuwa amegunduka kwamba kutokana na kilichokuwa kimetoka hapa haraka haraka, akili yangu ilikuwa imesizi ghafla na sikuwa nawaza sawasawa, nilikuwa kama niko kwenye bumbuwazi na uwepo wangu hapa ulikuwa unaendelea kumtia hasira huyu mzee.
Tulitoka jikoni na moja kwa moja kutokea sehemu ya mbele ya mgahawa ambayo tulikuwa tumekaa awali. Tulitembea haraka haraka na kutoka nje mpaka kwenye gari ya Winnie ambayo alikuwa amekuja nayo na kuingia ndani haraka.