Tumpara Dudu
JF-Expert Member
- Nov 15, 2016
- 662
- 606
Awezi kukulushia ubweche alipika nusu kiloMkuu The Bold sikukuu inaisha bila bila? Kama kuna chochote kirushe Mkuu tuendelee kufurahia sikukuu.
Oh! Kumbe
Mkuu The Bold sikukuu inaisha bila bila? Kama kuna chochote kirushe Mkuu tuendelee kufurahia sikukuu.
Mkuu ubarikiwe sana“I think we should get moving right now!”
“sorry Ray I won’t be joining you today… I have an appointment with someone!”
“A date?” nilimuuliza kwa utani lakini ajabu ni kwamba nilimuona anajiinamia chini kwa aibu fulani hivi kumaanisha kwamba kile ambacho nilikuwa nakisema kilikuwa sahihi. Nilisikia kama vile moyo wangu unawaka moto.
“My boyfriend is going to be in town today… I have to meet him.” Winnie aliongea huku akiwa amejiinamia chini.
Nilisikia kama kisu cha moto kimepenya moyoni. Mithiri ya kisu cha moto ambacho kinapita kwenye siagi. Mimi na Winnie hatukuwa wapenzi rasmi, lakini kulikuwa na kitu fulani katikati yetu, kitu ambacho kadiri ambavyo tulikuwa tunaepuka kukiongea ndivyo ambavyo kilikuwa kinazidi kuwa na nguvu zaidi. Moyo uliniuma niliposikia ametamka “my boyfriend”.
“Wow! Sounds cozy.” Nikajitahidi kuongea kwa sauti iliyo kawaida lakini kigugumizi kilikuwa dhahiri kabisa katika mwambo wa sauti. “so… see you later?” nikauliza kwa mashaka kabisa nikijua kabisa jibu ambalo nitalipata.
“No! ’ll see you tomorrow.!” Alinijubu na kuinua kichwa kuniangalia.
“send him my regards… will keep you posted!” Niliaga na kuanza kuondoka.
Winnie hakunijibu chochote alijiinamia tena chini, hakuinuka hata kunisindikiza. Hatukuwa wapenzi lakini dhahiri kabisa alikuwa anajisikia aibu kunieleza kuwa leo ataonana na mpenzi wake na watalala wote. Niliondoka roho ikiwa inafukuta, moyo kama vile unawake moto. Nilijisikia hasira na aibu kwa wakati mmoja. Nilisikia hasira kwa kuwa na wivu ambao ulikuwa unanijia kila ambapo nikifikiria kwamba leo hii Winnie atakuwa mikononi kwa mwanaume mwingine. Lakini wakati huo huo nilisikia aibu kwa mume wa mtu, mume wa mwanamke ananyenipenda kwa dhati kabisa kuruhusu hisia za namna hii juu ya mwanamke mwingine kukua moyoni mwangu.
“Stay focused kichwa… stay focused!” nilijisemesha mwenyewe nikiwa napanda taxi kutoka chuoni kwa Winnie kuelekea mtaa wa pertstrasse ambako Vihaan Singh alikuwa anaishi.
Kama dakika kumi na tano baadae taxi ilikuwa imesimama kwenye mtaa wa peterstrasse. Nikalipa na kushuka kuanza kutafuta namba ya nyumba ambayo ilikuwa kwenye anuani. Nilitembea kama dakika mbili hivi mpaka hatimaye nikaipata. Nikasogea mlangoni na kubofya kengele mlangoni. Nilibofya kengele kama mara tatu hivi ndipo niliposikia mtu akifungua mlango.
“Hello.!” Alikuwa ni mwanaume wa kihindi mtu mzima wa makamo ya kama katikati ya miaka arobaini hivi.
“Hello… ’m looking for Mr. Vihaan Singh!”
“This is him… who are you?” alinijibu kwa kingereza kilichojaa lafudhi nzito ya kihindi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Shukran sana mkuu.“My name is Ray, would like to ask you a few questions.” Niliongea huku mwenyewe nikihisi kabisa nilitumia sentesi ambayo haikuwa sahihi sana. Niliuliza kama mtu mwenye mamlaka fulani hivi.
“Who are you? Police?” aliniuliza kwa woga.
“No no no! ’m not with the police… if we can just speak for a few minutes.”
“what is it about?” aliniuliza huku ananiangalia kwa mashaka.
“can I come in?”
“No you can’t! what is it about?” aliniuliza huku nikiona kabisa mashaka yakiongezeka usoni mwake.
Nilikuwa nimefungua maongezi haya kwa sentesi ambazo hazikuwa sahihi kabisa na sasa nilikuwa nimebananishwa kwenye kona.
“its about a passenger you drove day befor…..”
“No no no man! I can’t share with you that kind of information unless you are with the polce.!” kAlinikatisha kabla sijamaliza kuongea na aliongea kwa hasira na kisha kufunga mlango kwa nguvu.
Nikabaki pale nje nimeduwaa tu. Taarifa ambayo nilikuwa nahitaji anipatie ilikuwa ni kinyume na maadili ya kazi yake kabisa na mbaya zaidi nilikuwa nimemuuliza kwa urahisi rahisi kama vile naomba maji ya kunywa. Nikachakata akili haraka haraka.
“it’s a job offer… hundred francs per hour!” niliongea kwa msamiati wa fumbo nikiamini atanielewa kabisa kwamba nataka kumpa hongo ili anipatie taarifa hiyo.
Ulipita ukimya wa kama sekunde thelathini hivi kisha nikasikia mlango unafunguliwa tena kwa nguvu.
“What do you want man?” aliongea kwa hasira kiasi.
Sikutaka kuchelewesha mambo. Nikaingiza mkono mfukoni na kuhesabu faranga hamsini haraka haraka na kumkabidhi mkononi, “You get another fifty after we talk.!” Niliongea huku nimemkazia macho.
Vihaan aligeuka kuangalia kushoto na kisha kuangalia kulia na kisha kufungua mlango niingie.
“you guys go to your room!” Vihaan aliwaambia watoto kama watatu ambao ambao walikuwa pale sebuleni mara baada ya sisi kuingia. “have a seat!” Vihaan alinikaribisha nikae kwenye sofa pale sebuleni. “what is your name again?”
“It’s Ray.!”
“Which customer exactly are you talking about!” aliniuliza huku naye akikaa kwenye sofa.
Nilielewa wazi kabisa kwamba anahudimia watu wengi kwa siku kwa hiyo nilihitaji kumueleza kwa ufasaha mno mpaka kumkumbuka ni mteja gani hasa ambaye nilikuwa namlenga. Lakini ajabu ni kwamba nilipoanza tu kumueleza kuhusu safari yake ya juzi chuo kikuu chA Zurich alimkumbuka ni nani ambaye nilikuwa namlenga.
“You want to know where I took that guy with a black hat and a long over coat?” aliniuliza huku anatabasamu.
“yes yes.. that guy. Wow you have a good memory!”
“Nah not good memory! I remember that guy well because you are not the first one to ask where I took him!”
“what? Someone else asked you about him? Who?” nilipatwa na mshituko wa ghafla kiasi kwamba kama ningekuwa nimesimama ningeliweza kudondoka. Kuna mtu kabla yangu amekuja kwa Vihaan kuuliza kuhusu yule jamaa wa kofia ya pama na koti refu jeusi. “who?” nikamuuliza tena.
“I will do this for three hundred francs!” Vihaan aliongea huku anatabasamu kifedhuli. Alijua kuwa amenibananisha kwenye kona na kwa muda huu nilihitaji taarifa hiyo zaidi ya nilivyokuwa nahitaji oksijeni.
Sikutaka kufikiri mara mbili. Uzuri nilikuwa nimejiandaa tangu nilipotoka hardstrasse, nilijua kuwa lazima nitahitaji fedha kumshawishi dereva taxi ili anipe taarifa hizo kitendo ambacho ni kinyume kabisa na maadili yake ya kazi.
Nikaingiza mkono mfukoni na kutoa kibunda cha fedha. Nikahesabu faranga mia tatu na kuziweka mezani.
“Now tell me where you took him and who is asking questions about him?”
Itaendelea…
Habibu B. Anga “The Bold”
To Infinity and Beyond
Sent using Jamii Forums mobile app
“My name is Ray, would like to ask you a few questions.” Niliongea huku mwenyewe nikihisi kabisa nilitumia sentesi ambayo haikuwa sahihi sana. Niliuliza kama mtu mwenye mamlaka fulani hivi.
“Who are you? Police?” aliniuliza kwa woga.
“No no no! ’m not with the police… if we can just speak for a few minutes.”
“what is it about?” aliniuliza huku ananiangalia kwa mashaka.
“can I come in?”
“No you can’t! what is it about?” aliniuliza huku nikiona kabisa mashaka yakiongezeka usoni mwake.
Nilikuwa nimefungua maongezi haya kwa sentesi ambazo hazikuwa sahihi kabisa na sasa nilikuwa nimebananishwa kwenye kona.
“its about a passenger you drove day befor…..”
“No no no man! I can’t share with you that kind of information unless you are with the polce.!” kAlinikatisha kabla sijamaliza kuongea na aliongea kwa hasira na kisha kufunga mlango kwa nguvu.
Nikabaki pale nje nimeduwaa tu. Taarifa ambayo nilikuwa nahitaji anipatie ilikuwa ni kinyume na maadili ya kazi yake kabisa na mbaya zaidi nilikuwa nimemuuliza kwa urahisi rahisi kama vile naomba maji ya kunywa. Nikachakata akili haraka haraka.
“it’s a job offer… hundred francs per hour!” niliongea kwa msamiati wa fumbo nikiamini atanielewa kabisa kwamba nataka kumpa hongo ili anipatie taarifa hiyo.
Ulipita ukimya wa kama sekunde thelathini hivi kisha nikasikia mlango unafunguliwa tena kwa nguvu.
“What do you want man?” aliongea kwa hasira kiasi.
Sikutaka kuchelewesha mambo. Nikaingiza mkono mfukoni na kuhesabu faranga hamsini haraka haraka na kumkabidhi mkononi, “You get another fifty after we talk.!” Niliongea huku nimemkazia macho.
Vihaan aligeuka kuangalia kushoto na kisha kuangalia kulia na kisha kufungua mlango niingie.
“you guys go to your room!” Vihaan aliwaambia watoto kama watatu ambao ambao walikuwa pale sebuleni mara baada ya sisi kuingia. “have a seat!” Vihaan alinikaribisha nikae kwenye sofa pale sebuleni. “what is your name again?”
“It’s Ray.!”
“Which customer exactly are you talking about!” aliniuliza huku naye akikaa kwenye sofa.
Nilielewa wazi kabisa kwamba anahudimia watu wengi kwa siku kwa hiyo nilihitaji kumueleza kwa ufasaha mno mpaka kumkumbuka ni mteja gani hasa ambaye nilikuwa namlenga. Lakini ajabu ni kwamba nilipoanza tu kumueleza kuhusu safari yake ya juzi chuo kikuu chA Zurich alimkumbuka ni nani ambaye nilikuwa namlenga.
“You want to know where I took that guy with a black hat and a long over coat?” aliniuliza huku anatabasamu.
“yes yes.. that guy. Wow you have a good memory!”
“Nah not good memory! I remember that guy well because you are not the first one to ask where I took him!”
“what? Someone else asked you about him? Who?” nilipatwa na mshituko wa ghafla kiasi kwamba kama ningekuwa nimesimama ningeliweza kudondoka. Kuna mtu kabla yangu amekuja kwa Vihaan kuuliza kuhusu yule jamaa wa kofia ya pama na koti refu jeusi. “who?” nikamuuliza tena.
“I will do this for three hundred francs!” Vihaan aliongea huku anatabasamu kifedhuli. Alijua kuwa amenibananisha kwenye kona na kwa muda huu nilihitaji taarifa hiyo zaidi ya nilivyokuwa nahitaji oksijeni.
Sikutaka kufikiri mara mbili. Uzuri nilikuwa nimejiandaa tangu nilipotoka hardstrasse, nilijua kuwa lazima nitahitaji fedha kumshawishi dereva taxi ili anipe taarifa hizo kitendo ambacho ni kinyume kabisa na maadili yake ya kazi.
Nikaingiza mkono mfukoni na kutoa kibunda cha fedha. Nikahesabu faranga mia tatu na kuziweka mezani.
“Now tell me where you took him and who is asking questions about him?”
Itaendelea…
Habibu B. Anga “The Bold”
To Infinity and Beyond
Sent using Jamii Forums mobile app
Kazi nzuri mkuu pamoja katika kuhamasiha usomaji vitabu TZView attachment 854810
Kitabu changu cha kwanza NYUMA YA ULIMWENGU WA SIRI & UJASUSI kiko tayari na kitakuwa mkononi mwako mwezi huu september... kaa tayari