VIP makanisani.....

VIP makanisani.....

Wadau, hivyi mnajua kuna makanisa yametenga siti maalum kwa watu (VIP) fulani n ukikaa hizo siti lazima utanyanyuliwa. Ukiuliza sababu unaambiwa wewe utaweza kulipa 250,000 kila jumapili kama sadaka? hivyi dini ndiyo imekuwa biashara kiasi hicho?

Kuondoa mzizi wa fitina ni bora ungetutajia kabisa hayo makanisa tuyajue na watu watadhibitisha kama ni kweli au laa.
Jf ;where we dare to talk openly.
 
Hakuna kitu kama hicho ni fikra potofu tu, jaribu kukaa hizo siti kama watakufukuza. St Peters na St Joseph nishakuwa member sana hakuna hiyo kitu aisee lol
 
nenda mikocheni kwa mama,dr,mchungaji,mheshimiwa kajaribu kukaa kitic chochote cha mbele kama hujaambiwa we! Kakae kuleeeee nyuma na usirudie tena kukaa hapa,hapa wapo wenyewe
haswaaaaaaaaaaa! Hapo ndiyo penyewe mkuu..........
 
Ray B,ushaambiwa makanisa halafu wewe unataja stpeters na stjoseph?mbona hauko serious?Mbonea namaanisha kwa MAMA,DPC,UFUFUO NA UZIMA,GRC na mengine ya aina hiyo.
 
Hata kama si viti, kuna ukweli kiasi kikubwa tu kwamba baadhi ya taasisi za dini/makanisa yanashobokea vigogo. Haya mambo ya imani za kidini ndio maana yanaangaliwa critically huko China. Hizi imani za kidini ukiziendekeza sana zitakuchanganya tu.
 
Hayo yatakuwa ni makanisa mapya mapya wao kwanza pesa na mambo mengine baadae wakale wapi, wakati kutwaaaaaaa wanashinda makanisani wakihubiri alaaaaaaa!!!!!!!
 
Naomba kutofautiana na wewe na kusema hiyo siyo kweli. Mimi ni muumini wa kawaida, na kwa maelezo yako unazungumzia Usharika wa Azania Front. Nina mfano wa kuthibitisha kuwa hilo unalosema siyo kweli. Miaka ya nyuma nilipata kutoa sadaka maalumu hapo usharika wa Azania. Kwavile tuliwahi sana kufika, tulikaa bench la mbele kabisa ili iwe rahisi ukifika wakati wa kwenda mbele tusipate usumbufu, HAKUNA aliyekuja kutuomba tutoke au tuhame. Utaratibu gani huo wa siri? Hebu weka wazi basi. Hapo nyuma nimeeleza kuwa kutokana na nafasi ya baadhi ya viongozi, ni kweli lazima watengewe nafasi maalum kwenye nyumba za ibada. Na naamini hii ni kwa madhehebu yote, na haina uhusiano na kiasi cha sadaka anayotoa mtu.

Mzawa Halisi,

Kwa jinsi nilivyomuelewa Ngongo, KKKT mjini kati ni usharika uliopo mjini Arusha, na baadhi ya watu aliowataja (Mfano Mzee Mshiu) wanasali Mjini Kati Arusha. Na siyo Azania front jijini Dar.

Ni vyema wanajamii kujua kuwa kwa upande wa viongozi wetu wakuu, hasa wa serikali. Kila mahali atakapokuwa lazima suala la usalama wake linapewa kipau mbale, hivyo watu wa usalama watamshauri ni sehemu gani bora yeye akae. Siyo kanisani, au msikitini tu, bali hata katika harusi, misiba nk huwa wanakuwa na sehemu zao za kuketi.

Masaiti.
 
Mzawa Halisi,

Kwa jinsi nilivyomuelewa Ngongo, KKKT mjini kati ni usharika uliopo mjini Arusha, na baadhi ya watu aliowataja (Mfano Mzee Mshiu) wanasali Mjini Kati Arusha. Na siyo Azania front jijini Dar.

Ni vyema wanajamii kujua kuwa kwa upande wa viongozi wetu wakuu, hasa wa serikali. Kila mahali atakapokuwa lazima suala la usalama wake linapewa kipau mbale, hivyo watu wa usalama watamshauri ni sehemu gani bora yeye akae. Siyo kanisani, au msikitini tu, bali hata katika harusi, misiba nk huwa wanakuwa na sehemu zao za kuketi.

Masaiti.
Tuko pamoja mkuu.
 
naomba niyataje hayo makanisa na vip seats.

1.azania front

edward lowasa huyu alipewa kiti cha mbele kushoto

2.saint joseph cathedral na some times saint peters oysterbay.

benny mkapa mbele kulia
kwa mama mikocheni kuna viti vya watu maalum
 
Wadau, hivyi mnajua kuna makanisa yametenga siti maalum kwa watu (VIP) fulani n ukikaa hizo siti lazima utanyanyuliwa. Ukiuliza sababu unaambiwa wewe utaweza kulipa 250,000 kila jumapili kama sadaka? hivyi dini ndiyo imekuwa biashara kiasi hicho?

hiyo ni kweli - huwezi kwenda kwa mama Rwakatare ukafika wa kwanza kwanza ukakae viti vya mbele mstari wa kwanza - heee utaona wazee wa kanisa wanakufuata palepale wanakuonyesha alternative sit - ni kweli haya makanisa ya binafsi yako hivyo.
 
Tuambie ushawahi kukaa wanapokaa ukafukuzwa!?? Hii mimi naona ni mazoea tu mtu unakuwa umezoea kukaa sehemu moja mpaka hata wasahrika wenzanko wanacram kama ni siti yako!!!
Mi nina mfano halisi wa mtu aliondolewa kiti cha mbele na mmpaka leo ameacha kusali na ni pale azania
 
kanisa flan la kkt pale mjini, kwani ni siri?
 
Wadau, hivyi mnajua kuna makanisa yametenga siti maalum kwa watu (VIP) fulani n ukikaa hizo siti lazima utanyanyuliwa. Ukiuliza sababu unaambiwa wewe utaweza kulipa 250,000 kila jumapili kama sadaka? hivyi dini ndiyo imekuwa biashara kiasi hicho?

Kwa viongozi kwa sababu za kiusalama lazima watengewe sehemu za kukaa katika nyumba za ibada,... Hii ni kuepuka watu kama yule aliempiga Raisi mstaafu Mwinyi kofi kali la shavu.
Ila mtoa mada uendelee kueleza zaidi na hizo 250 kilo'z kila ibada ni kanisa gani wanafanya hivyo? Sema tu unamuogopa nani?
 
ilo kkt apo mjini hata kwa wafanyabiashara wanasiti zao maalum! mbona jamani ilo kanisa la kkt si siri tena, its normal practise!
 
Wadau, hivyi mnajua kuna makanisa yametenga siti maalum kwa watu (VIP) fulani n ukikaa hizo siti lazima utanyanyuliwa. Ukiuliza sababu unaambiwa wewe utaweza kulipa 250,000 kila jumapili kama sadaka? hivyi dini ndiyo imekuwa biashara kiasi hicho?

Wewe ni mwongo na mzushi. Mwogope MUNGU.
 
Wewe ni mwongo na mzushi. Mwogope MUNGU.

rmashauri kabla hujamwita Mbonea mwongo, tembea uone.

Huu ubishi wako utachokoza mambo mengine ambayo wachungaji wako watakulamu kwa kuyachokoza.

Duniani kote sasa hivi kuna uhuni mkubwa sana unaendelea makanisani kwa sababu ya uongozi wa makanisa mengi kushikwa na watu wenye kupenda fedha na anasa za dunia.

Usitufanye tukamwaga hapa hadharani majina ya makanisa yanayotumika kuendesha biashara haramu.......naomba niishie hapo.

Ujue tu tuna mengi..yanatuumiza sana mioyo...unafiki unakera sana.

Nazima kompyuta nikae chini niugulie maumivu, halafu niamue nirudi jamvini kutoboa siri hadharani au lah!!!!!!TUNA MENGI SANA NA TENA TUNA USHAHIDI WA KUTOSHA!!!!!!!!!
 
Nadhani uliyeleta mada hii si Mkristo na kama ni Mkristo - ni Mkristo jina usiyepata hata muda wa kusoma Biblia. Watu uliyowatolea mifano ni Viongozi - Watu wanaopaswa KUHESHIMIWA ndivyo Biblia inavyoagiza - lakini si Biblia tu popote pale wanapokanyaga wanapaswa kupewa ulinzi - maana adui hachagui ni wapi ulipo hivyo lazima walindwe hata wanapokuwa katika kumwabudu MUNGU wao!!. Kwa sababu WAYAHUDI kuna wakati walitaka kumkamata BWANA YESU kwenye sinagogi lakini kwa kuwa yeye alikuwa anajua mawazo ya wanadamu aliwatangulia kabla hawajafanya ubaya maana wakati wake ulikusudiwa ulikuwa haujafika. Acheni kuleta mada zisizo na msingi BANA.
 
Mi nina mfano halisi wa mtu aliondolewa kiti cha mbele na mmpaka leo ameacha kusali na ni pale azania

Hii thread inazungumzia kupangiwa viti maalumu kutokana na utoaji wa sadaka. Huo aliyeondolewa mbele ni kwavile anatoa sadaka kidogo au anampisha mwenye sadaka kubwa? Unapokuwa na mfano ni vizuri ukatoa maelezo yenye ushawishi. Inawezekana kuombwa kukaa sehemu nyingine, hasa kama kanisa linategemea wageni (siyo lazima VIP), mfano kwaya au wazee wa kanisa toka usharika mwingine. Sasa ukitupa maelezo ya mazingira ya huyo jamaa yako tutapima mchele na pumba.
 
rmashauri kabla hujamwita Mbonea mwongo, tembea uone.

Huu ubishi wako utachokoza mambo mengine ambayo wachungaji wako watakulamu kwa kuyachokoza.

Duniani kote sasa hivi kuna uhuni mkubwa sana unaendelea makanisani kwa sababu ya uongozi wa makanisa mengi kushikwa na watu wenye kupenda fedha na anasa za dunia.

Usitufanye tukamwaga hapa hadharani majina ya makanisa yanayotumika kuendesha biashara haramu.......naomba niishie hapo.

Ujue tu tuna mengi..yanatuumiza sana mioyo...unafiki unakera sana.

Nazima kompyuta nikae chini niugulie maumivu, halafu niamue nirudi jamvini kutoboa siri hadharani au lah!!!!!!TUNA MENGI SANA NA TENA TUNA USHAHIDI WA KUTOSHA!!!!!!!!!
Ninapotaka mimi ni hapo tu! Chondechonde nakuomba hebu toboa hiyo siri tujue kilichomo.
 
Back
Top Bottom