Vipepeo weusi season 2: From Zurich with rules

Vipepeo weusi season 2: From Zurich with rules

Habari chiefs, kwa Wapenzi wa Simulizi hii ya vipepeo weusi Season 2, kuanzia leo jioni nitaweka muendelezo kama Episode 10 hivi.

Mnisamehe kwa ukimya, ratiba yangu imekuwa ngumu mno mno mno. Nikianza kuweka muendeleo leo jioni itakuwa imeanza rasmi kuendelea na mpaka tutafika mwisho.

Kumradhi kwa usumbufu uliojitokeza na asanteni kwa kusubiri.


Asante!


Habibu B. Anga alias "The bold"
To Infinity and Beyond
 
Barikiwa mkuu.... Huwenda kiu ikaisha... Lakini subira huvuta heri... Episode 10!!
 
Habari chiefs, kwa Wapenzi wa Simulizi hii ya vipepeo weusi Season 2, kuanzia leo jioni nitaweka muendelezo kama Episode 10 hivi.

Mnisamehe kwa ukimya, ratiba yangu imekuwa ngumu mno mno mno. Nikianza kuweka muendeleo leo jioni itakuwa imeanza rasmi kuendelea na mpaka tutafika mwisho.

Kumradhi kwa usumbufu uliojitokeza na asanteni kwa kusubiri.


Asante!


Habibu B. Anga alias "The bold"
To Infinity and Beyond
Jioni inatoweaka sasa kigiza kinaingia
Weka mambo basi Habibu B. Anga
 
Habari chiefs, kwa Wapenzi wa Simulizi hii ya vipepeo weusi Season 2, kuanzia leo jioni nitaweka muendelezo kama Episode 10 hivi.

Mnisamehe kwa ukimya, ratiba yangu imekuwa ngumu mno mno mno. Nikianza kuweka muendeleo leo jioni itakuwa imeanza rasmi kuendelea na mpaka tutafika mwisho.

Kumradhi kwa usumbufu uliojitokeza na asanteni kwa kusubiri.


Asante!


Habibu B. Anga alias "The bold"
To Infinity and Beyond
unazingua sana kamanda!!!
Ulisema jioni unashusha nondo ila tayari zimepita siku 3 sasa
 
Ukapotea kabisaaa Yaani,,, ukijitokeza naomba niongezee kwenye tag list yako chief
 
Habari chiefs, kwa Wapenzi wa Simulizi hii ya vipepeo weusi Season 2, kuanzia leo jioni nitaweka muendelezo kama Episode 10 hivi.

Mnisamehe kwa ukimya, ratiba yangu imekuwa ngumu mno mno mno. Nikianza kuweka muendeleo leo jioni itakuwa imeanza rasmi kuendelea na mpaka tutafika mwisho.

Kumradhi kwa usumbufu uliojitokeza na asanteni kwa kusubiri.


Asante!


Habibu B. Anga alias "The bold"
To Infinity and Beyond
Uwe unaacha uboya mzee...kama huwezi ni bora usiwe unaandika tu... uhuni gani huu unafanya wa kusema tar 11 unashusha uzi hadi leo ni tar 18

Mods njooni mmpige ban kwa kupotosha umma
 
The bold acha upotoshaji kama kazi haijawa tayari bora ukakaa kimya ,ulituahidi kuipost tarehe 11 Leo tarehe 19 bila kupost chochote wala sababu zakueleweka.

Bila kuja na sababu zinazoeleweka kufika Leo jioni uje hapa kuomba msamaha kwa kupotosha umma.
 
VIPEPEO WEUSI



SEASON 2 – FROM ZURICH WITH RULES



EPISODE 07




Niliamka kichwa kikiwa kizito na kikiniuma haswa. Nilianza kupepesa macho huku na huko ili niweze kutambua ni mahali gani hasa nilikuwepo muda huu. Nilikuwa nimelala juu ya sofa kwenye lichumba likubwa au kiuhalisia haswa hapapaswi kuitwa chumba bali lilikuwa ni ghala kubwa ambalo lilikuwa linaonekana halitumiki kwa sasa.

Nilijitahidi kujiiunua kutoka pale kwenye sofa kwa taabu kiasi kutokana na kichwa kuwa kizito na kizunguzungu kwa mbali ambacho nilikuwa nakisikia. Nilijitahidi hivyo hivyo mpka nikainuka na kukaa kitako pale sofani.



Hili lichumba lilikuwa ni kubwa hasa, na kama ambavyo nilihisi lilikuwa ni ghala ambalo kwa sasa lilikuwa halitumiki. Pale ndani kulikuwa na hili sofa nililokalia, pia mbele yangu kulikuwa na kiti na meza vya kiofisi huku pale juu ya meza kukiwa na makororo mengi mno pamoja na kompyuta. Pembeni ya hii meza kulikuwa na kiti kingine. Taa iliyokuwa inatia mwanga kwenye lichumba hili ilikuwa inaning’inia juu kutoka darini kwa waya wake wa umeme.

Kwa namna fulani chumba hiki kilikuwa kinanikumbusha vyumba vya mateso ambavyo nimekuwa naviona kwenye sinema za kuigiza watu wakiwa wanahojiwa huku wakipigwa na kupewa mateso ya kikatili ya kila namnaa.



Nilijaribu kwa uwezo wangu wote niweze kujua ni mahali gani ambapo nilikuwa lakini bado nilishindwa kung’amua. Ukizingatia ugeni wangu kwenye nchi hii ndio kabisa nilishindwa hata kuhisi tu niko mahala gani aumtaa gani. Kitu pekee nilichokuwa nakumbuka ni kile ambacho kilitokea pale kwenye mgahawa wa kichina. Nakumbuka namna ambavyo yule mzee wa kichina aliponitoa damu na kisha kunichoma sindano ya kimiminika fulani na baada ya hapo mwili uliisha nguvu na uanza kuona giza mbele yangu na kisha kupoteza fahamu.


”helloooooo”


Niliita ili kujua kama kuna mtu yeyote hapa zaidi zaidi yangu.


”helloooooo…anybody in here??”


Kimya!


Nikainuka kutoka kwenye sofa na kusimama. Niliendelea kkupepesa macho kila kona ya chumba ili kuona kama kulikuwa na mtu yeyote mule ndani zaidi yangu lakini bado nilihisi upweke tu wa chumba kizima. Dhahiri kabisa hakukuwa namwingine yeyote humu zaidi yangu.

Nikatembea kwa hatua za taratibu ili nisidondoke kutokana na kichwa bado kuwa kizito na nilikuwa nasikia kizunguzungu. Nilikwenda mpaka kwenye meza ile yenye makorokoro na kompyuta juu yake.



Nilitazama kwa makini kila kitu ambacho kilikuwa juu ya meza lakini sikuona maana yoyote ambayo ilikuwa inajengeka kichwani au kunipa maana ya chumba hiki kwa kuangalia vitu hivi juu ya meza. Makorokoro yalikuwa mengi sana pale mezani kiasi kwamba yalikuwa kama uchafu fulani hivi. Kulikuwa na bisibisi, CD zilizovunjika, spea za simu, hard disc za kompyuta, nati za vitu nisivyovijua, na makorokoro mengine mengi kweli kweli. Nilijaribu kufikiri na kufikiri na kufikiri tena, nikijaribu kuunganisha picha, au tuseme kuunganisha matukio na haya makororkoro yaliyopo hapa na hili lichumba, labda niweze kung’amua hapa ni wapi au hiki chumba ni cha dhumuni gani lakini sikuwa Napata jawabu lolote la kuridhisha kichwani.



Nikakaa kwenye kiti pale mezani na kuanza kutafakari. Nikatupa jicho upande mmoja wa lile lijichumba na kuona mlango. Nilitamani kuuendea ule mlango na kujaribu kuufungua labda niondoke kama hakutakuwa na mtu yeyote yule wa kunizuia lakini upande fulani wa roho yangu ulikuwa hautaki kuondoka mahali hapa mpaka nijue ni nini hasa kilikuwa kinaendelea hapa.



Sikutaka kufikiri zaidi na kuumiza kichwa, mara moja niliinuka na kuufuata mlango ambao ulikuwa upande mmoja wa chumba hiki na kuufungua. Ajabu ni kwamba mlango ulifunguka tofauti na nilivyofikiri labda utakuwa umefungwa na kwa funguo.

Nilipotoka nje ya mlango nilikutana na korido ndefu lakini hakukuwa na chumba kingine chochote au mlango mwingine bali ilikuwa ni korido ndefu tu. Niliifuata korido hii mpaka mwisho ambako nilikutana na mlango mwingine ambao nao nilipoufungua, ajabu nao haukuwa umefungwa. Ulifunguka bila tabu.


Nilipofungua, nilitokea nje kabisa kwenye uchochoro katikati ya majengo mengine ya mtaa. Yaani jengo hili ambalo nilikuwa imetoka, lilikuwa ni ghorofa ambalo lilikuwa katikati ya maghorofa mengine na chumba ambacho nilikuwepo kilikuwa kipo ‘ground floor’. Nilipoangalia mbele, mwishoni kabisa wa huu uchochoro niliona unaenda kutokea kwenye barabara kuu japokuwa sikuweza kuona gari lolote likipita au watu kutembea pembezoni mwa barabara. Uchochoro pamoja na mtaa wote huu ambao uchochoro ulikuwa unaenda kutokea, ulikuwa kimya sana. Nilihisi labda tayari ilikuwa ni usiku sana maana sikujua ni kwa muda gani nilikuwa nimepoteza fahamu tangu muda ule nilipokuwa pale kwenye mgahawa wa kichina.



Niliinua kichwa juu kulitazama hili jengo la ghorofa ambalo nilikuwa nimetoka. Lilikuwa ghorofa fulani hivi la namna ya majengo ambayo ukiyaangalia yanaonekana ni jengo la zamani sana na kuu kuu lakini linakupa picha kuwa ‘enzi zake’ lilikuwa ni moja ya majengo ya kifahari. Tofauti na maghorofa ya kisasa ambayo yanakuta za vioo kuanzia chini mpaka ghorofa ya mwisho, ghorofa hii yenyewe ilikuwa imejengwa kwa vitofali vidogo vidogo sana vya kuchoma.



Pale mlangoni nilipotokea kulikuwa na na kijimbao fulani kidogo cha saizi ya kati ambacho kilikuwa na maandishi ya kuonyesha anuani ya jengo hilo kama ilivyo desturi ya majengo yote niliyoyaona hapa Zurich. Nikatupa jicho langu kwenye hiki kijimbao na kusoma anuani.


HARDSTRASSE 201, 1985



Nilielewa kuwa hapa nilipo ni mtaa wa Hardstrasse, ambao ni mtaa namba 201 na hili jengo ni jengo namba 1985. Sikujua ni kwa nini lakini nafsi yangu ilikuwa kama inakorofisha hivi kwa ndani baada ya kusoma kibao hiki kidogo cha anuani.



Nikaanza kutembea kuufuata ule uchochoro kuelekea kule mbele ambako niliona ulikuwa unaenda kukutana na barabara kubwa. Nilitokeza mpaka barabarani. Magari machache sana yalikuwa yanapita kila baada ya dakika kadhaa na pembezoni mwa barabara sikuona watu wowote wale wakipita. Maduka mengi na biashara zilikuwa zimefungwa. Nilihisi kwa hakika kabisa huu utakuwa ni katikati ya usiku.



Ile hali ya kukorofishika nafsini mwangu ambayo niliisikia baada ya kusoma kile kibao cha anuani iliendelea ndani yangu japo sikujua ni kwa nini nilijisikia namna ile.


Nikaangaza macho kila upande wa mtaa kutoka pale ambako nilikuwa nimesimama kujaribu labda kuona kama kuna taxi itapita niweze kusimamisha. Mpaka muda huu nilikuwa sijajua niko mahala gani, na ukweli ni kwamba nilikuwa sina hata uhakika kama bado nilikuwa Zurich au mji mwingine ndani ya Switzerland ingawa jina la mtaa huu lilinifanya nihisi kuwa bado nilikuwa Zurich. Kwa hiyo tegemeo langu pekee la kuweza kurejea hotelini kwangu ni kupata taxi ili iweze kunipeleka.



Nikiwa bado nimesimama pale nikiwaza na kuwazua na labda kuendelea kutumaini muda wowote taxi yaweza kutokea na kunirejesha hotelini, ghafla ‘taa’ ikawaka kichwani mwangu. Wazo la ghafla likajiumba kichwani mwangu. Nilijisikia ile hisia mtu unaipata pale ghafla unapofanya gunduzi ya kitu fulani cha siri sana kilichojificha. Ilikuwa ni ile anuani; Hardstrasse 201, 1985. Nilihisi kuwa kuna ujumbe wa siri umefichwa kwenye anuani hii. Hasa mfuatano wa hizi namba, 201,1985. Mara ya kwanza niliposoma sikugundua ni nini hasa kilikuwa kimejificha kwenye maandishi haya lakini roho yangu nilisikia haina raha. Sasa hivi nilihisi nimetambua kwa nini roho yangu ilishituka niliposoma anuani hii.



Tarehe yangu ya kuzaliwa ni tarehe 20 Januari mwaka 1985. Au kama itaandikwa kwa namba tupu, itakuwa ni 20-1-1985, na jengo hili lilikuwa na anuani ya 201, 1985. Hii ilikuwa ni bahati mbya au? Katika majengo yote yaliyopo hapa Zurich, well kama bado niko Zurich! Lakini katika majengo yote yaliyopo hapa iweje nije kutupwa au kuletwa au kufichwa kwenye jengo lenye anuani sawa kabisa na tarehe yangu ya kuzaliwa.? Kuna ujumbe au jambo ambalo limejificha? Au ni bahati mbaya tu?


Yawezekana ni bahati mbaya tu lakini akili yangu haikutaka kukubali kirahisi namna hii. Niliamini kabisa hapa kuna jambo la zaidi. Nikageuza na kuanza kurejea kwenye ule uchochoro. Kisha moja kwa moja niliufuata ule mlango ambao nilitokea. Niliufungua kwa haraka na kuingia ndani na kutokea kwenye ile korido ndefu.

Moja kwa moja nikaelekea mpaka kwenye ule mlango wa lile lichumba likubwa au ghala ambalo muda mchache uliopita niliamka nikiwa ndani yake.



Kuna kitu kuhusu chumba hiki ambacho mara ya kwanza nilikuwa sijakigundua na nilikigundua safari hii baada ya kujaribu kufungua mlango na kugoma kufunguka. Pale pembeni ya mlango kulikuwa na kama screen ndogo hivi ama ‘tablet’ iliyogandishwa ukutani usawa wa kitasa ambayo katikati ya ile screen kulikuwa na alama ya kiganja cha mkono kimechorwa. Nilielewa kuwa ili mlango huu uweze kufunguka ulikuwa unatumia teknolojia ya kusoma alama za vidole ili kuruhusu muhusika halali tu kuingia ndani ya chumba hiki. Lakini kwa kuwa nilipotoka nilitoka tu bila kipingamizi chochote cha kuthibitisha alama za vidole mlangoni, hivyo niliamini kuwa teknolojia hii ya kuthibitisha alama za vidole ilikuwa inalinda pale tu mtu akitaka kuingia ndani lakini kwenye kutoka hakukuwa na shida yoyote ile.



Nikaanza kuchakata akili kichwani. Nifanyeje ili kuruka hiki kizingiti cha kuthibitisha hizi alama za vidole. Pale juu ya hii screen kulikuwa na kitufe kimeandikwa enter. Nikabofya hapo. Nikaona ile screen kama imewaka kwa kutoa mwanga kama vile inavyokuwa uwashapo simu ikiwa imezimwa. Sijui ni kitu gani kilinikuta kichwani lakini pasipo kufikiria mara mbili mbili nikaweka kiganja changu pale juu ya screen. Nikaona mwanga wa kijani umetokea kumaanisha kuwa alama zangu za vidole zilikuwa zinatambulika na zilikuwa sahihi na nilikuwa na ruhusa kuingia ndani ya hiki chumba.


Moyoni nilishituka haswa, na zaidi ya kushituka nilijikuta Napata hofu zaidi. Kwanza anuani ya jengo inayofanana na tarehe yangu ya kuzaliwa. Sasa hivi alama zangu za vidole vinatambuliwa na hii teknolojia ya ulinzi hapa mlangoni? Hii inawezekanaje? Sijawahi kufika kwenye jengo hili tangu nimezaliwa, na hii ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika hapa, na sina uhakika nimefika fikaje hapa… alafu ati alama zangu za vidole vinatambuliwa kwa usahihi kuwa nina ruhusa ya kuingia humu?



Sikutaka kupoteza muda zaidi kufikiri. Nikaingia ndani ya lile lijichumba.


Nilipoingia tu ndani nikasimama katikati ya chumba na kupepesa macho kila kona ya lile lijichumba. Nilibaki najiuliza tu. Hivi kuna kitu gani hasa ndani ya chumba hiki mpaka mtu afikie hatua ya kukiwekea teknolojia ya ulinzi wa alama za vidole?


Nilitazama lile sofa ambalo mara ya kwanza niliamka nikiwa juu yake. Nikatazama ile meza yenye makorokoro na kompyuta juu yake. Nikahisi labda kuna kitu fulani kwenye hii kompyuta.

Nikatembea na kuifuata mpaka pale mezani na kuketi kwenye kiti. Nikainama chini kuangalia nyaya zake kama ziko sawa sawa. Niliziona zote ziko sawa na zimechomekwa kwenye chanzo cha umeme. Nikaiwasha na mara moja iliwaka. Ilikuwa ni kompyuta fulani hivi si ya kizamani sana lakini pia haikuwa ya kisasa. Ilipowaka na kuanza kuperuzi ndani yake sikupata chochote. Hakukuwa na file wala document yoyote ndani ya kompyuta hii. Ilikuwa kama vile ilikuwa ni mpya kabisa kutoka dukani.



Nikatulia na kuegemea kiti. Nilianza kupata hisia kuwa kuna kitu fulani hivi nilikuwa siangaliia kwa umakini. Nilitulia kwa takribani dakika tatu nzima nikifikiri na huku nikipepesa macho pale chumbani kutoka kitu kimoja mpaka kingine mpaka macho yangu yaliporudi tena kwenye hii meza. Lakini safari hii yalitua kwenye kitu cha muhimu zidi ambacho nilikuwa sijakifikiria muda wote huu. Droo za hii meza. Nikaanza kuvuta droo moja moja na kuzikagua ndani yake. Droo zote mbili za mkono wa kushoto zilikuwa tupu. Nikahamia droo za mkono wa kulia. Nilipofungua tu droo ya juu kabisa nilikuta bahasha ya ukubwa wa A4. Juu yake ilikuwa imeandikwa;


20-1-1985


Tarehe yangu ya kuzaliwa na pia anuani ya jengo hili.


Nilihisi kama vile mkono unatetemeka. Nikaifungua taratibu sana ile bahasha. Ndani yake nilikuta simu ya mkononi pamoja na ‘flash disk’. Nikaiweka simu pembeni. Mshituko nilioupata ulikuwa unanifanya nifanye vitu kama roboti. Taratibu. Nikiwa nimeduwaa tu usoni.


Nikachomeka ile flash disk mahali husika kwenye kompyuta kisha nikaanza kuiperuzi ndani ya kompyuta. Flash disk hii ilikuwa na file moja tu ndani yake. Tena file la video yenye kichwa cha habari 004W01.


Nikabofya ili kuicheza ile video.


Sikuamini macho yangu kile ambacho nilikuwa nakiona mbele yangu. Alikuwa ni marehemu baba yangu, Mzee Charles Bernard Kajuna. Mwenyekiti wa The Board.



”Naitwa Charles Bernard Kajuna. Mwenyekiti wa The Board. Hii ni recording namba 004W01..”


Alianza kwa kujitambulisha video ilipoanza tu kucheza.


Mshituko ambao niliupata ndani yangu nilihisi kama vile dunia nzima imedondoshwa juu ya kichwa changu. Presha nilihisi imepanda na kijasho kikaanza kutoka. Nikaongeza sauti ili nisikie sawia alichokuwa anataka kukiongea.


Itaendelea…


HABIBU B. ANGA 'THE BOLD' - 0718 096 811
 
VIPEPEO WEUSI


SEASON 2 – FROM ZURICH WITH RULES



EPISODE 08


“Naitwa Charles Bernard Kajuna. Mwenyekiti wa The Board. Hii ni recording namba 004W01..”


Kwenye screen ya kompyuta alikuwa ni marehemu baba yangu, mzee Charles Kajuna. Nilikuwa nimepata mshtuko makubwa hasa… lakini nilijikuta naongeza sauti ili niweze kusikia sawia kile ambacho kilikuwa kinaongelewa.

“Mwanangu Rweyemamu..!”

Mzee alianza tena kuongea kana kwamba alikuwa anaongea nami mubashara. Japokuwa ilikuwa ni ‘recording’ lakini jinsi ambavyo alikuwa anaitazama kamera iliyokuwa inamrekodi na jinsi ambavyo alikuwa anaongea ilikuwa ni kama vile alikuwa anaongea nami katika maisha hakisi akiwa mbele yangu muda huu.
Nilijikuta nami namuangalia usoni pale kwenye screen kana kwamba ni mtu halisi.


“Video hii imetengenezwa kwa namna ambayo itacheza mara moja tu na kisha kujifuta… hivyo ni vyema uwe na kalamu na kipande cha karatasi.!”

Aliposema hayo akanyamaza kidogo kama vile alikuwa ananipa mida nitafute kalamu na karatasi.

Nikaanza kuhangaika haraka haraka pale mezani nikifungua kila droo kutafuta kalamu mpaka nikaipata kwenye droo ya chini kabisa. Nikachukua ile bahasha ambayo ilikuwa imewekewa simu na flash disk na kuamua niitumie kuandika hiki ambacho kitakuwa kinazungumzwa hapa.


“Kama leo hii unatazama ujumbe huu, ni matumaini yangu kwamba nitakuwa nimeshafariki… na labda umekuwa ukitafuta majibu ya maswali mengi kichwani au labda umefuata maelekezo yangu na hatimaye kufikia hapa na kukutana na ujumbe huu. Ujumbe huu ni mahususi kwa ajili moja kuu. Nataka uelewe kuhusu siri kuu zaidi kuhusu ulimwengu wetu na zaidi ni kuhusu nchi yako Tanzania. Na kisha ujue jukumu ulilonalo. Kama jumuiya ya The Board bado ipo na inafanya kazi nataka ubonyeze kotufe namba moja kwenye keyboard ili usikie ninacjotaka kukueleza. Pia kama kwa namna fulani jumuiya ya The Board imesambaratika, naomba ubofye kitufe namba mbili hapo kwenye keyboard. Kumbuka ujumbe huu utacheza mara moja tu na kujifuta hivyo kuwa makini na chaguzi yako.!”


Video kwenye screen ikaganda kama vile imewekwa ‘pause’ uku sura ya marehemu baba yangu ikiwa juu ya screen imeganda sehemu ya mwisho pale alipoongea.

“Kama The Board imesambaratika bofya kitufe namba mbili”. Nikairudia tena kichwani ile sentesi. Nikabofya kitufe namba mbili kwenye keyboard.

Video ikafanya kama imezimika kwa kuonyesha rangi nyeusi screen yote, kisha ikaanza tena kucheza.

“Kwa kuwa The Board imesambaratika kabisa… sababu kuu ya kukuongoza uje hadi hapa Zurich ni kukufahamisha uelewe hasa Th Board tulikuwa na lengo gani kuu na kama utakubali nataka ukishaelewe hilo lengo ulibebe wewe binafsi na kulitekeleza.!”


Nilijikuta naanza kutamani kuzima huu ujumbe nisiendelee kuusikiliza. Huu ulikiwa ni zaidi ya uwendawazimu. Nawezaje kukubali kufanya jukumu la jumuiya ambayo nilihatarisha mpaka maisha yangu ili niisambaratishe?

“Kuna mambo matatu tu ambayo nitakueleza katika ujumbe huu. Moja. Hili jengo ulilomo ndani yake limekodiwa kwa niaba yako kwa muda wa miaka mitatu. Si ghorofa lote, ni hapa ulipo na floor nyingine mbili kwenda juu. Kwa muda wa miaka mitatu ijayo pengine hii itakuwa ndio sehemu muhimu zaidi na salama kwako kuliko zote. Nyaraka zote kuhusu jengo hili ziko ukutani upande wa wa chumba hiki row namba tano kutoka chini. Password ni anuani ya jengo hili.!”


“Sielewi unachoongea!!” Nilijikuta naropoka kwa nguvu kabla ya kukumbuka kwamba nasikiliza na kuangalia recording ambayo imerekodiwa labda miaka kadhaa iliyopita. Niliandika haraka haraka kile ambacho alikuwa anakiongea.


“Mbili. Nadhani umepata simu ya mkononi ikiwa pamoja na kifaa chenye ujumbe huu unaoutazama. Ukimaliza kutazama nyaraka za jengo hili bofya ‘speed dial 1’ kwenye simu!”


Akanyamaza tena kidogo.

“Tatu. Recording namba mbili. Jina Charles Bernard Kajuna. OLYMPIAN KINGS. Kilala kheri Ray!”

Ghafla video ikaacha kucheza na kuwa rangi nyuesi tu juu ya screen.


“What the….” Nilijikuta nang’ata midomo kwa hasira.

Sikuelewa karibia asilimia mia Themanini ya kilichokuwa nakisikiliza hapa.

Hili suala la tatu ndio sikuelewa hata robo. “Recording namba tatu. Jina Charles Bernard Kajuna. OLYMPIAN KINGS”. Ni kitu gani alikuwa anaongea?

Nikajaribu kucheza tena ile video. Kila nilipojaribu iliniandikia tu ” this file doesn’t ezist!”

“Fuuuuccckk.!” Nikajikuta natoa tusi kwa nguvu na kusimama kwa hasira.

Mkononi bado nilikuwa nimeshikilia kile kikaratasi nilichokuwa nakiandika. Nilijaribu kukipitia tena haraka haraka kile ambacho nilikuwa nimekiandika. Mwanzoni nilirudia kusoma tena na tena kile ambacho niliandika kuanzia mwishoni. Ule ujumbe namba tatu. Lakini kadiri nilivyourudia ndivyo ambavyo ulizidi kunichanganya. Ikabidi nianze kukisoma nilichoandika kuanzia mwanzoni.

Nilipoanza kusoma kutoka mwanzoni walau nilielewa. Nilisoma tena kile ambacho mzee, ujumbe wa kwanza.

“Moja. Hili jengo ulilomo ndani yake limekodiwa kwa niaba yako kwa muda wa miaka mitatu. Si ghorofa lote, ni hapa ulipo na floor nyingine mbili kwenda juu. Kwa muda wa miaka mitatu ijayo pengine hii itakuwa ndio sehemu muhimu zaidi na salama kwako kuliko zote. Nyaraka zote kuhusu jengo hili ziko ukutani upande wa wa chumba hiki row namba tano kutoka chini. Password ni anuani ya jengo hili.!”


Japokuwa sikuelewa maana kamili ya ujumbe wote lakini walau nilikuwa na pa kuanzia.


Niliikatembea mpaka kwenye ukuta wa upande wa kulia wa hiki chumba. Ulikuwa ni ukuta wa aina fulani hivi ambao umejengwa kwa matofali ya kifahati ya kuchoma.

Sikuelewa hasa nilikuwa natakiwa kufanya nini, lakini nilikumbuka ile kauli aliyosema kwamba “row namba tano kutoka chini.!” Nikahesabu mstari kwa mstari kutoka chini sakafuni mpaka nikafika mstari wa tano wa matofali. Nilipoufikia mstari wa tano nilibaki nadokoa macho tu nisijue nifanye nini. Pamoja na maelezo haya ya ‘row namba tano’ pia nimeelezwa kuwa password ni anuani ya jengo hili. Sikujua hata ni namna gani napaswa nitumie password kwenye haya matofali.

Nikainama na kuweka sikio langu, pengine labda kuna sauti fulani nitasikia, lakini wapi hakukuwa na chochote.
Nikajaribu kugonga gonga kwa vidole kama napiga konzi yale matofali, mara ya kwanza sikugundua. Lakini nilipogonga gonga tena mara ya pili kama napiga konzi nilisikia sauti fulani hivi yale matofali yanatoa. Sauti kana kwamba kwa ndani kuna uwazi fulani hivi. Yaani kana kwamba nyuma ya haya matofali kulikuwa na uwazi mkubwa kama shimo au sanduku.

Nikajaribu kusukuma haya matofali lakini hakuna ambacho kilitokea.

Nilirudi mpaka pale juu ya meza kwenye makorokoro. Sikumbuki kama nilichukua spana au nondo, ninachokumbuka ni kwamba nilichukua kitu fulani kizito kutoka pale mezani na haraka nikaenda pale ukutani na kuanza kugonga kwa nguvu kuyaondoa yale matofali.

Kadiri ambavyo nilikuwa nagonga na kuyaondoa matofali ndivyo ambavyo ule uwazi uliomo nyuma yake kulikuwa dhahiri.

Nikaondoa matofali ukubwa wa eneo la kama mita moja hivi kutoka chini kwenda juu na upana.


Mbele yangu, ndani ya ule ukuta ilikuwa imefichwa ‘vault’ ndogo ambayo ilitengenezwa kwa kufunikiwa na zege nzito ukutani.


Sikutaka kupoteza muda… nilielewa bayana kwamba hapa ndipo ambapo ninatakiwa kutumia hiyo password ambayo ni anuani ya hili jengo.
Nikaifungua ile vault kwa kutumia anuani;


2-0-1-1-9-8-5


Bila hiyana au kokoro, vault ilifunguka.

Ndani ya vault kulikuwa na bahasha nyingine ya kaki. Nikaichukua haraka na kuifungua. Ndani yake kulikuwa na simu kama ile bahasha ya awali pamoja na makaratasi mengi sana.

Nikaanza kupitia kwa haraka haraka yale makaratasi. Mengine sikuyaelewa kwa haraka yalikuwa yanahusu nini. Lakini baadhi niliyaelwa yalikuwa ni mkataba wa upangaji wa jengo hili.

Kitu ambacho kilinishangaza ni kwamba, makaratasi mengine, mfano haya ya upangaji wa jengo hili yalikuwa na sahihi yangu halisi kabisa.

Sikutaka kupoteza muda. Nilichukua ile simu niliyoikuta kwenye bahasha ya kwanza na kubofya ‘speed dial 1’ kama ambavyo nilielekezwa.

Simu iliita kwa muda wa kama dakika moja hivi kisha ikapokelewa.


“Halloo!” Niliongea kwa tahadhali.

“Do you have all the papers?” Sauti nzito yenye lafudhi ya kifaransa iliongea upande wa pili.

Mara moja niling’amua kuwa huyu ndiye yule ambaye huwa namfahamu kama Hudini. Sikujua kama ni jina lake au la, lakini kichwani mwangu nilimuita Hudini.

“Yes! I have them!” Nikamjibu.

“Loose this phone… take the other one and take all the papers and get out of there… we will pick you up in thirty minutes!”

“Where should I wait for…….!”

Simu ilikatwa kabla hata sijamaliza kuuliza swali.

Nilibaki naitazama ile simu kwa hasira kana kwamba ndio huyo Hudini mwenyewe.


Japokuwa kadiri ambavyo hili suala lilikuwa linaenda ‘deep’ zaidi lilikuwa kinazidi kuwa la kuogofya, lakini ndani yangu nilijikuta hari ya kutaka kujua mwisho wake inakuwa kubwa zaidi.


Itaendelea…


THE BOLD
 
VIPEPEO WEUSI


SEASON 2 – FROM ZURICH WITH RULES



EPISODE 09


Karibia dakika kumi sasa zilikuwa zimepita tangu nisimame hapa barabarani. Sikuwa na uhakika kama ni hapa ambapo nilikuwa natakiwa kusubiri au nisimame. “We will pick you up in thirty minutes”, sentesi ya yule jamaa aliyeongea upande wa pili wa simu ilijirudia tena kichwani.

Hapa ambapo nimesimama muda huu ndipo hapa hapa ambapo nilisimama mara ya kwanza kabla ya kupata wazo la fumbo kuhusu anuani ya jengo nililojikuta nimeamka ndani yake bila kujua nimefikaje na kisha kurudi tena ndani ya jengo na hatimaye kuisikiliza ile recording ya Mzee wangu Charles Bernard kajuna.

Kwa asilimia kubwa niliamini kuwa kama kuna mahala ambako wanahitaji niwasubiri basi ni hapa barabarani, kwani ukitoka tu ndani ya lile jengo nililokuwemo moja kwa moja uchochoro wake unatokeza hapa kwenye barabara hii.

Nilitazama tena muda kwenye ile simu ambayo niliikuta ndani ya vault, tayari ilikuwa ni saa tisa na dakika nne usiku. Barabara ilikiwa kimya kabisa. Kwa muda wote ambao nilikuwa nimesimama hapa ni kama magari mawili au matatu tu ndio ambayo niliyaona yamepita. Kulikuwa kimya kabisa pale barabarani. Hakukuwa na hata mtembea kwa miguu mmoja ambaye alipita na wala hakukuwa na dalili yoyote kwamba kunaweza kupita kiumbe yeyote yule muda huu. Nilijihisi kama ndege nimewekwa ndani ya tundu kutokana na hapa nilipokuwa nimesimama.

Jambo la kwanza ambalo lilikuwa linanifurukuta rohoni ilikuwa ni kutokujua niko mahala gani hasa, au kwa usahihi zaidi niseme nilikuwa sijui niko upande gani wa jiji hili la Zurich. Kutokana na jina la mtaa ambalo nililisoma pale mlangoni mwa jengo “Hardstrasse” niliamini kabisa niko ndani ya Zurich lakini sikujua hasa ni upande gani wa Zurich ambao nilikuwa.

Jiji hili nilikuwa nalielewa vyema zaidi nikianza kuitafuta sehemu kwa kuchukulia Uwanja wa ndege wa Zurich kama ndio ‘center’ kichwani mwangu. Hii ndio sababu pia ya kunifanya hata kuchukua chumba cha hoteli karibia kabisa na uwanja huu wa ndege.

Rohoni mwangu sikupenda kabisa hii hali ya kutokujua niko mahala gani na dakika chache zijazo watu nisiowafahamu wanakuja kunichukua na kunipeleka mahali ambapo bado sikujua ni wapi.

Nilijikuta napata hamu nifahamu niko wapi ili iniwezeshe kujua ni wapi hasa nitapelekwa na watu ninaowasubiri hapa hata kama kwa namna fulani watajaribu kunificha wanakonipeleka.

Nilitazama tena saa katika simu. Ilibionyesha kuwa tayari ilikuwa ni saa tisa na dakika kumi. Kama dakika kumi na tano tu zilikuwa zimesalia kabla ya watu hao kuju kunichukua. Kichwani nilipata wazo kuwa nifanye kitu fulani kwa muda huu ukiosalia kabla ya watu hao kufika hapa.

Simu hii niliyoikta kwenye ile vault ndogo ukutani ilikuwa ni Smartphone aina ya Samsung ya kisasa japo sikujua haraka haraka ni tolea gani. Nilifungua mpaka upande wa internet lakini kutokana na simu kuwa mpya sikuweza kupata huduma za mtandao. Lakini nilijua kuwa maeneo mengi ya Zurich yalikuwa na huduma ya Wi-Fi bure, kwa hiyo nikaanza kuranda randa pale barabarani kutoka jengo moja mpaka lingine nikijaribu kuona kama naweza kupata Wi-Fi ya bure. Kama dakika mbili baadae nilikuwa mbele ya jengo moja ambalo mara moja simu yangu ikanasa huduma ya Wi-Fi na moja kwa moja nikafungua tena ‘browser’ ili niweze kuperuzi nilichokuwa nakikusudia.

Nikaingia kwenye ukurasa wa ‘Google Maps’ na kuandika ‘Zurich’. Mtandao ukatafuta kwa kama sekunde tatu tu kisha nikaletewa ramani yote ya Zurich kwenye screen ya simu.

Nikaanza kuikuza ramani ili iweze kuonyesha barabara na mitaa. Baada ya ramani kuwa kubwa nikaanza kutafuta mtaa wa Hardstrasse mpaka nilipoupata. Ulikuwa upande wa pili kabisa wa mji. Yaani mahala uwanja wa ndege wa na hoteli niliyofikia vilipo ni upande mmoa wa mji na hapa Hardstrasse ni upande mwingine kabisa. Yaani ni kama ilivyo mbagala na tegeta labda kwa mfano. Mji wa Zurich umegawanywa kwenye ‘Districts’. Hoteli yangu na uwanja wa ndege vipo ndani ya ‘District 1’ wakati huu mtaa wa Hardstrasse upo kwenye ‘District 5’.

Nikaisoma vyema tena ramani ili niweze kukariri vitu kadhaa muhimu. Kutoka hapa nilipo kurudi nyuma upande wa kusini, nitatokea ‘District 4’ na mbele yake kidogo kuna barabara kuu inayopinda kulia kuelekea mtaa wa Hohlstrasse. Ukienda mbele, kaskazini unakutana na barabara ambayo inachepuka kulia na kuzunguka kisha kurudi tena hapo Hardstrasse na nyingine inapinda kushoto kutokea kwenye taasisi ya elimu inayoitwa Toni-Areal.
Lakini kama utanyoosha moja kwa moja kuelekea kaskazini bila kukunja kona mahala kokote pale basi utakitana na daraja linalovuka kwenye mto mkubwa na kisha kutokea kwenye eneo linaitwa Wipkingen.

Walau nikaridhika kidogo, walau sasa nilikuwa najua niko mahala gani. Nikaondoka kutoka mbele ya jengo hili ambalo nilikuwa nimesimama ili niweze kupata Wi-Fi na kurejea pale pale barabarani amapo nilikuwa nimesimama awali. Saa kwenye simu ilikuwa inaonyesha kuwa tayari ilikuwa ni saa tisa na dakika ishirini na moja. Zilikuwa zimesalia kama dakika tano ama nne tu kabla ya hao ninaowasubiri hawajawasili hapa nilipo.

Damu ilikuwa inachemka kweli kweli nikiwa na shauku ya kuwaona hao ambao niliombiwa kuwa wanakuja hapa baada ya nusu saa. Mkononi nilikuwa nimeshikilia simu pamoja na yale makaratasi ambayo niliyapata ndani ya vault ndogo kwenye lile jengo.

Nikiwa bado nashangaa yale makabrasha mkononi mwangu, ghafla kuna gari ilikuja kwa kasi mbele yangu na kufunga breki kwa nguvu na kusimama. Gari ilikuwa ya rangi nyeupe na ilikuwa na muundo wa aina ya gari ambazo nyimbani tanzania tumezoea kuziita ‘hiace’. Gari yote mpaka madirisha yalikuwa na rangi nyeupe. Nikiwa niko kwenye taharuki kubwa nilishuhudia watu watatu walishuka kutoka kwenye ile gari na kunifuata kwa kasi kubwa pale ambapo nilikuwa nimesimama.

Mmoja wao bila salamu au kuniuliza chochote kile alinichukua simu na makabrasha mkononi mwangu huku mwenzake akinivesha kichwani linguo jeusi kama fuko la kitambaa ili kunifanya nisione.

Kwa kasi na kwa utemi, walinitutusa mpaka ndani ya gari na kisha kufunga milango. Gari lilipokuja lilitokea upande wa kusini na baada ya kunipakia kwa utemi ndani yake waliliondoa kwa kasi kubwa kuelekea upande wa kaskazini.

Waliendesha umbali mfupi kama dakika tano hivi na kisha kukunja kulia. Kichwani nilikumbuka kabisa hii ndio ilikuwa ile barabara ambayo inamichepuko kadhaa ukikunja kona lakini kama ukibakia kundesha kwa barabara hii kuu uliyochepukia basi inakurejesha tena Hardstrasse. Waliendesha gari kwa kasi bila kuchepuka mahakokote pale na kama baada ya dakika tano hivi dereva alikunja tena kona.

Nilitabasamu japokuwa nilikuwa nimefunikwa na hili lifuko jeusi la kitambaa, walikuwa wanajaribu kunichanganya akili nisielewe kule ambako wananipeleka lakini walikuwa wamechelewa na niliwazidi akili kabla.

Gari ilipokunja kona tulielekea kaskazini kwa muda wa karibia dakika kumi na tano nzima. Nilikuwa na uhakika kabisa kuwa tulipita daraja la ule mto mkubwa niliouona kwenye ‘Google Maps’ na muda huu tulokuwa tumeingia eneo la Wipkingen.

Baada ya kama dakika tano nyingine dereva alikunja kushoto na kisha akakunja kulia na gari likasimama. Nilishushwa mzobe mzobe kwa kututuswa kwa utemi kama ambavyo nilipandishwa. Upande huu wa mji ulikuwa na baridi kubwa tofauti kabisa na upande ule wa mji ambao nilikuwa awali. Nilihisi tumeingia kwenye jengo kutokana na milango mizito ambayo nilihisi ya chuma niliyokuwa naisikia ikifunguliwa.

Japokuwa nilikuwa sioni mbele lakini nilipokanyaga tu mguu wangu ndani ya jengo hili kitu cha kwanza nilichokihisi ilikuwa ni harufu ya damu. Na sio damu tu bali ni damu mbichi kabisa.

Mwili wote nilihisi umekufa ganzi ghafla. Japo nilikuwa najiamini kuwa siwezi kuuwawa kabla ya kuambiwa siri niliyokuja kuifukua huku, lakini harufu hii ya damu ilinifanya kujiamini kwangu kuanze kuyeyuka.


Itaendelea…


THE BOLD
 
VIPEPEO WEUSI


SEASON 2 – FROM ZURICH WITH RULES


EPISODE 10


Harufu ya damu ambayo nilikuwa naisikia ilikuwa ni mbichi kiasi kwamba mpaka ilikuwa inachefua rohoni. Nilihisi kwamba eneo hili tuliloingia lilikuwa na ‘hall’ kubwa kutokana na kuakisiwa kwa sauti ya hatua ambazo tulikuwa tunakanyaga sakafuni. Kuna muda nilikuwa nikikanyaga chini nasikia kabisa kwenye kiatu kwamba nimekanyaga kwenye dimbwi la kimiminika. Moyoni nilikuwa naomba iwe ni dimbwi la maji ambalo nilikuwa nakanyaga na si dimbwi la damu.

Tulitembea kama hatua thelathini hivi au arobaini nikasikia mlango mwingine unafunguliwa. Tulipoingia tu ile harufu ya damu ikakoma. Nilikuwa najitahidi kutumia hisia zangu kwa kadiri nilivyoweza ili kujua mazingira na kile ambacho kilikuwa kinaendelea. Lile fuko jeusi la kitambaa ambalo niliveshwa kichwani lilikuwa linanifanya nishindwe kabisa kupumua sawia na lilinifanya nisikie joto la haja.


Mikono yangu haikuwa imefungwa kamba kabisa bali mmoja wa wale watu alikuwa ameikunja na kuishikilia kwa nyuma. Kichwani kila aina ya video ya watu kuchinjwa ambayo nilikuwa nimewahi kuiona mitandaoni ilikuwa inanijia. Kwa hakika nilihisi ni namna gani ambavyo dakika zao za mwisho kabla ya vichwa vyao kutenganishwa na viwili viwili zinavyokuwa.

Tulitembea kama hatua ishirini hivi pale ambalo nilikuwa nahisi kwamba ni korido, kisha nikasikia mlango upande wangu wa kulia ukifunguliwa. Hatukuingia moja kwa moja ndani baada ya mlango kufunguliwa. Nilisikia kama watu wawili ambao tulikuwa nao waliingia kwanza huku mimi na mwenzao au wenzao wengine tukisubiri nje. Tulisubiri kama muda wa dakika mbili hivi kisha nikasikia mlango ukifunguliwa tena kisha tukaingia ndani.

Baada ya kuingia ndani niliongozwa mpaka upande mmoja wa chumba kisha nikaketishwa kwenye kiti. Lile fuko la tambala jeusi usoni likaondolewa.

Nikafikicha macho kutokana na kuuma kwasababu ya kukaa gizani kwenye lile fuko jeusi la kitambaa kwa karibia nusu saa nzima. Baada ya kufikicha macho ndipo nikayaangaza mbele yangu.

Tulikuwa kwenye chumba ambacho kwa kila namna kilionekana kabisa kilikuwa ni chumba cha hoteli. Na hakikuwa chumba cha hoteli ya kichovu, kilionekana ni chumba cha hoteli yenye hadhi fulani ya katikati. Hapa tulipokuwa ilikuwa ni sebule ya chumba hiki. Kulikuwa na masofa mawili upande wangu wa kushoto ambayo yana meza ndogo ya kioo mbele yao. Mimi nilikuwa nimeketishwa kwenye kiti kimoja wapo ambacho kilikuwa ni kiti cha meza ya chakula ambayo nilipogeuka niliona iko nyuma yangu.

Upande wangu wa kulia kulikuwa na meza ya ukubwa wa wastani ya kiofisi pamoja na kiti chake ambayo juu yake ilikuwa na makabrasha kadhaa pamoja na nyaraka zilizotawanywa tawanywa kuashiria kuwa kulikuwa na mtu muda si mrefu kabla hatujawasili alikuwa kuna kazi anaifanya kwenye meza hii.

Kwenye zile sofa upande wangu wa kushoto walikuwa wameketi majamaa wawili wa kizungu wote wamenyoa upara na wamevaa majaketi meusi ya ngozi.

Mlangoni pia alisimama mwingine, huyu alikuwa na ngozi nyeusi lakini naye kama wenzake alikuwa na upara pia amevaa jaketi jeusi la ngozi. Pia nyuma yangu kwenye meza ndogo ya chakula alikuwa ameketi mwingine wa nne. Huyu alikuwa mzungu… lakini naye vile vile pia alikuwa na upara na amevalia jaketi jeusi la ngozi.

Kwa kuwasoma haraka haraka tu, niligundua kwamba hawa walikuwa ni wale ambao walikuwa wamenitoa kule barabarani na kunileta hapa. Hata namna ambavyo walikuwa wamekaa na kunitazama ilionyesha dhahiri kwamba kuna mtu ambaye walikuwa wanamsubiri na nilikuwa na hakika kabisa mtu huyo alikuwa kwenye kile chumba cha kulala.

Nilijikuta akili yangu inawaza kuhusu ile harufu ya damu ambayo nimeisikia pale kwenye ‘hall’ kabla ya kuletwa hapa. Kama ingelitokea kwa namna fulani nimeamka ghafla tu ndani ya chumba hiki, moja kwa moja akili yangu ingeniambia kuwa niko kwenye chumba cha hoteli ya kifahari na kwa hakika ndivyo ambavyo hapa tulipo kulivyokuwa kunaonekana. Lakini swali ambalo nilikuwa najiuliza kichwani na lilikuwa likinitatiza ni namna gani au sababu gani hoteli itapakae harufu ya damu mbichi. Na kama ni hoteli wamewezaje kuniingiza wakiwa wamenivesha jifuko jeusi la kitambaa kichwani?

Majibu yote ambayo yalikuwa yanakuja kichwani yaliniambia kwamba hii haikuwa hoteli. Hili ndilo lilikuwa jibu lenye mantiki zaidi. Lakini wakati kichwani nikipata jibu hili ambalo ndilo hasa lina mantiki, mbele yangu macho yalikuwa yanaona mandhari ya chumba yenye kushawishi kwa asilimia zote kwamba hiki ni chumba cha hoteli.

Nikiwa bado naendelea kushangaa mandhari ya chumba hiki huku nikikinzana mwenyewe kichwani mwangu kupata tafsiri ya hapa nilipo, ghafla mlango wa chumba cha kulala ulifunguliwa na kutoka mwanaume mzee wa kizungu wa makamo hivi. Kwa makadirio ya haraka nilihisi atakuwa na kama miaka sitini hivi au labda sitini na mbili. Japokuwa hakuwa mzee sana lakini kichwani mwake zote zilikuwa nyeupe na alikuwa amezichana vyema kabisa nywele zake hizo za singa singa.

Alikuwa amevalia suti nadhifu yenye kuonekana ya gharama kubwa ya rangi ya kijivu ambayo ilishika vyema mwili wake ambao ulionekana kuwa ni wa mazoezi au labda huko nyuma alizoea sana kufanya mazoezi. Mdomoni alikuwa na kipisi cha masigara makubwa kwa umbo ambayo nimezoea kusikia yakiitwa ‘cigar’.

“Jambo Rweyemamu.!” Mzee alijitahidi kunisalimu kwa kiswahili kibovu kwa lafudhi nzito ya kifaransa.

Mara moja akili yangu iliweza kukumbuka sauti yake. Japokuwa ilikuwa na tofauti kidogo kuisikia kwa masikio uso kwa uso, lakini sauti hii ndiyo yenyewe hakika kabisa ambayo niliongea nayo kwenye simu nikiwa nyumbani Morogoro na kunipa maelezo ya kuja Zurich. Sauti hii ndiyo ambayo mapema usiku wa leo, au jana kwa usahihi zaidi ambayo ilinieleza kwenye simu nikiwa hotelini kwamba niende kwenye ile hoteli ya kichina. Na ni sauti hii pia ambayo ilinipigia simu muda mchache uliopita nikiwa kwenye lile jengo mtaa wa hardstrasse na kunieleza kuwa watakuja kunichukua ndani ya nusu saa. Huyu ndiye mtu ambaye kichwani mwangu nilikuwa namtamhua kama ‘Hudini’!


“Hudini?” Nikaongea kwa kuuliza bila kuitikia salamu yake.

“Hahah do you even know what that means?” Akaniuliza.

“Its you, right? The one I have been talking to on the phone all this time… its you!” Nikaongea kwa msisituzo mkubwa nikiwa na uhakika kabisa na nilichokuwa nakisema.

“Let’s get down to business, shall we?” Akaongea huku anaenda kuketi kwenye kiti kilichopo kwenye ile meza ya ukubwa wa wastani ya kiofisi na akakigeuza kiti upande wangu ili tutazamane sawia.


Alipogeuka kunitazama, tuliganda tukiwa tunaangaliana kwa taribani dakika nzima bila yeyote kati yetu kusema neno lolote lile.
Tuliangaliana mpaka nikamuona anaanza kutabasamu.

“What?” Nikamuuliza.

“Nothing… I just can’t believe it that you are the one who took down one the most powerful organisation in Africa!” Akaongea huku bado akiwa anatabasamu.

“I didn’t take down nothing… I just did what I had to do for my sake..!”

“No no no! For Cheupe… hahah is that what you call her? Cheupe right?” Akaongea huku safari hii akitabasamu kifedhuli.

Sikupenda muelekeo wa mazungumzo yalikokuwa yanakwenda.

“I thought you said we should get down to business?” Nikamkazia macho.

“Sure… here I am! Let’s get down to it..”

Akakohoa kidogo na kuzima lile lisigara likubwa na kuliweka pembeni kwenye kisahani fulani juu ya meza.
Akafungua droo ya meza kisha akatoa makabrasha kadhaa na nyaraka nyingi na kuziweka juu ya meza.

Akaanza kupekua pekua na kisha akachomoa kama nyaraka mbili hivi kutoka kwenye ule msitu wa zile nyaraka alizoIweka mezani. Akazishikilia mkononi na kuniangalia huku akijiandaa kuanza kuongea.

“I believe you know why you are here..!” Akaongea safari hii akiwa ‘serious’ haswa bila tabasamu la utani wala ufedhili.

“Honestly I don’t know why I am… its my curiosity that brought me here… but I don’t know exactly why am here!” Nikaongea kwa mtindo ule ule nikimuangalia nikiwa serious bila tabasamu wala kupepesa macho.

“I could assume why your father didn’t want to tell you exactly why you should come here… you wouldn’t have accepted it!! He wanted you to come here to see for yourself and decide!”

“I am listening!”

“You are ‘The Replacement’!” Akanijibu kwa kifupi tu huku amenikazima macho.

“Replacement for what?” Nikauliza kwa shauku.

Hakunijibu kitu. Akachukua nyaraka moja ambayo alikuwa ameishikilia mkononi na kunikabidhi.

Ilikuwa ni picha. Picha ambayo imepigwa na kutolewa kwenye karatasi kubwa ya A4. Picha ya ‘black and white’.

Picha hii iliwaonyesha watu watatu wakiwa wameketi nje ya nyumba. Watu wazima wawili na mmoja mtoto msichana. Yule mtu mzima mmoja alikuwa ni mzungu wa makadirio ya umri wa kama miaka thelathini hivi. Alikuwa amevalia sati yake nadhifu na tai. Mtu mzima wa pili alikuwa ni mtu mweusi. Mwanaume wa umri wa kama katikati ya thelathini, labda thelathini na tano au sita hivi. Mwanaume huyu alikuwa amembeba yule mtoto wa kike kwa kumpakata pajani. Mtoto huyu wa kike alikuwa wa kama miaka mitano hivi au sita.

Nilihisi moyo unataka kutoka ndani ya kifua kutokana na mapigo ya moyo kwenda kasi mno kwa ghafla. Mtoto huyu wa kike nilikuwa namfahamu kama ambavyo nilikuwa nafahamu kiganja cha mkono wangu. Alikuwa ni Cheupe wangu enzi za utoto wake na huyu aliyempakata alikuwa ni baba yake. Lakini kilichonishitua zaidi sio Cheupe na baba yake bali ni huyu mzungu ambaye alikuwa amekakaa pembeni yao. Sikujua ni kwa nini niliogopa na kushituka moyoni, lakini kwa hakika kabisa kichwani mwangu niliamini kwamba hii haikuwa mara yangu ya kwanza kumuona mzungu huyo na kunahisia mbaya ilikuwa inanijia kila ambavyo niliendelea kujiaminisha kuwa sio mara ya kwanza kumuona mzungu huyo.

Kana kwamba huyu mzee alikuwa ananisoma akili yangu namna nilivyokuwa nahangaika kukumbuka nimemuona wapi huyu mzungu, bila kunisemesha chochote alinikabidhi nyaraka nyingine ambayo ilikuwa imesalia mkononi mwake.

Nayo ilikuwa ni Picha nyingine ya ‘black and white’ ambayo imetolewa kwenye karatasi ya A4. Ilibakia kidogo nidondoke chini na kuzimia.

Picha hii ilikuwa inafanana kabisa na Picha ambayo niliikuta kwenye bahasha ambayo nilikabidhiwa na baba yangu, bahasha ambayo niliifungua siku ile usiku wa manane nilipogombana na Cheupe. Siku ambayo ndio ilizaa mfululizo wa matukio mpaka kunifanya nifike hapa leo hii.
Picha hii ilikuwa inainyesha watu wanne wakiwa eneo la kama bandari hivi muda wa usiku, katikati ya makontena. Watu wawili kati ya wale wanne wakionekana kama ni walinzi. Mmoja akionekana dhahiri ni Rais Albert Kafumu, Rais wa Jamuhuri Ya Muungano wa Tanzania. Na alikuwa naongea na mtu fulani, Mzungu. Mzungu huyo wa kwenye Picha ya Rais Albert Kafumu ndiye Mzungu yule yule ambaye yuko kwenye Picha ya Cheupe na baba yake. Tofauti pekee Picha ile aliyemo pamoja na Cheupe na baba yake ilipigwa zamani mno. Labda miaka hata ishirini na tano iliyopita. Lakini hii ambayo amepiga na Rais wa Tanzania ilionekana ni ya hivi karibuni, labda mwaka au miaka miwili tu iliyopita.

Jasho lilinitoka ghafla. Sikujua ni kwa nini au naogopa nini. Lakini jasho lilinitoka na presha ilinipanda.

“Ray! Now let’s get down to business… and let’s start from the beginning..!” Mzee aliongea kwa kujiamini huku anachukua nyaraka nyingine mezani.

Nilibaki nimeganda namtazama kama sanamu. Nilihisi mwili wote kama umepooza.


Itaendelea…


THE BOLD
 
VIPEPEO WEUSI



SEASON 1 – FROM ZURICH WITH RULES


EPISODE 11


Kiza kinene. Hicho ndicho kitu pekee ambacho nilikuwa nakikumbuka. Kiza kinene. Kiza kinene na baridi kali hasa maeneo ya tumboni pamoja na woga wa aina ambao ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuusikia ndani ya nafsi yangu. Maumivu ambayo nilikuwa nayasikia sikuwa nayaogopa kama ambavyo nilikuwa naogopa kila nikitazama damu mkononi mwangu. Sikuwahi kujua hapo kabla ni namna gani mtu anajisikia au anaona pale ambapo anakaribia kifo. Sikiwahi kujua namna ambavyo macho yanaanza kupoteza nuru na kitu pekee ambacho unakiona mbele yako ni kiza. Sikuwahi kujua ni namna gani mwili wako unaweza kuwa na siha njema lakini ukashindwa kuinua hata kidole na kukisogeza.

Nikarejesha tena mkono tumboni kuzuia damu zisiendelee kutoka. Nikalaza tena kichwa changu sakafuni na kutazama juu angani.

“Huu hauwezi kuwa mwisho wangu.!!”

Nilitamka tena kauli ile ile ambayo nilikuwa nairudia tena na tena tangu nimedondoka. Nikainua tena mkono kutoka tumboni na kuutazama namna ambavyo ulikuwa umeloa damu. Macho yalikuwa yameanza kulegea tena kuashiria kuwa naweza kupoteza tena fahamu au labda ndio ikawa safari yangu ya mwisho nisiyafumbue tena.

Sikuwahi kudhania kabla ni namna gani mtu anajisikia akikaribia kifo. Kwa miaka yangu yote duniani kila nikifikiria kifo kitu pekee ambacho kilikuwa kikinijia akilini ni maumivu. Maumivu makali. Lakini ukweli ni kwamba ukikikaribia kifo hakuna maumivu yoyote ambayo unayasikia. Uhalisia ni kwamba nilikuwa sisikii hisia yoyoye ndani yangu zaidi ya woga. Ndio, woga sio maumivu. Woga wa kufumba macho kwa mara ya mwisho nisiweze kuyafumbua tena. Woga wa kulala usingizi ambao sitaweza kuamka tena. Woga wa kutohisi chochote tena, woga wa kutosikia chochote tena. Licha ya risasi ambayo ilikuwa tumboni mwangu lakini sikusikia maumivu yoyote kadiri mwili wangu ulivyoishiwa nguvu, kadiri macho yangu yalivyozidi kupoteza nuru, hakuna cuembe ya maumivu ambayo nilikuwa naisikia. Kitu pekee ambacho nilikuwa nakihisi kwenye nafsi kilikuwa ni woga.

Niliangalia mkono wangu namna ulivyojaa damu kisha nikaurejesha tena tumboni.

Nikajikuta natabasamu. Japokuwa nilikuwa natabasamu lakini kona za macho yangu machozi yalikuwa yanatiririka. Kwa kuwa nilikuwa nimejilaza chali sakafuni, niliyasikia machozi yakitiririka na kuingia masikioni.
Nilikuwa naogopa kufumba macho kwa mara ya mwisho, lakini nilichokuwa nakiogopa zaidi ilikuwa ni kuondoa kwa namna hii, mahali hapa ambapo naweza kuoza kama mzoga kwa wiki kadhaa bila mtu yeyote kujua.

Nikajikuta naanza kutathimini na kujitathimini mimi mwenyewe na chaguzi zote nilizozifanya katika maisha yangu. Nikajikuta natamani kama ningepata nafasi nyingine nirekebishe baadhi ya mambo au labda nipate fursa ya kuyafanya tofauti.
Nikakumbuka namna ambavyo wiki yangu ya mwisho nilivyokuwa nyumbani Tanzania kabla ya kusafiri kuja Zurich namna ambavyo tuligombana na mkewangu Cheupe. Nikakumbuka hasira ambayo nilikuwa nayo kutokana na kumuona kama vile anaondoka kutoka mikononi mwangu kwa kung’ang’ana kwenda Nairobi kufanya kazi.

Japokuwa uamuzi wangu wa kuja Zurich ulikuwa ni kutokana na kiu ambayo ilikuwa ndani yangu kutamani kujua na kung’amua fumbo ambalo baba yangu alikuwa amenipa kutokana na ile bahasha ambayo aliniachia, lakini pia safari yangu hii ya Zurich pia ilichangiwa na kutamani kupata walau wiki chache kuwa mbali na Cheupe. Uhusiano wetu, ndoa yetu haiko sawa kabisa. Nilijua bila shaka kabisa kwamba ndoa yangu na Cheupe inapitia katika kipindi kigumu na labda Cheupe inawezekana kuna mambo amebadilika tofauti kabisa na Cheupe ambaye nilimpenda kutoka utotoni, tofauti kabisa na Cheupe tuliyepambana kuidondosha jumuiya ya The Bold, lakini kitu kimoja ambacho kamwe hakikubadilika ni kiwango changu cha kumpenda.

Hakuna jambo linaloumiza moyo kama kushuhudia ukiwa unampoteza mtu unayempenda kutoka mikononi mwako. Akilini mwangu wiki kadhaa zilizopita nilijiapiza kuwa ni vyema niende Zurich kukonga kiu ya kung’amua fumbo nililoachiwa na marehemu baba yangu kuliko kuendelea kukaa nyumbani nikishuhidia mapenzi yangu na Cheupe yakizama siku baada ya siku.
Lakini muda huu ambao nilikuwa sina hakika kama nitaweza kufikisha hata masaa matatu mbele, hakuna kitu ambacho nilikuwa nakitamani kama kumuona Cheupe akiwa pembeni yangu. Hakuna ambacho nilikuwa natamani muda huu kama nitafumba macho kwa mara yangu ya mwisho basi niyafumbe nikiwa mikononi mwa Cheupe, nipate fursa tena kumueleza jambo moja tu. Moja tu… kwamba nampenda kuliko kitu chochote kile.

Nilitabasamu tena na kuinua mkono kutoka tumboni na kuungalia jinsi ulivyofunikwa na damu. Nikatabasamu. Kila ambavyo nilitabasamu ndivyo ambavyo mchozi nao ulitiririka kutoka kwenye kona za macho na kudondokea masikioni. Ilikuwa kana kwamba najifariji na hiki kitendo cha kuutoa mkono tumboni na kuungalia mara kwa mara labda kungeweza kusaidia kufanya damu tumboni isiendelee kutoka. Lakini kila ambapo niliinua mkono kutoka tumboni na kuungalia ndivyo woga ndani yangu ulizidi maradufu. Woga wa kufumba macho kwa mara ya mwisho na nisipate nafasi ya kuyafumbua tena.

Nikaanza kufikiria siku mbili zilizopita. Siku ambayo nilipelekwa mtaa wa Wipkingen hapa hapa Zurich. Siku ambayo nilizibwa sura kwa tambara jeusi la kitambaa ili nisione. Siku ambayo nilipitishwa kwenye korido yenye kunuka harufu ya damu mbichi na kisha kuingizwa kwenye chumba cha kufanana na hoteli ya hadhi, chumba ambacho nilikutana na mzee ambaye nilikuwa namfahamu kama Hudini kutokana na sauti yake. Mzee ambaye tulianza maongezi kwa kunikabidhi picha mbili zenye utata. Moja ikionyeaha watu wanne mmoja nikimtambua kama Rais wa Tanzania Albert Kafumu na walinzi wake wawili wakiwa na mwanaume mmoja wa kizungu wa umri wa makamo kwenye eneo la kufanana na bandari. Picha ya pili ambayo ilinishangaza sana ilimuonyesha mtu huyo miaka mingi iliyopita akiwa kwenye picha ya pamoja na Cheupe akiwa mtoto na baba yake.

Katika maongezi yetu Hudini alionekana hakuwa anajua zaidi yangu kuhusu fumbo ambalo baba yangu alikuwa anataka niling’amue au labda alikuwa anafanya kusudi kutoniambia… kitu pekee ambacho alinieleza ni kwamba ananikabidhi maagizo kama ambavyo alielekezwa na hana la zaidi ambalo atanieleza. Alinikabidhi tu bahasha yenye nyaraka nyingi ndani yake na kisha kunieleza kuwa atanitafuta baada ya wiki mbili kunikabidhi bahasha nyingine. Nilipomuuliza natakiwa kufanya nini ndani ya wiki mbili hizobili, alinijibu huku anatabasamu kifedhuli… “I don’t know… I am just following my orders!” Na nilipomuuliza hizo “orders” zinatoka kwa nani alinijibu, “its none of your business.!”
Kwa mtindo ule ule wa walionichukua kutoka mtaa wa Hardstrasse, ndivyo ambavyo walinirudisha… lakini hawakunirudisha pale mtaa wa Hardstrasse bali walinirudisha hotelini nilipofikia karibu na uwanja wa ndege wa Zurich.

Kutokana na purukushani hizi za kunichukua na kunipeleka kule mtaa wa Wipkingen kutokea usiku wa manane, waliponirudisha hotelini tayari kulikuwa kunapambazuka. Ilikuwa ni asubuhi alafajiri. Kabla ya kuifungua ile bahasha niliyopewa na Hudini kwamba ilinipasa kulala ili kuweka akili yangu sawa. Nilikuwa najihisi kama nina karibia siku tatu sijapata usingizi. Na hakika ilikuwa ni zaidi ya siku tatu. Kuanzia safari yangu ya zaidi ya masaa kumi na sita kutoka Tanzania mpaka hapa Uswisi. Jumlisha usiku nilioenda kwenye mgahawa wa kichina na kufanyiwa mambo niliyopoteza fahamu na baadae kuamka kwenye jengo ambalo silifahamu mtaani Hardstrasse. Na baadae kupelekwa Wipkingen kuonana na Hudini. Kichwa kilikuwa kizito na kilikuwa kinauma haswa nilihitaji kupumzika kwa masaa kadhaa.

Nakumbuka nililala kwa siku nzima. Kuna muda nilihisi nilikuwa nalala tu sitamani kuamka kwa kuwa sikuwa nataka kukabiliana na uhalisia uliokuwa unanisubiri pindi nikiamka. Lakini hakuna marefu yasiyo na ncha na siwezi kulala milele. Hatimaye jioni yake niliamka na kufungua ile bahasha ambayo nilipewa na Hudini. Nilipoifungua na kusoma zile nyaraka zilizomo ndani nilielewa kwanini roho yangu ilikuwa nzito na kulala siku nzima bila kutamani kuamka. Nilielewa roho rangu ilikuwa inaogopa kukutana na uhalisia wa aina gani. Uamuzi ambao nilichukua baada ya kusoma zile nyaraka ndizo ambazo zimenifanya kuingia kwenye dhahama kubwa kwenye nchi hii ya ugenini niliyopo.

Lakini hayo yote yalikuwa ni siku mbili zilizopita. Leo hii nilikuwa nakabiliana na uhalisia mkubwa zaidi. Uhalisia wa kama nitathubutu kufumba macho basi kuna uwezekano mkubwa sitayafumbua tena. Uhalisia wa kiza kinene mbele yangu. Uhalisia wa kifo.

Nikatabasamu tena. Machozi yalitiririka tena kwenye kona za macho. Nikainua tena mkono kutoka tumboni na kuangalia namna ulivyoloa damu. Nikaurudisha tena tumboni kujishika damu isitoke kwa kasi zaidi. Macho yalikuwa yanazidi kulegea na nuru kupotea. Maumivu yote yalikuwa yamepotea. Sio kwamba hayakuwepo lakini mwili wangu ulikuwa unakufa ganzi na nilikuwa siyasikii kabisa. Uhalisia ni kwamba nilikuwa hata sihisi mwili wangu mwenyewe. Kitu pekee ambacho nilikihisi, kitu pekee ambacho kilikuwa ni halisi kwa sasa ni woga. Woga wa uhalisia kwamba nikifumba macho tu sasa hivi hakika sitafumbua tena.

Nikaanza kufikiria hatua kwa hatua mpaka mahali hapa nilipo muda huu. Sikuwa hotelini, na nina zaidi ya masaa ishirini na nne sijui kitanda cha hoteli yangu. Kwa uzuri zaidi niseme sijakiona kitanda cha hoteli yangu tangu juzi niliporejeshwa hotelini alfajiri na vijana wa Hudini na kisha kulala siku nzima mpaka jioni. Nipo koridoni mwa jengo ambalo visanga na vitimbi vyote vilikoanzia, jengo la HARDSTARASSE 201, 1985. Jengo ambalo siku kadhaa zilizopita nilijikita nimeamka ndani yake. Jengo ambalo nilisikiliza kipande cha video cha ujumbe ambao uliachwa na marehemu baba yangu. Jengo ambalo nilikuta nyaraka kwenye vault ndogo zikionyesha kwamba ninalimiliki. Hapa ndipo nilipo muda huu. Kwenye korido nje ya mlango wa kuingia kwenye kile chumba ambacho siku kadhaa niliamka ndani yake.

Nilikuwa nimelala hapa koridoni nikihesabu sekunde zilizobakia za uhai wangu. Nilikuwa nimelala nikiwa na jeraha la risasi tumboni linalovuja damu.

Japokuwa mwili ulikuwa umeishiwa nguvu na hata akili yangu kushindwa kufikiria sawa sawa nikiona maluweluwe tu, lakini nilijitahidi kuwaza. Kuwaza ni nini hasa kilikuwa nyuma ya pazia. Kuwaza nimewezaje kutegeka kirahisi hivi?

Niliwaza kweli kweli, ni nani hasa alikuwa nyuma ya pazia ya hiki kilichofanyika? Hudini? Lakini akili yangu ilikataa… Hudini alikuwa na uwezo wa kuniua Kyle Wipkingen kama angekuwa na nia hiyo. Lakini kila nilipotaka kumsafisha kichwani mwangu Hudini, akili ilikataa…. Hudini ndiye pekee anayejua uwepo wangu hapa Zurich. Au labda kuna mwingine? Ndio… nilijijibu mwenyewe… yule mzee wa kichina na vijana wake? Inawezekana wao ndio walikuwa nyuma ya pazia? Hapana… akili yangu ilikataa… nao walikuwa na uwezo wa kuniua siku ile ambayo walinipotezesha fahamu kwa kunichoma sindano ya kemikali.! Au kuna mwingine anayefahamu uwepo wangu hapa Zurich bila mimi kujua?

Ghafla nikasikia mlango wa komeo wa kule nje wa kutoka kwenye uchochoro, nikasikia unafunguliwa kwa staili ile ile niliyoisikia mara ya kwanza kabla ya kupigwa risasi. Macho yangu yaliyokuwa yanasinzia kwa kuchoka kutokana na mwili kuishiwa nguvu, niliyatoa kama vile nimekabwa. Woga ambao niliusikia ulikwa halisi mpaka niliweza kuuhisi kwenye ngozi yangu ya mwili. Kifo kilikuwa halisi mbele yangu kuliko hata nilivyohisi mwili wangu.

“Huu hauwezi kuwa mwisho wangu.!”

Nikajifariji japo nilikuwa siwezi hata kuinuka kupiga hatua moja.



Itaendelea…


THE BOLD
 
VIPEPEO WEUSI


SEASON 1 – FROM ZURICH WITH RULES


Ilipoishia Episode 11

Ghafla nikasikia mlango wa komeo wa kule nje wa kutoka kwenye uchochoro, nikasikia unafunguliwa kwa staili ile ile niliyoisikia mara ya kwanza kabla ya kupigwa risasi. Macho yangu yaliyokuwa yanasinzia kwa kuchoka kutokana na mwili kuishiwa nguvu, niliyatoa kama vile nimekabwa. Woga ambao niliusikia ulikwa halisi mpaka niliweza kuuhisi kwenye ngozi yangu ya mwili. Kifo kilikuwa halisi mbele yangu kuliko hata nilivyohisi mwili wangu.

“Huu hauwezi kuwa mwisho wangu.!”

Nikajifariji japo nilikuwa siwezi hata kuinuka kupiga hatua moja.



EPISODE 12


Siku hii ndipo ambapo niligundua kuwa hakuna kitu imara juu ya uso wa dunia kushinda roho ya binadamu. Haijalishi kuna tumaini dogo kiasi gani, lakini roho ya binadamu ina uwezo wa kuhuisha tumaini hilo na kulifanya tumaini kubwa kuliko uhalisia.

Niliposikia ile sauti ya komeo kufunguliwa kule nje kwenye mlango ambao unatokea uchochoroni, nilijiapiza kuwa safari hii sitasubiri niuwawe hivi hivi. Nitapambana. Kwa kuwa nilikiwa katikati ya korido kama ningelisema nijikongoje ili nijifungie kule ndani kwenye chumba kulikuwa na umbali mkubwa zaidi kutoka hapa ambapo nipo mpaka kufikia ulipo mlango wa kuingia kwenye kile chumba. Lakini nilikuwa karibu zaidi na mlango wa ule ambao unatoka nje. Kwa hiyo kichwani mwangu nikajiapiza kwamba safari hii nitapambana.

Sijui nilipataje nguvu, ninachokumbuka ni kwamba katika hali hii ya kupigania uhai wangu, katika hali hii ya eidha kufa au kupona nilijikuta napata nguvu ya kujiburuza kuelekea kwenye ule mlango unaotoka nje. Kutokana na kuvuja damu nyingi macho yalikuwa yelegea na nilokuwa naona nusu na nusu sioni, lakini nilijiburuza mpaka mlango ulipo. Kutokana na jengo hili kutokuwa linatumika kwa muda mrefu lilikuwa na takataka nyingi njiani hapa koridoni. Nikiwa najiburuza kuelekea mlangoni nilifanikiwa kuokota kipande cha kamba. Sikumbuki sawia ilikuwa ni kamba ya namna gani lakini ilikuwa kama vile imetengenezwa kwa plastiki na ilikuwa ngumu kiasi chake. Nikaishikilia hii kamba mkononi na kujiburuza mpaka nikafika nyuma ya mlango wa kutokea nje na kujibanza. Mkakati wangu ulikuwa ni kwamba mtu huyu yeyote ambaye alikuwa anajaribu kuja kunidhuru nitamuwahi na kumnyonga kwa hii kamba kabla ajatimiza azma yake dhidi yangu.


Nikajibanza kimya kabisa nyuma ya mlango. Nilikuwa nusu na ufahamu na nusu nilikuwa sijitambui. Nilikuwa nimepoteza damu nyingi sana.

Huyu mtu ambaye alikuwa anafungua mlango huko nje ilikuwa dhahiri kwamba hakuwa na funguo kutokana na kuhangaika sana kufungua mlango. Nilikuwa na hakika kabisa alikuwa anajitahidi kufungua kufuli kwa magendo kwa kutumia nyaya au vijiti vya chuma bila funguo. Nikaanza kukiuliza kichwani… huyu ambaye alikuwa anafungua mlango niliamini kabisa ndiye yule ambaye alinipiga risasi… sasa inakiwaje aliufunga mlango akijua kabisa hana fungua na kwamba atahitaji kurudi tena? Au labda kwa namna fulani amegundua kwamba risasi ambayo alinipiga haikuniua kwa hiyo amerejea kuja kumaliza kazi?

Nikajibanza kusubiri. Jasho lilikuwa linanitoka kweli kweli. Macho yalikuwa yanataka kifumba lakini nikajikaza yasifumbe. Kimoyo moyo nikasema tena ile kauli ya kujipa moyo.

“Huu hauwezi kuwa mwisho wangu”


Mlango ukafunguliwa taratibu na mtu ambaye hakuonekana kuwa na haraka. Taratibu nikaona anakanyaga hatua ya kwanza kuingia ndani.

Kwa nguvu zangu zote ambazo zilibakia mwilini, nilifaytua miguu yangu kumkata mtama baada ya kuona miguu yake yote amekanyaga ndani.

“Woo wooo!”

Nilimsikia analalamika kwa taharuki kana kwamba alikuwa hatarajii kushambuliwa.
Mwili ukiwa umeniishia nguvu hivyo hivyo nikajipa juu yake na kupeleka mkono shingoni mwake ili nimkabe.
[7/16, 23:49] The Bold: Sikuwa na nguvu za kutosha ili kumkaba nikajikuta naishia kumgusagusa tu shingo.

“Woo woo! Chill out mate… chill out! I am Jimmy chill mate!”

Akaongea kwa kusisitiza kana kwamba kunitajia jina lake kulikuwa na maana fulani hivi ya kunituliza munkari yangu.

“Who are you? What are doing here?” Nikauliza kwa sauti kama ya kilevi hivi kutokana na mwili kuishiwa nguvu kabisa.

“Chill mate! I am Jimmy… this is Jimmy!”

Nikamsikia anajitetea tena kwa kunitajia jina lake ambalo kwangu halikuwa na maana yoyote ile.
Kitu pekee ambacho nilikitambua ni kwamba mtu huyu hakuwa na hatari yoyote kwangu japo nilikiwa simtambui na wala sikujua kwa nini alikuwa hapa.

Nilimkazia macho kumwangalia usoni kwa usahihi zaidi. Alikuwa ni mtu fulani ambaye hakuwa nadhifu. Mwanaume wa chotara wa kizungu mwenye uasia kwa mbali. Uso wake ulikuwa umechakaa japokuwa hakuwa mzee.

Kichwani nilijitahidi kuwaza tena na tena ni nini huyu?

Kabla hajaingia humu ndani nilikuwa na hakika kabisa kuwa mtu huyu mtu alikuwa amekuja hapa ili kunidhuru baada ya kugundua risasi ambayo alikuwa amenipiga mara ya kwanza haikuniua papo papo hapo, lakini sasa kwa muonekano wa huyu mtu tu kwa kumuangalia haraka haraka nilihisi kwa asilimia kubwa mtu huyu alikuwa ni chokoraa wa mtaani, mtu asiye na makazi.

Nilijikuta najiuliza tena na tena alikuwa amekuja kufanya nini hapa? Masaa kadhaa yaliyopita yametokea mfululizo wa matukio yaliyonifanya nirudi tena kwenye jengo hili na kusababisha nipigwe risasi. Sasa hivi kwa mazingira ya kutatanisha Chokoraa anaingia humu ndani? Hii ni ‘coincidence’? Au kuna mpango fulani wa kunichezea akili?

“Hey mate! Are you OK?”

Yule mtu aliongea huku ananiondoa juu yake nilipokuwa nimemlalia kwa lengo la kumshambulia. Mwili ulikuwa umeisha nguvu kabisa. Sikuweza hata kuleta upinzani alipokuwa ananitoa juu yake.

“You are bleeding badly mate! You need a doctor!”

Akaendelea kuongea huku akiniegemeza ukutani. Lafudhi yake na maneno waliyokuwa anaongea yakinifanya nihisi kwamba mtu huyu hakuwa mwenyeji wa miaka mingi hapa Zurich au sehemu yoyote ya hapa Uswisi. Lafudhi yake ilikuwa ni ya Uibgereza na hata maneno anayotumia, mfano neno ‘mate’ kwenye kila sentensi ni namna ambayo waingereza wengi ndivyo wanavyoongea.

Maswali yakazidi zaidi kichwani mwangu!

Inamaana huyu ni raia wa Uingereza aliyegeuka chokoraa nchini uswisi? Inawezekanaje hii? Na kama hiyo haitoshi kwa mazingira ya ajabu tu ametokea kuingia kwenye jengo ambalo mimi nimo na nimepigwa risasi dakika kadhaa tu zilizopita.

“Hey mate! We need to get you to a hospital… you need a doctor mate.!”

Aliongea tena yule mtu huku akinitingisha tingisha kichwani nisilale na kupoteza fahamu. Nilijiegemeza tu pale ukutani aliponilaza nikiwa nusu na fahamu na nusu nikiwa ufahamu haupo kabisa.

“What happened to you mate??”

Aliongea akiwa amechanganyikiwa akijishika kichwa huku anashangaa jinsi damu ilivyotapaa pale koridoni.

“What happened? We need to get you to a hospital mate!”

Aliongea tena kwa kuchanganyikiwa huku amejishika kichwa anatazama damu zilizotapakaa kila sehemu kwenye korido.

“No…no…don’t take me to a hospital… please! Don’t take me…to…hospital!”

Niliongea kwa taabu sana na kwa kujikakakua.

“Are you crazy why not!! You need a doctor mate!”

Yule jamaa alisisitiza tena.

Kwa matukio ambayo yamenitokea kwa masaa 24 yaliyopita sikudhani kama hospitali itakuwa mahala sahihi mimi kupelekwa. Kwanza kabisa sikutaka kuulizwa na maafisa wa serikali ilikuwaje mpaka nikapigwa risasi. Swali hilo lingeweza kujaribu kila kitu na labda hata safari yangu hapa Zurich ikawa haina maana kabisa.

“Please… don’t… take… to… a…. hospital.!”

Nikaongea tena kwa taabu sana.

“You are insane mate! You need a doctor!”

Aliongea tena akiwa amechachawa huku amejishika kichwa akitembea huku na huko pale koridoni.

Nikajikuta naanza kujiuliza tena huyu mtu ni nini hasa. Ni chokoraa kweli kama anavyoonekana au labda ni mtego tu? Mwingereza Chokoraa ndani ya Zurich, Uswisi? Na kwa sababu zisizoeleweka amekuja kutokea mahala ambapo nimepigwa risasi ambapo ningekufa na kuoza kwa miezi bila yeyote kujua?

Nilimwangalia tena na tena kwa umakini zaidi. Macho yalikuwa yamelegea kabisa yanataka kufumba lakini nilijitahidi kuyaakaza niweze kuangalia. Alikuwa amevalia nguo za hovyo hovyo sana ambazo nilianza kuzisikia zikitoa harufu fulani kali kuonyesha kwamba inawezekana zilikuwa hazijafuliwa kwa muda mrefu kidogo.

“Who are….” Nilishindwa kumalizia sentesi yote, mwili wote uliisha nguvu, macho yakafumba. Kiza kilitanda kila mahala. Kila nilivyojaribu kuyafungua macho haikuwezekana. Kiza kikatanda zaidi. Sikujua kama nilikuwa nalala usingizi au ndio uhai ulikuwa unaondoka. Sikuelewa kilichoendelea. Macho yakafumba kabisa. Ufahamu ukapotea.


Itaendelea…


THE BOLD
 
VIPEPEO WEUSI


SEASON 2 – FROM ZÜRICH WITH RULES



EPISODE 13


Nilikuwa nasikia baridi kali licha ya kuyahisi mashuka mazito ambayo nilikuwa nimefunikwa. Nilifumbua macho kuhisi mwanga hafifu uliokuwa unapenyeza hapa nilipo kuonyesha kwamba ilikuwa ni asubuhi au mchana kumepambazuka.

Kichwa kilikuwa kinaniuma na nilikuwa nakisikia kikiwa chepesi sana. Nikajaribu kujiinua lakini maumivu makali tumboni yakanifanya nijilaze tena pale chini. Nilipoyasikia haya maumivu tumboni ndipo ambapo kumbukumbu ya jana ilianza kunirejea kichwani. Kwanza yule ambaye alinipiga risasi na baadae yule chokoraa ambaye niliongea naye kabla sijapoteza fahamu.

Nikaangalia kwa usahihi zaidi hapa nilipo, nilikuwa pale pale koridoni ambapo nilipigwa risasi jana usiku. Kichwani bado nilikuwa na kumbukumbu ya damu ambazo zilikuwa zimetapakaa pale koridoni jana usiku, lakini sasa hivi kila ambavyo nilipepesa macho kutazama sikuona damu hata tone moja. Kwa haraka haraka palionekana kama vile mtu alipapiga deki kwa uzuri kabisa kuondoa damu yote.

Nikanyoosha mkono tumboni kugusa eneo lile ambalo nilikuwa nimepigwa risasi jana usiku. Nilihisi kama bandeji nimefungwa sehemu hiyo. Ilinibidi nifunue shuka ili nipate kuhakikisha kama kweli ilikuwa ni bandeji ama kitu gani. Nilifunua shuka kuu kuu ambalo nilikuwa nimefunikwa na kukuta kwa hakika kabisa ni kweli ilikuwa ni bandeji. Nilionekana nilikuwa nimesafishwa kidonda vizuri kupatiwa matibabu na hatimaye kufungwa hiyo bandeji.

Nilitamani kukaa kitako ili nifikiri sawa sawa kuhusu ni nani hasa amenifunga bandeji hii lakini maumivu tumboni yalinilazimisha nijilaze tena chini sakafuni. Kuna shuka lingine kuu kuu lilikuwa limevingirishwa vingirishwa na kisha kuwekewa kichwani nilalie kama mto.

Niliwaza na kuwazua. Ni nani hasa alikuwa amenipa matibabu ya jeraha langu la risasi? Yule chokoraa? Haikuingia akilini kabisa.

Nikiwa naendelea kuwaza hivi ghafla nilisikia mlango ule wa kutokea nje uchochoroni unafunguliwa. Safari hii hakufunguliwa kwa tabu. Ulifunguliwa kama vile mtu ambaye alikuwa anafungua alikuwa na funguo au kufuli haikufungwa. Baada ya mlango kufunguliwa hatua ambazo nilisikia zinapigwa kuingia ndani koridoni zilisikika kama vile zilikuwa hatua za watu zaidi ya mmoja.

Sikusogea wala kutingishika. Nilikaa pale pale nilipo bila hata kujitingisha nikisubiria kuona hao ambao walikuwa wanaingia.
Ndani ya sekunde kadhaa walikuwa tayari wametokezea hapa koridoni. Hapa ambapo nilikuwa nimejikuta nimeamka nikiwa nimelazwa kwenye mashuka makuu kuu kulikuwa ni mwishoni kabisa mwa korido. Kwa hiyo walipotokezea tu koridoni walikiwa mwisho wa upande mwingine mwa korido. Katikati yetu kukikuwa na umbali usiopungua mita kama tano hivi. Walikuwa ni wanaume wawili, mmoja nilimtambua alikuwa ni yule mtu wa jana usiku ambaye nilimuhisi kuwa ni chokoraa japo nilimuona gizani jana usiku lakini niliweza kumtambua muda huu wa mchana kweupe.

Alikuwa ni mwanaume wa kizungu wa umri wa makamo, kama miaka arobaini hivi au arobaini na mbili. Alikuwa na nywele nyeusi za singa za asili ya kiasia ya mashariki au kusini ambazo zilikuwa ndefu kiasi zikiwa na muonekano wa wazi kabisa kwamba hazikuwa zinatunzwa vizuri. Mwenzake ambaye alikuwa amekuja naye alionekana mkubwa zaidi kwa umri, labda katikati ya miaka hamsini… kwenye hamsini na nne hadi hamsini na sita hivi. Nywele zake za singa za kizungu zilikuwa zimekatwa kwa urefu wa wastani pamoja na ndevu za wastani kidevuni.

Yule jamaa ninaye muhisi kuwa ni chokoraa ambaye tulionana tangu jana usiku alikuwa amevalia suruali kuu kuu ya jinzi na fulana nyeusi ya mikono mirefu. Mwenzake huyu aliyekuja naye alikuwa amevaa kwa unadhifu kabisa, amevalia jinzi ya bluu na fulana nyeupe ambayo juu yake alivalia jaketi jeusi la ngozi.

Walialsimama pale mbele yangu tukiangaliana kwa takribani dakika mbili nzima bila yeyote kati yetu kusema neno.

“It’s not him!” Yule jamaa nadhifu alimuambia mwenzake yule ambaye nilikuwa nahisi ni chokoraa.

“You sure mate?” Yule jamaa akajibu kwa kunong’ona.

“I am hundred percent sure! Its not him…” akamwambia tena.

Wakageuka kunitazama tena. Walinitazama kwa kuanzia juu kichwani na mwili wote. Walinitazama kwa kunikazia macho kana kwamba walikuwa wananifananisha na mtu fulani hivi au kitu fulani.

Kuna muda tulijikuta macho yangu na huyu jamaa nadhifu yakagongana. Kuna kitu fulani rohoni mwangu kilikuwa kinanitatiza kuhusu huyu jamaa. Huyu ambaye amevaa nadhifu. Kuna jambo rohoni mwangu lilikuwa linang’amuliwa lakini sikuweza kulipambanua akilini mwangu na kulielewa.

“So what do I do with him?” Yule chokoraa akamuuliza yule mwenzake nadhifu.

“Leave him here! Go on with your life.” Yule jamaa nadhifu akajibu bila kumuangalia mwenzake huku akiingiza mkono mfukoni mwake kutoa kitu.

“What? You are insane mate… he gonn’ die if I leave him here!” Yule chokoraa aliongea huku ametumbua macho.

“Its non of your business… leave him here!” Yule jamaa nadhifu aliongea huku ametoa wallet kutoka kwenye mfuko wa nyuma wa jinzi na kuhesabu noti kadhaa na kisha kumpa yule chokoraa.

Nilikuwa nawaangalia tu namna wanavyobisha na kuongea kana kwamba siko hapa. Sikuwa nataka kusema neno lolote lile wala kuuliza chochote. Lakini kwa hiki nilichokisikia tu wanaongea nilijua kwa hakika kabisa kwamba huyu chokoraa jana hakunikuta hapa kwa bahati mbaya. Kulikuwa na kitu cha ziada ambacho kilikuwa kinaendelea. Japo haya maongezi yao yalikuwa yananitisha lakini sikutaka kusema chochote ili nisiwakatishe hiki ambacho walikuwa wananizungumza ili nisikie vya kutosha na nianze kuunga nukta kichwani mwangu.

Kile kitu kinachofurukuta rohoni mwangu kiliendelea. Kila nilipomwangalia yule jamaa nadhifu kuna jambo lilikuwa linajengeka kichwani lakini sikuweza kung’amua ni kitu gani.

Yule jamaa nadhifu baada ya kumkabidhi zile noti mwenzake chokoraa aligeuka na kuanza kuondoka. Yule chokoraa aligeuka na kuanza kuniangalia kwa huruma. Alikuwa ananinagalia katika namna ambayo macho yake tu na uso wake niliweza kusoma kile ambacho alikuwa anataka kukisema lakini alikuwa hakisemi. “Natamani nikusaidie lakini siwezi”.

Akiwa ananiangalia hivi huku yule mwenzake akiwa anakaribia kutokomea kutoka hapa koridoni ghafla tu kichwani nikang’amua kile ambacho kilikuwa kinanikorofisha rohoni kuhusu huyu jamaa nadhifu. Yalikuwa ni yale mavazi yake, na mahususi lile jaketi lake jeusi la ngozi. Lilifanana kabisa na wale vijana wa Hudini, vijana ambao walionekana kama walikuwa walinzi wake ambao siku tatu zilizopota walikuja kunichukua barabarani karibu na jengo hili na kunipeleka maeneo ya Wipkingen kwenye jumba ambalo sikulijua mpaka leo hii, jumba lenye harufu ya damu mbichi. Vijana wale wa Hudini wote walikuwa wamenyoa upara na walikuwa wamevalia majaketi meusi ya ngozi ya kufanana kabisa na jaketi ambalo jamaa huyu alikuwa amevaa. Tofauti yake pekee huyu jamaa alikuwa na umri mkubwa zaidi tofauti na wale vijana wa pia yeye kichwani hakuwa na upara.

Nilikuwa nimeyasikia maongezi yao ambayo walikuwa wanabishana, huyu jamaa nadhifu na yule chokoraa. Yule jamaa nadhifu alikuwa ameamuru kuwa kwa kuwa huyo anayemuhitaji si mimi basi waniache hapa na kuondoka zao. Na hawakuwa wa wanafanya utani. Walikuwa wameanza kuondoka kweli. Kama wataniacha hapa nikiwa na hali hii nisingeweza kutoka hapa na hakika peke yangu nisingeweza kukabiliana na kifo ambacho ni jana usiku tu kilinikosakosa.

Japokuwa watu hawa sikuwa nawaelewa hasa ni akina nani na wala sikuwa nawaamini lakini kwa hakika kabisa kama nilitaka kuishi watu hawa walikuwa pengine ndio fursa pekee niliyokuwa nayo.

Nikakata shauri kichwani kwamba nisilaze damu, nifanye chochote hapa ili kuokoa maisha yangu hata kama ni kitu cha kijinga au kitu cha kuhatarisha maisha yangu.

“I know Hudini.!” Nikaongea kwa sauti kubwa kwa kujitutumua hasa japo kwa sauti ya uchovu kutokana na maumivu tumboni.

Wote wawili wakiwa wanatembea kutoka hapa koridoni, yule jamaa nadhifu na yule chokoraa walisimama ghafla na kugeuka.

Yule nadhifu alipogeuka alikuwa na taharuki kubwa usoni tofauti na yule chokoraa ambaye uso wake haukuonyesha chochote kile. Taharuki yake ilikuwa ni kana kwamba amesikia siri kubwa ambayo haipaswi kusikika kokote.

“What did you say?” Yule jamaa nadhifu aliniuliza bado akiwa na mshangao.

Sikujibu chochote. Moyoni nilijipa ‘tano’. Jiwe nililorusha lilikuwa limetua sawia kwa mlengwa. Nilimuona namna ambayo alijawa na mshangao usoni. Namna ambavyo ghafla tu alibadilika kutoka kuwa kwenye mtu mwenye kujiamini kupitiliza mpaka kuwa katika hali ya kuhitaji kujua kile ambacho nilikuwa nakijua.

Alipogeuka aliganda kwa karibia dakika nzima akichakata kichwani kile ambacho nilikiwa nimekiongea. Kwa namna fulani niliweza kuhisi namna ambavyo sentesi yangu ilikuwa imemchanganya. Inaonekana ni kitu ambacho hakukitegemea kabisa. Kwa namna fulani pia niliweza kuhisi uoga usoni mwake, hakuwa ananiogopa mimi bali alionyesha kuwa alikuwa anaogopa kile ambacho nilikiwa nakifahamu. Na nilidhamiria nimtese haswa. Sio kumtesa kwa mwili wake, bali nimtese kisaikolojia.

Hakujua kwamba kile ambacho nilikitamka nilitamka kwa bahati tu baada ya kuhisi ile jaketi yake inafanana kabisa na zile jaketi za vijana wa Hudini. Lakini nilitaka nimuache katika hali hii hii, aamini kwamba nafahamu zaidi. Nimuache kwenye hali hii hii na niwatumie kujinasua kwenye haya masaibu ambayo niko nayo.

“What did you just said?” Yule jamaa nadhifu aliuliza tena kwa taharuki huku akianza kupiga hatua kurejea pale ambapo nimejilaza.

“Nothing.!” Nikamjibu kwa kifupi na kugeukia pembeni.

“No no no! What do you know about Hudini?” Akaniuliza tena safari hii akiwa ametembea na kusogea karibu yangu kabisa.

“Is it him?” Yule Chokoraa naye alikuja kwa hatua za haraka huku anatabasamu.

Mwenzake hakumjibu chochote. Tulikuwa tumegongesha macho tukiangaliana.

“I asked you, what do you know about Hudini?” Akarudia tena swali lake.

“I am not going to tell you anything before you tell me who the hell are you.!!” Nilijitutumua na kujaribu kufoka kwa hasira.

“No no no! First you tell us, who you are mate!” Yule chokoraa akadakia kwa kujitutumua kama vile mtoto mdogo wa shule afanyavyo.

“I am not going to tell you shit.! I never asked for you to come here… you all came here by yourselves… so you tell me who the hell are you guys!” Nikafoka safari hii kwa hasira za kweli.

“Why were you here?” Yule jamaa nadhifu akauliza. Safari hii sauti yake haikuwa na woga bali ilikuwa imejaa mamlaka na kujiamini. Ilikuwa kana kwamba kuna ‘taa’ ya ung’amuzi imewaka kichwani mwake. Aliniuliza swali hili la “kwa nini niko hapa” katika namna ambayo alionyesha kuwa alihisi jambo hilo akilifahamu linaweza kumfanya afahamu hicho ambacho alikuwa anahitaji kufahamu.

Binafsi yangu, nikaanza kuhisi inawezekana kabisa watu hawa walikuwa na mambo yao mengine tu na walinikuta hapa kwa bahati mbaya. Kwa sababu kilichokuwa kinanishangaza ni kitendo cha wao kutonijua mimi ni nani na nilikuwa hapa kwa ajili gani.

Lakini kwa upande mwingine wa akili niliwaza… kuna mtu walikuwa wanamtafuta, alikuwa nani? Na kwanini wamtafute kwenye jengo langu? Yes, jengo langu! Kwa mujibu wa ujumbe wa marehemu baba yangu nilioungalia siku tatu zilizopita na zile nyaraka nilizozipata ndani kwenye ile vault ndogo, zilionyesha mimi ndiye mmiliki wa jengo hili kutoka kwa baba yangu.

Kila nilivyojitahidi kufikirj akili yangu ilikuwa inaniambia kuwa kama watu hawa kama kuna mtu walikuwa wanamtafuta basi nitasema mtu huyo ni mimi, lakini wanaonekana dhahiri walikuwa hawanijui na wala walikuwa hawajui ni kwa nini niko hapa.

Nikawaza tena labda wana mambo yao, labda wana mtu wao wanamtafuta, labda ni bahati mbaya tu tumekutana. Lakini kila nilipowaza hivi upande mwingine wa akili ulikuwa unakataa. Ni nani amenitibia jeraha langu la risasi? Na kwa nini huyu mtu ameshituka nilipotaja Jina la Hudini?
Japokuwa alivaa mavazi ya kurandana na vijana wa ulinzi wa Hudini lakini nilihisi bila shaka kabisa huyu hakuwa moja ya timu ya Hudini… kwanza hakuwa na upara kama wenzake na pili vijana wa Hudini wananifahamu kwa kuwa wao ndio walinipeleka kwa Hudini. Sasa kwa nini amevaa mavazi ya kurandana nao? Ni bahati mbaya tu? Haiwezekani kuwa bahati mbaya kwa sababu nilipotaja Hudini ameshituka kama ameona jini.

Hawa watu ni akina nani? Ni nani wanamtafuta? Kwa nini wako hapa?

Pia swali ambalo nimeliweka kiporo muda mwingi nalo lilikuwa linanijia kichwani Mara kwa mara, ni nani amenitibia jeraha la risasi?

“Who are you? What are you doing here?” Yule jamaa nadhifu aliuliza tena safari hii kwa hasira na kujiamini.

Nikajisemea kimoyo moyo. Liwalo na liwe. Nikatupa karata yangu ya mwisho.

“I own this place!” Niliongea kwa sauti thabiti ya kujiamini huku nimemkazia macho.

Mshtuko ambao nilimuona usoni mwake ulikuwa ni kama kwamba mtu aliyetokewa na jini au malaika. Alishtuka mpaka karibia apepesuke adondoke. Niling’amua kwamba jibu langu hili liliwasha taa ndani ya akili yake na ameng’amua jambo.

“You….!” Aliongea huku anahema bila kumalizia sentesi yake huku ametumbua macho kama mjusi aliyebanwa mlangoni huku mkono mmoja amejishika kifuani kwa taharuki na woga. Aliniangalia kwa mshangao na kwa heshima fulani hivi kwa mara ya kwanza.

Japokuwa nilifurahi kwamba hatimaye nimeweza kuwateka akili za watu hawa na walikuwa sasa wananiangalia kwa heshima, lakini kwa upande mwingine rohoni nilikiwa na hofu. Nilikuwa nahofia ni kitu gani hasa mtu huyu ameng’amua kutokana na jibu langu?

Swali langu kiporo nalo likarejea kichwani, hawa watu dakika kadhaa tu zilizopita walikuwa wanaonekana hawanijui… je, ni nani alinitibia lile jeraha la risasi? Kwa nini hakunipeleka hospitali? Je ni huyu chokoraa… ilikuwa haiingii akilini.!


Itaendelea…


THE BOLD
 
VIPEPEO WEUSI



SEASON 1 – FROM ZURICH WITH RULES


EPISODE 11


Kiza kinene. Hicho ndicho kitu pekee ambacho nilikuwa nakikumbuka. Kiza kinene. Kiza kinene na baridi kali hasa maeneo ya tumboni pamoja na woga wa aina ambao ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuusikia ndani ya nafsi yangu. Maumivu ambayo nilikuwa nayasikia sikuwa nayaogopa kama ambavyo nilikuwa naogopa kila nikitazama damu mkononi mwangu. Sikuwahi kujua hapo kabla ni namna gani mtu anajisikia au anaona pale ambapo anakaribia kifo. Sikiwahi kujua namna ambavyo macho yanaanza kupoteza nuru na kitu pekee ambacho unakiona mbele yako ni kiza. Sikuwahi kujua ni namna gani mwili wako unaweza kuwa na siha njema lakini ukashindwa kuinua hata kidole na kukisogeza.

Nikarejesha tena mkono tumboni kuzuia damu zisiendelee kutoka. Nikalaza tena kichwa changu sakafuni na kutazama juu angani.

“Huu hauwezi kuwa mwisho wangu.!!”

Nilitamka tena kauli ile ile ambayo nilikuwa nairudia tena na tena tangu nimedondoka. Nikainua tena mkono kutoka tumboni na kuutazama namna ambavyo ulikuwa umeloa damu. Macho yalikuwa yameanza kulegea tena kuashiria kuwa naweza kupoteza tena fahamu au labda ndio ikawa safari yangu ya mwisho nisiyafumbue tena.

Sikuwahi kudhania kabla ni namna gani mtu anajisikia akikaribia kifo. Kwa miaka yangu yote duniani kila nikifikiria kifo kitu pekee ambacho kilikuwa kikinijia akilini ni maumivu. Maumivu makali. Lakini ukweli ni kwamba ukikikaribia kifo hakuna maumivu yoyote ambayo unayasikia. Uhalisia ni kwamba nilikuwa sisikii hisia yoyoye ndani yangu zaidi ya woga. Ndio, woga sio maumivu. Woga wa kufumba macho kwa mara ya mwisho nisiweze kuyafumbua tena. Woga wa kulala usingizi ambao sitaweza kuamka tena. Woga wa kutohisi chochote tena, woga wa kutosikia chochote tena. Licha ya risasi ambayo ilikuwa tumboni mwangu lakini sikusikia maumivu yoyote kadiri mwili wangu ulivyoishiwa nguvu, kadiri macho yangu yalivyozidi kupoteza nuru, hakuna cuembe ya maumivu ambayo nilikuwa naisikia. Kitu pekee ambacho nilikuwa nakihisi kwenye nafsi kilikuwa ni woga.

Niliangalia mkono wangu namna ulivyojaa damu kisha nikaurejesha tena tumboni.

Nikajikuta natabasamu. Japokuwa nilikuwa natabasamu lakini kona za macho yangu machozi yalikuwa yanatiririka. Kwa kuwa nilikuwa nimejilaza chali sakafuni, niliyasikia machozi yakitiririka na kuingia masikioni.
Nilikuwa naogopa kufumba macho kwa mara ya mwisho, lakini nilichokuwa nakiogopa zaidi ilikuwa ni kuondoa kwa namna hii, mahali hapa ambapo naweza kuoza kama mzoga kwa wiki kadhaa bila mtu yeyote kujua.

Nikajikuta naanza kutathimini na kujitathimini mimi mwenyewe na chaguzi zote nilizozifanya katika maisha yangu. Nikajikuta natamani kama ningepata nafasi nyingine nirekebishe baadhi ya mambo au labda nipate fursa ya kuyafanya tofauti.
Nikakumbuka namna ambavyo wiki yangu ya mwisho nilivyokuwa nyumbani Tanzania kabla ya kusafiri kuja Zurich namna ambavyo tuligombana na mkewangu Cheupe. Nikakumbuka hasira ambayo nilikuwa nayo kutokana na kumuona kama vile anaondoka kutoka mikononi mwangu kwa kung’ang’ana kwenda Nairobi kufanya kazi.

Japokuwa uamuzi wangu wa kuja Zurich ulikuwa ni kutokana na kiu ambayo ilikuwa ndani yangu kutamani kujua na kung’amua fumbo ambalo baba yangu alikuwa amenipa kutokana na ile bahasha ambayo aliniachia, lakini pia safari yangu hii ya Zurich pia ilichangiwa na kutamani kupata walau wiki chache kuwa mbali na Cheupe. Uhusiano wetu, ndoa yetu haiko sawa kabisa. Nilijua bila shaka kabisa kwamba ndoa yangu na Cheupe inapitia katika kipindi kigumu na labda Cheupe inawezekana kuna mambo amebadilika tofauti kabisa na Cheupe ambaye nilimpenda kutoka utotoni, tofauti kabisa na Cheupe tuliyepambana kuidondosha jumuiya ya The Bold, lakini kitu kimoja ambacho kamwe hakikubadilika ni kiwango changu cha kumpenda.

Hakuna jambo linaloumiza moyo kama kushuhudia ukiwa unampoteza mtu unayempenda kutoka mikononi mwako. Akilini mwangu wiki kadhaa zilizopita nilijiapiza kuwa ni vyema niende Zurich kukonga kiu ya kung’amua fumbo nililoachiwa na marehemu baba yangu kuliko kuendelea kukaa nyumbani nikishuhidia mapenzi yangu na Cheupe yakizama siku baada ya siku.
Lakini muda huu ambao nilikuwa sina hakika kama nitaweza kufikisha hata masaa matatu mbele, hakuna kitu ambacho nilikuwa nakitamani kama kumuona Cheupe akiwa pembeni yangu. Hakuna ambacho nilikuwa natamani muda huu kama nitafumba macho kwa mara yangu ya mwisho basi niyafumbe nikiwa mikononi mwa Cheupe, nipate fursa tena kumueleza jambo moja tu. Moja tu… kwamba nampenda kuliko kitu chochote kile.

Nilitabasamu tena na kuinua mkono kutoka tumboni na kuungalia jinsi ulivyofunikwa na damu. Nikatabasamu. Kila ambavyo nilitabasamu ndivyo ambavyo mchozi nao ulitiririka kutoka kwenye kona za macho na kudondokea masikioni. Ilikuwa kana kwamba najifariji na hiki kitendo cha kuutoa mkono tumboni na kuungalia mara kwa mara labda kungeweza kusaidia kufanya damu tumboni isiendelee kutoka. Lakini kila ambapo niliinua mkono kutoka tumboni na kuungalia ndivyo woga ndani yangu ulizidi maradufu. Woga wa kufumba macho kwa mara ya mwisho na nisipate nafasi ya kuyafumbua tena.

Nikaanza kufikiria siku mbili zilizopita. Siku ambayo nilipelekwa mtaa wa Wipkingen hapa hapa Zurich. Siku ambayo nilizibwa sura kwa tambara jeusi la kitambaa ili nisione. Siku ambayo nilipitishwa kwenye korido yenye kunuka harufu ya damu mbichi na kisha kuingizwa kwenye chumba cha kufanana na hoteli ya hadhi, chumba ambacho nilikutana na mzee ambaye nilikuwa namfahamu kama Hudini kutokana na sauti yake. Mzee ambaye tulianza maongezi kwa kunikabidhi picha mbili zenye utata. Moja ikionyeaha watu wanne mmoja nikimtambua kama Rais wa Tanzania Albert Kafumu na walinzi wake wawili wakiwa na mwanaume mmoja wa kizungu wa umri wa makamo kwenye eneo la kufanana na bandari. Picha ya pili ambayo ilinishangaza sana ilimuonyesha mtu huyo miaka mingi iliyopita akiwa kwenye picha ya pamoja na Cheupe akiwa mtoto na baba yake.

Katika maongezi yetu Hudini alionekana hakuwa anajua zaidi yangu kuhusu fumbo ambalo baba yangu alikuwa anataka niling’amue au labda alikuwa anafanya kusudi kutoniambia… kitu pekee ambacho alinieleza ni kwamba ananikabidhi maagizo kama ambavyo alielekezwa na hana la zaidi ambalo atanieleza. Alinikabidhi tu bahasha yenye nyaraka nyingi ndani yake na kisha kunieleza kuwa atanitafuta baada ya wiki mbili kunikabidhi bahasha nyingine. Nilipomuuliza natakiwa kufanya nini ndani ya wiki mbili hizobili, alinijibu huku anatabasamu kifedhuli… “I don’t know… I am just following my orders!” Na nilipomuuliza hizo “orders” zinatoka kwa nani alinijibu, “its none of your business.!”
Kwa mtindo ule ule wa walionichukua kutoka mtaa wa Hardstrasse, ndivyo ambavyo walinirudisha… lakini hawakunirudisha pale mtaa wa Hardstrasse bali walinirudisha hotelini nilipofikia karibu na uwanja wa ndege wa Zurich.

Kutokana na purukushani hizi za kunichukua na kunipeleka kule mtaa wa Wipkingen kutokea usiku wa manane, waliponirudisha hotelini tayari kulikuwa kunapambazuka. Ilikuwa ni asubuhi alafajiri. Kabla ya kuifungua ile bahasha niliyopewa na Hudini kwamba ilinipasa kulala ili kuweka akili yangu sawa. Nilikuwa najihisi kama nina karibia siku tatu sijapata usingizi. Na hakika ilikuwa ni zaidi ya siku tatu. Kuanzia safari yangu ya zaidi ya masaa kumi na sita kutoka Tanzania mpaka hapa Uswisi. Jumlisha usiku nilioenda kwenye mgahawa wa kichina na kufanyiwa mambo niliyopoteza fahamu na baadae kuamka kwenye jengo ambalo silifahamu mtaani Hardstrasse. Na baadae kupelekwa Wipkingen kuonana na Hudini. Kichwa kilikuwa kizito na kilikuwa kinauma haswa nilihitaji kupumzika kwa masaa kadhaa.

Nakumbuka nililala kwa siku nzima. Kuna muda nilihisi nilikuwa nalala tu sitamani kuamka kwa kuwa sikuwa nataka kukabiliana na uhalisia uliokuwa unanisubiri pindi nikiamka. Lakini hakuna marefu yasiyo na ncha na siwezi kulala milele. Hatimaye jioni yake niliamka na kufungua ile bahasha ambayo nilipewa na Hudini. Nilipoifungua na kusoma zile nyaraka zilizomo ndani nilielewa kwanini roho yangu ilikuwa nzito na kulala siku nzima bila kutamani kuamka. Nilielewa roho rangu ilikuwa inaogopa kukutana na uhalisia wa aina gani. Uamuzi ambao nilichukua baada ya kusoma zile nyaraka ndizo ambazo zimenifanya kuingia kwenye dhahama kubwa kwenye nchi hii ya ugenini niliyopo.

Lakini hayo yote yalikuwa ni siku mbili zilizopita. Leo hii nilikuwa nakabiliana na uhalisia mkubwa zaidi. Uhalisia wa kama nitathubutu kufumba macho basi kuna uwezekano mkubwa sitayafumbua tena. Uhalisia wa kiza kinene mbele yangu. Uhalisia wa kifo.

Nikatabasamu tena. Machozi yalitiririka tena kwenye kona za macho. Nikainua tena mkono kutoka tumboni na kuangalia namna ulivyoloa damu. Nikaurudisha tena tumboni kujishika damu isitoke kwa kasi zaidi. Macho yalikuwa yanazidi kulegea na nuru kupotea. Maumivu yote yalikuwa yamepotea. Sio kwamba hayakuwepo lakini mwili wangu ulikuwa unakufa ganzi na nilikuwa siyasikii kabisa. Uhalisia ni kwamba nilikuwa hata sihisi mwili wangu mwenyewe. Kitu pekee ambacho nilikihisi, kitu pekee ambacho kilikuwa ni halisi kwa sasa ni woga. Woga wa uhalisia kwamba nikifumba macho tu sasa hivi hakika sitafumbua tena.

Nikaanza kufikiria hatua kwa hatua mpaka mahali hapa nilipo muda huu. Sikuwa hotelini, na nina zaidi ya masaa ishirini na nne sijui kitanda cha hoteli yangu. Kwa uzuri zaidi niseme sijakiona kitanda cha hoteli yangu tangu juzi niliporejeshwa hotelini alfajiri na vijana wa Hudini na kisha kulala siku nzima mpaka jioni. Nipo koridoni mwa jengo ambalo visanga na vitimbi vyote vilikoanzia, jengo la HARDSTARASSE 201, 1985. Jengo ambalo siku kadhaa zilizopita nilijikita nimeamka ndani yake. Jengo ambalo nilisikiliza kipande cha video cha ujumbe ambao uliachwa na marehemu baba yangu. Jengo ambalo nilikuta nyaraka kwenye vault ndogo zikionyesha kwamba ninalimiliki. Hapa ndipo nilipo muda huu. Kwenye korido nje ya mlango wa kuingia kwenye kile chumba ambacho siku kadhaa niliamka ndani yake.

Nilikuwa nimelala hapa koridoni nikihesabu sekunde zilizobakia za uhai wangu. Nilikuwa nimelala nikiwa na jeraha la risasi tumboni linalovuja damu.

Japokuwa mwili ulikuwa umeishiwa nguvu na hata akili yangu kushindwa kufikiria sawa sawa nikiona maluweluwe tu, lakini nilijitahidi kuwaza. Kuwaza ni nini hasa kilikuwa nyuma ya pazia. Kuwaza nimewezaje kutegeka kirahisi hivi?

Niliwaza kweli kweli, ni nani hasa alikuwa nyuma ya pazia ya hiki kilichofanyika? Hudini? Lakini akili yangu ilikataa… Hudini alikuwa na uwezo wa kuniua Kyle Wipkingen kama angekuwa na nia hiyo. Lakini kila nilipotaka kumsafisha kichwani mwangu Hudini, akili ilikataa…. Hudini ndiye pekee anayejua uwepo wangu hapa Zurich. Au labda kuna mwingine? Ndio… nilijijibu mwenyewe… yule mzee wa kichina na vijana wake? Inawezekana wao ndio walikuwa nyuma ya pazia? Hapana… akili yangu ilikataa… nao walikuwa na uwezo wa kuniua siku ile ambayo walinipotezesha fahamu kwa kunichoma sindano ya kemikali.! Au kuna mwingine anayefahamu uwepo wangu hapa Zurich bila mimi kujua?

Ghafla nikasikia mlango wa komeo wa kule nje wa kutoka kwenye uchochoro, nikasikia unafunguliwa kwa staili ile ile niliyoisikia mara ya kwanza kabla ya kupigwa risasi. Macho yangu yaliyokuwa yanasinzia kwa kuchoka kutokana na mwili kuishiwa nguvu, niliyatoa kama vile nimekabwa. Woga ambao niliusikia ulikwa halisi mpaka niliweza kuuhisi kwenye ngozi yangu ya mwili. Kifo kilikuwa halisi mbele yangu kuliko hata nilivyohisi mwili wangu.

“Huu hauwezi kuwa mwisho wangu.!”

Nikajifariji japo nilikuwa siwezi hata kuinuka kupiga hatua moja.



Itaendelea…


THE BOLD
Asante. The Bold..
 
VIPEPEO WEUSI


SEASON 1 – FROM ZURICH WITH RULES



EPISODE 14


“Rweyemamu?” Yule jamaa nadhifu alitamka jina langu kwa tabu kwa lafudhi yake ya kingereza huku amejishika mkono kifuani kwa mshangao.

Kitendo cha kutamka jina langu sio tu kwamba kilinishangaza bali pia kilinichanganya akili. Mtu huyu muda mchache uliopita alikuwa anakaribia kuondoka kwa madai kuwa aliyekuwa wanamtafuta si mimi lakini ghafla tu baada ya kutamka kuwa mimi ni mmiliki wa hili jengo wanaonekana kunifahamu mpaka jina.
Nilijitahidi nifiche mshangao ambao nilikuwa nao ili niendelee kuyapeleka mazungumzo vile ambavyo nilikuwa nataka.

“I have been waiting for you for years!” Akatamka sentesi inayofanana kabisa na sentesi ambayo alitamka yule mzee wa kichina kwenye mgahawa. Kwamba kwa miaka kadhaa amekuwa akisubiria kukutana na mimi.

“Who are you guys?” Nikamuuliza yule jamaa akiwa tayari anainama ili kukaa chini pembeni yangu pale nilipokuwa nimejilaza.

“I am Luke and this is my friend Jimmy.!” Akajitambulisha na mwenzake wote wakiwa wameketi pembeni yangu. “Jimmy go get us some breakfast!” Akatoa noti nyingine kadhaa mfukoni mwangu na kisha kumpa yule mwenzake ninayemuhisi chokoraa ili aende kununua chakula.

Maumivu tumboni yalikiwa yamenifanya hata nisahau kama nilikuwa na karibia masaa ishirini na nne sijaweka kitu chochote tumboni.

Jimmy akapokea hela kutoka kwa Luke na kwenda kuchukua chakula. Tulibaki watu wawili tu hapa koridoni. Mimi na Luke, na nikaona huu ndio wakati hasa wa kunieleza yeye ni nani na nini kilikuwa kinaendelea hapa.

Nilitumia karibia dakika tano za awali kumshawishi Luke anieleze ukweli kuhusu yeye na kile kinachoendelea ambacho nilikuwa sikijui. Kwa mara kadhaa kila ambavyo nilimshawishi alijaribu kupindisha maongezi kwa kuingiza mjadala kuhusu jeraha langu la risasi na kujifanya kama anajali sana maendeleo yake. Lakini mwishowe nikafanikiwa kumshawishi aongee.

Aliongea kwa karibia nusu saa nzima, na muda wots huo Jimmy alikuwa bado hajarudi na chakula. Sikujua kama alikuwa ameenda mbali kuchukua chakula au labda walipeana ishara bila mimi kujua kwamba acheleqe kurudi ili mimi na Luke tupate faragha ya kuongea.

Katika maelezo yake, Luke alinieleza kwamba amewahi kutumikia jeshi kwa kipindi cha miaka nane kabla ya kujiunga kwenye kikundi cha siri kinachofanya kazi ndani ya nchi karibia saba ndani ya ulaya.

“A fraternity? Secret Society?” Nilimuuliza huku nimemkazia macho.

Haksema neno lolote lile. Alivua jaketi lake la ngozi na kisha akavua fulana. Kifuani mwake kwenye titi la kushoto kulikuwa na mchoro wa ajabu wa nyoka aliyejinyongorota huku akiwa anateka kitu kama moto. Kitendo cha kuona tu ule mchoro mwili wote ulisisimka.

“HUDINI.!” aliongea kwa kifupi tu.

Nilimkodolea macho nikiwa sielewi ni nini hasa alikuwa anajaribu kumaanisha. Jina la yule mzee mwenye lafudhi ya kifaransa linahusiana nini na tatoo yake kifuani.

“I don’t get your point!” Nilimueleza huku namuangalia kwa sura ya kwamba niko ‘confused’.

“Its a mark! Each member has one!” Akaongea

“Member of what?” Nilimuuliza tena

“HUDINI” akanijibu tena kwa kifupi.

Kwa mara ya kwanza ndipo akanifafanukia kuwa Hudini si mtu bali ni kikundi cha siri.

Nilishituka kidogo kwa sababu kwa muda wote huu nilikuwa nadhani kwamba Hudini lilikuwa ni jina la mtu, yule mzee ambaye alinipa picha za Rais Albert Kafumu na yule mzungu na picha za mzungu huyo akiwa na familia ya mke wangu Cheupe.

Katika maelezo yake alinieleza kwamba kikundi hiki cha Hudini kilikuwa ni kama kampuni ya siri ya kujitegemea ya masuala ya ulinzi, usalama na ujasusi na wanachama wake wote ni wanajeshi wastaafu, majasusi na polisi wachache wa vitengo Maalumu.
Alinieleza kuwa alitumikia kikundi hiki kwa muda wa miaka ishirini na mbili na kufanikiwa kushika baadhi ya nyadhifa za juu kabisa ndani ya kikundi hicho mpaka miaka miwili iliyopita ambapo alikosana vikali na wenzake na akalazimika kukitoa kwenye kikundi hicho.

“What happened?”

Nakumbuka nilimuuliza anieleze kuhusu huo mgogoro ambao ulitokea kati yake na wenzake. Nilimuuliza mara nyingi sana lakini alikataa katakata kunijibu. Kitu pekee ambacho alinieleza tena na tena kila nilipomuuliza ni kwamba, “kuna deni nahitaji kuwalipa?” Ndivyo ambavyo alinijibu kila nilipomuuliza.

Nilielewa fika kabisa sentensi hii ilikuwa ni fumbo alilokuwa analitumia kumaanisha hicho ambacho aligombana na wenzake.

Nikaona hakuna maana kwangu kuendelea kumuuliza swali ambalo kamwe hatonijibu na halikuwa na faida yoyote ile kwangu. Nikahamishia maswali yangu kwenye masuala ambayo nilihisi yalikuwa na maslahi ya moja kwa moja kwangu.

“Why were you looking for me?” Nikamuuliza.

“Because you are Charles Kajuna’s son.!” Alinijibu huku anatabasamu.

“So what?” Nikamjibu kwa kukereka kiasi.

Akaanza kunipa tena maelezo, kwamba alikuwa na uhakika kama akifanikiwa kunipata mimi basi atampata kiongozi wa sasa wa Hudini. Nilipomuuliza kiongozi wa HUDINI anamtaka wa nini, akarejea tena kauli yake ya fumbo, “Kuna deni nataka kuwalipa!”

Baada ya hapo akaendelea tena kunipa maelezo ambayo kwa kiasi fulani nilikuwa nayajua, kwa usahihi zaidi niseme nilikuwa nimeng’amua mwenyewe baada ya kikao changu cha juzi na yule mzee mwenye lafudhi ya kifaransa ambaye muda wote huu ndiye nilikuwa nikidhani kuwa jina lake alikuwa anaitwa Hudini.

Luke alinieleza kwamba, katika miaka ya mwishoni ya 1990s mwenyekiti wa jumuiya ya siri ya The Board kutoka nchini Tanzania, yaani baba yangu marehemu Charles Kajuna alitoa kandarasi kwa kikundi hiki cha Hudini kwa ajili ya kazi maalumu. Kazi ambayo ilikuwa ni nadra mno kwa kikundi kama chao kuipata.

Alinieleza kuwa kikundi chao kilikuwa kwa miaka mingi walikuwa wakipokea kandarasi za kutoa ulinzi kwenye usafirishaji wa biashara za magendo, ulinzi wa wafanyabiashara wakubwa, utekaji wa watu mashuhuri na muda mwingine hata kufanya oparesheni ‘chafu’ za siri za kijeshi kwa niaba ya baadhi ya serikali ambazo zilikuwa hazitaki skendali hizo zije kuchafua serikali zao ikitokea mambo yakafichuka na kuwa hadharani kwenye oparesheni hizo ‘chafu’.

Alipoongea kuhusu oparesheni ‘chafu’ za siri za kijeshi, nikakumbuka ile picha niliyoonyeshwa ya yule mzungu akiwa na Rais Albert Kafumu wakiongea mafichoni kwenye makontena. Nikajiuliza kama yule mzungu naye ni mwanachama wa Hudini. Hakukuwa na haja ya haraka au papara ya kuuliza maswali. Nikahifadhi swali langu hili moyoni nikamuacha Luke aendelee kuongea.

Luke akanieleza katika kandarasi hii ambayo walipewa na jumuiya ya The Board, kazi yao ilikuwa kwa macho ya kawaida ilionekana ni rahisi lakini ilikuwa ni kubwa na yenye kuhitaji umahiri na usiri mkubwa kuifanya.
The Board walikuwa wanahitaji kutunza baadhi ya siri zao kubwa ambazo wao wenyewe The Board walikuwa hawajiamini kuzitunza kutokana na uzito wake. Na si kutunza siri bali pia walihitaji kitu ambacho wenyewe walikuwa wamekiita “REPLACEMENT”. Yaani kama ikitokea jumuiya yao yote imesambaratika basi siri zao hizo zitue kwenye mikono Salama na kuwe na mfumo wa kumuwezesha mtu huyo atakaekabidhiwa siri hizi kufufua tena jumuiya ya kurandana na The Board kama kutakuwa na ulazima wa kufanya hivyo.

Nikakumbuka ile barua ambayo niliikuta kwenye bahasha niliyopewa na marehemu baba yangu ikiwa na neno moja tu la kifaransa “REMPLACEMENT”. Nikajiuliza mambo kadhaa kichwani. Lakini kwa mara nyingine sikutaka kuwa na papara ya kuuliza swali, nikamuacha Luke aendelee kuongea.

Luke akanieleza kwamba kutokana na uzito wa suala la The Board, suala hilo lilipaswa kuwekewa mfumo mgumu na wa siri kubwa sana.

“What was the secret about?” Nilimuuliza kwa kumjaribu.

Japokuwa nilijua wazi kuwa hata kama angelikuwa anajua asingenieleza kirahisi rahisi namna hii, lakini yeye mwenyewe alinitamkia kuwa hakuwa anafahamu. Alinieleza kwamba baada ya kupokea kandarasi hiyo, viongozi wakuu wa kikundi cha Hudini walitengeneza mfumo wa siri na mgumu kuhusu ‘details’ walizopewa na The Board katika namna ambayo watu wachache tu ndani ya Hudini kila mmoja wao alikuwa anajua details chache tu na hakukuwa na yeyote yule ambaye alifahamu suala hilo kwa ujumla wake.

Nilihisi hasira fulani hivi moyoni kwamba nkmesafiri maelfu ya maili kutoka nyumbani Tanzania mpaka hapa lakini naambiwa kwamba hata hawa ambao nilitegemea watakuwa na uelewa juu ya kilichonileta hapa nao ati hakuna kati yao anayejua kila kitu.

“I think i have said enough… its your turn now! What happened to you? How did you get shot?” Akauliza huku anatoa tabasamu hafifu.

Nikakumbuka siku tatu zilizopita niliporejeshwa hotelini kwangu kutoka kule Wipkingen. Nikakumbuka kilichotokea masaa ishirini yaliyopita. Nikajiuliza kama ni sahihi kwangu kumuamini huyu mtu na kumueleza kila ambacho kilitokea. Nikakumbuka msemo wake wa fumbo kuwa “Kuna deni anataka kuwalipa Hudini”. Nikakumbuka alivyoeleza kuwa amekuwa akinitafuta kwa miaka kadhaa kwa kuwa aliamini akinipata mimi atawapata Hudini hasa kiongozi wao wa sasa, ambao alikuwa amekorofishana nao.

Nikakumbuka namna ambavyo hakunitambua mara ya kwanza na kutaka kuondoka. Nikakumbuka namna ambayo baada ya kumwambia mimi ni mmiliki wa hili jengo aliniita jina langu. Nikajiuliza kama alifahamu jina langu, na pia alifahamu mimi ni mtoto wa Charles kajuna, ameshindwaje kuijua sura yangu? Iweje anitafute miaka yote kama anavyosema na asiwahi kuona hata picha yangu?

Nikajiuliza tena kwa nini anieleza siri zote hizi. Kuanzia tatoo yake kifuani. Uanachama wake ndani ya Hudini. Shughuli za Hudini na hata ugomvi walio nao na juhudi zake za kuwapata ili “awalipe deni” kama anavyosema.

Nikajiuliza kama hakuna mtego hapa nimewekewa.

Nilikuwa nawaza haya huku nimejiinamia. Nikainua uso kumtazama. Alikuwa ananiangalia huku anatabasamu kama vile anaisoma akili yangu.

“What happened Ray? How did you get shot?” Akauliza tena huku anatabasamu.

Nikavuta pumzi ndefu na kuishusha. Isingelikuwa jeraha tumboni mwangu, ningeweza kuinuka na kutimua mbio.


Itaendelea…


THE BOLD
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom